Tindo
Platinum Member
- Sep 28, 2011
- 69,594
- 123,099
Hiyo ndo shida ya kutojitambua. Wapi kwenye katiba ya ulaya na marekani iliruhusu ubaguzi wa Rangi, wazungu hawa walianza kutupenda lini kama walitufanya watumwa na kututesa kwa miaka mingi na baadae kututawala chini ya ukoloni. Hizo ndio human rights wanazotupigia kelele? Kuwaua kina Kwame nkrumah na kuwatesa kina Mandela was it right. Kama wanaheshimu human rights kwa dhati, leo hii Iraq, Iran, Congo, Libya, Yemen, Syria watoto, wanawake na wengine wasio na hatia wangekua Hai leo. Eti human rights wakati wanaendesha gereza la Guantanamo bay, unadhani kuna haki za binadamu huko? Waandishi wa habari marekani wanatafutwa ili kufunguliwa mashtaka. Watoa taarifa za uhuni wa nchi zao wanasakwa wafunguliwe makosa ya uhaini. Huzijui nchi zao zinavyoendeshwa so acha kuropoka. Kagame is right, wajisafishe wao kwanza ndipo waanze kutuhubiria hayo mambo yao.
Rudi ukajipange, hao wazungu unaosema hawatupendi, zaidi ya 1/2 ya maendeleo ya nchi ni misaada au mikopo yao, hawa wasomi wetu wengi wamesomea kwao. Unataka watupende kwani sisi tunawapenda? Tunachoangalia ni wao kusimamia haki na sio kupendana. Unatuletea historia za mabaya yao ukidhani ndio utapata kuhalalisha huu ushenzi unaoendelea hapa nchini kwa sasa? Tukiamua kuandika mazuri ya wazungu tutajaza vitabu 200. Kwa taarifa yako ni bora kutawaliwa na wazungu wa sasa maana ni wastaarabu kuliko awamu hii ya tano.