Sildenafil Citrate
JF-Expert Member
- Jan 29, 2021
- 573
- 2,553
Mnamo tarehe 26 Juni, 2023 manyabiashara Bw. Rostam Azizi wakati akiongea na vyombo vya habari kuhusu masuala ya uwekezaji alinukuliwa akiituhumu aliyoiita Mahakama ya Kisutu kwa kutokuwa huru katika uendeshaji wa shughuli zake.
Kutokana na taarifa hiyo tunapenda kuhabarisha umma yafuatayo:
Hakuna Jaji anayehudumu katika Mahakama hiyo kama ilivyoripotiwa na mzungumzaji wa taarifa hiyo.
Mahakama ya Tanzania ni chombo pekee cha utoaji haki nchini kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na huendesha shughuli zake kwa uhuru bila kuingiliwa na mtu au chombo chochote.
Uongozi wa Mahakama na au Chama Cha Majaji na Mahakimu haujawahi kupokea tuhuma au lalamiko lolote kutoka kwa mtu yeyote ikionyesha Maafisa wa Mahakama kupigiwa simu na kuelekezwa namna ya kutoa maamuzi katika mahakama hiyo.
Kutokana na maelezo hayo Chama cha Majaji na Mahakimu Tanzania tunatoa kauli zifuatazo:
Akishindwa kutoa uthibitisho tunamtaka atumie Jukwaa lile lile kuomba radhi kwa uzito ule ule.
Imetolewa na:
UONGOZI WA CHAMA CHA MAJAJI NA MAHAKIMU TANZANIA (JMAT)
4 JULAI 2023
Pia soma:
Kutokana na taarifa hiyo tunapenda kuhabarisha umma yafuatayo:
Hakuna Jaji anayehudumu katika Mahakama hiyo kama ilivyoripotiwa na mzungumzaji wa taarifa hiyo.
Mahakama ya Tanzania ni chombo pekee cha utoaji haki nchini kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na huendesha shughuli zake kwa uhuru bila kuingiliwa na mtu au chombo chochote.
Uongozi wa Mahakama na au Chama Cha Majaji na Mahakimu haujawahi kupokea tuhuma au lalamiko lolote kutoka kwa mtu yeyote ikionyesha Maafisa wa Mahakama kupigiwa simu na kuelekezwa namna ya kutoa maamuzi katika mahakama hiyo.
Kutokana na maelezo hayo Chama cha Majaji na Mahakimu Tanzania tunatoa kauli zifuatazo:
- Tumesikitishwa sana na kauli za Bw Rostam Aziz ambaye hatukutegemea aongee mambo mazito kama hayo bila kuwa na uhakika wala uthibitisho.
- Matamshi ya Bw Rostam Aziz yanaweza kuhatarisha uhusiano na ushirikiano katika mihimili mitatu ya dola ndani ya nchi yetu.
- Tunaomba wananchi wenye nia njema na Mahakama na mihimili mingine waendelee kuwa na Imani na mfumo wa utoaji haki nchini.
Akishindwa kutoa uthibitisho tunamtaka atumie Jukwaa lile lile kuomba radhi kwa uzito ule ule.
Imetolewa na:
UONGOZI WA CHAMA CHA MAJAJI NA MAHAKIMU TANZANIA (JMAT)
4 JULAI 2023
Pia soma: