Tanzania tulikosea wapi na Kenya walipatia wapi?

Tanzania tulikosea wapi na Kenya walipatia wapi?

Unajua wale wajinga darasani huwaga na tabia moja ya kumbeza mwenye akili au anayewaongoza darasani .. Usiwe mmoja wa hao wanaouliza nani alimpa degree

sasa mfano wako una uhusiano gani!!!

nakuelekeza,elimu haihusiani na akili za mtu,labda kama hujui akili ni nini. zilikuwako kwao binaadamu kabla elimu za kidishwa darasani hazijaanza kutolewa mpaka kufikia hatua ya kupewa vyeti.

kwahiyo kupata elimu sio kupata akili.
 
kenya ni wapi mpaka unamuuliza swali la ajabu hivyo mtu.

huu ushamba nao!!!
Mkuu kama Kenya hujawahi fika unaezaje itolea sifa ambazo huzijui. Tembea uwone mkuu ndio utajua huku tanzania bado tunapoteza muda mwingi kukimbizana na wapinzani wakat masuala ya maendeleo yanatusubiri
 
Inabidi pia ueleze watu Kenya anapatia kwenye nini.

Kenya inaongoza kwa tatizo la ajira ukanda huu
Kenya inaongoza kwa rushwa mbaya ukanda huu
Kenya ina raia wenye maisha duni zaidi ukanda huu
Kenya gharama za maisha ziko juu zaidi, mbali ya kwamba wana uchumi mkubwa wakiwa wachache zaidi yetu
Kenya ina siasa chafu, sisi zina kasoro moja ndogo tu
Ukabila na ukosefu wa umoja wa kitaifa ni tatizo sugu Kenya

Kwa kukutaarifu tu, wana mabaya mengi zaidi kuliko mazuri machache waliyotuzidi, ambayo hata hivyo yanakwenda yakibadirishwa kuwazidi siku si nyingi.

Msiishi kwa stori za mitandaoni, tembeeni.
Kumbuka kwamba kwa utajiri tulionao TZ kuanzia ardhi nzuri ya kilimo na ufugaji (nusu ya ardhi ya Kenya ni almost jangwa), Mbuga za wanyama na misitu mingi, mito, maziwa, na kila aina ya madini. Lakini Kenya bado wametuzidi kiuchumi kwamba bajeti ya nchi inajitosheleza kwa asilimia mia moja, hakuna habari za topping up toka kwa mabeberu, so kwa mimi this is greatest achievement... hebu fikiria kama wangekuwa na resources kama zetu si wangekuwa mbali sana??
 
sasa mfano wako una uhusiano gani!!!

nakuelekeza,elimu haihusiani na akili za mtu,labda kama hujui akili ni nini. zilikuwako kwao binaadamu kabla elimu za kidishwa darasani hazijaanza kutolewa mpaka kufikia hatua ya kupewa vyeti.

kwahiyo kupata elimu sio kupata akili.
Inaelekea una akili
 
Tanzania tuna wapenda madaraka CCM na sio wapenda maendeleo ni kuangalia matumbo yao tu

Wako tayari kuua kwa yeyote anayetaka kuhatarisha kula yao na sio maendeleo ya watanzania.

CCM watakapoondoka madarakani kwa njia yeyote ndipo Tanzania tutapata mafanikio makubwa kuwahi kutokea.

Tuondoe nidhamu ya woga CCM haitufai pamoja na washirika wake wote.
Umejibu nje ya mada,Hama basi na upinzani kushika nchi labda maji yapande mlima
 
Kumbuka kwamba kwa utajiri tulionao TZ kuanzia ardhi nzuri ya kilimo na ufugaji (nusu ya ardhi ya Kenya ni almost jangwa), Mbuga za wanyama na misitu mingi, mito, maziwa, na kila aina ya madini. Lakini Kenya bado wametuzidi kiuchumi kwamba bajeti ya nchi inajitosheleza kwa asilimia mia moja, hakuna habari za topping up toka kwa mabeberu, so kwa mimi this is greatest achievement... hebu fikiria kama wangekuwa na resources kama zetu si wangekuwa mbali sana??

bajeti ya kenya inajitoshereza!!!!!!...........ah wewe jamaa kweli huijui kenya.

ndio maana tunapomuona magufuli anahangaika tunamuunganisha kwenye sala zetu kila tusalipo.

kiukweli kabisa tanzania ikiwa serious namna hii miaka 10 ijayo hali itakuwa tofauti kabisa.
 
Tanzania hatujakosea popote, kesi yetu ni sawa na China vs South Korea. Maendeleo ya china ni ya juhudi za Wachina bila msaada wa ushirikiano na nchi nyingine ila wa Korea ni vibaraka wa mmarekani.

Kenya ni changudoa wa Marekani, Marekani ikianguka hakutakua na nchi ya kenya. Wanategemea stability ya Marekani. Sisi tunavyokwenda hakuna cha kututeteresha.

Ukiona mafuta Kenya ni bei ndogo jua kuna mkono wa USA, hata hivyo kwa kuangalia kenya wangapi wanaweza kuafford kutumia hayo mafuta ya bei ndogo? Sisi tumejenga stable state.
Hii ni dhana ya kipumbavu sana, hata kwenye maisha binafsi ukitaka kufanikiwa kwa jirani yako aliyefanikiwa au rafiki au bosi wako don't start calling names na kujifanya ujuaji na kiburi cha kipuuzi. Tumia akili yako, uvumilivu na maarifa yote aliyokujaalia Mungu ili uweze kujifunza na wewe kujiimarisha ili hatimaye nawe ifanikiwe kama wao. Ndiyo maana wahenga walisema mtaka cha uvunguni sharti ainame, ukijifanya mbabe na kuinua kitanda chote itakula kwako mazima. This applies to country diplomacy as well na hapa nchini bingwa alikuwa the late Mahiga, huyu hakuwa na mpinzani....
 
Tanzania na Kenya zilipata uhuru mapema miaka ya 1960s. Leo zinakaribia miaka 60 tangu zipate uhuru.

Nchi hizi mbili ni kama makaka wawili waliozaliwa tumbo moja ila kila mmoja kachukuwa njia tafauti katika kutafuta maisha. Na kwa mtazamo wa haraka Tanzania imefeli vibaya sana katika miaka yote 60 wakati Kenya angarau anapigia hatuwa kwenda mbele japo kuwa kwa mwendo wa ponda.

Tanzania imeshindwa hata kuinuka bado inapiga usigizi wa mtoto mchanga. sasa swali la kujiuliza Tanzania tumekosea wapi na kenya wamepatia wapi? Swali hili nitalijibu simple sana kenya pamoja na makosa mengi lakini kwenye upande wa elimu walipatia kwa kiwango kikubwa.

Mkenya wa darasa la saba anaweza kumzidi marifa Mtanzania wa form six. Tanzania elimu yetu ni zero tangu enzi za Nyerere. Yaani elimu yetu sio ya kuelimisha bali ni ya kufaulu mitihani. Ndio maana tuna watu wenye PHD lakini matendo yao na fikira zao ni kama mtu ambaye hajaenda shule kabisa.

Kwa mfano ukiangalia PHD holders wa Tanzania wengi wanafanya kazi za kuteuliwa na watawala kama wa kuu wa mikowa au mawaziri. na ukiangalia performances zao ni ziro. Kwanini? Kwasababu wao kitu mhimu kwao ni cheo sio matokeo. Kwasababu tangu wakiwa mashuleni walifundishwa kufaulu mtihani mwisho wa muhula ndio mhim kuliko kuelewa.
Wakuu wa "Mikowa"?????
 
Hii ni dhana ya kipumbavu sana, hata kwenye maisha binafsi ukitaka kufanikiwa kwa jirani yako aliyefanikiwa au rafiki au bosi wako don't start calling names na kujifanya ujuaji na kiburi cha kipuuzi. Tumia akili yako, uvumilivu na maarifa yote aliyokujaalia Mungu ili uweze kujifunza na wewe kujiimarisha ili hatimaye nawe ifanikiwe kama wao. Ndiyo maana wahenga walisema mtaka cha uvunguni sharti ainame, ukijifanya mbabe na kuinua kitanda chote itakula kwako mazima. This applies to country diplomacy as well na hapa nchini bingwa alikuwa the late Mahiga, huyu hakuwa na mpinzani....

mkuu diplomacy ipi unazungumzia!!!

kuna kitu kinaitwa diplomacy kwa picha ya nje na jumla jumla,ila nyuma yake kuna kitu kinaitwa sabotage,ukikaa kizembe unapigwa kwa mgongo wa diplomacy.

diplomacy ikikaa kama yenyewe ina rangi na harufu nzuri sana ya undugu na ubinaadamu,ikiishahusisha hicho kitu nilichotaja,huwa haifai tena kutizamwa.
 
Wakenya wanajitambua sana, likija suala la kupigania haki zao wako tayari kupoteza hata uhai wao ili wapate wanachotaka, ila kwetu sisi ni tofauti, tunataka tukae nyumbani tuletewe mabadiliko na wengine, hapo ndipo tunapofeli.

Katiba ndio msingi wa maendeleo, wakenya waliipigania Katiba yao ya sasa mpaka wengine kupoteza uhai wao, atleast leo wanafurahia matunda ya demokrasia.

Ukisema sababu ya elimu nayo naitilia shaka, mbona elimu yetu inaonekana ni bora zaidi ya Uganda lakini waganda nawaona wakipigania haki zao kwa vitendo, sio wanaume tu hata wanawake wote wanaingia barabarani kumtaka mtu wao aachiwe na polisi, sisi hatuwezi, watanzania tumezubaa sana.
Mkuuu tutake radhi yaani tumezubaa??
 
Inabidi pia ueleze watu Kenya anapatia kwenye nini.

Kenya inaongoza kwa tatizo la ajira ukanda huu
Kenya inaongoza kwa rushwa mbaya ukanda huu
Kenya ina raia wenye maisha duni zaidi ukanda huu
Kenya gharama za maisha ziko juu zaidi, mbali ya kwamba wana uchumi mkubwa wakiwa wachache zaidi yetu
Kenya ina siasa chafu, sisi zina kasoro moja ndogo tu
Ukabila na ukosefu wa umoja wa kitaifa ni tatizo sugu Kenya

Kwa kukutaarifu tu, wana mabaya mengi zaidi kuliko mazuri machache waliyotuzidi, ambayo hata hivyo yanakwenda yakibadirishwa kuwazidi siku si nyingi.

Msiishi kwa stori za mitandaoni, tembeeni.
Acha uongo mkuu, nimekaa Kenya almost 6 years, labda useme wazawa wenyenacho ni wachache sema wanakuwanacho kingi na swala la ardhi kule ni utata sana. Foreigners ndiyo wana maisha mazuri Kenya. Ila elimu yao iko vizuri sana. Kuna sehemu very famous inaitwa Kibila, siku nikipata nafasi ntakuja kuandika niliyoyaona Kibila.
 
Kenya Uhuru waliupigania toka kwa wazungu Tanzania tulipewa,Kenya haki wanaitafuta Tanzania tunasubiri kupewa.utaskia profesa anasema mheshimiwa Raisi umenitoa jararani asante sana
 
Uongo Wakenya wengi hawana ardhi
Sasa inakuwaje wana uwezo wa bajeti yao kujiendesha yenyewe bila misaada ya mabeberu? Yaani kama bajeti ni Trilioni 20 basi unakuta yote wameikusanya na wanayo mkononi, sisi hata asilimia 80 ya bajeti bado, why?
 
Acha uongo mkuu, nimekaa Kenya almost 6 years, labda useme wazawa wenyenacho ni wachache sema wanakuwanacho kingi na swala la ardhi kule ni utata sana. Foreigners ndiyo wana maisha mazuri Kenya. Ila elimu yao iko vizuri sana. Kuna sehemu very famous inaitwa Kibila, siku nikipata nafasi ntakuja kuandika niliyoyaona Kibila.

mkuu sasa umekanusha nini kwenye bandiko langu!!!

sijataja elimu kwenye bandiko langu,maana nakubali ina ahueni ukilinganisha na yetu ya masomo 12 kwa mtoto wenye ndoto ya kuwa mfamasia.
 
Sasa inakuwaje wana uwezo wa bajeti yao kujiendesha yenyewe bila misaada ya mabeberu? Yaani kama bajeti ni Trilioni 20 basi unakuta yote wameikusanya na wanayo mkononi, sisi hata asilimia 80 ya bajeti bado, why?

mkuu nchi gani unayoizungumzia hapa???
 
Hamia Kenya boss, kama hujafa kwa njaa sijui
 
Back
Top Bottom