Intelligence Justice
JF-Expert Member
- Oct 23, 2020
- 3,840
- 4,396
Mkuu,Kuna sababu nyingi zilizoleta tofauti kubwa katika nyanza nyingi kati ya Tanzania na Kenya iliyopata Uhuru miaka miwili baada ya sisi. Sababu kubwa kabisa ni elimu iliyoharibiwa toka Awamu ya Kwanza muda mfupi tu baada ya Uhuru katika juhudi ya kuleta elimu nzuri ya Kitanganyika tofauti na ile ya Kikoloni. Elimu hiyo mpya ilikuwa na makosa mengi yaliyoadhiri ubora lakini kosa kubwa kabisa ilikuwa kuondoa kabisa Darasa la Nane ambalo lilikuwa la mwisho Shule za Msingi. Hii ikawa sawa na kubomoa msingi wa nyumba ukaendelea kujenga nyumba ukitegemea itakuwa imara ya kudumu. Kenya nao waliiga mtindo huo lakini waligundua kosa hilo mapema na kurekabisha miaka michache tu baadaye na kurudisha Darasa la Nane hadi leo badala yake waliondoa kabisa Form Six. Wakenya wakaja na mfumo wa 8-4-4 ikiwa na maana ya miaka 8 Msingi, miaka 4 Sekondari na miaka 4 Chuo Kikuu digrii ya kwanza. Hii ina maana Form Five ilihamishiwa Chuo Kikuu kumuandaa mwanafunzi kuingia Chuoni. Huu ndo mfumo uliokuwapo Chuo Kikuu cha Makerere kabla ya Uhuru wa nchi zote tatu za Afrika Mashariki. Zambia wao walifutilia mbali Form Five na Six wakabaki na Form Four tu na wanafunzi wao wanapokelewa vyuo vyote duniani wa kwetu wa Form Six wakikataliwa. Bahati mbaya sana toka Awamu ya Kwanza kila Waziri anayeteuliwa kuongoza Wizara ya Elimu alikuja na mbinu zake za kuboresha elimu lakini amekuwa akimaliza kwa kuharibu zaidi. Matokeo yake sasa hivi kila kiongozi Serikalini, Bungeni na Mahakamani ana PhD ambayo haijulikani ni ya Chuo gani wala fani gani ikileta hisia tofautitofauti juu ya elimu ya viongozi wetu.
Umeeleza uzuri kwa hiyo ni muda muafaka sasa wenye dhamana na mamlaka ya unongozi wa nchi wawasikilize wadau namna bora ya kuboresha utoaji elimu yenye tija kwa vija ili malalamiko ya kukosa ajira yapungue kwa kuwezeshwa kuwa na maarifa yanayomwongoza mtu kupambana na changamoto za kimaisha.
Mfano, vyuo vya ufundi vya enzi hizo kama Dar Tech, Arusha, Moshi Tech nk walikuwa na ujuzu wa hali ya juu sana kuliko sasa pampja na kwamba vyuo hivyo vimepandishwa hadhi kutoa mafunzo ya shahada!!!
Mwarobaini ni kutoa mafunzo bunifu na milikishi kwenye ubungo ambayo mhitimu wa ngazi yoyote aweze kuanzisha shughuli za kiuchumi kwa kuzingatia mahitaji ya soko la ndani na nje yaliyoboreshwa kwa teknolojia ya kisasa. Serikali itoe mikopo yenye riba ya asilimia 6% kwa shughuli za ufundi, biashara, kilimo, mazao ya maliasili kwa mjibu wa sheria. Matumizi ya lugha fasaha ya Kiswahili, Kiingereza, Kichina, Kifaransa nk. Kujenga uelewa mpana na kujiamini kutokana na ufahamu wa kinadhaniria unapohamishiwa kitafsiri kwa vitendo kwa matokeo chanya. Kuajiri walimu waliofaulu vizuri sekondari na chuo badala ya hao wa madaraja ya tatu na nne-haifai. Wahadhiri wa chuo kikuu ni sharti utaratibu wa zamani urejeshwe kwa ni lazima awe amepata daraja bora la kwanza badala ya sasa hadi daraja la pili wanachukuliwa. Serikali itoe elimu bila malipo ya ada na michango yenye usumbufu kwa wazazi kuanzia kidato cha kwanza hadi cha sita. Wanafunzi wote wanaofaulu na kuchaguliwa kujiunga vyuo vikuu katika fani yoyote waoewe mkopo kwa mrejesho wa riba ndogo baada ya kufuzu, kuajiriwa au kujiari kwa kipato cha kueleweka nk.

