Tanzania tulikosea wapi na Kenya walipatia wapi?

Tanzania tulikosea wapi na Kenya walipatia wapi?

Ulivyo anza mada yako inaonyesha kwamba huijui Tanzania (Tanganyika) kabla ya uhuru na huijui Kenya kabla ya uhuru! Pia hujui Tanganyika na Kenya zilivyopata uhuru. Ukiyajua hayo, hutalinganisha Tanzania na Kenya mpaka unakufa!
Anzisha mada yako na uweke hayo unayosema, sawa? Ni ujinga kuparamia mada za watu huku ukijifanya mjuaji kumbe huna lolote!! Huoni watu wanachangia mawazo yao kwa maana ya kwamba wameelewa kunachozungumzwa? Au wawaona woootee wanachangia ni vilaza kama wewe?
 
Tanzania na Kenya zilipata uhuru mapema miaka ya 1960s. Leo zinakaribia miaka 60 tangu zipate uhuru.

Nchi hizi mbili ni kama makaka wawili waliozaliwa tumbo moja ila kila mmoja kachukuwa njia tafauti katika kutafuta maisha. Na kwa mtazamo wa haraka Tanzania imefeli vibaya sana katika miaka yote 60 wakati Kenya angarau anapigia hatuwa kwenda mbele japo kuwa kwa mwendo wa ponda.

Tanzania imeshindwa hata kuinuka bado inapiga usigizi wa mtoto mchanga. sasa swali la kujiuliza Tanzania tumekosea wapi na kenya wamepatia wapi? Swali hili nitalijibu simple sana kenya pamoja na makosa mengi lakini kwenye upande wa elimu walipatia kwa kiwango kikubwa.

Mkenya wa darasa la saba anaweza kumzidi marifa Mtanzania wa form six. Tanzania elimu yetu ni zero tangu enzi za Nyerere. Yaani elimu yetu sio ya kuelimisha bali ni ya kufaulu mitihani. Ndio maana tuna watu wenye PHD lakini matendo yao na fikira zao ni kama mtu ambaye hajaenda shule kabisa.

Kwa mfano ukiangalia PHD holders wa Tanzania wengi wanafanya kazi za kuteuliwa na watawala kama wa kuu wa mikowa au mawaziri. na ukiangalia performances zao ni ziro. Kwanini? Kwasababu wao kitu mhimu kwao ni cheo sio matokeo. Kwasababu tangu wakiwa mashuleni walifundishwa kufaulu mtihani mwisho wa muhula ndio mhim kuliko kuelewa.

Naungana na wewe, kuongezea ni kwamba;

(1)kenya ilikuwa ni settler colony kwamba viwanda vingi vilijengwa kwao na miundombinu,hata social services zilikuwa impoved by that time na hata wazungu wamechangia pakubwa sana ktk uchumi wao

(2)Capitalism as their national ideology na siku zote penye ushindani maendeleo yanakuja haraka ukilinganisha na mwendo wetu slow ila sio kwamba hatutafika waliko ila ni swala la mda tu
 
Kuna sababu nyingi zilizoleta tofauti kubwa katika nyanza nyingi kati ya Tanzania na Kenya iliyopata Uhuru miaka miwili baada ya sisi. Sababu kubwa kabisa ni elimu iliyoharibiwa toka Awamu ya Kwanza muda mfupi tu baada ya Uhuru katika juhudi ya kuleta elimu nzuri ya Kitanganyika tofauti na ile ya Kikoloni. Elimu hiyo mpya ilikuwa na makosa mengi yaliyoadhiri ubora lakini kosa kubwa kabisa ilikuwa kuondoa kabisa Darasa la Nane ambalo lilikuwa la mwisho Shule za Msingi. Hii ikawa sawa na kubomoa msingi wa nyumba ukaendelea kujenga nyumba ukitegemea itakuwa imara ya kudumu. Kenya nao waliiga mtindo huo lakini waligundua kosa hilo mapema na kurekabisha miaka michache tu baadaye na kurudisha Darasa la Nane hadi leo badala yake waliondoa kabisa Form Six. Wakenya wakaja na mfumo wa 8-4-4 ikiwa na maana ya miaka 8 Msingi, miaka 4 Sekondari na miaka 4 Chuo Kikuu digrii ya kwanza. Hii ina maana Form Five ilihamishiwa Chuo Kikuu kumuandaa mwanafunzi kuingia Chuoni. Huu ndo mfumo uliokuwapo Chuo Kikuu cha Makerere kabla ya Uhuru wa nchi zote tatu za Afrika Mashariki. Zambia wao walifutilia mbali Form Five na Six wakabaki na Form Four tu na wanafunzi wao wanapokelewa vyuo vyote duniani wa kwetu wa Form Six wakikataliwa. Bahati mbaya sana toka Awamu ya Kwanza kila Waziri anayeteuliwa kuongoza Wizara ya Elimu alikuja na mbinu zake za kuboresha elimu lakini amekuwa akimaliza kwa kuharibu zaidi. Matokeo yake sasa hivi kila kiongozi Serikalini, Bungeni na Mahakamani ana PhD ambayo haijulikani ni ya Chuo gani wala fani gani ikileta hisia tofautitofauti juu ya elimu ya viongozi wetu.
Daah huu nao ni ukweli mchungu...
 
elimu ipi unayoizungumzia!!

hii ya wakoroni inayotambua maendeleo ya nchi kwa kuangalia GDP,isiyokupa nafasi hata kufikiri nje ya hapo!!!
Elimu ya kuweza kujitegemea, kuvumbua visaidia maisha, ubunifu na uweledi mkubwa kwenye kuanzisha na kuendesha viwanda, makampuni, mashamba makubwa ili kutengeneza ajira. Siyo elimu ya kukariri na kufaulia mitihani... Elimu ambayo unaweza kwenda kufanya kazi popote duniani etc etc
 
Acha uongo mkuu, nimekaa Kenya almost 6 years, labda useme wazawa wenyenacho ni wachache sema wanakuwanacho kingi na swala la ardhi kule ni utata sana. Foreigners ndiyo wana maisha mazuri Kenya. Ila elimu yao iko vizuri sana. Kuna sehemu very famous inaitwa Kibila, siku nikipata nafasi ntakuja kuandika niliyoyaona Kibila.
Ni Kibra. Zamani ilikuwa yaitwa Kibira. Sina haja ya kusoma utakayoyaandika ikiwa hata jina la mahali lakuchenga. Najua wataka kuandika nini. Watu wengi wanaotoa mfano wa umaskini Kenya wanazungumzia ubaya wa Kibra. Lakini hapa Tanzania tuna Kibra ngapi? Umekwenda vijijini wewe uone Maisha ya watu huko. Kibra ilianza kama mji-tnzu wa Nairobi unaowapokea watu wanaotoka vijijini kuja mjini kutafuta Maisha. Hiyo ni miaka ya 50. Ina historia ndefu ya umaskini na deprivation. Lakini hivi karibuni serikali imetengeneza sana na inazidi kuboreshwa.
Na si kweli kuwa foreigners pekee ndiyo wana Maisha mazuri.
 
Hivi hatuwezi kufanya dua mwezi mzima ili taifa letu liondokane na umasikini na tuingie moja kwa moja kwenye kundi la nchi zinazoongoza kwa uchumi wa juu? Yaani tuingie G8 countries??
 
Uvivu wa kujielimisha nini kinatokea mataifa mengine yanatunuyima uwepo wa kuchambua yanatokea kwetu, Fuatisha yanayotokea Russia, Greece, Italy,USA, Argentina, Brazil, and host of other countries utagundua siasa ni mchezo mchafu, muhimu kama mshindani umejipanga vipi.

Mshindani hutumia kila mbinu na taratibu za kupata ushindi hata bao la mkono ili matokeo yawe na manufaa kwa mshindani aliye jipanga.

Tutalalamika sana, suali jee tunafanya nini baada ya matokeo. Tunaenda kwa Armterdam atusaidie kupata majawabu ya matatizo yetu?

Na bila uchambuzi wa kina kuhusu nini kimefanyika ushindi kuwa hivi, tutalia lia kama mbwa aliye popolewa mawe bila kuwa na majawabu. CCM ni chama cha siasa kinangia kwenye ushindani ili kipate dola na kufaidi mamlaka.

Tumepewa makombo ya viti 19 ambavyo vitatupa nafasi ya kulipia ofisi Ufipa na kundesha chama bila kukua.
Hata tukikataa million 65 kwa mwezi kwa kutopeleka wabunge, tumejipanga kivipi kukabiliana na ukata ambao kwa sasa hatuna jibu nao?.

Wapiga kelele kwenye mitandao wangeanza kampeni ya kuchangisha pesa kuwalipa makatibu wa kanda na ni shs 18 million tuu kwa mwezi.

We must be forward looking members to forestall more damage to our party which shall come into open just before March next year.


UKILALAMIKA KUUMWA KICHWA UNATAKIWA UWE UNAKIMBILIA HOSPITALI ILI KUEPUKA KIFO KWA KUWAHI MATIBABU.
Huu ni mfano mzuri wa tatizo la elimu la Tanzania, unaweza kukuta huyu ana digrii 2 au 3....
 
Wakenya ndio watu wa kwanza kuanza kulima maua na kusafirisha nje wakaambukiza na mikoa ya Arusha kilimo cha maua, jiulize huo mfumo wa kilimo wa kutumia greenhouse walianza wakenya ndio ukaja hadi Tanzania, na Tanzania kwa position iliyopo ingepata viongozi makini jumlisha bandari tu ya DSM basi biashara ingeshamiri sana na ukanda wote huu ungechangamka na kututegemea lakini ndio hivo
Halafu watanzania wakaamua kuharibu green house ya Mtanzania mwenzao aliyekuwa anauza maua na Green beans nje ya nchi na kulipa kodi na kutoa ajira. Kisa tuu tafauti za kisiasa za kijinga. Badala ya kumpiga faini ili waendelee kupata kodi mbalimbali wao wakaamua kumuua ng'ombe wa maziwa.
 
Tanzania na Kenya zilipata uhuru mapema miaka ya 1960s. Leo zinakaribia miaka 60 tangu zipate uhuru.

Nchi hizi mbili ni kama makaka wawili waliozaliwa tumbo moja ila kila mmoja kachukuwa njia tafauti katika kutafuta maisha. Na kwa mtazamo wa haraka Tanzania imefeli vibaya sana katika miaka yote 60 wakati Kenya angarau anapigia hatuwa kwenda mbele japo kuwa kwa mwendo wa ponda.

Tanzania imeshindwa hata kuinuka bado inapiga usigizi wa mtoto mchanga. sasa swali la kujiuliza Tanzania tumekosea wapi na kenya wamepatia wapi? Swali hili nitalijibu simple sana kenya pamoja na makosa mengi lakini kwenye upande wa elimu walipatia kwa kiwango kikubwa.

Mkenya wa darasa la saba anaweza kumzidi marifa Mtanzania wa form six. Tanzania elimu yetu ni zero tangu enzi za Nyerere. Yaani elimu yetu sio ya kuelimisha bali ni ya kufaulu mitihani. Ndio maana tuna watu wenye PHD lakini matendo yao na fikira zao ni kama mtu ambaye hajaenda shule kabisa.

Kwa mfano ukiangalia PHD holders wa Tanzania wengi wanafanya kazi za kuteuliwa na watawala kama wa kuu wa mikowa au mawaziri. na ukiangalia performances zao ni ziro. Kwanini? Kwasababu wao kitu mhimu kwao ni cheo sio matokeo. Kwasababu tangu wakiwa mashuleni walifundishwa kufaulu mtihani mwisho wa muhula ndio mhim kuliko kuelewa.
Hata wakenya wenyewe wakiisoma habari hii, watakushangaa sana mwandishi.
 
Matatizo yote ya Tanzania yametokana na Nyerere na misimamo yake ya hovyo isiyokuwa na kichwa wala miguu.
Kimsingi hatutakiwi kujilinganisha na Kenya hata kidogo maana ukiangalia factors zote za kuwezesha maendeleo labour & capitals kwa maana ya resources tunawazidi Kenya kwa mbali sana.

Kama wakenya ndio wangekuwa na nchi yetu ya Tanzania sasa hivi wangekuwa zaidi ya S.A.imagine nyerere alidhinisha katiba yenye mapungufu ili imsaidie katika kipindi chake cha uongozi na alikiri kabisa katiba ina maoungufu na alikuwa na uwezo was kubadilisha lakini akaamua kuiacha hivyo hivyo.

Uoga wa Watanzania ambao unatokana na ujinga ulipitiliza ,kwa sehemu kubwa umesababishwa na nyerere-ambapo alijiona yeye ndio kila kitu.laiti kambona asingefanya upumbavu wake kipind like ambapo tayari dola ilikuwa imisha mponyoka nyerere Leo hii tungekuwa nbali sanauw
 
The education system in the UK is divided into four main parts, primary education, secondary education, further education and higher education. Children in the UK have to legally attend primary and secondary education which runs from about 5 years old until the student is 16 years old.

Education System in Zambia
The Zambian education system has a 7-5-4 structure, namely 7 years at primary school, 2 and 3 years at junior and higher secondary school respectively, and 4 years at university for undergraduate degrees.

The system of education in Uganda has a structure of 7 years of primary education, 6 years of secondary education (divided into 4 years of lower secondary and 2 years of upper secondary school), and 3 to 5 years of post-secondary education, according to Education News Uganda The government of Uganda recognizes
 
Ni Kibra. Zamani ilikuwa yaitwa Kibira. Sina haja ya kusoma utakayoyaandika ikiwa hata jina la mahali lakuchenga. Najua wataka kuandika nini. Watu wengi wanaotoa mfano wa umaskini Kenya wanazungumzia ubaya wa Kibra. Lakini hapa Tanzania tuna Kibra ngapi? Umekwenda vijijini wewe uone Maisha ya watu huko. Kibra ilianza kama mji-tnzu wa Nairobi unaowapokea watu wanaotoka vijijini kuja mjini kutafuta Maisha. Hiyo ni miaka ya 50. Ina historia ndefu ya umaskini na deprivation. Lakini hivi karibuni serikali imetengeneza sana na inazidi kuboreshwa.
Na si kweli kuwa foreigners pekee ndiyo wana Maisha mazuri.
Mkuu kama unasema kuwa Kenya siyo foreigners tu ndiyo wana maisha mazuri basi huijui Kenya. Swala la Kibira kuwa ni Kibra hilo silifahamu so yaweza kuwa kweli au si kweli, unajua watu kama waalimu, manesi, drivers and the like kwa Kenya wanaishi wapi? Anyway sipendi kuzungumzia sana hiyo nchi kwani hainihusu lakini ntakuja kuleta story ya niliyoyaona Kibira(wewe waita kibra).
 
Inabidi pia ueleze watu Kenya anapatia kwenye nini.

Kenya inaongoza kwa tatizo la ajira ukanda huu
Kenya inaongoza kwa rushwa mbaya ukanda huu
Kenya ina raia wenye maisha duni zaidi ukanda huu
Kenya gharama za maisha ziko juu zaidi, mbali ya kwamba wana uchumi mkubwa wakiwa wachache zaidi yetu
Kenya ina siasa chafu, sisi zina kasoro moja ndogo tu
Ukabila na ukosefu wa umoja wa kitaifa ni tatizo sugu Kenya

Kwa kukutaarifu tu, wana mabaya mengi zaidi kuliko mazuri machache waliyotuzidi, ambayo hata hivyo yanakwenda yakibadirishwa kuwazidi siku si nyingi.

Msiishi kwa stori za mitandaoni, tembeeni.
Naona umepandwa na wazimu, hizi hapa takwimu za world bank na IMF waliosema nyinyi ni low middle income na mkashangilia.

i) 32% ya Kenya ndio maskini yani wanatumia chini ya $1.9 kwa siku, Tanzania ni 60% kwa sababu hiyo idadi wanaishi chini ya $1.9 kwa siku (IMF).

ii) Kenya raia wana afya nzuri kulingana na world bank na WFP. Tanzania inaongoza eac kwa kuwa na watoto wenye utapia mlo ingawa mnapanda chakula na kuuza mpaka kenya na watoto ambao akili zao hazikui vizuri kwa kukosa lishe bora. (WFP na WHO).

iii) Ikifika kwa elimu hata usitaje ukanda huu ni Uganda tu ndio infata Kenya.(University rankings, IMF na World bank).

iv) Kwa kutimiza malengo ya maisha Kenya ni namba ya tatu afrika ikifata sychelles na mauritius.Yani mtoto akizaliwa na kusoma Kenya ako na 62% chance ya kutimiza malengo yake kwa maisha. (Human capital index report 2020)

v) Mkenya wa kawaida anaishi miaka 4 zaidi kushinda mtanzania (WHO).

v) Kwa inequality Tanzania inashinda Kenya, Tanzania iko na millionaires wengi kushinda kenya lakini pia 60% ya watu Tanzania ni maskini wa kutupwa. (IMF poverty report). Tanzania bado iko katika nchi 28 maskini kabisa duniani.

vi) Kwa miundo mbinu Tanzania iko chini sana, port ya mombasa (2.7 million teus capacity) kwa sahi ni mara 2 ya port zote nne za Tanzania nikiunganishwa na bado inazidi kupanuliwa itafikia 4 million teus mwaka 2022 december. Kenya iko na bara bara kubwa kushinda Tanzania na sahi tunajenga flyover highway ya 27km ikipita kati kati ya jiji la Nairobi kutoka kwa uwanja wa ndege.

vii) Tanzania na burundi zinaongoza eac kwa kuwa na watoto wanaofariki kabla ya kufika miaka 5. Hapa tena lishe bora na usafi iliangaziwa na World bank.

Kwa hivyo najua unataka kujipa consolation lakini hiyo propaganda yenyu yote ni kelele.
 
Huna mantiki ndugu yangu. Na pengine mzee wangu! Kwanza wanikosoa kwa dhana ya per capita, kana kwamba hii yatumiwa Kenya pekee. Tukisema per capita Tanzania inaifanya kuwa nchi ya pato la katikati ya chini…..hiyo wakubali! Lakini Kenya...nongwa, siyo?. Punguza jazba ndugu yangu, aliye mbele yuko mbele tu. Kenya yatupita sana. Na hayo mapungufu ambayo nayaita 'changamoto' nani hanayo? Litakalokukasirisha Zaidi ni habari hii kuwa kama tukiendelea na siasa hizi za kujipiga kifua na kutoa povu, tusichanganyike na dunia na kujifunza….miaka kumi kutoka sasa Kenya itakuwa zaidi yetu mara mbili (Wakati miaka ya 2005-8 tulikuwa twaikaribia, kiasi miaka miwili tulikuwa mbele yao kwa mapato!). Hawatatuzidi kwa uchumi tu, bali kisiasa, kijamii na.….furaha ya Maisha (joie de vivre). Wee utabakia kuchukia tu. Chuki namna hii dhidi ya mtu aliyetangulia kwa juhudi zake, ndiyo huwafanya wengine wakawa wachawi, chunga! Nasikitika utawala huu umefanya 'uzalendo' kuwa na tafsiri mbaya sana, ya kubeza, kuwatazama chini na hata kuchukia wengine. Maana hasa ya uzalendo ni kuipenda nchi yako kiasi cha kutaka kuiga yote mazuri ya nchi nyingine.
Hebu nikukasirishe Zaidi: Juzi Kenya imelipa deni lake loke kwa Uingereza! Tanzania kwa miaka minne iliyopita imekopa dola bilioni 9! Hiyo ni rekodi haijawahi kufanywa. Unajua na kusoma Kiingereza wewe? Basi soma ripoti za nje pia. Ndiyo maana aliyesema tumekosea 'elimu' hakukosea kabisaaaaa. Haki ya Mungu!
Salute kwako mkuu ... Yaani hapo uliposema kujifunza kwa aliyekuzidi is everything, hata kwenye maisha yetu, nina mifano: katika maisha nimekutana na jamaa mmoja, pamoja na tabia yake ya kujisikia, niliweza kujifunza meengii sana na kujikwamua kiuchumi kutoka kwa huyo jamaa. Mara ya kwanza kwenda abroad kwenye workshop fulani tulikuwa Waafrika 2 tu mimi na Mkenya, the rest ni wazungu na from Asia. It was my first presentation outside, Sasa nikaamua kuonyesha yule Mkenya my presentation kwani ili same field but tofauti ni nchi tuu. Yule Mkenya akaniambia nifanye presentation kwake as if nawasilisha kwenye warsha,na nilipomaliza tukaanza kujadili, aise yaani tuliifumua whole presentation na ikabidi jamaa zangu wanitumie some good and new pics. Yaani niseme kama siyo yule Mkenya kwa kweli ningeadhirika sana kwani maandalizi yangu was very poor na hayakuwa yanajibu objectives za ile workshop. Alinipa many techniques na kufanya many rehearsals mpaka ilipofika siku ya actual presentation it was superb, and eventually project yetu ilipata funds kwenye hiyo component as a result of the presentation. So the guy is one of the family friends todate na tunatembeleana sanaaaaa, kwao ni Nyeri. So mimi mtu aliyefanikiwa ndiye kwa kweli napenda sana kujifunza alifikaje hapo.
 
Mkuu kama unasema kuwa Kenya siyo foreigners tu ndiyo wana maisha mazuri basi huijui Kenya. Swala la Kibira kuwa ni Kibra hilo silifahamu so yaweza kuwa kweli au si kweli, unajua watu kama waalimu, manesi, drivers and the like kwa Kenya wanaishi wapi? Anyway sipendi kuzungumzia sana hiyo nchi kwani hainihusu lakini ntakuja kuleta story ya niliyoyaona Kibira(wewe waita kibra).
Hawa ndio top 10 kwa utajiri kenya
i) Vimal shah
ii) Jimnah mbaru
iii) Peter munga
iv) James Mwangi
v) Chris Kirubi
vi) Bhimji Depar shah
vii) Naushad Merali
viii) Mama Ngina Kenyatta
xi) Manu Chandaria
x) Uhuru Kenyatta.

Kwa hio list hakuna foreigner wote ni wakenya.
 
Back
Top Bottom