TANESCO bado hawajashusha bei ya umeme kwa mlaji

TANESCO bado hawajashusha bei ya umeme kwa mlaji

Gharama za kuzalisha umeme zimeshuka kwa 50% lakini inashangaza kwamba TANESCO bado hawajashusha bei za umeme kwa kiwango cha kuridhisha.

Zamani wateja wa kikabwela (KCC) tulikuwa twapata unit 2.7 kwa gharama ya Tsh 1000. Baada ya hili punguzo feki (linalopigiwa kelele sana na serikali kwa sababu ya kukaribia uchaguzi mkuu wa Oktoba), sasa mlaji hupata unit 2.8 kwa thamani ya Tsh 1000! Maana yake ni kwamba kwa kila Tsh 10,000 unapata unit 1 ya umeme! Hii ni dharau, kebehi na kejeli kwa wavuja jasho wa nchi hii.

Badala haya mafisadi yashushe bei ya umeme kwa walalahoi, wamefanya hivyo kwa wafanyabiashara na mapapa wakubwa ambao wana uwezo mkubwa wa kulipia umeme. Ni bora hili punguzo la kipuuzi liondolewe badala ya serikali kujitapa kwamba wameshusha bei ya umeme wakati hawajashusha chochote.

Ndugu zangu, nyie wote ni mashahidi mnapolipia ankara za umeme mahali mlipo. Ifike wakati tufunguke akili na kuing'olea mbali hii serikali ya wachumia tumbo mwezi Oktoba. Tusikubali kudanganywa tena na haya mafisadi.
Hilo TANESCO na serikali yao ya Sisiem, wanaloliita ni punguzo la bei ya umeme, ni changa la macho la hali ya juu, lenye lengo la kuingia kwenye kampeni za uchaguzi wa mwaka huu, wakijinadi kwa wananchi kuwa, hamuoni jinsi chama chenu kilivyotekeleza ilani yake ya kuwaletea maisha bora kwa kila Mtanzania?

Ukichunguza punguzo hilo,halina tofauti na la mzazi aliyemuahidi mwanae kumnunulia nguo mpya, lakini badala yake anarejea nyumbani na pipi ya ivory ya Jero na kumzawadia mwanae huyo ili 'kumnyamazisha' asiendelee kupiga kelele.

Hata hivyo waTZ mwaka huu tumeapa kuwa hatudanganyiki tena, na hata wakitugawia na khanga na mafulana yao ya bure, tutatekeleza ile slogan yetu mpya inayosema KULA SISIEM, lakini KURA kwa UKAWA.
 
sawa mama,ila mimi nafikiri ubinafsishaji hautashusha gharama,ila at least ubora wa huduma utaongezeka unless iwe unazungumzia ubinafsishaji wenye kutoa nafasi ya ushindani mkubwa wa kibiashara ndani yake na sio ubinafsishaji huu tuliozowea hapa nchini kwetu ambao tender zinadhibitiwa ili wale wale wanaoua mashirika ya umma wapewe biashara yake.

Likibinafsishwa na kugawanywa na kuwa na ushindani, gharama lazima zishuke na huduma lazima iboreke. Hukumbuki simu? tulivyokuwa tunaumizwa? Labda hukuwepo enzi za shirika moja tu la simu.
 
Ninadhani wanataka kupunguza deni walilo nalo kwasababu wakishusha itakula kwao itafika siku tuta kosa umeme ______ Tunadaiwa sana ....Naipenda ________ yangu
 
Libinafsishwe ki kanda na kikazi: ufuaji, usambazaji, usafirishaji viwe vinamilikiwa na kampuni tofauti ki kanda ili kuwe na ushindani. Ukizubaa kwa kutokufua umeme wewe wa Kusini, wa Mashariki anakupiga bao na hali kadhalika.

hapo sawa mkuu.
 
Hapana ni "wasomi" wetu hao wanaoiendesha TANESCO.

Hapo ndipo mtapojuwa maana ya kuviondoa vichwa madarasani mkaweka mapakacha kuyasomesha. Hayo ndiyo matokeo yake.

Serikali makini haiwezi kuburuzwa na "wasomi" na kushindwa kuchukua hatua stahiki kwa wakati
 
Likibinafsishwa na kugawanywa na kuwa na ushindani, gharama lazima zishuke na huduma lazima iboreke. Hukumbuki simu? tulivyokuwa tunaumizwa? Labda hukuwepo enzi za shirika moja tu la simu.

njia rahisi ya kumaliza hili tatizo ni kuruhusu wawekezaji binafsi katika sekta ya umeme washindane na tanesco (kama ilivyo kwenye makampuni ya simu). ni kwanini serikali yako "sikivu" ya CCM inazuia wawekezaji binafsi kuzalisha umeme badala ya kuwaacha TANESCO wakiritimbe soko la nishati peke yao?
 
na hii yote ni kwa sababu ya serikali ya CCM kusiasisha elimu yetu. haya ndio matokeo ya divishen 5 za CCM na wala hawaoni haya kushuka kwa elimu yetu kwa kuwa lengo ni kuwadunisha watanzania kielimu ili waendelee kuiba rasilimali za nchi hii na kuficha fedha uswisi.

mimi nasema TANESCO haitaperform hadi CCM watakapong'oka madarakani mwezi wa Oktoba. hakuna mkato wala muujiza mwingine zaidi ya huu. get me?

Hayo ni matokeo ya kutokuwa na misingi mizuri ya elimu kuanzia tulipopata Uhuru, kutokujenga mashule ya kutosha na kutokujenga vyuo vya kutosha, matokeo yake ni akina fulani wanachaguliwa na akina Ndalichako, hata kama hawafai, mradi tu ni mpwa wa Ndalichako basi atachaguliwa.

Fursa zilikuwa zikibanwa ili akina fulani wasome na wawe katika uongozi hata kama hawafai na wale wenye uwezo wameminywa na kunyimwa hizo fursa kwa sababu tu hawakutakiwa wawe na elimu, hayo ndiyo matokeo yake.

Tunashukuru, ujio wa Kikwete kaliona hilo na kalipiga vita ki sayansi, kwa kuongeza mashule na kuongeza vyuo. Tutarajie mema zaidi na muendelezo wa hayo katika awamu ijayo.
 
liuliwe tena,,,,kwani serikali imeshindwa kulisimamia,,,,,,

Serikali ilishindwa siku nyingi sana kusimamia biashara na ilishajitowa katika biashara toka enzi ya Mwinyi, lakini naona hili shirika watu wanafanya kila njia kulibakisha Serikalini ili liwe ndiyo sehemu ya kujichotea, kwani biashara yake ni kubwa sana.

Hayo ma "coma" uliyoyajaza katika maandiko yako maana yake nini? Ndivyo mwalimu wako alivyokufundisha namna ya kutumia "coma" hivyo?

Unazidi kutuhakikishia kuwa hizo shule mlienda kusomea ujinga.
 
TANESCO hawajashusha na wala hawatoshusha daima mpaka hilo shirika liwe la kibinafsi.

Kuna wizi wa kila aina unafanyika TANESCO katika ngazi zote.

Sitegemei kama watashusha.

Inabidi hilo shirika lote liuliwe kabla ya kuanza kushusha.

Hhaha!
CCM imeshindwa DADANGU
 
Punguzo la umeme hakika ni geresha. kama ni geresha kwa kupata kura haitoshi. serikali ijue tunalipa umeme kwa hasira na chuki kwani tunajua tunadhulumiwa. wako nyoka wenye makengeza wamekinga bomba wanawanyonya wananchi. ewura wafanye uadilifi tunataka bei ya umeme ishuke kufuatana na soko la mafuta dunia na kukata mirija ya wezi na wanyonyaji.
 
Hayo ni matokeo ya kutokuwa na misingi mizuri ya elimu kuanzia tulippopata Uhuru, kutokujenga mashule ya kutosha na kutokujenga vyuo vya kutosha, matokeo yake ni akina fulani wanachaguliwa na akina Ndalichako, hata kama hawafai, mradi tu ni mpwa wa Ndalichako basi atachaguliwa.

Fursa zilikuwa zikibanwa ili akina fulani wasome na wawe katika uongozi hata kama hawafai na wale wenye uwezo wameminywa na kunyimwa hizo fursa kwa sababu tu hawakutakiwa wawe na elimu, hayo ndiyo matokeo yake.

Tunashukuru, ujio wa Kikwete kaliona hilo na kalipiga vita ki sayansi, kwa kuongeza mashule na kuongeza vyuo. Tutarajie mema zaidi na muendelezo wa hayo katika awamu ijayo.

ina maana unalenga kumlaumu mwalimu nyerere? mbona haya mambo ya divisheni faivu na watoto kwenda sekondari huku hawajui kusoma wala kuandika yameanza katika utawala wa mwislamu mwenzako, profesa kikwete?
 
ina maana unalenga kumlaumu mwalimu nyerere? mbona haya mambo ya divisheni faivu na watoto kwenda sekondari huku hawajui kusoma wala kuandika yameanza katika utawala wa mwislamu mwenzako, profesa kikwete?

Nisome tena vizuri, utanielewa tu. Hata kama hupendi lakini ukweli unajulikana.
 
Yaan nchi hii viongozi wapo kwa maslah binafsi tu, na si kwa ajili ya kusaidia wananchi, kwan hata mafuta yameshuka bei lakini nauli katika vyombo vya usafiri iko pale pale haijashuka, sasa sijui wanamsaidiaje mwananchi mwenye kipato cha chini ili na yeye aweze kunufaika kwa kushuka kwa bei za mafuta, endapo wangeshusha nauli ingesaidia hadi kupungua kwa bei za bidhaa sokoni, ambapo ingekuwa imepunguza ukali wa maisha kwa mtanzania mwenye kipato cha chini kwa kiasi fulani. Haya MASUMATRA sijui yapo kwa ajili gani.
TANESCO na nyie punguzeni gharama za umeme mnatugandamiza wananchii

Kwel nimeamini mafisadi huwa hayana huruma hata kidogo

October kitaeleweka tuu
 
Hawa jamaa ni wahuni sana. Walitangaza kuanzia Machi 1, watashusha bei, cha ajabu mimi wamenibadilishia tarrif number na kunipeleka ya juu zaidi sijuwi Kwa sababu gani. Mwezi Februari nilinunua umeme wa Tshs. 35,000 nikapata unit 134. Mwezi huu nimenunua umeme wa pesa hiyohiyo nimepewa unit 77 tu, so funny.
 
Kile kiofisi cha tanesco heri kitiwe kiberiti tu, ni kichefuchefu.
 
ina maana unalenga kumlaumu mwalimu nyerere? mbona haya mambo ya divisheni faivu na watoto kwenda sekondari huku hawajui kusoma wala kuandika yameanza katika utawala wa mwislamu mwenzako, profesa kikwete?
kwani hao wanaofanya kazi huko tanesco ni product ya Kikwete? hapo anahusika zaidi nyerere kwa 98%. mwinyi na mkapa kwa mbali.
 
ndugu mompome yaani hii nchi ni ya ajabu sana. na wakati tunateseka hv na ugumu wa maisha kuna mifisadi inamiliki hela nyingi sana za wizi ambazo imezibatiza majina ya ajabu kama HELA YA UGOLO/MBOGA, VIJISENTI, nk.

Na pamoja na udhalimu tunaofanyiwa na serikali hii ya kifisadi, kuna mijitu itakuja hapa kama laki si pesa, ifweero, MUSSA ALLAN (MSALANI), Ritz FaizaFoxy, MwanaDiwani, thatha, TataMadiba, gsu, mjepo, Agogwe, Simiyu Yetu, Cybercrime, Queen P, et al itakuja hapa na kuanza kutetea ufisadi huu unaofanywa na TANESCO kwa maelekezo ya CCM.

Tanescrow! Hii kampuni inayogawa nguzo badala ya umeme? Hawawezi punguza gharama wakati wamefulia. Hakuna pesa, kipato cha taifa imekuwa ni mali ya familia moja. Ni ile hadithi ya Mobutu aliyekuwa akipongezwa na wafaransa, huyu wetu anapongezwa na wamarekani ingawa naona kama wameshagundua hakuna kitu darini.

Hao akina FaizaFoxy wamenifanya niamini kwamba kumbe hata wenye IQ ndogo wanaweza kutumia kompyuta! Sitegemei kuishi kijiji kimoja na watu kama hawa wanaodhani mwana CCM au kabila lao au dini yao akiiba ni sawa sana!
 
Last edited by a moderator:
Hayo ni matokeo ya kutokuwa na misingi mizuri ya elimu kuanzia tulipopata Uhuru, kutokujenga mashule ya kutosha na kutokujenga vyuo vya kutosha, matokeo yake ni akina fulani wanachaguliwa na akina Ndalichako, hata kama hawafai, mradi tu ni mpwa wa Ndalichako basi atachaguliwa.

Fursa zilikuwa zikibanwa ili akina fulani wasome na wawe katika uongozi hata kama hawafai na wale wenye uwezo wameminywa na kunyimwa hizo fursa kwa sababu tu hawakutakiwa wawe na elimu, hayo ndiyo matokeo yake.

Tunashukuru, ujio wa Kikwete kaliona hilo na kalipiga vita ki sayansi, kwa kuongeza mashule na kuongeza vyuo. Tutarajie mema zaidi na muendelezo wa hayo katika awamu ijayo.

Kama ni hivi hatuendi kokote. Sayansi gani unayozungumzia? Hata upendeleo ni sayansi? Utawezaje sayansi ktk siasa wakati shuleni ilikushinda?

Hebu tuamini kwamba ametumia sayansi, ni shule ipi au chuo kipi unachoamini kakianzisha profesa wetu, ambacho ni mfano wa mafanikio? Mafanikio ya mtu anayefaa, usiniletee mfano wa mtu sifuri.
 
Back
Top Bottom