Asalam,
Leo nimeona sio mbaya kujadili mada hii,
NBS inaonesha karibia 65% ya Watanzania wanajihusisha na kilimo. Kilimo cha kujikimu na kiasi kidogo kubadilishia mboga. Tukichanganya ufugaji na uvuvi kama sehemu ya kilimo (maana karibu wate hawa ni wabangaizaji) basi ni 83%. Sasa maswali ninayojiuliza;
1. Je, hawa ndio Waziri anahangaika nao? Au yuko bize na wale vijana wa Kinondoni wanaosafisha ekari moja kwa milioni 15?
2. Je, hawa ndio Mh. Rais wetu mpendwa Mama Samia atakutana nao kesho? Au atakutana na wakulima wa Instagram, FB na WhatsApp?
3. Je, tunaelewa hili ndio kundi likiendelezwa linaweza kuzalisha ajira na kuongeza urali wa Biashara kimataifa kuliko kundi jingine lolote? Au tunawaangalia hawa wa WhatsApp waliojazana hapa viwanja vya Maonesho Mwakangale Mbeya?
4. Je, tumetekeleza kwa kiasi gani ASDP (Agricultural Sector Development Programme) huu ndio mpango wa kitaifa.
5. Je, hawa asilimia 65 ndio wataguswa na zile bilioni 360 za AFDB? Au zile zitaenda kwa hawa wa kinondoni?
Maswali ni mengi lakini naona Wizara inabangaiza, Serikali inabangaiza, pale Mwakangale wamejaa wasanii.
Turudie sera zetu. Tunaangamiza nchi.
Karibu Mbeya Rais wetu. Tupige picha na kukagua tembele na ng'ombe ambae huwezi jua anapatikana wapi Umasaini, Usukumani, au Ukuryani.
Leo nimeona sio mbaya kujadili mada hii,
NBS inaonesha karibia 65% ya Watanzania wanajihusisha na kilimo. Kilimo cha kujikimu na kiasi kidogo kubadilishia mboga. Tukichanganya ufugaji na uvuvi kama sehemu ya kilimo (maana karibu wate hawa ni wabangaizaji) basi ni 83%. Sasa maswali ninayojiuliza;
1. Je, hawa ndio Waziri anahangaika nao? Au yuko bize na wale vijana wa Kinondoni wanaosafisha ekari moja kwa milioni 15?
2. Je, hawa ndio Mh. Rais wetu mpendwa Mama Samia atakutana nao kesho? Au atakutana na wakulima wa Instagram, FB na WhatsApp?
3. Je, tunaelewa hili ndio kundi likiendelezwa linaweza kuzalisha ajira na kuongeza urali wa Biashara kimataifa kuliko kundi jingine lolote? Au tunawaangalia hawa wa WhatsApp waliojazana hapa viwanja vya Maonesho Mwakangale Mbeya?
4. Je, tumetekeleza kwa kiasi gani ASDP (Agricultural Sector Development Programme) huu ndio mpango wa kitaifa.
5. Je, hawa asilimia 65 ndio wataguswa na zile bilioni 360 za AFDB? Au zile zitaenda kwa hawa wa kinondoni?
Maswali ni mengi lakini naona Wizara inabangaiza, Serikali inabangaiza, pale Mwakangale wamejaa wasanii.
Turudie sera zetu. Tunaangamiza nchi.
Karibu Mbeya Rais wetu. Tupige picha na kukagua tembele na ng'ombe ambae huwezi jua anapatikana wapi Umasaini, Usukumani, au Ukuryani.