TANESCO yaingia mkataba wa kukodi software kutoka India kwa USD 30M

Kuna Halmashauri niliwahi kufanya kazi Idara ya Ardhi waliibia Halmashauri huku madiwani wakimwaga sifa nyingi kwa ubunifu wa ile Idara. Walidownload Google Map wakadai wamenunua software kwa gharama ya Sh 20 milioni ili kusaidia mipango mji.

Lile dude tulilibeba mpaka Maonesho ya Nane Nane kuwaonesha wananchi jinsi Halmashauri yetu ilivyopiga hatua katika Idara ya Mipango Miji. Sidhani mpaka leo kama ile Halmashauri ilishagundua iliibiwa. Tuligundua vijana wawili tu kitoka Idara nyingine ambao tulikuwa ndo tumepata ajira.

Just imagine kama Halmashauri inaibiwa kienyeji namna hiyo hali ikoje katika mambo makubwa ambayo Watanzania wengi hawana utaalam nayo?
Nimecheka sana.
 
Software kama hizi serikali inatakiwa iwawezeshe wataalam wa ndani kupitia Mamlaka ya Serikali Mtandao kutengeneza, kama vile mfumo wa malipo serikalini ulivyotengenezwa na wataalam wetu wa ndani kwa kuwezeshwa na serikali.

Kuna maprofesa wa IT pale jalalani (udsm), ukienda DIT kuna maprofesa wa komoyuta wa kutosha ukirudi SUA, UDOM wataalamu wamejazana!

Hata kama hawataki kutumia wasomi je hata hapo wizarani hawa watu hawapo mpaka tuwatumie wahindi kweli?
 
Mnaolalamika tengenezeni software zenu halafu mkawauzie Tanesco kwa bei nafuu kama mnaona ni kazi nyepesi. Kwa nini mnataka kuandikia mate wakati wino upo? Changamkeni fanyeni kazi andikeni hizo software halafu mkauzie hayo mashirika ya umma.
Unaijua eGA mkuu? Kwanini utumie wahindi wakati eGA ipo?
 
Je kwenye hizo gharama kuna ukweli hapo?
Tatizo ni kuwa Tanesco huenda wamechukua mfumo kwa ukamilifu wake badala ya kuwaambia wawatengenezee mfumo ambao ni 'taylor made' kwa matumizi ya Tanesco ambao ungekuwa nafuu na Chande analijuwa hilo. lakini nahisi alikuta faili mezani ikabidi amalizie mchakato..
 
R.I.P JPM, kama ni kweli Mama Nchi imemshinda JWTZ wachukue Nchi 😭😭😭😭
Unaelewa Unachojaribu Kukimaanisha?
Muombe Sana Mungu Afungue Ufahamu Wako Na Kamwe Usirudie Kuandika Kitu Kama Hiki.
 
Kuna uharaka gani wa kutengeneza huo mfumo bila kushirikisha watalaamu wa ndani ya nchi, au japo kutangaza hiyo tender?

Je, mfumo ungeleta maji au kujaza mto Ruvu au kufanya mvua inyeshe ikiwa umetengenezwa na wahindi?

Tatizo kubwa la TANESCO kwa sasa ni kutokuwepo kwa huo mfumo?

1. Nina uhakika 100% huo mfumo unatengenezwa hapa nchini Tanzania bila shida yoyote
2. Hiyo hela inayolipwa kwa wahindi ni "overwhelming"
3. Tungetumia wataalamu wetu, mfumo ungekuwa ni wetu, watalaamu au vijana wetu wangepata ajira, hela ambayo ingetumika ingekuwa ni kiasi kidogo sana ukilinganisha na hiyo waliyolipwa wahindi
4. Usimamizi, usalama/ulinzi, maboresho, na matengenezo ya mfumo, vingeendelea kuwa chini ya wataalamu wetu kwa gharama ndogo
5. Tungeendelea kukua na kujitegemea katika sekta ya software

Matumizi na functionalities za huo mfumo hazitakuwa tofauti sana logically na za huu mfumo Need Human Resource Information/Management System (HRIS/HRMS) (***** - HR SERVICE na mifumo mingine iliyoelezewa hapa https://www.ega.go.tz/uploads/pressreleases/sw-1574867949-ERMS ENG.pd? Kinachotakiwa ni kuadapt tu mifumo iliyopo, kucustomize/kumodify, kuongeza modules na functionalities pale inapotakiwa. Pia Wataalamu wetu wana uwezo wa kutengeneza huo mfumo from scratch.

Huo mfumo unafanana na ipi kati ya hii The 11 Best ERP Solutions for Government and Public Sector Workers?
Makamba yeye kila kitu huwa anawaza nje tu , mifumo kama gepg, plann rep , GotTHoMis imetengenezwa na wataalam wetu
 
Back
Top Bottom