sikumbuki kama kunasehemu nimeandika per capita inapimwa kwa namna hiyo kenya peke yake.halafu sina jazba labda wewe ndugu yangu ndio sababu hata kuruka mistari unaona utachelewa.
siasa hizi hizi tutaenda nazo,maana lengo ni kuboresha maisha ya mtazania mmoja mmoja,sio kukuza GDP ambayo haiakisi maisha ya watu.
sijui kama nawewe ni mkenya au ni mtz,ila nikupe taarifa mbaya,deni la kenya limefikia 70% ya pato la taifa,na itakwenda kuwa kubwa zaidi mpaka rais aliyepo atkapoachia nchi.
nimekubali tokea awali,kenya wanatuzidi baadhi ya mambo,hii habari ya kusema wametuzidi mbaali ndio inanisukuma nikuulize wanatuzidi namna gani!!!
Sasa hapo umefanya la maana, kuuliza:
1- Wanatuzidi 'quality' elimu. Hii ni elimu bora, si bora elimu
2- Wanatuzidi ukubwa wa uchumi
3- Wanatuzidi uhuru na haki za raia
4- Wanatuzidi pato la mtu binafsi
5- Wanatuzidi kwa uenevu wa mtandao wa internet (Yaani watu wengi wana broadband internet nyumbani). Watanzania wengi internet wanaiona kwenye simu tu (hii ina maana kubwa kwa wanaojua maana!)
6- Wanatuzidi kwa 'quality of life' (kama wajua)
7- Katika Nyanja nyingine nyingi pia: stock market, exchange rate, mipango miji, barabara (ya 7 Afrika, Tanzania hata haimo katika 10 bora!) Kuna Library nyingi zaidi mjini Mombasa tu kuliko hata Tanzania nzima;
Lakini pengine twawazidi kwa baa nyingi, bendi nyingi za muziki naa….ndiyo, pengine Tanzania mtu aweza kukaa tu bila kufanya kazi na akapata hela na kula (kama alivyosema mmoja!).
Hii siyo kuiweka chini nchi yangu Tanzania, ila nasema tunayobidi tuige. Na kwa kweli, baadhi ya maendeleo ya Kenya ni kwa sababu za Kihistoria. Pia, Tanzania tuna mustkbali mzuri Zaidi (kama…) kuliko Kenya. Kikubwa Zaidi ninachokichukia ni watu kudanganywa-danganywa. Ukweli hapa Tanzania wanao tu wale wanaoweza kufuatilia vyombo vya nje tu au kusafiri. Juu ya deni la Kenya kuwa 70% ya GDP hiyo siyo neon ndungu. Deni la Japan ni 120% GDP na Marekani?
La muhimu ni vibrancy ya uchumi wako kuweza kurudisha. Mo anaweza kukopeshwa bilioni mbili za dola hivi sasa akitaka! Jee, utasema ana madeni Zaidi kuliko wewe uliekopa sh. laki tano?
Kwanza hao wanaokopesha wasingemkopesha hivyo kama hawajui wataweza kurudisha. Deni ni hatari Zaidi kwa Tanzania hivi sasa kuliko Kenya!