Ramadhani Dau aliitwa mdini/mujahidina kisa ni kuonyesha mapenzi kwa dini yake waziwazi.Laiti dau angekuwa mlevi na mla nguruwe angezeekea NSSF tena bila kelele.Sikuwahi kusikia mtumishi wowote wa NSSF kwamba alishawahi kunyanyaswa kwa dini yake.Hii nchi inahitaji uvumilivu wa kiwango cha mwisho.
MIUNDOMBINU YA TANESCO
Miongoni mwa kero kubwa inayolalamikiwa sana na wateja wetu ni kukatika umeme kunakosababishwa na uchakavu wa miundombinu. Ukweli ni kwamba baadhi ya miundombinu tuliyo nayo ni ya siku nyingi wakati matumizi ya umeme
yameendelea kuongezeka kwa kasi sana. Kwa mfano nyingi ya Substations katika jiji la Dar es Salaam zimejengwa katika miaka ya 80 na 90. Wakati huo wakazi wa jiji la Dar es Salaam walikuwa chini ya milioni 3. Sasa hivi wakazi wa jiji ni zaidi ya milioni 5 na hivyo miundombinu iliyopo inaelemewa sana.
Jitihada za kurekebisha hali hii zilikwishaanza ambapo sasa kuna miradi mikubwa inaendelea katika jiji la Dar es Salaam na itakapokamilika itasaidia sana kupunguza tatizo la kukatika kwa umeme. Kwa kiasi fulani kukatika huko kwa umeme hasa katika jiji la Dar es Salaam kunatokana pia na utekelezaji wa miradi hiyo.
Miradi inayotekelezwa ni pamoja na ule unaojengwa kusini mwa Dar es Salaam kwa mkopo wa Benki ya Dunia ambao utaboresha umeme maeneo ya Kigamboni, Kurasini, Mbagala, Mkuranga, Kisarawe, Gongolamboto, Ukonga, Kitunda, Vingunguti na Tabata
Mradi mwingine ni unaotekelezwa kwa ufadhili wa Serikali ya Japan ambao utasaidia kuondoa matatizo yaliyo katika maeneo ya Muhimbili na Upanga, Mwananyamala na Kinondoni, Oysterbay na Masaki, Jangwani Beach, Bahari Beach na Mbezi Beach.
Mradi mwingine ni ule unaotekelezwa kwa mkopo kutoka Benki ya Maendeleo ya Afrika ambao unaendelea katika mikoa ya Dar es Salaam, Arusha, Shinyanga, na Geita.
Mradi mwingine ni ule unaofadhiliwa na Serikali ya Finland ambao utasaidia sana kuimarisha umeme kati kati ya jiji la Dar es Salaam na kusaidia kuimarisha umeme katika eneo lenye majengo mengi marefu la Samora, Azikiwe, Kariakoo na Sea view.
Sambamba na miradi hiyo inayotekelezwa Dar es Salaam, mradi mkubwa wa kupeleka umeme wa 400KV kutoka Iringa kupitia Mtera, Dodoma, Singida hadi Shinyanga uko kwenye hatua za mwisho za kukamilika na hivyo kutuhakikishia umeme wa uhakika katika kanda ya ziwa hasa jiji la Mwanza.
Kazi ya kuunga Songea na Gridi ya Taifa kutokea Makambako kwa 220KV inaendelea na Makandarasi wako kazini.
Kazi za kuunga Tanzania na Kenya kwa umeme wa 400KV inatarajiwa kuanza hivi karibuni kwani zabuni za kuwapata Makandarasi ziko katika hatua za mwisho. Ujenzi unategemewa kuanza mwakani.
Kazi nyingine ambazo hazijaanza lakini zitaanza hivi karibuni ni pamoja na Dar es Salaam – Somanga (400KV), Bulyankhulu – Geita – Nyakanazi – Rusumo (220KV)
Miradi hii ya kuimarisha miundombinu ikikamilika itasaidia kulipunguza kwa kiasi kikubwa tatizo la kukatika kwa umeme kutokana na mfumo wa Usambazaji.
Nawaomba wateja wetu, wakati kazi hii kubwa inapoendelea, wawe na subira na uvumilivu kwa usumbufu wa hapa na pale utakaokuwa unatokea. Hata hivyo TANESCO itajitahidi kurekebisha kasoro zinazoweza kurekebishwa katika miundombinu ya sasa ili kupunguza usumbufu huo wakati marekebisho makubwa yakiendelea