TAMKO la TEC: Upo uwezekano baadhi ya ma Baba Askofu hawajui kilichomo

Pengo ni TISS kwa hiyo ni kawaida kwa watu kama yeye wanapogundulika hujigeuza kulingana na sura inayomhakikishia usalama. Waraka uliotolewa ni huru nje ya uongozi wake kwa hiyo wala asijiabishe bure kila mmoja anamtambua ni mtumishi mtiifu wa kipenyo
wew umejuaje kuwa Pengo ni TISS? hlf kanisa halijui
 
Na Ezekiel Kamwaga

KUELEKEA kipindi cha Kwaresma na Sikukuu ya Pasaka ya mwaka 2018, Baraza la Maaskofu wa Katoliki Tanzania (TEC) lilitoa waraka ambao kimsingi ulikosoa vitendo vya uminyaji wa demokrasia na uhuru wa watu kujieleza uliokuwepo wakati wa utawala wa hayati Rais John Magufuli.

Waraka ule ulikuwa na sehemu nne lakini sehemu iliyozua mjadala zaidi ilikuwa ni sehemu ya tatu iliyokuwa na kichwa cha habari kisemacho; “Dalili za Nyakati Zetu Tanzania” ambapo pamoja na mambo mengine, Maaskofu walieleza kutofurahishwa kwao na maandamano na mikutano ya kisiasa kuzuiwa na vyombo vya dola huku vyombo vya habari vikifungiwa.

Siku chache baadaye, Mwadhama Polycarp Kadinali Pengo, alizungumza na vyombo vya habari na kutoa maelezo yaliyokuwa na sura ya kutokubaliana na waraka ule. Kwanza alisema kwamba hakuwa anajua chochote kilichoandikwa ndani ya waraka ule na kwamba jina lake alilikuta tu kwenye lile tamko. Na pili, Pengo ambaye pengine alikuwa ndiye Mkatoliki mashuhuri na anayeheshimika zaidi nchini, alieleza kutokubaliana na yaliyomo kwenye waraka ule – hasa masuala yasiyo ya kidini yaliyojumuishwa humo.

Kuna mambo makubwa mawili ambayo tunaweza kujifunza kutoka kwenye maelezo hayo ya Pengo wakati tukianza kudadavua waraka wa hivi karibuni uliotolewa na TEC kuhusu suala zima la mkataba wa uendeshaji wa bandari za hapa nchini baina ya Serikali ya Tanzania na Dubai.

La kwanza ni kwamba waraka wa TEC si neno la Mungu. Kama ingekuwa waraka huo ni neno, mtu wa hadhi ya Kadinali Pengo asingeweza kutoka hadharani na kueleza mapungufu ya waraka wa mwaka 2018. Mwadhama Pengo ni mlinzi wa imani ya Kikatoliki na kwa vyovyote vile asingeweza kupingana na jambo lenye kulinda imani au la maelekezo ya Kimungu.

Jambo la pili linahusu wanaosaini waraka. Maelezo ya Pengo yalitufundisha kwamba unapoona waraka umesainiwa na Maaskofu 37 – kama ilivyokuwa kwa waraka uliosomwa kwa waumini Wakatoliki kwenye makanisa ya Tanzania Jumapili iliyopita, si lazima Maaskofu wote wawe wanajua kilichomo. Inawezekana kazi hiyo imefanywa na Maaskofu wachache tu – na wengine hawakujua chochote hadi waraka huo ulipojitokeza; kwanza kwenye vyombo vya habari na pili makanisani.

Na Mwadhama alikuwa na swali moja muhimu alilouliza TEC baada ya waraka ule wa mwaka 2018; kwamba Maaskofu wanajua nini kuhusu haki za kidemokrasia na kubana uhuru wa watu kujieleza? Pengo aliwaambia waandishi wa habari kwamba hayo si maeneo ambayo viongozi wa dini wanayajua zaidi kuliko wanasiasa na vyama vya siasa.

Ndilo swali ambalo pia nadhani Kadinali Pengo angeuliza kuhusu waraka huu wa TEC wa wiki iliyopita. Kwamba Maaskofu wanajua nini kuhusu masuala ya uendeshaji wa bandari? Wanajua nini kuhusu masuala ya haki za kibiashara za Tanzania na nchi nyingine kwenye uwekezaji?

Hili ni swali muhimu kwa sababu; kama Maaskofu wakianza kuhoji kuhusu uwekezaji bandarini, mpaka wa kuhoji utaishia wapi? Nini kitawafanya wasihoji kuhusu gharama za ujenzi wa Reli ya SGR au Bwawa la Mwalimu Nyerere? Kama wanaruhusiwa kuhoji uwekezaji bandarini, nini kitawazuia wasihoji kuhusu bei za korosho na kahawa kwa wakulima?

Hofu kubwa ya Pengo wakati ule – na naamini ndiyo hofu kubwa ya baadhi yetu kwenye waraka huu wa Maaskofu ni kwamba, Tanzania imebaki kuwa nchi ya mfano kwa Umoja na Amani yetu kwa sababu ya mgawanyo mzuri wa majukumu baina ya masuala ya kiserikali na yale ya kidini.

Kama Serikali ingekuwa imetangaza Jumapili kuwa siku ya kazi na watu hawataruhusiwa kwenda kanisani, waraka wa TEC kupinga hilo na kuusambaza na kusomwa makanisani lingekuwa jambo linaloingia kichwani. Kama Serikali ingelazimisha watu kufanya mambo ambayo ni kinyume cha misingi na imani ya kidini, waraka ungekuwa na maana kubwa.

Lakini suala la uwekezaji tayari lina mijadala yake kupitia itikadi za vyama. Ziko itikadi zinazoamini kwamba uchumi wa unatakiwa kumilikiwa na dola na watu wake na ziko itikadi za kisiasa zinazoamini uchumi unatakiwa kuamuliwa na nguvu ya soko. Rais wa Awamu ya Tatu, hayati Benjamin Mkapa, aliliweka hili vema kwa kutumia mfano wa paka.

Akimnukuu Kiongozi wa zamani wa China, Deng Xiaoping, Mkapa alisema yeye ni mfuasi wa kuamini kwamba cha msingi ni kuona paka anakamata panya na si paka ni wa rangi gani. Kuna wengine, wanaamini kwamba rangi ya paka ni muhimu kwenye kukamata panya. Ukisoma tamko la TEC, utaona kwamba wao wanaamini katika rangi ya paka. Lakini, hili ni jambo ambalo vyama vinatakiwa kushindana na wapiga kura kuamua. Si jambo ambalo Kanisa linatakiwa kutoa maelekezo – nikimnukuu Pengo; “wanajua nini” kuhusu paka au rangi yake?

Hekima ya Kidini

Wakati TEC ikitoa tamko lake, kulikuwa na dalili ya mgawanyiko wa kidini kuhusu jambo hili la uwekezaji kwenye bandari kupitia kampuni ya DP World kutoka Dubai. Busara ya kawaida kabisa, ilihitaji TEC kufanya tafakuri jadidi kuhusu ni wakati gani na namna gani wangeweza kutoa waraka wao.

Kwa mfano, wapo Waislamu wanaoamini kwamba Kanisa Katoliki limekuwa na utaratibu wa kuwa “wakali” zaidi wakati Rais anapokuwa Mwislamu kuliko Rais anapokuwa Mkristo. Kwamba Rais Samia Suluhu Hassan anakosolewa na kuandikiwa waraka kwa sababu za kidini zaidi kuliko suala lenyewe la uwekezaji.

Na wanatumia mifano kadhaa. Kwamba wakati wa utawala wa Mkapa – aliyekuwa Mkatoliki, Kanisa halikuwahi kutoa waraka wa kusomwa makanisani kuhusu kupinga ubinafsishaji wa viwanda, mabenki na mali nyingine za umma uliofanyika wakati wa utawala wake. Mkapa ndiye Rais aliyebinafsisha mali nyingi za umma kuliko mwingine yeyote.

Hata uwekezaji wa kwanza binafsi kufanywa kwenye Bandari ya Dar es Salaam kupitia kampuni ya TICTS ulifanyika wakati wa utawala wa Mkapa. Wanaoamini kuhusu ukali wa Maaskofu kwa marais Waislamu wanatoa pia mfano wa utawala wa Rais Jakaya Kikwete ambapo matamko ya namna hii takribani matatu yalitolewa wakati wake. Enzi za Magufuli, waraka ulitoka mmoja – na bado Mkatoliki anayesheshimika na maarufu zaidi alikwenda hadharani kuukosoa.

Kwenye mazingira ya namna hii, kulikuwa na namna bora zaidi ya kuwasilisha waraka huu. Namna hiyo ilikuwa ni kushirikisha wadau wengine kutoka Baraza Kuu la Waislamu Tanzania (Bakwata) na Jumuiya ya Kikristo Tanzania (CCT) . Na hili liliwezekana kwa sababu TEC wenyewe kwenye waraka wao wameonyesha kwamba wamewahi kukutana na Rais Samia kwa umoja wao kujadili kuhusu suala hili Juni mwaka huu.

Sasa, kama TEC, CCT na Bakwata walikutana na Rais kwa umoja wao na kuna mambo ya msingi walikubaliana naye – ilikuwaje waraka huo ukatoka wa dhehebu moja katika mazingira ambayo infahamika kuna kundi linaamini Wakatoliki huwa hawatendi haki kwa Rais Mwislamu? Siku chache baada ya waraka kusomwa kwenye makanisa ya Wakatoliki, Mkuu wa KKKT, Askofu Frederick Shoo, alizungumza hadharani kueleza kuwa bado wana imani kuwa Rais atatekeleza yale waliyokubaliana.

Inawezekana Askofu Shoo pia hakubaliani na spidi ya serikali kwenye utekelezaji wa masuala waliyokubaliana lakini pengine busara ilimfanya ajiepushe na kuweka msimamo mkali wa kanisa lake wakati huu – au akijua kwamba jambo hilo linaweza kuwagawa zaidi wananchi kuliko kupata kile wanachotarajia kukipata.

Bakwata – kwa upande wao, hawajasema chochote, kama ambavyo hakukuwa na taarifa iliyotolewa mara baada ya mkutano baina ya Rais Samia na wawakilishi wa TEC, KKKT na Bakwata. Labda kauli ya Bakwata kuunga mkono wakati huu ingeonekana kama kumuunga mkono Rais Mwislamu dhidi ya Kanisa, au pengine wakati sahihi wa kutoa matamko haujafika.

Kwa bahati nzuri, wenzetu Waislamu wana msemo mmoja maarufu kuhusu tabia ya kusubiri; Innallaha Ma Sabireen (Wamejaaliwa wale wenye Subra). Pengine subra, si jambo jepesi kwa kila mtu – na labda kwa kila dhehebu la dini.

Mwandishi ni Msomi wa Masuala ya Maridhiano ya Kisiasa mwenye Shahada ya Uzamili katika African Politics kutoka Chuo Kikuu cha London School of Oriental and African Studies (SOAS) nchini Uingereza. Anapatikana kupitia email: ekamwaga57@gmail.com
Hivi wewe una maana gani? Issue ya mwaka 2018 unaileta leo ili ionekane ni kuwa ni hii ya kuhusu Bandari. Ukweli ni kuwa kuhusu tamko la juzi, Mwadhama Cardinal Pengo hakuwemo maana ni Askofu Mstaafu. Kwa rejea lipo hapo chini
 

Attachments

  • TAMKO PDF.pdf
    2.2 MB · Views: 1
Habari za Pasaka

Ongelea tamko la TEC juu ya mkataba feki wa Bandari we vipi
Kwani la bandari ni tamko la kwanza kulitoa ?!!!

Hatuwezi kuwazuia wala kuwapinga kutoa matamko bali tunaangalia "contents" ya matamko tu

Enheeee shem kwa hiyo maaskofu wakaighushi saini ya mhashamu P.P ?!!!
 
Huwa sihami kwenye hoja hata siku moja. Nilichokujibu ndicho. Huyo mwandishi wenu ameumba story ambayo haikuwahi kuwepo ili apate pa kusimamia kuijenga hoja yake.


Kwa hiyo amemzushia mhashamu Pengo ?!!

Duuh yaani unatulazimisha 2+2=7 ?!!!

Kamwaga kawabana "P M B U"....
 
Huyu ndiye Kamarada Ezekiel Kamwaga nimjuaye

Huyu ndiye mjamaa mwenzangu wa kweli nimjuaye

Hakika amefunguka KISOMI....

"...mwaka 2018 baada ya waraka ule wa TEC ,Kardinal P.Pengo alisema kuwa "alichomekwa bila ya yeye kujua"

Hebu jiulize watu wanaweza mpaka "kumchomeka" kiongozi wao mkuu ili tu sisi wanywa Wanzuki tuone kuwa ni msimamo mmoja wa kanisa....hatari sana hili....

Na ndio maana hayati baba wa taifa akakataa TAIFA LENYE DINI....resty easy El Commandante JKN ,amen

#Nchi Kwanza kabla yangu mimi Mkunazi Njiwa

#Dini ya taifa hili ni amani ,utulivu na uwepo wake bila ya baguzi za KIDINI ,KIKABILA NA KIKANDA

#Mh.Rais SSH atapita ila JMT itabaki milele dumu

#SiempreJMT
Chezea bahasha toka DP world weye 🤣🤣 ni mwendo wa mapambio tu 😂😂
 
Wanatengenezo story wapate kusimika hoja zao. Pengo alitofautiana na wenzake lakini hakuwahi kukataa kushiriki kuuandika ule Waraka bali alileta siasa tu.

Alileta siasa ?!!!

Unatufanya wanaJF kuwa watoto wa kubugizwa "ubuge"?!!

Hamtoki humu...

Humu Jandoni hamtoki na mazunga yenu....chaliii

Baada ya kupitishwa jandoni karibu Wanzuki
 
Kwani huyu Kamwaga alitakaje ? Wasitoe waraka ? Pili, Kamwaga anasemaje juu ya zile hoja 8 ndani ya waraka? Achilia mbali wawe wanaelewa wote au wachache ? Tuwe makini na akili za tumbo
....hoja ni KUGHUSHIWA kwa ile saini....
 

Kwa Nini Waandishi Mahiri wa Safu Wanapungua?​

By Ezekiel Kamwaga|Published On: November 9, 2018|Categories: Articles|1 Comment

1-2.png

Kwa Nini Waandishi wa Safu Wanapungua?
Na Ezekiel Kamwaga
MIAKA kumi ya utawala wa Rais Jakaya Kikwete itakumbukwa kwa kuwa na kada maarufu ya waandishi wa safu mahiri ambao waliongeza sana mauzo ya magazeti na kulisha maarifa na taarifa mbalimbali kwa wasomaji wake.

Ingawa ni utawala wa Ali Hassan Mwinyi ndiyo uliofungua milango kwa vyombo vya habari binafsi kufanya kazi zake, kilele cha utendaji na kufahamika kwake kilikuwa wakati wa utawala wa Kikwete ambapo mitandao ya kijamii ilisaidia kupaisha umaarufu wa waandishi hao wa safu.

Katika miaka ya awali ya Rais Mwinyi, waandishi kama Stanley Kamana (RIP), Ndimara Tegambwage, na Kajubi Mukajanga walikuwa maarufu kwa sababu ya kazi zao murua kwa wasomaji.

Kwenye utawala wa Rais Benjamin Mkapa, gazeti maarufu zaidi lilikuwa RAI ambapo wanasafu kama Jenerali Ulimwengu, John Rutayisingwa (RIP), Johnson Mbwambo, na wengine wengi walikuwa wakitimiza wajibu wao wa kiuandishi ipasavyo.

Kuna wakati watu walikuwa hawanunui RAI kwa sababu ya kilichoandikwa nje (habari) bali walinunua kwa sababu walitaka kuwasoma wanasafu mahiri waliomo ndani.

Sitasahau namna watu walivyokuwa wakinunua RAI mwaka 2005 wakati Mhariri Mtendaji wa Habari Corporation wakati huo, Salva Rweyemamu, alipokuwa akifanya uchambuzi wa wasifu wa waliokuwa wamejitokeza kutaka kuwania urais wa Tanzania kupitia CCM.

Kwenye utawala wa Kikwete, magazeti yaliyokuwa na wasomaji wengi kwa sababu ya wanasafu yalikuwa ni MwanaHALISI, Raia Mwema, na Tanzania Daima ambapo waandishi kama Privatus Karugendo, Joseph Mihangwa, Ansbert Ngurumo, Ulimwengu, Msomaji Raia, M.M Mwanakijiji, Saed Kubenea, na wengine walijipambanua kwa uandishi wao wenye kalamu kali.
1-5.jpg

Katika utawala wa Rais John Magufuli – walau kwa miaka hii mitatu ya kwanza, hakuna gazeti jipya wala wanasafu wapya waliojitokeza katika magazeti wanaosisimua watu kama ilivyokuwa huko nyuma.

Kimsingi, kama kuna mtu anayesomwa na watu wengi hivi sasa basi atakuwa ni Mange Kimambi ambaye si mwandishi kitaaluma lakini anaandika taarifa zake kupitia mitandao ya kijamii.

Mimi ninaamini kwamba umaarufu wa Mange unatokana na hali halisi iliyopo nyumbani. Wakati wa utawala wa Kikwete kulikuwa na Bunge lililooneshwa mubashara, vyama vya siasa viliweza kuzunguka mikoani kufanya kampeni na vyombo vya habari vilikuwa na uhuru mkubwa zaidi wa kukosoa kuliko ilivyo sasa.

Kwa sababu hali hiyo ya uhuru imebadilika hapa nchini, mfumo umeamua kutafuta njia nyingine ya kupumua ambayo sasa ndiyo amekuwa Kimambi. Mange alikuwa anaandika tangu wakati Kikwete akiwa madarakani lakini hakuwa maarufu sana kwa sababu aliyokuwa akiyasema yalikuwa yakisemwa hapa pia.
3.png

Hata hivyo, hii ni mada nyingine tofauti na mada ya leo. Turejee kwenye hoja yangu mahususi kuhusu kupotea kwa wale wanasafu mashuhuri au kupungua kwa makali ya safu zao.

Hakuna sababu moja pekee ambayo ndiyo imesababisha wanasafu wapungue. Nimekuwa nikiulizwa maswali kuhusu kutoonekana kwa Mbwambo kwenye gazeti la Raia Mwema lakini huyu ni mwandishi ambaye aliaga kabisa wakati akiandika makala yake ya mwisho.

Mbwambo ambaye ni mmoja wa wakurugenzi wa kampuni ya Raia Mwema, ameamua kwenda kuishi kijijini kwao wilayani Same mkoani Kilimanjaro tangu mwaka 2015. Huu ni uamuzi wa tofauti na wengine.

Wapo wanasafu ambao wameacha kuandika kwa sababu malipo wanayopewa na vyombo vya habari vya hapa nchini ni kiduchu na mbaya zaidi sasa hawalipwi kwa wakati au hawalipwi kabisa.

Vyombo vya habari vya Tanzania vinapita katika kipindi kigumu kimapato na hivyo vingi vinashindwa hata kulipa mishahara wafanyakazi wake.

Chukulia kampuni kama Sahara Communications ambayo ina tatizo la mishahara kwa wafanyakazi wake kwa takribani miaka miwili sasa.
1-6.jpg

Kampuni ambayo haiwezi kuwalipa wafanyakazi wake, inawezaje kuwalipa wanasafu ambao mara nyingi si waajiriwa wake? Kwa sababu ya kutolipwa, wapo wanasafu ambao wameamua kuacha kuandika ili kutumia muda wao kufanya mambo mengine.

Wanasafu wengine hawaonekani kwenye magazeti kwa sababu magazeti ambayo yangeweza kukubaliana na uandishi wao yamefungiwa na serikali. Wiki moja iliyopita nilikutana na aliyekuwa Mhariri wa MwanaHALISI, Jabir Idrissa, ambaye alinieleza kwamba kwa mwaka mzima sasa amekosa nafasi kwenye magazeti kwa sababu makala zake ‘zinaogopwa’ kwa kuwa zinaweza kusababisha gazeti kufungiwa. Kwa hiyo, kama huoni makala za Jabir Idrissa, ujue sababu mojawapo ni hiyo.

Wapo pia wanasafu ambao wameamua kuacha kuandika kwa kuhofia kwamba wanaweza kuingia matatizoni na vyombo vya dola. Wameamua kutulia hadi pale watakapoona mazingira yamebadilika.

Kuna mwanasafu mmoja mashuhuri ambaye ameacha kuandika kwa madai kwamba siku hizi akiandika, makala zake huwa zinahaririwa kiasi cha kubadili kabisa alichotaka kukisema.

Badala ya kuandika na kushuhudia makala zake zikibomolewa na kuundwa upya, ameamua aache kuandika ili abaki na heshima yake ya nyuma.
2-4.jpg

Wapo wanasafu ambao sasa wamepata vyeo serikalini na kwa sababu hiyo hawawezi tena kuendelea na aina yao ya uandishi wa kukosoa iliyowapa umaarufu huko nyuma.

Kimsingi, kila anayepunguza makali au kuacha kabisa kuandika ana mojawapo ya sababu nilizozitaja hapo juu.
 
Hivi wewe una maana gani? Issue ya mwaka 2018 unaileta leo ili ionekane ni kuwa ni hii ya kuhusu Bandari. Ukweli ni kuwa kuhusu tamko la juzi, Mwadhama Cardinal Pengo hakuwemo maana ni Askofu Mstaafu. Kwa rejea lipo hapo chini
....msomi asifanye REJEA kuntu kisa ni mwaka 2018 ?!!

Kamarada Kamwaga ameeleweka na wenye kutaka kumuelewa.....endelea kuandamana...ameshapita kisu na "zunga" amebaki nalo
 
Ni jukumu letu kuaminii kuwa watanzania wana uelewa au bado wapo gizani. Na je upande uliochagua upo sahiihi au kwa sababu flanni
 
Ni vema Kamwaga ajikite kwenye hoja za maaskofu na mkataba baina ya Tanzania na Dubai. Suala la kuchambua uelewa wa askofu mmoja mmoja halimuhusu. Kamwaga akumbuke kuwa hata ndani ya serikali kuna uwajibikaji wa pamoja hivyo siyo kila hoja lazima wote wakubaliane lakini wanapokubali wengi hoja ni ya wote!
 
Chezea bahasha toka DP world weye ni mwendo wa mapambio tu
Nina miezi 6 sijanywa bia....unadhani ninapenda kila siku kuwa na chupa hii ya shengena iliyo mbele yangu hapa ubandani?!!!

Hakuna cha bahasha bali ni ujamaa wangu wa kiafrika na mapenzi yangu makubwa juu ya uadhimu kuntu wa taifa hili
 
Na Ezekiel Kamwaga

KUELEKEA kipindi cha Kwaresma na Sikukuu ya Pasaka ya mwaka 2018, Baraza la Maaskofu wa Katoliki Tanzania (TEC) lilitoa waraka ambao kimsingi ulikosoa vitendo vya uminyaji wa demokrasia na uhuru wa watu kujieleza uliokuwepo wakati wa utawala wa hayati Rais John Magufuli.

Waraka ule ulikuwa na sehemu nne lakini sehemu iliyozua mjadala zaidi ilikuwa ni sehemu ya tatu iliyokuwa na kichwa cha habari kisemacho; “Dalili za Nyakati Zetu Tanzania” ambapo pamoja na mambo mengine, Maaskofu walieleza kutofurahishwa kwao na maandamano na mikutano ya kisiasa kuzuiwa na vyombo vya dola huku vyombo vya habari vikifungiwa.

Siku chache baadaye, Mwadhama Polycarp Kadinali Pengo, alizungumza na vyombo vya habari na kutoa maelezo yaliyokuwa na sura ya kutokubaliana na waraka ule. Kwanza alisema kwamba hakuwa anajua chochote kilichoandikwa ndani ya waraka ule na kwamba jina lake alilikuta tu kwenye lile tamko. Na pili, Pengo ambaye pengine alikuwa ndiye Mkatoliki mashuhuri na anayeheshimika zaidi nchini, alieleza kutokubaliana na yaliyomo kwenye waraka ule – hasa masuala yasiyo ya kidini yaliyojumuishwa humo.

Kuna mambo makubwa mawili ambayo tunaweza kujifunza kutoka kwenye maelezo hayo ya Pengo wakati tukianza kudadavua waraka wa hivi karibuni uliotolewa na TEC kuhusu suala zima la mkataba wa uendeshaji wa bandari za hapa nchini baina ya Serikali ya Tanzania na Dubai.

La kwanza ni kwamba waraka wa TEC si neno la Mungu. Kama ingekuwa waraka huo ni neno, mtu wa hadhi ya Kadinali Pengo asingeweza kutoka hadharani na kueleza mapungufu ya waraka wa mwaka 2018. Mwadhama Pengo ni mlinzi wa imani ya Kikatoliki na kwa vyovyote vile asingeweza kupingana na jambo lenye kulinda imani au la maelekezo ya Kimungu.

Jambo la pili linahusu wanaosaini waraka. Maelezo ya Pengo yalitufundisha kwamba unapoona waraka umesainiwa na Maaskofu 37 – kama ilivyokuwa kwa waraka uliosomwa kwa waumini Wakatoliki kwenye makanisa ya Tanzania Jumapili iliyopita, si lazima Maaskofu wote wawe wanajua kilichomo. Inawezekana kazi hiyo imefanywa na Maaskofu wachache tu – na wengine hawakujua chochote hadi waraka huo ulipojitokeza; kwanza kwenye vyombo vya habari na pili makanisani.

Na Mwadhama alikuwa na swali moja muhimu alilouliza TEC baada ya waraka ule wa mwaka 2018; kwamba Maaskofu wanajua nini kuhusu haki za kidemokrasia na kubana uhuru wa watu kujieleza? Pengo aliwaambia waandishi wa habari kwamba hayo si maeneo ambayo viongozi wa dini wanayajua zaidi kuliko wanasiasa na vyama vya siasa.

Ndilo swali ambalo pia nadhani Kadinali Pengo angeuliza kuhusu waraka huu wa TEC wa wiki iliyopita. Kwamba Maaskofu wanajua nini kuhusu masuala ya uendeshaji wa bandari? Wanajua nini kuhusu masuala ya haki za kibiashara za Tanzania na nchi nyingine kwenye uwekezaji?

Hili ni swali muhimu kwa sababu; kama Maaskofu wakianza kuhoji kuhusu uwekezaji bandarini, mpaka wa kuhoji utaishia wapi? Nini kitawafanya wasihoji kuhusu gharama za ujenzi wa Reli ya SGR au Bwawa la Mwalimu Nyerere? Kama wanaruhusiwa kuhoji uwekezaji bandarini, nini kitawazuia wasihoji kuhusu bei za korosho na kahawa kwa wakulima?

Hofu kubwa ya Pengo wakati ule – na naamini ndiyo hofu kubwa ya baadhi yetu kwenye waraka huu wa Maaskofu ni kwamba, Tanzania imebaki kuwa nchi ya mfano kwa Umoja na Amani yetu kwa sababu ya mgawanyo mzuri wa majukumu baina ya masuala ya kiserikali na yale ya kidini.

Kama Serikali ingekuwa imetangaza Jumapili kuwa siku ya kazi na watu hawataruhusiwa kwenda kanisani, waraka wa TEC kupinga hilo na kuusambaza na kusomwa makanisani lingekuwa jambo linaloingia kichwani. Kama Serikali ingelazimisha watu kufanya mambo ambayo ni kinyume cha misingi na imani ya kidini, waraka ungekuwa na maana kubwa.

Lakini suala la uwekezaji tayari lina mijadala yake kupitia itikadi za vyama. Ziko itikadi zinazoamini kwamba uchumi wa unatakiwa kumilikiwa na dola na watu wake na ziko itikadi za kisiasa zinazoamini uchumi unatakiwa kuamuliwa na nguvu ya soko. Rais wa Awamu ya Tatu, hayati Benjamin Mkapa, aliliweka hili vema kwa kutumia mfano wa paka.

Akimnukuu Kiongozi wa zamani wa China, Deng Xiaoping, Mkapa alisema yeye ni mfuasi wa kuamini kwamba cha msingi ni kuona paka anakamata panya na si paka ni wa rangi gani. Kuna wengine, wanaamini kwamba rangi ya paka ni muhimu kwenye kukamata panya. Ukisoma tamko la TEC, utaona kwamba wao wanaamini katika rangi ya paka. Lakini, hili ni jambo ambalo vyama vinatakiwa kushindana na wapiga kura kuamua. Si jambo ambalo Kanisa linatakiwa kutoa maelekezo – nikimnukuu Pengo; “wanajua nini” kuhusu paka au rangi yake?

Hekima ya Kidini

Wakati TEC ikitoa tamko lake, kulikuwa na dalili ya mgawanyiko wa kidini kuhusu jambo hili la uwekezaji kwenye bandari kupitia kampuni ya DP World kutoka Dubai. Busara ya kawaida kabisa, ilihitaji TEC kufanya tafakuri jadidi kuhusu ni wakati gani na namna gani wangeweza kutoa waraka wao.

Kwa mfano, wapo Waislamu wanaoamini kwamba Kanisa Katoliki limekuwa na utaratibu wa kuwa “wakali” zaidi wakati Rais anapokuwa Mwislamu kuliko Rais anapokuwa Mkristo. Kwamba Rais Samia Suluhu Hassan anakosolewa na kuandikiwa waraka kwa sababu za kidini zaidi kuliko suala lenyewe la uwekezaji.

Na wanatumia mifano kadhaa. Kwamba wakati wa utawala wa Mkapa – aliyekuwa Mkatoliki, Kanisa halikuwahi kutoa waraka wa kusomwa makanisani kuhusu kupinga ubinafsishaji wa viwanda, mabenki na mali nyingine za umma uliofanyika wakati wa utawala wake. Mkapa ndiye Rais aliyebinafsisha mali nyingi za umma kuliko mwingine yeyote.

Hata uwekezaji wa kwanza binafsi kufanywa kwenye Bandari ya Dar es Salaam kupitia kampuni ya TICTS ulifanyika wakati wa utawala wa Mkapa. Wanaoamini kuhusu ukali wa Maaskofu kwa marais Waislamu wanatoa pia mfano wa utawala wa Rais Jakaya Kikwete ambapo matamko ya namna hii takribani matatu yalitolewa wakati wake. Enzi za Magufuli, waraka ulitoka mmoja – na bado Mkatoliki anayesheshimika na maarufu zaidi alikwenda hadharani kuukosoa.

Kwenye mazingira ya namna hii, kulikuwa na namna bora zaidi ya kuwasilisha waraka huu. Namna hiyo ilikuwa ni kushirikisha wadau wengine kutoka Baraza Kuu la Waislamu Tanzania (Bakwata) na Jumuiya ya Kikristo Tanzania (CCT) . Na hili liliwezekana kwa sababu TEC wenyewe kwenye waraka wao wameonyesha kwamba wamewahi kukutana na Rais Samia kwa umoja wao kujadili kuhusu suala hili Juni mwaka huu.

Sasa, kama TEC, CCT na Bakwata walikutana na Rais kwa umoja wao na kuna mambo ya msingi walikubaliana naye – ilikuwaje waraka huo ukatoka wa dhehebu moja katika mazingira ambayo infahamika kuna kundi linaamini Wakatoliki huwa hawatendi haki kwa Rais Mwislamu? Siku chache baada ya waraka kusomwa kwenye makanisa ya Wakatoliki, Mkuu wa KKKT, Askofu Frederick Shoo, alizungumza hadharani kueleza kuwa bado wana imani kuwa Rais atatekeleza yale waliyokubaliana.

Inawezekana Askofu Shoo pia hakubaliani na spidi ya serikali kwenye utekelezaji wa masuala waliyokubaliana lakini pengine busara ilimfanya ajiepushe na kuweka msimamo mkali wa kanisa lake wakati huu – au akijua kwamba jambo hilo linaweza kuwagawa zaidi wananchi kuliko kupata kile wanachotarajia kukipata.

Bakwata – kwa upande wao, hawajasema chochote, kama ambavyo hakukuwa na taarifa iliyotolewa mara baada ya mkutano baina ya Rais Samia na wawakilishi wa TEC, KKKT na Bakwata. Labda kauli ya Bakwata kuunga mkono wakati huu ingeonekana kama kumuunga mkono Rais Mwislamu dhidi ya Kanisa, au pengine wakati sahihi wa kutoa matamko haujafika.

Kwa bahati nzuri, wenzetu Waislamu wana msemo mmoja maarufu kuhusu tabia ya kusubiri; Innallaha Ma Sabireen (Wamejaaliwa wale wenye Subra). Pengine subra, si jambo jepesi kwa kila mtu – na labda kwa kila dhehebu la dini.

Mwandishi ni Msomi wa Masuala ya Maridhiano ya Kisiasa mwenye Shahada ya Uzamili katika African Politics kutoka Chuo Kikuu cha London School of Oriental and African Studies (SOAS) nchini Uingereza. Anapatikana kupitia email: ekamwaga57@gmail.com
Unajua kilichomkuta Pengo kwa hatua ile, au unadhani alistaafu? Kuna usichokijua.
Wenzio wale hawakurupuki ,
Baraza la Maaskofu lina mfumo na misingi yake kwenye kufikia maamuzi ya pamoja.
 
Na Ezekiel Kamwaga

KUELEKEA kipindi cha Kwaresma na Sikukuu ya Pasaka ya mwaka 2018, Baraza la Maaskofu wa Katoliki Tanzania (TEC) lilitoa waraka ambao kimsingi ulikosoa vitendo vya uminyaji wa demokrasia na uhuru wa watu kujieleza uliokuwepo wakati wa utawala wa hayati Rais John Magufuli.

Waraka ule ulikuwa na sehemu nne lakini sehemu iliyozua mjadala zaidi ilikuwa ni sehemu ya tatu iliyokuwa na kichwa cha habari kisemacho; “Dalili za Nyakati Zetu Tanzania” ambapo pamoja na mambo mengine, Maaskofu walieleza kutofurahishwa kwao na maandamano na mikutano ya kisiasa kuzuiwa na vyombo vya dola huku vyombo vya habari vikifungiwa.

Siku chache baadaye, Mwadhama Polycarp Kadinali Pengo, alizungumza na vyombo vya habari na kutoa maelezo yaliyokuwa na sura ya kutokubaliana na waraka ule. Kwanza alisema kwamba hakuwa anajua chochote kilichoandikwa ndani ya waraka ule na kwamba jina lake alilikuta tu kwenye lile tamko. Na pili, Pengo ambaye pengine alikuwa ndiye Mkatoliki mashuhuri na anayeheshimika zaidi nchini, alieleza kutokubaliana na yaliyomo kwenye waraka ule – hasa masuala yasiyo ya kidini yaliyojumuishwa humo.

Kuna mambo makubwa mawili ambayo tunaweza kujifunza kutoka kwenye maelezo hayo ya Pengo wakati tukianza kudadavua waraka wa hivi karibuni uliotolewa na TEC kuhusu suala zima la mkataba wa uendeshaji wa bandari za hapa nchini baina ya Serikali ya Tanzania na Dubai.

La kwanza ni kwamba waraka wa TEC si neno la Mungu. Kama ingekuwa waraka huo ni neno, mtu wa hadhi ya Kadinali Pengo asingeweza kutoka hadharani na kueleza mapungufu ya waraka wa mwaka 2018. Mwadhama Pengo ni mlinzi wa imani ya Kikatoliki na kwa vyovyote vile asingeweza kupingana na jambo lenye kulinda imani au la maelekezo ya Kimungu.

Jambo la pili linahusu wanaosaini waraka. Maelezo ya Pengo yalitufundisha kwamba unapoona waraka umesainiwa na Maaskofu 37 – kama ilivyokuwa kwa waraka uliosomwa kwa waumini Wakatoliki kwenye makanisa ya Tanzania Jumapili iliyopita, si lazima Maaskofu wote wawe wanajua kilichomo. Inawezekana kazi hiyo imefanywa na Maaskofu wachache tu – na wengine hawakujua chochote hadi waraka huo ulipojitokeza; kwanza kwenye vyombo vya habari na pili makanisani.

Na Mwadhama alikuwa na swali moja muhimu alilouliza TEC baada ya waraka ule wa mwaka 2018; kwamba Maaskofu wanajua nini kuhusu haki za kidemokrasia na kubana uhuru wa watu kujieleza? Pengo aliwaambia waandishi wa habari kwamba hayo si maeneo ambayo viongozi wa dini wanayajua zaidi kuliko wanasiasa na vyama vya siasa.

Ndilo swali ambalo pia nadhani Kadinali Pengo angeuliza kuhusu waraka huu wa TEC wa wiki iliyopita. Kwamba Maaskofu wanajua nini kuhusu masuala ya uendeshaji wa bandari? Wanajua nini kuhusu masuala ya haki za kibiashara za Tanzania na nchi nyingine kwenye uwekezaji?

Hili ni swali muhimu kwa sababu; kama Maaskofu wakianza kuhoji kuhusu uwekezaji bandarini, mpaka wa kuhoji utaishia wapi? Nini kitawafanya wasihoji kuhusu gharama za ujenzi wa Reli ya SGR au Bwawa la Mwalimu Nyerere? Kama wanaruhusiwa kuhoji uwekezaji bandarini, nini kitawazuia wasihoji kuhusu bei za korosho na kahawa kwa wakulima?

Hofu kubwa ya Pengo wakati ule – na naamini ndiyo hofu kubwa ya baadhi yetu kwenye waraka huu wa Maaskofu ni kwamba, Tanzania imebaki kuwa nchi ya mfano kwa Umoja na Amani yetu kwa sababu ya mgawanyo mzuri wa majukumu baina ya masuala ya kiserikali na yale ya kidini.

Kama Serikali ingekuwa imetangaza Jumapili kuwa siku ya kazi na watu hawataruhusiwa kwenda kanisani, waraka wa TEC kupinga hilo na kuusambaza na kusomwa makanisani lingekuwa jambo linaloingia kichwani. Kama Serikali ingelazimisha watu kufanya mambo ambayo ni kinyume cha misingi na imani ya kidini, waraka ungekuwa na maana kubwa.

Lakini suala la uwekezaji tayari lina mijadala yake kupitia itikadi za vyama. Ziko itikadi zinazoamini kwamba uchumi wa unatakiwa kumilikiwa na dola na watu wake na ziko itikadi za kisiasa zinazoamini uchumi unatakiwa kuamuliwa na nguvu ya soko. Rais wa Awamu ya Tatu, hayati Benjamin Mkapa, aliliweka hili vema kwa kutumia mfano wa paka.

Akimnukuu Kiongozi wa zamani wa China, Deng Xiaoping, Mkapa alisema yeye ni mfuasi wa kuamini kwamba cha msingi ni kuona paka anakamata panya na si paka ni wa rangi gani. Kuna wengine, wanaamini kwamba rangi ya paka ni muhimu kwenye kukamata panya. Ukisoma tamko la TEC, utaona kwamba wao wanaamini katika rangi ya paka. Lakini, hili ni jambo ambalo vyama vinatakiwa kushindana na wapiga kura kuamua. Si jambo ambalo Kanisa linatakiwa kutoa maelekezo – nikimnukuu Pengo; “wanajua nini” kuhusu paka au rangi yake?

Hekima ya Kidini

Wakati TEC ikitoa tamko lake, kulikuwa na dalili ya mgawanyiko wa kidini kuhusu jambo hili la uwekezaji kwenye bandari kupitia kampuni ya DP World kutoka Dubai. Busara ya kawaida kabisa, ilihitaji TEC kufanya tafakuri jadidi kuhusu ni wakati gani na namna gani wangeweza kutoa waraka wao.

Kwa mfano, wapo Waislamu wanaoamini kwamba Kanisa Katoliki limekuwa na utaratibu wa kuwa “wakali” zaidi wakati Rais anapokuwa Mwislamu kuliko Rais anapokuwa Mkristo. Kwamba Rais Samia Suluhu Hassan anakosolewa na kuandikiwa waraka kwa sababu za kidini zaidi kuliko suala lenyewe la uwekezaji.

Na wanatumia mifano kadhaa. Kwamba wakati wa utawala wa Mkapa – aliyekuwa Mkatoliki, Kanisa halikuwahi kutoa waraka wa kusomwa makanisani kuhusu kupinga ubinafsishaji wa viwanda, mabenki na mali nyingine za umma uliofanyika wakati wa utawala wake. Mkapa ndiye Rais aliyebinafsisha mali nyingi za umma kuliko mwingine yeyote.

Hata uwekezaji wa kwanza binafsi kufanywa kwenye Bandari ya Dar es Salaam kupitia kampuni ya TICTS ulifanyika wakati wa utawala wa Mkapa. Wanaoamini kuhusu ukali wa Maaskofu kwa marais Waislamu wanatoa pia mfano wa utawala wa Rais Jakaya Kikwete ambapo matamko ya namna hii takribani matatu yalitolewa wakati wake. Enzi za Magufuli, waraka ulitoka mmoja – na bado Mkatoliki anayesheshimika na maarufu zaidi alikwenda hadharani kuukosoa.

Kwenye mazingira ya namna hii, kulikuwa na namna bora zaidi ya kuwasilisha waraka huu. Namna hiyo ilikuwa ni kushirikisha wadau wengine kutoka Baraza Kuu la Waislamu Tanzania (Bakwata) na Jumuiya ya Kikristo Tanzania (CCT) . Na hili liliwezekana kwa sababu TEC wenyewe kwenye waraka wao wameonyesha kwamba wamewahi kukutana na Rais Samia kwa umoja wao kujadili kuhusu suala hili Juni mwaka huu.

Sasa, kama TEC, CCT na Bakwata walikutana na Rais kwa umoja wao na kuna mambo ya msingi walikubaliana naye – ilikuwaje waraka huo ukatoka wa dhehebu moja katika mazingira ambayo infahamika kuna kundi linaamini Wakatoliki huwa hawatendi haki kwa Rais Mwislamu? Siku chache baada ya waraka kusomwa kwenye makanisa ya Wakatoliki, Mkuu wa KKKT, Askofu Frederick Shoo, alizungumza hadharani kueleza kuwa bado wana imani kuwa Rais atatekeleza yale waliyokubaliana.

Inawezekana Askofu Shoo pia hakubaliani na spidi ya serikali kwenye utekelezaji wa masuala waliyokubaliana lakini pengine busara ilimfanya ajiepushe na kuweka msimamo mkali wa kanisa lake wakati huu – au akijua kwamba jambo hilo linaweza kuwagawa zaidi wananchi kuliko kupata kile wanachotarajia kukipata.

Bakwata – kwa upande wao, hawajasema chochote, kama ambavyo hakukuwa na taarifa iliyotolewa mara baada ya mkutano baina ya Rais Samia na wawakilishi wa TEC, KKKT na Bakwata. Labda kauli ya Bakwata kuunga mkono wakati huu ingeonekana kama kumuunga mkono Rais Mwislamu dhidi ya Kanisa, au pengine wakati sahihi wa kutoa matamko haujafika.

Kwa bahati nzuri, wenzetu Waislamu wana msemo mmoja maarufu kuhusu tabia ya kusubiri; Innallaha Ma Sabireen (Wamejaaliwa wale wenye Subra). Pengine subra, si jambo jepesi kwa kila mtu – na labda kwa kila dhehebu la dini.

Mwandishi ni Msomi wa Masuala ya Maridhiano ya Kisiasa mwenye Shahada ya Uzamili katika African Politics kutoka Chuo Kikuu cha London School of Oriental and African Studies (SOAS) nchini Uingereza. Anapatikana kupitia email: ekamwaga57@gmail.com
mtoa mada we ni stupid! Yan pengo umeona ndo wa kumtolea mfano humu! We hujui kama mtu akizeeka sana akili yake inachanganyikiwa? Hujiuliz why now kuna cardinal mpya? Yule now n kama mtoto wa miaka saba! Muachen apumzke
 
Unajua kilichomkuta Pengo kwa hatua ile, au unadhani alistaafu? Kuna usichokijua.
Wenzio wale hawakurupuki ,
Baraza la Maaskofu lina mfumo na misingi yake kwenye kufikia maamuzi ya pamoja.
Mkuu naomba uelewe kuwa Mungu hajawahi kuumba kiumbe kinaitwa Askofu
 
Back
Top Bottom