Wakuu JF.
Nimesoma kwenye mtandao kuwa Tariki Azizi wa TZ leo angetoa tamko la Serikali Kuhusu Mengi.
Tafadhali mlioko nyumbani tupasheni habari kama kalitoa na amesema nini.
=====
Rostam Na Mengi: Serikali Yatoa Tamko
MONDAY, MAY 11, 2009
Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni na Michezo Mh. Joel Bendera
SERIKALI imewataka Wafanyabiashara Rostam Aziz na Mwenyekiti wa Makampuni ya IPP, Reginald Mengi kuacha mara moja malumbano kati yao na kutotumia vyombo vyao vya habari kwa maslahi yao binafsi.
Sambamba na hilo imewataka kuwasilisha vielelezo na madai yao kwa mamlaka husika ili hatua zinazofaa zichukuliwe na wananchi wapewe taarifa na vyombo hivyo.
Akitoa tamko la serikali leo mbele ya waandishi wa habari, Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni na Michezo, Joel Bendera kwa niaba ya Waziri wake, George Mkuchika alisema serikali haitakubali kusikia malumbano hayo ambayo yanaweza kuleta uvunjifu wa amani nchini yakiendelea.
“Serikali imeyatafakari malumbano ya wafanyabiashara hawa na kubaini yanalipeleka taifa letu mahali pabaya kwani yana mwelekeo wa uvunjaji wa amani kama yataachwa kuendelea.
"…pia haitavumilia kuona vyombo vya habari nchini vikichangia kuligawa taifa katika makundi na kudumaza maendeleo”,alisema.
Badala yake amevitaka vyombo hivyo vya habari kutotomiwa kwa manufaa binafsi ya mmiliki au mtendaji; viongozwe na maadili ya taaluma na jamii husika na kisitangaze habari kwa misingi ya ubaguzi wa rangi, kabila, dini, jinsia au ulemavu na kuchochea uhasama.
Nimesoma kwenye mtandao kuwa Tariki Azizi wa TZ leo angetoa tamko la Serikali Kuhusu Mengi.
Tafadhali mlioko nyumbani tupasheni habari kama kalitoa na amesema nini.
=====
Rostam Na Mengi: Serikali Yatoa Tamko
MONDAY, MAY 11, 2009
Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni na Michezo Mh. Joel Bendera
SERIKALI imewataka Wafanyabiashara Rostam Aziz na Mwenyekiti wa Makampuni ya IPP, Reginald Mengi kuacha mara moja malumbano kati yao na kutotumia vyombo vyao vya habari kwa maslahi yao binafsi.
Sambamba na hilo imewataka kuwasilisha vielelezo na madai yao kwa mamlaka husika ili hatua zinazofaa zichukuliwe na wananchi wapewe taarifa na vyombo hivyo.
Akitoa tamko la serikali leo mbele ya waandishi wa habari, Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni na Michezo, Joel Bendera kwa niaba ya Waziri wake, George Mkuchika alisema serikali haitakubali kusikia malumbano hayo ambayo yanaweza kuleta uvunjifu wa amani nchini yakiendelea.
“Serikali imeyatafakari malumbano ya wafanyabiashara hawa na kubaini yanalipeleka taifa letu mahali pabaya kwani yana mwelekeo wa uvunjaji wa amani kama yataachwa kuendelea.
"…pia haitavumilia kuona vyombo vya habari nchini vikichangia kuligawa taifa katika makundi na kudumaza maendeleo”,alisema.
Badala yake amevitaka vyombo hivyo vya habari kutotomiwa kwa manufaa binafsi ya mmiliki au mtendaji; viongozwe na maadili ya taaluma na jamii husika na kisitangaze habari kwa misingi ya ubaguzi wa rangi, kabila, dini, jinsia au ulemavu na kuchochea uhasama.
Yussuf Makamba amwinda Reginald Mengi, yeye awataja mafisadi Papa rasmi!
Makamba amwinda Mengi Ahoji safari za mikoani Mwandishi Wetu Aprili 22, 2009 Raia Mwema~Muungwana ni Vitendo HUKU kukiwa na shinikizo la kutaka kumuondoa katika nafasi yake Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Yussuf Makamba, mwanasiasa huyo machachari, ametajwa sasa...
www.jamiiforums.com
Tamko la Rostam Aziz dhidi ya Reginald Mengi na yatokanayo. Amuita fisadi Nyangumi
Mbunge wa Igunga na Mweka hazina wa zamani wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Rostam Aziz, hatimaye amejibu rasmi madai mazito yaliyotolewa na Reginald Mengi kuhusu "mafisadi papa". Tamko hilo rasmi linapatikana katika ukurasa wa 6 wa gazeti la 'The Citizen' la leo Alhamisi, tarehe 30 Aprili 2009...
www.jamiiforums.com