Kituko kuna kitu unalazimisha sana kiwepo wakati sio kweli.
Burundi ni mali ya warundi wenyewe, wao ndio mwenye mamlaka na nchi yao, regardless kamaa Uganda, Rwanda, Kenya, Tanzania nk tuna maslahi hapo.
Hoja ya msingi ni hizi hapa.
1/Hali ya usalama nchini Burundi ni tete sana, watu wanazidi kuuwawa. Hakuna usalama wa maisha ya warundi na mali zao. Ni muhimu na lazima jeshi la AU la kulinda amani liende sasa, wakati taratibu zingine za kutatua mzozo zikiendelea. Hili ni kwa maslahi ya warundi wote na pande zinazovutana.
2/Piere Nkurunzinza anadaiwa amevunja makubaliano ya Amani ya Arusha na Pia amevunja katiba ya Burundi kwa kutaka kuendelea kutawala. Na hichi ndio kiini cha Mzozo wote. Sasa hizo story za kuitaja Rwanda au Uganda ndizo hizo hizo Zinaitaja Tanzania pia katika kuivuruga Amani ya Burundi. Tusikwepe kiini cha Tatizo ili kutaka kuharalisha mauaji na ukandamizaji wa warundi.