TANESCO yaingia mkataba wa kukodi software kutoka India kwa USD 30M

image_c184dac1-9265-4737-a2aa-e81994b00f1c20211004_135721.jpg
 
Akili iliyotumika kutengeneza Corolla na IST, ndio hiyo hiyo iliyotumika kutengeneza Landcruiser V8.
Waliotengeneza GePG hawawezi shindwa erps
🤣 Haya pigeni marufuku software zote za nje ili zote ziandikwe na eGA. Microsoft, Android, Apple pigeni marufuku fanyeni kila kitu wenyewe. Software za kuongoza ndege airport tengenezeni wenyewe. Za mashine za hospitali tengenezeni wenyewe. Software ni software tuu ukitengeneza moja utaweza kutengeneza zote. 🤣
 
Kipindi cha kula hiki... wacha watu wale...hii nchi ni ya kuliwa liwa na wajanja...JPM alipowabana kwa pamoja walimuandama kwa matusi na dhihaka...
 
Mbona huulizi wakati serikali inanunua software za Microsoft Windows? Kwa nini eGA hawaandiki OS itumike serikalini?
We ungenyamaza tu mkuu. La sivyo unaweza ukahoji kwanini maisha yana ngazi tofauti. Unachotakiwa kuelewa ni kwamba kila kitu ni msukumo tu. Serikali ikiwa na dira ya kwamba Tanzania itengeneze OS yake na computer zake inawezekana kabisa.

Ila kulinganisha ERP na OS ni ngazi tofauti.
 
🤣 Haya pigeni marufuku software zote za nje ili zote ziandikwe na eGA. Microsoft, Android, Apple pigeni marufuku fanyeni kila kitu wenyewe. Software za kuongoza ndege airport tengenezeni wenyewe. Za mashine za hospitali tengenezeni wenyewe. Software ni software tuu ukitengeneza moja utaweza kutengeneza zote. 🤣
Inawezekana kabisa. Ila itachukua muda kukamilisha miradi yote hiyo. Watu wenye akili kama zako wangeenda nje ya nchi kutafuta GePG.
eGa tayari software ya ERP wanayo, kama kuna mahitaji mahsusi ya Tanesco ingefanyiwa marekebisho, ili pesa zibaki hapahapa nchini mikononi mwa waTanzania.
 
Watanzania naona tulisahau kabisa ajenda ya ufisadi wakati wa Magufuli, mpaka sasa kuna ufisadi umefanyika fasta fasta bila ya watu hata kushtuka.

Mkataba uliosainiwa baina ya Serikali ya Tanzania (kupitia TANESCO) na kampuni ya Tech Mahindra ya India wenye thamani ya dola milioni 30 ni wa kukodisha software ya Enterprise Resources Planning (ERP) - ambayo wahindi hawa wenyewe wanaiita Corporate Management System (CMS), kama inavyosomeka kwenye bango pichani chini.

Software ya aina hii huwa inaunganisha vitengo vyote vya taasisi katika software moja kwa ajili ya urahisi wa kuendesha taasisi. Hivyo basi kwa lugha nyingine ni kwamba Wahindi hawa watafunguliwa milango ya kuingia kila mahali ndani ya TANESCO, na hivyo kuwa na siri zote za mfumo wetu wa umeme.

Jambo kama hili ni hatari sana kwa usalama wa taifa. Hakuna njia rahisi ya kuiangusha nchi bila ya kufyatua hata kombora moja kama kuangusha mfumo wa nchi wa umeme.

Software kama hizi serikali inatakiwa iwawezeshe wataalam wa ndani kupitia Mamlaka ya Serikali Mtandao kutengeneza, kama vile mfumo wa malipo serikalini ulivyotengenezwa na wataalam wetu wa ndani kwa kuwezeshwa na serikali.

Zabuni ya kukodisha software hii ilianzaga kwenye dakika za lala salama za utawala wa Kikwete. Hivyo basi kitendo cha zabuni hii kukaa benchi kwa miaka mitano ya Magufuli kinaonesha kuwa hakuwa amekubaliana nayo. Baada ya Magufuli kufa naona wadau wa zabuni hii wameiendeleza na kuimwagia wino fasta, kama wanavyotaka kufanya kuhusu bandari ya Bagamoyo.

img-618a884f193e3.jpg
Najua taasisi zetu,TRA,NIDA,Zina mifumo kama hii,lakini Haina ubora kabisa,lakini kuchukua hayo mapesa ukawapa watu wa nje,badara ya kuzipa Taasisi zetu za ICT zitengeneze hiyo software,ni matumizi mabaya sana ya pesa ya umma,hapo haitaishia kununua software tu,itabidi tukodishe na hardware ambazo ni compatible na hiyo software,na hata kama kulikuwa na haja ya kukodisha software,kwanini hatukwenda South Afrika?au Misri?kwanini twende nje ya Afrika.
 
TAtizo la mtoa Uzi ni mshamba, mill 30 kwa software ni ya kawaida kwa kampuni kubwa kama TANESCO

Mmezoea kutumia software za uwizi unafikiri kampuni kubwa kama TANESCO nao watatumia hapana
hujaona dollar hapo,
ni usd 30 million sawa na 69,000,002,280.00 Tanzania shillings {69 Billion }
Screenshot_20211124-095921.png


Jaribu kuangalia source zako za habari sidhani kama ni mill 30
tupeni source mkuu, tujihakiki.
 
Hiyo software hatuwezi kutengeneza? Mbona serikali inatoa mamilioni ya fedha kusomesha wataalamu wa IT kila mwaka?
 
Inawezekana kabisa. Ila itachukua muda kukamilisha miradi yote hiyo. Watu wenye akili kama zako wangeenda nje ya nchi kutafuta GePG.
eGa tayari software ya ERP wanayo, kama kuna mahitaji mahsusi ya Tanesco ingefanyiwa marekebisho, ili pesa zibaki hapahapa nchini mikononi mwa waTanzania.
Kama wanayo si wangerekebisha halafu wangewapa Tanesco wanasubiri nini? Tena ERP software yetu tuanze kufanya export nayo kama biashara tuuze au tukodishe nchi zingine ituingizie hela. Tuendelee na kutengeneza hizo zingine tushindane na Microsoft, Android, Apple na makampunzi mengine tunazonunua software zao unaonaje bosi?
 
34 Reactions
Reply
Back
Top Bottom