Tanzania tulikosea wapi na Kenya walipatia wapi?

Tanzania tulikosea wapi na Kenya walipatia wapi?

Inabidi pia ueleze watu Kenya anapatia kwenye nini.

Kenya inaongoza kwa tatizo la ajira ukanda huu
Kenya inaongoza kwa rushwa mbaya ukanda huu
Kenya ina raia wenye maisha duni zaidi ukanda huu
Kenya gharama za maisha ziko juu zaidi, mbali ya kwamba wana uchumi mkubwa wakiwa wachache zaidi yetu
Kenya ina siasa chafu, sisi zina kasoro moja ndogo tu
Ukabila na ukosefu wa umoja wa kitaifa ni tatizo sugu Kenya

Kwa kukutaarifu tu, wana mabaya mengi zaidi kuliko mazuri machache waliyotuzidi, ambayo hata hivyo yanakwenda yakibadirishwa kuwazidi siku si nyingi.

Msiishi kwa stori za mitandaoni, tembeeni.

Ndugu umenena
 
Matatizo yote ya Tanzania yametokana na Nyerere na misimamo yake ya hovyo isiyokuwa na kichwa wala miguu.
Kimsingi hatutakiwi kujilinganisha na Kenya hata kidogo maana ukiangalia factors zote za kuwezesha maendeleo labour & capitals kwa maana ya resources tunawazidi Kenya kwa mbali sana.

Kama wakenya ndio wangekuwa na nchi yetu ya Tanzania sasa hivi wangekuwa zaidi ya S.A.imagine nyerere alidhinisha katiba yenye mapungufu ili imsaidie katika kipindpi chake cha uongozi na alikiri kabisa katiba ina maoungufu na alikuwa na uwezo was kubadilisha lakini akaamua kuiacha hivyo hivyo.

Uoga wa Watanzania ambao unatokana na ujinga ulipitiliza ,kwa sehemu kubwa umesababishwa na nyerere-ambapo alijiona yeye ndio kila kitu.laiti kambona asingefanya upumbavu wake kipind like ambapo tayari dola ilikuwa imisha mponyoka nyerere Leo hii tungekuwa nbali sanauw
Unafikira za kujidanganya au umedanganywa. Kuna maelezo mengi ambayo hayana
Ukweli umeandika hapa. Nitakutafuta tuzungumzie yawezekana ukasaida wengi ambao wana ufahamu kama wako.
 
Kumbuka kwamba kwa utajiri tulionao TZ kuanzia ardhi nzuri ya kilimo na ufugaji (nusu ya ardhi ya Kenya ni almost jangwa), Mbuga za wanyama na misitu mingi, mito, maziwa, na kila aina ya madini. Lakini Kenya bado wametuzidi kiuchumi kwamba bajeti ya nchi inajitosheleza kwa asilimia mia moja, hakuna habari za topping up toka kwa mabeberu, so kwa mimi this is greatest achievement... hebu fikiria kama wangekuwa na resources kama zetu si wangekuwa mbali sana??
Sisi ni sawa na yule aliyepewa talanata halafu akazichimbia ili ku mrudishia mwenyewe badala ya kuzalisha. Huu ni mfano wa zaidi ya miaka 2000.. Je sis tunazitumia hizo talanta!!?
 
Elimu ya kuweza kujitegemea, kuvumbua visaidia maisha, ubunifu na uweledi mkubwa kwenye kuanzisha na kuendesha viwanda, makampuni, mashamba makubwa ili kutengeneza ajira. Siyo elimu ya kukariri na kufaulia mitihani... Elimu ambayo unaweza kwenda kufanya kazi popote duniani etc etc

embu niambie daktari wa tz akienda nchi gani anakosa sifa!!!vipi eng??

wote sisi tumetohoa elimu za kikoloni ambazo kimsingi haimjengi msomi katika kujikomboa,na ukitaka ujue wana ujinga zaidi wanatudharau kwa kutojua kiingereza,kwao majengo na madaraja yanaanguka.
 
Fafanua hizo namba
System mpya ipo Hivi Mkuu, lengo kuu ni kuondoa dhana kuwa tunasoma tupite mitihani bali sio watoto wetu kupata elimu.
Fafanua hizo namba
Infographic-illustration-of-the-competency-Based-Curriculum-CBC-in-Kenya-2.png


All students take 2 years of Pre-primary, then 6 years of Primary, and then 3 years of Junior School. If you pass the Grade 9 exams at 15 at the end of Junior School, you can then go on to take 3 years of Senior School. University under CBC will be just 3 years instead of 4..
cbc-vs-844.jpg
 
Tanzania ilipata Uhuru wake kwa porojo, ila Wakenya walipigana vita vya MAUMAU ambayo viliua wakenya wengi sana hasa wa kabla la wakikuyu. Kupata kwetu Uhuru kwa njia ya porojo ndipo kunakoliponza Taifa letu - dhana ya woga na kutojiamini ndiko kunaliangamiza taifa letu - killing softly... Porojo porojo tu ni kila pahala !!
 
Tanzania na Kenya zilipata uhuru mapema miaka ya 1960s. Leo zinakaribia miaka 60 tangu zipate uhuru.

Nchi hizi mbili ni kama makaka wawili waliozaliwa tumbo moja ila kila mmoja kachukuwa njia tafauti katika kutafuta maisha. Na kwa mtazamo wa haraka Tanzania imefeli vibaya sana katika miaka yote 60 wakati Kenya angarau anapigia hatuwa kwenda mbele japo kuwa kwa mwendo wa ponda.

Tanzania imeshindwa hata kuinuka bado inapiga usigizi wa mtoto mchanga. sasa swali la kujiuliza Tanzania tumekosea wapi na kenya wamepatia wapi? Swali hili nitalijibu simple sana kenya pamoja na makosa mengi lakini kwenye upande wa elimu walipatia kwa kiwango kikubwa.

Mkenya wa darasa la saba anaweza kumzidi marifa Mtanzania wa form six. Tanzania elimu yetu ni zero tangu enzi za Nyerere. Yaani elimu yetu sio ya kuelimisha bali ni ya kufaulu mitihani. Ndio maana tuna watu wenye PHD lakini matendo yao na fikira zao ni kama mtu ambaye hajaenda shule kabisa.

Kwa mfano ukiangalia PHD holders wa Tanzania wengi wanafanya kazi za kuteuliwa na watawala kama wa kuu wa mikowa au mawaziri. na ukiangalia performances zao ni ziro. Kwanini? Kwasababu wao kitu mhimu kwao ni cheo sio matokeo. Kwasababu tangu wakiwa mashuleni walifundishwa kufaulu mtihani mwisho wa muhula ndio mhim kuliko kuelewa.
Baada ya Uhuru Tanzania tulifuata ujamaa na kuelimisha wananchi wetu. Nyerere alitaka kila mtanzania awe kasoma ili tuweze kujitawala wenyewe baadaye na ndiyo maana tukawa na elimu ya watu wazima na Tanzania ndiyo iliyokuwa inaongoza Afrika kwa literacy ikifuatiwa na Misri. Nyerere alita wananchi wake wawe wanamiliki ardhi yao na wajitegemee. Kenya wao walibaki na sera za kibeberu, sehemu kubwa ya ardhi nchini kwao inamilikiwa na wazungu ama wahindi (mpaka leo) wakati wananchi hawana kitu. Someni historia ya nchi zetu mjuwe, msipende kuandika ujinga tu.
 
Shida ni Kiingereza, sidhani kama kuna kingine
Yaani sijapata kusoma majibu ya kijinga kama haya....Kiingereza ni lugha tu wala si kigezo cha maendeleo hii ni kasumba ya kijinga sana. Mkuu hujasoma hata kidogo maishani mwako?
 
Moi amekaa madarakani 22yrs (1978-2020)
Nyerere amekaa24yrs (1961-1985), na ccm 59yrs (1961-2020
Unajua Moi alikaa madarakani muda gani? Unajua Wakenya wangapi wanauliwa hadharani na kamera zinashuhudia? Acha ujuaji kijana, Kenya sio nchi ni genge kati kati ya nchi. BBC leo wametoa uchunguzi wao wa namna watoto wanauzwa Nairobi kwa shilingi laki 7. Tuwe na shukurani.
Moi amekaa madarakani 22yrs (1978-2020)
Nyerere amekaa24yrs (1961-1985), na ccm 59yrs (1961-2020)
Mambo mapungufu mabayakiasi ya Kenya tunaweza kuyajua vizuri. Maovu mabaya sana ya Tanzania sio rahisi sana kujulikana hasa na wasioelimika/wavivu wa kutafuta habari. Ni sababu kenya kuna uhuru wa habari, sisi vyombo vya habar vimewekwa mfuko.Mfano mdogo: mwanahabari anatoa habari kupitia chombo chake kuwa eneo fulani barabara imeharibika, anapata matatizo kibao eti unatakiwa utoe taarifa hizo srikalini, wewe sio mzalendo ni kibaraka wa mabeberu nk. Tz ili meanahabari uwe salama tangaza tu habari za kumsifu Magufuli na serikali. Tanzania usiku na mchana ni kujipa tu sifa za uongo. Ukisikiliza tbc utadhani tanzania imegeuka kuwa ulaya nyingine. Tunajenga hiki, tunajenga kile. Tunajenga hapa tunajenga pale. Tumenunua ndege tumenunua kile. Nchi nyingine wanafanya mengi zaidi huwezi sikikia makelele ya kujisifu.
 
Baada ya Uhuru Tanzania tulifuata ujamaa na kuelimisha wananchi wetu. Nyerere alitaka kila mtanzania awe kasoma ili tuweze kujitawala wenyewe baadaye na ndiyo maana tukawa na elimu ya watu wazima na Tanzania ndiyo iliyokuwa inaongoza Afrika kwa literacy ikifuatiwa na Misri. Nyerere alita wananchi wake wawe wanamiliki ardhi yao na wajitegemee. Kenya wao walibaki na sera za kibeberu, sehemu kubwa ya ardhi nchini kwao inamilikiwa na wazungu ama wahindi (mpaka leo) wakati wananchi hawana kitu. Someni historia ya nchi zetu mjuwe, msipende kuandika ujinga tu.
Unataka kutuaminisha waTz wameelimika kuliko wakenya? Unataka tuamini wakenya wamekosa ardhi ya kulima? Sio kweli. Kenya kuna matajiri wakubwa wanamiliki ardhi kihalali, wamewekeza miradi ya uzalishaji, wanaajiri na wanalipa kodi . Sisi ardhi kubwa imekaa tuu bure tunafaidika vipi? Naona kama wewe ndio mjinga hujajitambua.
 
Ok
Tanzania hatujakosea popote, kesi yetu ni sawa na China vs South Korea. Maendeleo ya china ni ya juhudi za Wachina bila msaada wa ushirikiano na nchi nyingine ila wa Korea ni vibaraka wa mmarekani.

Kenya ni changudoa wa Marekani, Marekani ikianguka hakutakua na nchi ya kenya. Wanategemea stability ya Marekani. Sisi tunavyokwenda hakuna cha kututeteresha.

Ukiona mafuta Kenya ni bei ndogo jua kuna mkono wa USA, hata hivyo kwa kuangalia kenya wangapi wanaweza kuafford kutumia hayo mafuta ya bei ndogo? Sisi tumejenga stable state.
 
Hii ni dhana ya kipumbavu sana, hata kwenye maisha binafsi ukitaka kufanikiwa kwa jirani yako aliyefanikiwa au rafiki au bosi wako don't start calling names na kujifanya ujuaji na kiburi cha kipuuzi. Tumia akili yako, uvumilivu na maarifa yote aliyokujaalia Mungu ili uweze kujifunza na wewe kujiimarisha ili hatimaye nawe ifanikiwe kama wao. Ndiyo maana wahenga walisema mtaka cha uvunguni sharti ainame, ukijifanya mbabe na kuinua kitanda chote itakula kwako mazima. This applies to country diplomacy as well na hapa nchini bingwa alikuwa the late Mahiga, huyu hakuwa na mpinzani....
dhana ya kipumbavu ni ulochoandika, the thing is : kenya is not a country in itself. It's a proxy of USA Africa, would you be proxy of a wealthy person just to rub shoulders with the VIP? that's the question Tanzania asked themselves and decided our dignity comes first. We are our own country, we fight our own wars, we choose who to support free willy. Kenya can only support who the USA is supporting.
 
Kosa tumejengwa kwenye msingi wa kuongozwa na viongozi miyungu watu, hawahojiwi hawaambiliki,wanakuwa watakatifu kipindi cha uchaguzi wakijipitisha kwa njia za haramu wanakuwa juu ya waajiri wao ambao ni wananchi kwa kuwacharaza mijeledi.
 
Mkuu kama unasema kuwa Kenya siyo foreigners tu ndiyo wana maisha mazuri basi huijui Kenya. Swala la Kibira kuwa ni Kibra hilo silifahamu so yaweza kuwa kweli au si kweli, unajua watu kama waalimu, manesi, drivers and the like kwa Kenya wanaishi wapi? Anyway sipendi kuzungumzia sana hiyo nchi kwani hainihusu lakini ntakuja kuleta story ya niliyoyaona Kibira(wewe waita kibra).
Na pia ulete stori ya watu wanaoishi vijijini Tanzania. Chukua Kijiji kimoja tu, tena nakuruhusu uchague kile kinachoonekana ni kielelezo cha ustawi, halafu ulinganishe na Kibra, tuone!
 
Back
Top Bottom