Rostam Aziz ameomba radhi kwa majaji akisema ulimi uliteleza na hakumaanisha ambacho alikisema kuhusu majaji kuhongwa. Nadhani amefanya jambo la kiungwana sana.
===
Leo Jumanne July 4, 2023 mfanyabiashara mashuhuri nchini, Rostam Aziz ameongea na vyombo vya habari, pamoja na mambo mengine ameomba radhi na kusema hakukusudia kudharau mahakama.
Rostam Aziz: Baada ya kuona tamko la chama cha majaji na mahakimu kuhusiana na kauli niliyoitoa Jumatatu iliyopita wakati nikiongea kuhusiana na uwekezaji wa kampuni yetu kule Zambia.
Nimesoma taarifa ya chama, kwasababu ya kutambua na kuheshimu dhima, hadhi na wajibu wa kikatiba wa mahakama, ningependa kusema yafuatayo
Ningependa kuuhakikishia umma kwamba wakati nikizungumzia kuhusu uwekezaji, halikuwa kusudio langu kudharau mahakama zetu. Kama nilisema hivyo ilikuwa ni kuteleza kwa ulimi maana kusudio langu lilikuwa likilenga kuhusu uwekezaji nchini na maana yangu ilikuwa ni kwamba ili tuweze kupata uwekezaji nchini mwetu hatuna budi kuendana na taratibu zinazoongoza uwekezaji Duniani.
===
Kauli ya Rostam Azizi kujusu Majaji na Mahakimu wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu: Rostam Aziz: Hakuna mwekezaji atakubali kuwekeza halafu umwambie aende Mahakama ya Kisutu ambapo Majaji wanaweza kupigiwa simu na watu wa Serikali
Tamko la kumtaka athibitishe kauli yake: Chama cha Majaji na Mahakimu Tanzania chamtaka Rostam Aziz kuthibitisha tuhuma alizotoa dhidi ya Majaji na Mahakama ya Kisutu
===
Leo Jumanne July 4, 2023 mfanyabiashara mashuhuri nchini, Rostam Aziz ameongea na vyombo vya habari, pamoja na mambo mengine ameomba radhi na kusema hakukusudia kudharau mahakama.
Rostam Aziz: Baada ya kuona tamko la chama cha majaji na mahakimu kuhusiana na kauli niliyoitoa Jumatatu iliyopita wakati nikiongea kuhusiana na uwekezaji wa kampuni yetu kule Zambia.
Nimesoma taarifa ya chama, kwasababu ya kutambua na kuheshimu dhima, hadhi na wajibu wa kikatiba wa mahakama, ningependa kusema yafuatayo
Ningependa kuuhakikishia umma kwamba wakati nikizungumzia kuhusu uwekezaji, halikuwa kusudio langu kudharau mahakama zetu. Kama nilisema hivyo ilikuwa ni kuteleza kwa ulimi maana kusudio langu lilikuwa likilenga kuhusu uwekezaji nchini na maana yangu ilikuwa ni kwamba ili tuweze kupata uwekezaji nchini mwetu hatuna budi kuendana na taratibu zinazoongoza uwekezaji Duniani.
===
Kauli ya Rostam Azizi kujusu Majaji na Mahakimu wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu: Rostam Aziz: Hakuna mwekezaji atakubali kuwekeza halafu umwambie aende Mahakama ya Kisutu ambapo Majaji wanaweza kupigiwa simu na watu wa Serikali
Tamko la kumtaka athibitishe kauli yake: Chama cha Majaji na Mahakimu Tanzania chamtaka Rostam Aziz kuthibitisha tuhuma alizotoa dhidi ya Majaji na Mahakama ya Kisutu