Tamko la Serikali dhidi ya Reginald Mengi na Rostam Aziz

mnozya

JF-Expert Member
Feb 25, 2009
207
44
Wakuu JF.

Nimesoma kwenye mtandao kuwa Tariki Azizi wa TZ leo angetoa tamko la Serikali Kuhusu Mengi.

Tafadhali mlioko nyumbani tupasheni habari kama kalitoa na amesema nini.

=====

Rostam Na Mengi: Serikali Yatoa Tamko

MONDAY, MAY 11, 2009
1608032731052.png

Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni na Michezo Mh. Joel Bendera

SERIKALI imewataka Wafanyabiashara Rostam Aziz na Mwenyekiti wa Makampuni ya IPP, Reginald Mengi kuacha mara moja malumbano kati yao na kutotumia vyombo vyao vya habari kwa maslahi yao binafsi.

Sambamba na hilo imewataka kuwasilisha vielelezo na madai yao kwa mamlaka husika ili hatua zinazofaa zichukuliwe na wananchi wapewe taarifa na vyombo hivyo.

Akitoa tamko la serikali leo mbele ya waandishi wa habari, Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni na Michezo, Joel Bendera kwa niaba ya Waziri wake, George Mkuchika alisema serikali haitakubali kusikia malumbano hayo ambayo yanaweza kuleta uvunjifu wa amani nchini yakiendelea.

“Serikali imeyatafakari malumbano ya wafanyabiashara hawa na kubaini yanalipeleka taifa letu mahali pabaya kwani yana mwelekeo wa uvunjaji wa amani kama yataachwa kuendelea.

"…pia haitavumilia kuona vyombo vya habari nchini vikichangia kuligawa taifa katika makundi na kudumaza maendeleo”,alisema.

Badala yake amevitaka vyombo hivyo vya habari kutotomiwa kwa manufaa binafsi ya mmiliki au mtendaji; viongozwe na maadili ya taaluma na jamii husika na kisitangaze habari kwa misingi ya ubaguzi wa rangi, kabila, dini, jinsia au ulemavu na kuchochea uhasama.


 
Wakuu JF.

Nimesoma kwenye mtandao kuwa Tariki Azizi wa TZ leo angetoa tamko la Serikali Kuhusu Mengi.

Tafadhali mlioko nyumbani tupasheni habari kama kalitoa na amesema nini.

Kwenye mtandao wapi? Tariki Azizi wa TZ ndiye nani? Mbona vitu vinaelea ela tu?
 
Halafu wote wamehamia Busanda ,kutafuta ushindi unaoelekea kuiangukia CUF.
 
Tariq Aziz was a hell of an eloquent speaker. He was Saddam's mouthpiece on the international stage.

Sasa nani bongo unayemlinganisha na Tariq Aziz? Au unachanganya kati ya Comical Ali na Tariq Aziz?
 
Mkuchika ndio Tareq Aziz.ila anamsakizia Bendera leo ndio atatoa tamko rasmi.
 
Serikali imewalaumu Mengi na Rostam kwa kutumia vibaya vyombo vyao vya habari.

Wamepewa onyo na kuelezwa wakirudia tena wataadhibiwa
 
serikali imewalaumu mengi ya rostam kwa kutumia vibaya vyombo vyao vya habari. wamepewa onyo na kuelezwa wakirudia tena wataadhibiwa

serikali itawaadhibu vipi sasa hawa? kwa nini serikali iingilie malumbano ya watu? Miafrika bana....
 
BREAKING NEWS!!! TAMKO LA SERIKALI
JAMHURI VA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA HABARI, UTAMADUNI NA MICfIEZO


TAMKO LA SERIKALI KUHUSU MALUMBANO KATI YA MWENYEKITI MTENDAJI WA MAKAMPUNI YA IPP, BWANA REGINALD MENGI, NA MBUNGE WA IGUNGA, MHESHIMIWA ROSTAM AZIZ
1. Takribani wiki mbili sasa, kupitia vyombo mbalimbali vya habari, Taifa limegubikwa na malumbano makali kati ya wafanyabiashara wawili, Bwana Reginald Mengi, Mwenyekiti Mtendaji wa Makampuni ya IPP, na Mheshimiwa Rostam Aziz, Mbunge wa Igunga, malumbano ambayo yamejikita katika suala la Ufisadi na Mafisadi.
2. Wafanyabiashara hawa wawili, Bwana Reginald Mengi na Mheshimiwa Rostam Aziz, kwa nyakati tofauti, wametumia vyombo mbalimbali vya habari vikiwemo wanavyomiliki huku kila mmoja akimtuhumu rnwenziwe kuwa fisadi.
3. Kwa mfano, tarehe 23 Aprili, 2009, Bwana Reginald Mengi aliandaa Mkutano wa Waandishi wa Habari (Press Conference) ambapo aliyataja makampuni na wafanyabiashara watano wa hapa nchini, akiwamo Mheshimiwa Rostam Aziz, akiwaita kuwa ni "MAFISADI PAPA" na kuwaornba wananchi kuungana nave iIi kupambana na "mafisadi" hao.
4. Sikuchache baadaye.mmoja wa waliotajwa kuwa "Mafisadi Papa", Mheshimiwa Rostam Aziz, alijibu taarifa ya Bwana Mengi kupitia mkutano wa waandishi wa habari, akikanusha tuhul11a hizo. Aidha, alimtaja Bwana Reginald Mengi kuwa ni "FISADI NYANGUMI" na kuorodhesha tuhuma kadhaa za ufisadi zilizofanywa na Bwana Mengi.
5. Serikali imeyatafakari malumbano ya wafanyabiashara hawa na kubaini kwamba yanalipeleka Taifa letu mahali pabaya, kwani malumbano have yana mwelekeo wa uvunjaji wa amani kama yataachiwa kuendelea.

6. Ni Kweli kwamba Katiba ya Nchi yetu inatoa uhuru wa kila mwananchi kuongea, kutoa na kupokea habari; lakini I
7. Serikali imebaini kuwa malumbano ya Mheshimiwa Rostam Aziz na Bwana Reginald Mengi yamewagawa wailanchi katika makundi mawili; ya wale wanaounga mkono kauli ya Mheshimiwa Rostam Aziz, na wale wanounga mkono kauli ya Bwana Reginald Mengi.
8. Aidha, Serikali imebaini kwamba katika malumbano haya kumekuwepo na "matumizi mabaya" ya vyombo vya habari vinavyomilikiwa na Bwana Mengi, (televisheni, magazeti na radio), na kwa Mheshimiwa Rostam Aziz, (magazeti). Kila mmoja ametumia vyombo vya habari anavyomiliki kwa manufaa yake binafsi kinyume na maelekezo ya Sera ya Habari na Utangazaji ya Mwaka 2003, inayobainisha wazi kwamba:-
• Chombo eha habari kisitumiwe kwa manufaa binafsi ya mmiliki au mtendaji bali kitatumiwa kwa manufaa ya umma;
• Chombo eha habari kiongozwe na maadili ya taaluma na jamii husika; na
• Chombo eha habari kisitangaze habari kwa misingi ya ubaguzi wa rangi, kabila, dini, jinsia au ulemavu au kuehoehea uhasama.
9. Katika hali hiyo malumbano ya Mheshimiwa Rostam Aziz na Bwana Reginald Mengi yakiachiwa kuendelea yanaweza kulitumbukiza Taifa letu katika uvunjaji wa amani.
10. Kutokana na hali hiyo basi, Serikali inawataka Mheshimiwa Rostam Aziz na Bwana Reginald Mengi kuacha mara moja malumbano kupitia vyombo vya habari, na badala yake wawasilishe madai na vielelezo vyao kwa mamlaka husika ili hatua zinazofaa zichukuliwe,na wananchi wapewe taarifa na vyombo hivyo.

11. Serikali haitakubali kusikia malumbano ya Mheshimiwa Rostam Aziz na Bwana Reginald Mengi ambayo yanaweza kuleta uvunjaji wa amani nchini, yakiendelea. Serikali pia haitavumilia kuona vyombo vya habari nchini vikichangia kliligawa Taifa katika makundi, na kudumaza maendeleo.
12. Aidha, Serikali inawataka Bwana Reginald Mengi na Mheshimiwa Rostam Aziz kuvitumia vyombo vyao vya habari kwa manufaa ya Wananchi wote wa Tanzania, na si kwa manufaa yao binafsi. Wakumbuke kwamba malumbano yao hayo kwa kutumia vyombo vyao binafsi, na wakati mwingine kuonekana kana kwamba wanalihutubia Taifa, ni kutowatendea haki watu wengine ama kampuni/mashirika ambayo yametajwa katika malumbano hayo, lakini hawana vyombo binafsi (redio, televisheni, rnagazeti) ambavyo wangeweza kuvitumia kujieleza na kujitetea kama walivyofanya Bwana Reginald Mengi na Mheshimiwa Rostam Azizi.
13. Serikali imesikitishwa na kitendo eha Bwana Reginald Mengi eha kuzungumzia kesi ambazo tayari ziko Mahakamani. Sheria za nchi zinakataza mtu, watu kuzungumzia ama klljadili suala ambalo tayari liko Mahakarnani. Kwa kufanya hivyo, Bwana Reginald Mengi arnewahukumu watuhumiwa l1ao na kuwatia hatian; bila wao kupewa fursa ya kusikilizwa ("They have been condemned unheard''). Kwa mujibu wa Sheria za nehi, Mal1akama peke yake ndiyo inayoweza kumtia hatiani mtuhurniwa.
14. Aidha, Serikali inawatahadharisha Wahar;,.i wa Wanahabari kwa ujurnla kuwa makini katika kutirniza wajibu wao kwa weledi na kuzingalia maadili ya taalurna yao, badala ya kuandika au kutangaza habari kulingana na matakwa ya mmiliki wa chombo kinachohllsika.
15. Hivyo basi kuanzia sasa, Serikali haitasita kuchukua hatua za kisheria dhidi ya wamiliki wa vyombo vya habari ambao hawatazingatia weledi (professionalism), Sheria ya Magazeti ya mwaka 1976 na Sheria ya Utangazaji ya Mwaka 2003, katika kutekeleza kazi zao za I

16. Mwisho, Serikali kwa mara nyingine inasisitiza kwamba mapambano dhidi ya vitendo vya rushwa na ufisadi bade yanaendelea, na inawahimiza wananchi wote wenye taarifa za vitendo kama hivyo watoe taarifa hizo kwenye vyombo vya dol a vilivyopewa majukumu hayo, iIi hatua ziweze kuchukuliwa kwa mujibu wa sheria. Hivyo basi, Serikali inawataka wananchi wote kufuata taratibu na Sheria za nchi yetu katika kuwasilisha hoja zao, iIi kuendelea kudumisha amani ya nchi yetu.
Kapt. (Mst) George H. Mkuchika (Mb) WAZIRI WA HABARI, UTAMADUNI NA MICHEZO
11 Mei,2009

the saga continue
 
Mhh huyu mkuchika si alishasema serikali itamchukulia hatua bwana Mengi? sasa kabadili msimamo baada ya Mheshimiwa naye kufanya kama alivyofanya Mengi? Msimamo aliuonyesha mwanzo baada ya taarifa ya Mengi nilifikiri angeuendeleza na kuwachukulia hatua wote wawili yaani Bwana Mengi na Fisadi Papa Rostam Aziz.

Naanza kuamini yale yanayosemwa kuhusu RA kuwa na nguvu kubwa kuliko Mtanzania yoyote!
 
makofi "kwa kwa kwa kwa!"

tena! "kwa kwa kwa kwa!"

Hadithi hii kakufundisha nani? na amekuambia ina maana gani?
 
We have long way to go.
Hivi hawa viongozi wetu huwa wanafikiri nini??
Nilitegemea serikali ingetoa kauli ya kupongeza ama kukemea baadhi ya mambo yaliyosemwa kama ni kweli au la hili la kupiga mikwala halisaidii.
Maswali yangu kwa Kumkuchika
je Aliyosema Mengi ni ukweli au ?
Je aliyosema Rostam ni ukweli au la?
Na kama kuna ukweli je wao serikali wanampango gani na hizi taarifa??
Kwani TAKUKURU kuna habari nyingi sana zimepelekwa hawafanyi kitu.
DPP ana mafaili ya kufungua kesi hataki.
Polisi wamepewa taarifa za kumwaga wako kimya.
Wananchi wanachokipata ni matusi na watoa habari kuwekwa uchi na kuwa wahanga wa wahalifu.
Sasa kama hawataki wenye habari kutumia njia hii ya media kutangaza na kutoa habari za wezi, wala rushwa na mafisadi hawaoni wao serikali ni baadhi na injini ya ufisadi na umasikini unao tutafuna.???
Hawajui kuwa hili linalotokea ni kushindwa kwa serikali kushughulikia uhalifu unaokuwa siku hadi siku.
Mangapi yalisemwa na wangapi tayari wananchi wamesha pigia kelele kuanzia bungeni lakini hakuna linalofanyika.
Naona street justice should be next.
 
8. Aidha, Serikali imebaini kwamba katika malumbano haya kumekuwepo na "matumizi mabaya" ya vyombo vya habari vinavyomilikiwa na Bwana Mengi, (televisheni, magazeti na radio), na kwa Mheshimiwa Rostam Aziz, (magazeti). Kila mmoja ametumia vyombo vya habari anavyomiliki kwa manufaa yake binafsi kinyume na maelekezo ya Sera ya Habari na Utangazaji ya Mwaka 2003, inayobainisha wazi kwamba:-

Aaa! kumbe TBC aliyotumia Rostam kumkashifu Mengi nayo ni ya Rostam. Sasa nemeelewa!

Amesema magazeti ya Rostam, TBC ni gazeti?
 
1. TAKURURU walipewa ushahidi Richmond wakasema Lowasa safi, hadi tume ya Mwakyembe iliposema kulikuwa kuna rushwa!

2. Yaani upeleke ushahidi serikalini kuwa pesa za KAGODA ndo zilitumika kuiweka madarakani CCM 2005- je nani atakusikiliza?

3. Serikali iache kuwatisha watu na kuwafunga watu midomo!!!
 
Viongozi wa bongo yaani old skool new skool wote IQ ni zero!.....wanafikriia maslahi yao na wala siyo ya wananchi...both chama tawala na vyama cya upizani....

je tutafika>?.....garlie!...
 
Back
Top Bottom