Tamko la Wapiganaji CCM Feb 10, 2010

Tamko la Wapiganaji CCM Feb 10, 2010

Tamko limekuja wakati muafaka?

  • Ndiyo

    Votes: 8 57.1%
  • Hapana

    Votes: 5 35.7%
  • Sijui

    Votes: 1 7.1%

  • Total voters
    14
  • Poll closed .
Hivi ile single ya Jerry Muro ndio imeishaeeh?

Naona kimepakuliwa kitu kipya...tatizo prodyuza ndo hajulikani!
 

Hatuwezi kamwe kukubali kwa namna
yoyote ile kuendelea kukaa na wahusika wa kashfa hizo kwa kisingizio au sababu​
yoyote ile
.
!

Mimi nafikiri wamechelewa kuwasha moto.

Washa moto ikibidi ongeza nguvu kupitia chama chochote. Mapambano ni kushinda au kushindwa hila kwa mapambano haya nina uhakika Ushindi ni lazima.

Nakumbuka Mbowe mwaka 2005 alisema ni kupiga kiberiti tu.

Tanzania ya sasa inasubiri nani aanzishe. Ngoma ikisha pigwa wachezaji ni wengi tu.
 
Mimi nafikiri wamechelewa kuwasha moto.

Washa moto ikibidi ongeza nguvu kupitia chama chochote. Mapambano ni kushinda au kushindwa hila kwa mapambano haya nina uhakika Ushindi ni lazima.

Nakumbuka Mbowe mwaka 2005 alisema ni kupiga kiberiti tu.

Tanzania ya sasa inasubiri nani aanzishe. Ngoma ikisha pigwa wachezaji ni wengi tu.
tutajitokeza mstari wa mbele, maana nnchi hii imekosa mtu wakujitoa muhanga kama Mrema alipojaribu miaka ile, tunahitaji watu wa aina ile, lakini tuwe tayari kwa mapambano.
 
wamejawana uwoga na ufitini hawana lolote ni wivu tu unawasumbua na roho ya kwanini?mngekuwa wapiganaji mngekuwa mnapokea posho mara mbili kama sio upunguani ni nini?

Inaelekea mkuu unawafahamu, ebu tutajie
 
Wapiganaji wanaficha majina yao?

Basi na sisi huku kwetu Kyela tuongeze madai yetu. Wale waliofanya yafuatayo wasimamishwe:
- Walioiba pesa za mafuriko na wakajengea mahekalu Kunduchi
- Walioba michango ya shule na wakanunua majengo ya NBC Tukuyu,
- Waliolipwa mamilioni kwamba wanaenda kutibiwa Ujerumani kumbe walijifungia hapo Kunduchi.
- Wale wanaoteka wapiga kura wao na kuwafungia majumbani kwao.
- Wale wanaochukua posho mbili kinyume na sheria.

Ningeona wa maana kama wangeombe serikali iwachukulie hatua watu wanaotuhumiwa kwa madhambi mbalimbali. Lakini kusema chama kiwafukuze watu uanachama wakati hawajashitakiwa na chombo chochote nafiki ni mawazo yaliyojaa chuki zaidi kuliko uongozi bora.

Wakitaka tuwaelewe wajitoe CCM na kupoteza mafao yao, hapo ndio tutajua kweli wana nia njema. Mbona Mrema alijitoa na kupoteza kila kitu na wananchi tulimwunga mkono.
 
"Tunakataa​
juhudi zozote za kujaribu kuwaondoa wanachama wenye uwezo wa
kuongoza na walioonesha uwezo huo kwa vitendo kwa kisingizio cha umri ili
kuwapisha “vijana”. Tunaamini kama Taifa tutafanya kosa kubwa sana kuamua mara
moja kuliachia taifa mikononi mwa vijana kwa sababu ya umri tu. Tunaamini kila
mwana CCM mwenye uwezo wa kuongoza na anayekubalika kwa wananchi wake
asinyimwe nafasi ya kuongoza kwa kisingizio cha umri. Tunawaunga mkono wana
CCM ambao ya kuwa na uwezo wa kuongoza wameamua kukaa pembeni ili kuruhusu
wanachama wengine kuingia katika safu ya uongozi. Uamuzi huu usionekane kuwa ni
udhaifu au ni njia ya kuwalazimisha wengine kuufuata. Kustaafu nafasi ya uongozi

kunaweza kufanywa na mtu yeyote pasipo kujali umri wake."

Hii inanipa wasiwasi na style ya upiganaji wao.
 
Wapiganaji wanaficha majina yao?

Basi na sisi huku kwetu Kyela tuongeze madai yetu. Wale waliofanya yafuatayo wasimamishwe:
- Walioiba pesa za mafuriko na wakajengea mahekalu Kunduchi
- Walioba michango ya shule na wakanunua majengo ya NBC Tukuyu,
- Waliolipwa mamilioni kwamba wanaenda kutibiwa Ujerumani kumbe walijifungia hapo Kunduchi.
- Wale wanaoteka wapiga kura wao na kuwafungia majumbani kwao.
- Wale wanaochukua posho mbili kinyume na sheria.

Ningeona wa maana kama wangeombe serikali iwachukulie hatua watu wanaotuhumiwa kwa madhambi mbalimbali. Lakini kusema chama kiwafukuze watu uanachama wakati hawajashitakiwa na chombo chochote nafiki ni mawazo yaliyojaa chuki zaidi kuliko uongozi bora.

Wakitaka tuwaelewe wajitoe CCM na kupoteza mafao yao, hapo ndio tutajua kweli wana nia njema. Mbona Mrema alijitoa na kupoteza kila kitu na wananchi tulimwunga mkono.
baada ya kumkamata tayari ukombozi wa watanzania utakua umepatikana.....?
 
Siwaamini sana!! Anyway, subira yavuta..........................!!!!!!!!!!!!!!
 
ngonjera nzuri, it has been a while since i heard one,.good one thou
 
Wajiondoe ndani ya chama ili waiokoe nchi. Huwezi kuokoka/kuokoa basi linalopinduka ukiwa ndani ya basi hilohilo wakati wewe si dereva.

Dereve wao kikwete doesn't care hata basi likipinduka, na wao wakiwa ndani!!!!!!
 
Hakuna jipya na wala haina nguvu....njaa na woga unawasumbua.....kama kweli wapo wajitokeze tuwajue lakini CCM ili idumu na iende na wakati lazima kuwe na GOD FATHERS ndani yake...ambao wana nguvu ya kiuchumi.(ufisadi ndio unapoingia hapo)..huo ndio ukweli hata mkaandika matamko mangapi haintosaidia kitu...kama mko kamili kweli jitoeni muanzishe chama chenu..lakini CCM ni kama ilivyo na itadumu milele hivyohivyo I SWEAR!!!
 
i have mixed feelings with it ,they have some good points but who are they?

moja ya ahadi za mwana tanu ambazo kama wao wanazifuata inasema nitasema ukweli daima,fitina kwangu mwisho,sasa hawa ndugu zetu kwa kuwa wanasema ukweli ingefaa tuwatambue halafu isije kuwa wanawanyooshea vidole wenzao kwa kuwa wao wamekosa

twaweza jikuta tunapeana mafumbo ya TAARABU HAPA
 
I have mixed feelings with this statement

wametoa maelezo mazuri na mwongozo mzuri but who are they?waje mbele yetu tuwatambue kwa nini wajifiche?
Moja ya ahadi za mwana tanu ambayo wao wanadai kuzifuata inasema nitasema kweli daima,fitina kwangu mwiko, sasa kama wao hawalaeti fitina na wanasema ukweli kwa nini wasijitokeze?pia isije kuwa wana machungu kwa kuwa wamekosa na wenzao wamepata ndo mana wanajifanya wana machungu mbona wengine wanahusishwa na uwekezaji bomu wa tanzania na wengine walikuwa na dili yao ya umeme wa kule singida?

isijekuwa ni madongo ya taarabu haya
 
Hapana.. kwa upande wangu.. Enigma hawezi kutoa chochote hapa bila ya ridhaa yangu, at least not kwa kutumia handle hiyo ya Enigma. Sijui nani aliruhusu itumwe huko ilikotoka.
Mzee hii ni tungo tata, hasa hapo kwenye red. La muhimu iwe imetoka kwako ama umeruhusu itoke au hukuruhusu itoke, bado tamko kama tamko, limebeba bango ambalo mwanaccm yeyote makini yafaa apime na achukue maamuzi sahihi ya nini kinachofaa kwa sasa!
 
mmmh .......hawa wapiganaji hawana jina? au ndio usawa ule ule wa siasa za `kuogopana` na `kuoneana haya`?
Huu ni unafiki tu ndugu zangu wana JF. Hawa jamaa kama ni wapiganaji wangetaja majina yao halafu nasi tutambue ni akina nani. Kufanya hivyo, kungesaidia kupunguza maswali kwa mfano "je, kama huo waraka umeandikwa na mtu mmoja tu na akaamua kutumia neno kundi?" Je, kama siyo wanachama? Huu ni woga tu ndugu zangu. Upiganaji hauishii na kutaja maneno kama mlivyo/ulivyofanya kwa kuweka waraka hapa jamvini! Tuwajue sasa ili hata kuna wengine tungependa kuungana nanyi tuelewe. Vinginevyo, nyie siyo wapiganaji maana mnaogopa kujitokeza hadharani kwa manufaa ya wengi kuwapa nguvu juu ya hilo. Natoa mfano, Dk. Slaa alijitokeza japo hakuwa na si wa CCM watu wakamuona wakati anatangaza orodha ya mafisadi kipindi kile. Tabia yetu watanzania tulio wengi tu wazembe wa kusoma. Je, wanaCCM wasioingia humu jamvini kwa mfano watapateje taarifa hizi? Nashauri tunapoamua kujitokeza kwa ajili ya kutetea au kuanzisha vuguvugu lenye lengo la kuleta maboresho kwenye jamii kisiasa, kiuchumi na kijamii tusiwe vinyonga.
 
Jamani hata watabiri wetu wa mvua huwa wanatabiri mvua itanyesha lkn wakati mwingine hainyeshi na wakati mwimgine wanapatia na mvua inanyesha tena kwa nguvu hata kuleta maafa. Na kumbuka elnino walitabiri watu tukasema aaaaaah bwana hiwezekani lakini ukwauliza wa mabondeni watakuambia.na hili linaonekana kama utani kaeni chonjo maafa yanakuja na kiama kwa ccm.
 
Katiba ya CCJ ilikua na "Kwa kua" nyingi na huku naona "Kwamba" nyingi kama alivyosema PM hii kitu imesheheni lugha inayoshabihiana sana na lugha za humu JF ,kero zinazopigiwa kelele kila siku humu zimo na watuhumiwa nambari moja wa humu JF ni walewale walioainishwa humu, Mwenye macho haambiwi tazama ngoja tujionee what next...!
 
Haya ni mapambano au vita kama walivyotangulia kusema wengine,ni rahisi sana kushindwa vita kama utaonekana hadharani mbele ya adui yako,inajulikana wazi kwamba ukishamjua adui yako ni rahisi kummaliza,kwa hiyo kuficha majina yao ni sehemu ya mbinu ya kushinda vita,ninaamini utafika wakati watajitokeza hadharani ,lengo la waraka nafikiri ni ujumbe uwafikie walengwa ili kujua hisia za watanzania na kama hawatatekeleza wajue wazi kwamba kuna hatari mbele inakuja.
 
Back
Top Bottom