Tanzania sio Burkina Faso

Tanzania sio Burkina Faso

Tanzania hakuna ukabila wala udini...? Kwahiyo ule wa CHADEMA na CUF mara vyama vya Kikiristo au kiilamu, ukabila mara hoo ukanda kumbe unathibitisha huwa mnapiga mayowe ya kimapepo tu....?

Halafu unaposema jeshi letu linanidhamu. Umeshawahi kufikiria hili: Inajulikana wazi kuwa wakuu wa mikoa na wilaya ni makada wa Chama Tawala. Sasa twende ...hapa: wanateuliwa na mwenyekiti wa CCM kwa kutumia mwamvuli wa Urais.
wengi ni maafisa wastaafu wa majeshi.

Sasa swali hawa makuu wa mikoa na wilaya hata wenye vyeo vingine vinavyotokana na ukada wa chama Walianza lini uanachama huo hata wakaaminiwa kuwa wanatosha kushika nyadhifa za kikada kama za ukuu wa mikoa na wilaya?

Obviously walikuwa wanachama na walijipambanua vilivyo tangu wakiwa watumishi wa vyombo hivyo vya dola. How? Wote tunashuhudia vyombo vyetu vya dola jinsi vinavyorumiwa kisiasa kulinda maslahi ya chama tawala na kukandamiza upinzani

So si nidhamu hiyo maslahi

hapa mungu ametumia kinywa chako kusema
 
Nadhani kama mwanzisha thread angesema raia wa Tanzania ni woga kama kunguru ningemfahamu haraka kuliko hizo hoja zilizotolewa.

Hio ya woga ni fact kabisa, Nyerere alifanikiwa kukaa madarakani kwa miaka nenda miaka rudi akihubiri ujamaa huku watu wakila sembe la njano.Raia walifanya nini walikaa kimya - kama wamemwagiwa maji!

Na hicho ndio kinachoendelea kutokea.Kama Tanzania ingekuwa Bukina Faso au nchi yoyote ya kule West Afrika - Basi hata BMK lisingemaliza kwa salama na amani.Siku ile 2/3 inachakachuliwa tayari kingekuwa kishawaka.

Huo ni utamaduni wa raia, kwa mfano huwezi fananisha raia wa ufaransa na uholanzi.Raia wa ufaransa ukmzidishia centi moja au mbili kwenye mkate - nchi yote haikaliki raia wako barabarani hadi kieleweke.

Wakati uholanzi wanaweza kuzisha hata x2 ya bei iliopo - wala kusitokee chochote.Huo ni mfano wa tofauti ya kitabia za raia.

Kwa hio haishangazi yanayotokea TZ tena naweza sema pengine ni Tanganyika zaidi.Maana kule Zanzibar ni wazi jeshi ni wengi kuliko sehemu yoyote ile duniani!Probably kila raia mmoja anaweza lindwa na wanasheji 5 !!!

Edit:
Nimesahau pengine Zanzibar unaweza linganisha na Palestine.
 
UKAWA wengi wamekuwa wakilinganisha mambo ya kisiasa ya Burkina Faso na Tanzania.Niwasaidie tu

1.Burkina faso KUNA UKABILA NA UDINI wakati Tanzania hakuna.

2.Rais aliyeondoka madarakani hakuingia kidemokrasia aliua mwenzie tena rafiki yake mkubwa (THOMAS sankara) kwa mapinduzi ya Kijeshi .Tanzania Rais alichaguliwa kwa kura kidemokrasia.

3.Burkina FASO jeshi halina nidhamu na ni moja ya majeshi yasiyo na nidhamu Afrika likishika nafasi ya pili Africa kwa ukosefu wa nidhamu baada ya yale ya Jamhuri ya kidemokrasia ya Kongo yakifuatiwa na majeshi ya nchi zinazoongea kifaransa Afrika na yale ya nchi za Kaskazini mwa Afrika kule kulikotokea Arab SPRINGS.Tanzania ni jeshi lenye nidhamu ya hali ya juu mno Afrika na highly organized.

4.Majeshi ya BURKINA FASO hayana nguvu za kudhibiti waandamanaji au waasi maruhuni. Tanzania POLISI TU wanatosha hamna haja ya kuita jeshi kushughulikia waandamanaji maruhuni.Uwezo wa polisi na jeshi pia hupimwa kwa uwezo wake wa kudhibiti organized crimes kupitia CIVIL STRIFES zinazoweza fanywa na raia wahuni waliojipanga kuharibu utengamano katika nchi kwa sababu zozote.

5.Raia wengi wa Burkina FASO NI WAHUNI WASIOPENDA kutii sheria.Ni kama wafuasi wa CHADEMA.Tanzania ni tofauti raia wengi ni watii wa sheria bila shuruti.

Kifupi BURKINA FASO na TANZANIA ni nchi tofauti,zenye majina tofauti,watu tofauti na siasa tofauti.Kulinganisha nchi hizi mbili si sahihi.

Katika yale maandamano kuna police na jeshi humo humo,hivyo hapa tz siku watu wakichoka utaona police kavua gwanda nae ka join na raia wenzake,Ndugu zake.
 
Katika yale maandamano kuna police na jeshi humo humo,hivyo hapa tz siku watu wakichoka utaona police kavua gwanda nae ka join na raia wenzake,Ndugu zake.

Mungu akulinde sana mkuu .
 
Tanzania hakuna ukabila wala udini...? Kwahiyo ule wa CHADEMA na CUF mara vyama vya Kikiristo au kiilamu, ukabila mara hoo ukanda kumbe unathibitisha huwa mnapiga mayowe ya kimapepo tu....?

Halafu unaposema jeshi letu linanidhamu. Umeshawahi kufikiria hili: Inajulikana wazi kuwa wakuu wa mikoa na wilaya ni makada wa Chama Tawala. Sasa twende ...hapa: wanateuliwa na mwenyekiti wa CCM kwa kutumia mwamvuli wa Urais.
wengi ni maafisa wastaafu wa majeshi.

Sasa swali hawa makuu wa mikoa na wilaya hata wenye vyeo vingine vinavyotokana na ukada wa chama Walianza lini uanachama huo hata wakaaminiwa kuwa wanatosha kushika nyadhifa za kikada kama za ukuu wa mikoa na wilaya?

Obviously walikuwa wanachama na walijipambanua vilivyo tangu wakiwa watumishi wa vyombo hivyo vya dola. How? Wote tunashuhudia vyombo vyetu vya dola jinsi vinavyorumiwa kisiasa kulinda maslahi ya chama tawala na kukandamiza upinzani

So si nidhamu hiyo maslahi
Kuna askari polisi mmoja nilimsikia akilalamika sana lakini chini chini kuwa jamaa mmoja amekuja na kuwakuta lakini amepanda ghafla na sasa ana cheo kikubwa kwenye jeshi ambapo wao wanatakiwa kumlinda. Analalamika kuwa pamoja na kupanda haraka utendaji wake haukuwa mzuri kufikia kushika hicho cheo. Kisa, yuko kweye mtandao.
Sasa kama unafuatilia Burkinafaso siku ya kwanza polisi waliweza kuwazuia waandamanaji, siku ya pili waandamanaji wakawa na nguvu hivyo ikabidi jeshi liungane na polisi kuwazuia.
Siku ya tatu baadhi ya wanajeshi na polisi wakaungana na waandamanaji!
Kilichotokea jana wote tunakijua.

 
Alyekuambia UKAWA wanafanya ulinganifu, kuweweseka ni kubaya sana.
 
Unapozungumzia Nidhamu ya jeshi unamaanisha nn? Hv jeshi letu la Tanzania bila kuweka ndugu za watawala kuliongoza ingekuwaje?

Jeshi letu lina nidhamu ya woga maana wengi wa wakuu wa vikosi ni ndugu wa vigogo kwamaana wanajitengenezea mazingira mazr ya ulaj ili baadae museme tuna jeshi na tuna tutawapiga…!!! Museme wapigwe tu kwa faida zenu binafsi…!!! Jesh la Tanzania kwa upande wa mwingine linatumika vibaya na ndio maana yule mkuu wa majeshi mstaafu aliwai kisema katika uchaguz furan kuwa "hatuwez kuwaachia wahuni waongoze nchi" akimaanisha kuwa chama hawawezi kuruhusu chama pinzani kiongoze nchi (dola) apo unaweza anza pata picha ya jeshi la Tz, bila undugu tunaofanya hakuna kitu alafu usseme jesh la BF halina uwezo wa kudhibiti maandamano, nguvu ya umma inatisha mkuuu…………


Wangeua wangapi?
 

Attachments

  • 1414839796412.jpg
    1414839796412.jpg
    40.7 KB · Views: 101
Mkuu hata usipoteze muda , kama mtu unaijua Tanzania vizuri upande wa usalama na jeshi huwezi hata siku moja kuwaza yanayotokea huko yatatokea Tanzania katika hili ni lazima tumshukuru Mungu Amani jamani ni kitu kingine kabisa
 
Endelea kujazia maiti damu na kujipa moyo JK mwenyewe ameshakiri akiwa china ameshachoka sasa subiri muda ufike yaliyotokea burkinafaso yanaweza kutokea tanzania wanajeshi na polisi hawaweza kuzuia nguvu ya umma
 
Ulivyoweka tu uhuni na CHADEMA ndipo uliponichefua, kumbe umeiandika kishabiki story yako!!??? Nilianza kukuelewa ulipokuwa unatoa tofauti za siasa za Burkina Faso na Tanzania. Ila kwa kuweka ushabiki tu nimeipuuza story yako na pengine Tz na Burkina Faso huenda zikawa zinafanana katika mambo mengi tu sema umeandika kwa kuogopa yasije kutokea nchini OVER!!
 
Nawapongeza wananchi na muungano wa Upinzani nchini Burkinafaso kwa Maandamano makubwa yalimuondoa mamlakani Dikteta Blaise Compaore.

Zaidi nalipongeza Jeshi la Wananchi wa Bukina Faso kwa kusimama na Wananchi.

Eti walitaka wabadili katiba bungeni kw wingi wao kisha washeherekee kwa ngoma na kukata viuno kama wale wa CCM walivyofanya kule Dodoma baada ya kupindua maoni ya wananchi

Jeshi la Burkina Faso Ni Jeshi la Wananchi kweli kweli.Hili ndio jeshi jasiri linalojitambua.

I wonder the kind of stuff our African Leaders are made of.

This is the same man who came into power almost three decades ago but still wants to cling onto it to the grave,Chai! !.

Africa must have a fundamental issue.

When few leaders turn the public offices as their birthrights,and when the poverty level of their governed majority become unbearable ,Revolution is inevitable.

Tanzanian government and the ruling party should take note.

Get prepared.

Mwenzako akinyolewa zako tia maji. Hii ndio dawa ya Marais wasaliti kwa wananchi wao na kudhani kuwa urafiki wao na Marekani au Ufaransa utawasaidia pale wananchi wanapoamua.

Wananchi wa Burkina Faso walimua kupambana barabarani na Dikteta aliyekaa madarakani kwa zaidi ya miaka 27 sasa na anabadili katiba ya nchi ili agombee tena Urais kwa kupeleka mswada Bungeni kwa matarajio kuwa wingi wao Bungeni ungetosha kupitisha lolote.Alitaka agombee kwa awamu ya Tano.Wananchi walizingira Dodoma yao na kuchoma moto jengo la Bunge na maandamano makubwa huku baadhi ya askari wakiwafyatulia Risasi.

Rais Blaise Compaore ambaye yupo katika list yangu ya wasaliti wakubwa wa Africa amevuna alichopanda.

Mwaka 1987 alimpindua rafiki yake wa Tangu Utotoni Thomas Sankara na kumuua kikatili. Thomas Sankara ambaye ninamuhusudu kama mwanamapinduzi halisi wa Africa,Adui wa Ubeberu na muumini mwenye msimamo mkali wa Mrengo wa Kushoto alianza kwa kasi kuijenga Burkina Faso akawa tishio kwa mataifa ya Magharibi kabla hajapinduliwa na kuuawa na huyu Kibaraka wa Magharibi. Malipo ni hapa hapa Duniani . Burkina Faso wameamua.

Blaise Compaore aliyekua mtu wa Kujipendekeza Ufaransa na Marekani na kujifanya kuwa msuluhishi wa migogoro kwenye Ukanda wa ECOWAS leo Marekani na Ufaransa wanatangaza kusimama na wananchi wa Burkina Faso.

Burkina Faso ni ya 4 kwa uzalishaji wa Dhahabu Baada ya Afrika Kusini,Ghana na Tanzania lakini takribani nusu ya Raia wake wanaishi chini ya Dola moja kwa siku huku chama tawala na viongozi wakijilimbikizia mali na kushirikiana na makampuni na serikali za nje kusaini mikataba ya siri na kusifiwa mara kadhaa na Marekani na Ufaransa kama taifa la kuigwa kidemokrasia na utawala bora.Tanzania haina tofauti

Ndio ninasema Utawala wetu hauna tofauti na utawala wa Burkina Faso na pia aina ya viongozi wetu hawana tofauti.

Natazamia hali iliyoanza kujitokeza ya kugombania madaraka kati ya Mkuu wa Majeshi Jenerali Traore na Luteni Kanali Isaac Zida itapatiwa ufumbuzi wa haraka kupitia timu ya dharura iliyoundwa na kamisheni ya Umoja wa Afrika, ECOWAS na UN .Serikali ya mpito irejeshe utawala wa kikatiba na kuondoa hali ya hatari(Emergency State) iliyotangazwa tangu juzi.

Tangu vuguvugu la mapinduzi ya uarabuni lilipoanza kumetokea mapinduzi na majaribio 6 ya kupindua Serikali za Afrika.

Narudia tena,Mwenzako akinyolewa basi zako tia maji.

Vijana wa Tanzania tuna mengi ya kujifunza kutoka Burkina Faso.

Tena nalipongeza Jeshi la Burkina Faso kusimama na wananchi.

Mwisho natoa wito kwa serikali ya Tanzania kupitia waziri wa Mambo ya Nje Bernard Membe itoe Msimamo wake kuhusu kutambua Mapinduzi ya Serikali ya Burkina Faso,isimame na kaka na dada zetu wa Burkinabe na pia ifanye jitihada za kuokoa watanzania ambao kwa namna moja au nyingine wako stranded kwenye machafuko Nchini Burkina Faso.

Pumzika kwa Amani Mwana wa Africa Thomas Sankara(Che Guevara wetu tuliyenyang'wanywa na Wasaliti wa Afrika), Mungu Ibariki Afrika ! We Shall Rise Again !

Aluta Continua,Victory Ascerta....

Ben Saanane
 
Magamba naona POVU zimeshaanza kumwagika asante CHADEMA kwakuleta SIASA za kweli manake watawala wanaweweseka sana wakikumbuka dhurma wanawafanyia watanganyika Vinginevyo mtu alieanzisha hii thread cjui kutakuwa na Lugha gani nzuri yakusema zaidi ya WOGA wa kung"olewa,,,! Tutaheshimiana tu
Ningekuwa na TIME ACCELERATING MACHINE, ningeupeleka muda mbele kwa kasi ili 2015 muone tunavyouzika upinzani hususan CDM. nina hofu huenda wengine hamtafika mwakani. Tuna plan za miaka 50 ijayo kwa ajili ya taifa letu na katika plan hizo Chadema haipo.
We are born to lead and you are born to follow
 
Tofautisha kuweko ukabila na udini katika nchi na katika vyama.Tanzania kama nchi udini na ukabila haupo.

Lakini vyama viko vyenye udini na ukabila.CHADEMA kabila dominant katika chama ni Wachaga na kidini ni cha wakristo tena waprotestant hasa walutheri na walokole wakati CUF kabila dominant lililojaa ni Wapemba na kidini ni waislamu wa itikadi kali.

Sasa unaposema Tanzania hakuna udini wala ukabila tukuelewe vp mbona unatuchanganya
 
La kujua binaadamu.wote wanafanana. Hua ni watiifu na waoga lkn maonevu yakizidi kidogo kidogo hugain courage. Na hapo ndipo utamjua.

Tena ogopa watu wapole na wajinga kama.watanzania wakichoka kupumbaa kinachofuata mziki wake kuliko wa huko wa bukinafaso
 
Yakhe, wasema Tanzania hakuna udini? nenda unguja kauze nyama ya nguruwe (Astaghfirullah), wakati wa mwezi mtukufu kama hutachakaa kwa viboko au kukatwa kichwa kabisa!
 
UKAWA wengi wamekuwa wakilinganisha mambo ya kisiasa ya Burkina Faso na Tanzania.Niwasaidie tu

1.Burkina faso KUNA UKABILA NA UDINI wakati Tanzania hakuna.

2.Rais aliyeondoka madarakani hakuingia kidemokrasia aliua mwenzie tena rafiki yake mkubwa (THOMAS sankara) kwa mapinduzi ya Kijeshi .Tanzania Rais alichaguliwa kwa kura kidemokrasia.

3.Burkina FASO jeshi halina nidhamu na ni moja ya majeshi yasiyo na nidhamu Afrika likishika nafasi ya pili Africa kwa ukosefu wa nidhamu baada ya yale ya Jamhuri ya kidemokrasia ya Kongo yakifuatiwa na majeshi ya nchi zinazoongea kifaransa Afrika na yale ya nchi za Kaskazini mwa Afrika kule kulikotokea Arab SPRINGS.Tanzania ni jeshi lenye nidhamu ya hali ya juu mno Afrika na highly organized.

4.Majeshi ya BURKINA FASO hayana nguvu za kudhibiti waandamanaji au waasi maruhuni. Tanzania POLISI TU wanatosha hamna haja ya kuita jeshi kushughulikia waandamanaji maruhuni.Uwezo wa polisi na jeshi pia hupimwa kwa uwezo wake wa kudhibiti organized crimes kupitia CIVIL STRIFES zinazoweza fanywa na raia wahuni waliojipanga kuharibu utengamano katika nchi kwa sababu zozote.

5.Raia wengi wa Burkina FASO NI WAHUNI WASIOPENDA kutii sheria.Ni kama wafuasi wa CHADEMA.Tanzania ni tofauti raia wengi ni watii wa sheria bila shuruti.

Kifupi BURKINA FASO na TANZANIA ni nchi tofauti,zenye majina tofauti,watu tofauti na siasa tofauti.Kulinganisha nchi hizi mbili si sahihi.

You just said so... lakini uliona MABOMU MAKANISANI; Kwenye MIKUTANO YA KISIASA na HADI leo hii CULPRIT hawajashikwa na hawajulikwani ni wa aina gani... kwahiyo wapo HAI na watafanya chochote tena wakati wowote

Nchi hii hakuna anayefuata SHERIA; Kama tunajua WAUZA MADAWA ya kulevya lakini tunaogopa kuwataja sababu VIONGOZI ndani ya serikali inawalinda ina MAANA sisi Wananchi ni WAHUNI????

Wewe unaongelea ukiwa wapi? Issue ya SHEIKH MPONDA Jeshi pia linashiriki kuwasaidia POLISI kwa ULINZI

Marais wa UGANDA na RWANDA waliingia Madarakani kama huyo Rais wa huko; na Wanaiendeleza nchi zao vizuri sana nadhani hata wewe unaitamani Maendeleo ya RWANDA...

Yeah... Enzi ya Utawala wa Rais wa kwanza tunaweza kuringa ya kuwa hatukuwa na UKABILA; UDINI wala MATABAKA
Lakini Sasa hivi tunavyo vyote na vinaimarishwa na UONGOZI wetu...

-- Ajira hakuna ni who's who... UDINI na UKABILA --- Unadhani hii itaendelea mpaka lini bila kutuchafulia nchi yetu?

-- MATABAKA sasa hadi wauza UNGA wapo MABILIONEA na wengine hawajamaliza hata Darasa la 7 ni Ujanja wao wa kuweza kupitisha hiyo MIZIGO na kitu wanachofanya ni kujiunga na Chama Tawala na kujenga POLICE stations

Sisi na Burkina Faso ni sawasawa... ni wanadamu tunaohitaji Demokrasia ya kweli; Isiyotugandamiza na kutudharau kwa manufaa ya hao wachache... kwahiyo PEOPLE POWER... Wananchi wakiamua sasa basi, ni sasa basi hakuna cha hili wala lile...

Government of the people, by the people, for the people, shall not perish from the Earth

** Wewe hauoni hayo Mabadiliko ??



c.c East African Eagle
 
Back
Top Bottom