Hiyo ndo shida ya kutojitambua. Wapi kwenye katiba ya ulaya na marekani iliruhusu ubaguzi wa Rangi, wazungu hawa walianza kutupenda lini kama walitufanya watumwa na kututesa kwa miaka mingi na baadae kututawala chini ya ukoloni. Hizo ndio human rights wanazotupigia kelele? Kuwaua kina Kwame nkrumah na kuwatesa kina Mandela was it right. Kama wanaheshimu human rights kwa dhati, leo hii Iraq, Iran, Congo, Libya, Yemen, Syria watoto, wanawake na wengine wasio na hatia wangekua Hai leo. Eti human rights wakati wanaendesha gereza la Guantanamo bay, unadhani kuna haki za binadamu huko? Waandishi wa habari marekani wanatafutwa ili kufunguliwa mashtaka. Watoa taarifa za uhuni wa nchi zao wanasakwa wafunguliwe makosa ya uhaini. Huzijui nchi zao zinavyoendeshwa so acha kuropoka. Kagame is right, wajisafishe wao kwanza ndipo waanze kutuhubiria hayo mambo yao.