Huyo Kimburu lengo lake la kuhara hapa ni kuuharibu huu uzi, Kimburu mkubwa huyo wa kuonekana usiku tu.
Mikakati ya Kupunguza Gharama za Kuunganisha Umeme kwa Wateja, Kuongeza idadi ya Watanzania wanaopata na waliofikiwa na umeme: Katika kutekeleza azma yake ya kutimiza lengo la asilimia 30 ya wananchi watakaounganishiwa umeme ifikapo Mwaka 2015, Serikali ilipunguza gharama za kuunganisha umeme kwa wananchi. Katika punguzo hilo, mathalan gharama ya kuunganishwa umeme wa njia moja (single phase) kwa wateja wadogo mijini na vijijini ilipungua kwa wastani wa kati ya asilimia 30 na 77. Kutokana na juhudi hizo za Serikali, idadi ya Watanzania wanaopata umeme imeongeka kutoka asilimia 11 Mwaka 2005ÂÂ hadi kufikia asilimia 24 mwaka 2015. Pia jitihada hizo zimewezesha Watanzania asilimia 36 kufikiwa na miundombinu ya umeme.