Tamko la CHADEMA - Aprili 14, 2013

Tamko la CHADEMA - Aprili 14, 2013

Status
Not open for further replies.
.... ndugu Dennis Msacky ni rafiki yangu wa karibu sana. Ninaamini kabisa kwamba katika suala hili Dennis Msacky ni victim......

Kwani huwa uko naye 24/7? Never trust anything that can think for itself if you can't see where it keeps its brain.
 
Chadema lazima ijichunge sana...huwezi kusema intelligensia yako iko juu na ni makini wakati mkuu wako wa intellijensia anany...ea debe mahabusu....still huyu unayemtegemea ni afisa wa serikali....mtalijua jiji mwaka huu.
 
Ndugu zangu wana JF

Namba hiyo iliyotajwa hapo juu imewahi kuwa namba yangu ya Simu. Namba hii nimeacha kuitumia toka mwezi Juni/Julai mwaka 2012. Hata hivyo namba hii bado inaonekana kwenye businesscard yangu na kwenye email zangu sehemu ya anuani. Namba hii haijawahi kuwa ya Zoka. Imewahi kuwa ya Zitto Zuberi Kabwe peke yake. Namba hii haitumiki toka katikati ya mwaka 2012.

Kama JF inataka kuthibitisha hili waunde jopo la wanaJF watakaopata taarifa za namba hii popote wanapoweza kupata.

Mambo 2, ama namba hii imewekwa kwa bahati mbaya kwenye tamko tajwa au imewekwa makusudi kwa sababu maalumu zenye lengo la kutoa ujumbe fulani kwa watu.

Kwa namna namba hii ilivyochomekwa kwenye tamko hili au hapa JF au vyote kwa pamoja, ni dhahiri kuna juhudi za kunihusisha na upuuzi huu wa ugaidi na unyama dhidi ya binaadamu.

Napenda kusisitiza kwamba, sihusiki kwa namna yeyote ile katika kuwaza, kupanga au kutekeleza mipango yeyote ya kudhuru mtu ama kwa njia za kigaidi au za kijinai. Sihusiki kwa namna yeyote ile kupanga mpango wowote ule wenye lengo la kuhusisha chama changu na vitendo vyovyote vya kigaidi au kudhuru mtu yeyote yule. Juhudi zozote zinazofanywa na maadui wa chama changu za kunihusisha na mambo haya zitashindwa kwani siku zote ukweli huwa bayana.

Napenda kuweka wazi kwamba Mhariri wa Mwananchi ndugu Dennis Msacky ni rafiki yangu wa karibu sana. Ninaamini kabisa kwamba katika suala hili Dennis Msacky ni victim. Juhudi zozote zile za kutaka kumgeuza 'victim' kuwa mtuhumiwa lazima zitashindwa tu kwani siku zote HAKI hutamalaki.

Mtu yeyote anayetaka kutumia urafiki wangu na Dennis Msacky kutaka kujifurahisha kisiasa ajue kuwa furaha yake hiyo itakuwa ni ya muda mfupi sana maana ukweli ukidhihiri atapata aibu kubwa sana.

Ni muhimu sasa mambo haya tuiachie mahakama itende haki.
Hofu yangu kubwa ni kwamba isijekuwa kiongozi wa CHADEMA anayetajwa kila siku na Mwigulu Nchemba kwamba yupo tayari kutoa ushahidi mahakamani ukawa ni wewe! Haiwezekani Msacky ashiriki kwenye propaganda hii ya kukiua chama halafu wewe usijue? Msacky alikuwa ana agenda gani na Ludovick? Sisi tunasubiri kiongozi wa CHADEMA ambaye Mwigulu atakwenda naye mahakamani. Kama utakuwa wewe, basi tutathibitisha kwa dhati kabisa kwamba wewe si mwenzetu.

Mara nyingi nimekushauri Zitto kule wanabidii na hata hapa nimekufungulia thread kabisa kukuomba ufanye mambo yako kwa utulivu na jitahidi kushirikiana kwa karibu na wenzako. Hivi unajiuliza ni kwanini kila kuchwapo ni wewe tu unaandamwa na kashifa za kukiua chama ambacho ulikijenga kwa shida kubwa? Nakumbuka sana harakati zako za kukijenga chama tukiwa UDSM, wakati huo nikiwa CCM, ninakumbuka sana ulivyojitolea muda na pesa kwenda kwenye vikao vya kila leo vya CDM, ni kwa vipi tena leo unakuwa mwiba kwa chama ulichokihangaikia vile?

Nashangaa sana Zitto, ni kwanini kila siku unasakamwa wewe tu? Kwani wewe una tofauti gani na akina Mnyika, Msigwa, Lissu au Wenje au akina Mdee? Kwanini hawakuwahi kusemwa wengine badala yake uwe wewe tu Zitto? Kwanini hawajawa akina professor safari au akina Marando pamoja na uchanga wao ndani ya chama? Mimi nafikiri kuna mahali ambapo Zitto umepotoka, lakini wewe mwenyewe hujijui. Inawezekana unatumika pasipo wewe mwenyewe kujijua au inawezekana unakijua unachokifanya.

Ukumbuke shutuma dhidi yako zilianza mara tu ulipoanza kuwa na urafiki wa karibu na JK. Pale mlipoanza kukokotana kwenda Sudani kusini na mliposhirikiana kuzika report ya kamati ya uchunguzi wa mkataba wa Buzwagi, basi tangu hapo umekuwa ukitiliwa mashaka mengi ndani ya CDM. Ni dhahiri kwamba kuna kitu ambacho hakipo sawa upande wako. Na inawezekana ni kweli kwamba JK anakutumia, au inawezekana unasumbuliwa na kasumba ya kutaka uonekane ni mwema zaidi kuliko wengine au kutaka kujionyesha mbele za watu ndiyo inayokuweka kwenye wakati mbaya. Jaribu kuwa kama Mnyika, I am sorry kumtaja huyu kila wakati, but kwangu mimi Mnyika ni role model. Jifunze kutoka kwake juu ya utulivu na subira.

Usinie makuu, muache Mungu akupe yale unayostahili. Usitafute umaarufu wa haraka maana gharama yake ni kubwa mno, inaweza kuwa ni kuupoteza kabisa huo umaarufu unaoutafuta. Tulia ndugu yangu.
 
Jamani hivi mtu unaponunua simu unapangiwa mtu wa kuwasiliana naye?. Usalama wa taifa ni watu kama watu wengine. Wana ndugu na marafiki wa kila namna, kwani hawaruhusiwi kuwasiliana na ndugu/marafiki zao?.

Mawasiliano ya simu kati ya waliotajwa hapo juu kwangu mimi sioni tatizo, bali itakuwa tatizo kama yakipatikana maneno yalikuwa yanasemwa kwenye hayo mawasiliano na kama yatakuwa yanahusika na huo ugaidi unaosemwa.

La mwisho naomba tuelewe kwamba siasa si uhasama bali ni kuwa na mtizamo tofauti wa kiitikadi. Ni sawa na upenzi wa timu za mpira wa miguu, mimi nikipenda Yanga na mke wangu akipenda Simba bado tutaishi pamoja ila utani ndani ya nyumba utakuwepo na hasa siku za mechi. Mwigulu Nchemba kuwasiliana na Joseph Ludovick bado si tatizo kwani inawezekana ni marafiki na tofauti za kiitikadi haziwezi kuwatenganisha. Jamani ebu tusione uvivu kufikiria, hivi ina maana Mbowe hana namba ya simu ya Kikwete?, je hawezi kuwasiliana na Kikwete kama anataka kufanya hivyo?. Mimi na Baba yangu tuna itikadi tofauti za kisiasa, je ni vibaya kwa mimi kuwasiliana na Baba yangu?.

Sipendi Chama chochote cha siasa ama genge lolote liendeshe ugaidi, ila ninachosema ni kwamba mawasiliano ya simu yaliyokuwepo si kigezo kwamba CCM na serikali yake inafanya ugaidi. Kwa umakini zaidi kinatakiwa kilichokuwa kinasemwa katika mawasiliano hayo.
 
Video ya lwaka ni mwiba mkuu kwa chadema, take it from me na jinsi siku zinavyozidi kwenda wanazidi kuchanganyikiwa...nawapongeza wote waliofanikisha kupatikana kwa video hii ya magaidi
 
Jamani hivi mtu unaponunua simu unapangiwa mtu wa kuwasiliana naye?. Usalama wa taifa ni watu kama watu wengine. Wana ndugu na marafiki wa kila namna, kwani hawaruhusiwi kuwasiliana na ndugu/marafiki zao?.

Mawasiliano ya simu kati ya waliotajwa hapo juu kwangu mimi sioni tatizo, bali itakuwa tatizo kama yakipatikana maneno yalikuwa yanasemwa kwenye hayo mawasiliano na kama yatakuwa yanahusika na huo ugaidi unaosemwa.

La mwisho naomba tuelewe kwamba siasa si uhasama bali ni kuwa na mtizamo tofauti wa kiitikadi. Ni sawa na upenzi wa timu za mpira wa miguu, mimi nikipenda Yanga na mke wangu akipenda Simba bado tutaishi pamoja ila utani ndani ya nyumba utakuwepo na hasa siku za mechi. Mwigulu Nchemba kuwasiliana na Joseph Ludovick bado si tatizo kwani inawezekana ni marafiki na tofauti za kiitikadi haziwezi kuwatenganisha. Jamani ebu tusione uvivu kufikiria, hivi ina maana Mbowe hana namba ya simu ya Kikwete?, je hawezi kuwasiliana na Kikwete kama anataka kufanya hivyo?. Mimi na Baba yangu tuna itikadi tofauti za kisiasa, je ni vibaya kwa mimi kuwasiliana na Baba yangu?.

Sipendi Chama chochote cha siasa ama genge lolote liendeshe ugaidi, ila ninachosema ni kwamba mawasiliano ya simu yaliyokuwepo si kigezo kwamba CCM na serikali yake inafanya ugaidi. Kwa umakini zaidi kinatakiwa kilichokuwa kinasemwa katika mawasiliano hayo.

sasa subiri mvua ya matusi kutoka kwa vijana wa kinondoni mtaa wa manhattan karibu na pale makaburini
 
Habari za usiku wanabodi.

Mimi natoa yaliyo moyoni kwa mawazo yangu HURU.

Mimi DONYONGIJAPE, mzawa wa SIMANJIRO, naamini kabisa kwamba mtu mbaya kwa CHADEMA ni LWAKATARE. Inaonekana kabisa amefanya lile Tukio akijua kabisa anarekodiwa, na ndio maana akaongea hayo aliyoongea eili kuiharibia CHADEMA. NDIYO, ana uwezo huo, tena inaonekana alijipanga kabisa kuongea hayo yeye na huyo Ludovick. Ndio maana walikuwa wakipeana leading Questions.

Ninachokiona ni kwamba, Bw. Lwakatare amekula njama na Mwigulu, Ludo, Zoka, Zitto etc ili waichafue CHADEMA. Huyu siyo mtu wa kutetea kabisa katika sakata hili. Ni mtu aliyekuwa anafanya kile anachojua na ni MSALITI.

CHADEMA isipoteze nguvu na MUDA kumtetea huyu MSALITI, kwa maana mwisho wa siku ATAKIRI na CHADEMA itashindwa kesi kwa KISHINDO na NDIO itakuwa MWISHO WAKE.

1. Sipingani na mawazo yako kwani una uhuru wa kuandika ulichokiandika lakini kumbuka Kova alisema kesi hii inamuhusu Lwakatare na haihusishi chama, Chama kimeingia kumtetea kwa sababu ni kiongozi mkubwa na pia kuna dalili za uonevu na kubambikiwa kesi hiyo, hivyo ukisema Lwakatare mwisho wa siku atakiri kosa atahukumiwa yeye kama yeye kwa hiyo hawezi kufanya hivyo atakuwa amejiangamiza mwenyewe.

2. Upande wa pili nina wasiwasi na wewe mleta mada ni wale mliokuwa mkitaka chama kimfukuze kutokana na tukio hili, hilo limeshindikana sasa mnaona mje na njia nyingine ambayo usitegemee kufanikiwa CHADEMA wapo makini kuliko unavyofahamu wewe.
 
mie hii mechi cjui inaanza lini natamani sana ili nishuhudie watu wakiumbuka mahakamani duh mpaka ulimboka ndani dah mbona raha
 
Ni ujinga ku quote habari yote halafu unaandika sentensi moja tu, wewe wa wapi?

Mkuu nimecheka kwa sauti ghafla yaelekea kakuuzi sana. Ulitaka aki quote nusu page nayeye atoe maelezo nusu page? Ila hawa wanao quote lihabari lote wanatupa shida watumia simu hata mimi wananiuzi
 
Leo magaidi hawalali...hivi tangu lwakatare akamatwe hili ni tamko la ngapi vile? Mtasema yote mwaka huu...mnataka kuongoza watu halafu mnapanga kuwauwa?? What a shame is this?
 
Maskini MARANDO anaweza kutaja namba za simu kwa ufasaha LAKINI hajatueleza wananchi PROOF yake kuhusu U FAKE wa ile video!!! That is what we want to hear right now. EBO,!
 
Wanasemaga, its just the matter of time! Kitaeleweka tu!
 
Ndugu zangu wana JF

Namba hiyo iliyotajwa hapo juu imewahi kuwa namba yangu ya Simu. Namba hii nimeacha kuitumia toka mwezi Juni/Julai mwaka 2012. Hata hivyo namba hii bado inaonekana kwenye businesscard yangu na kwenye email zangu sehemu ya anuani. Namba hii haijawahi kuwa ya Zoka. Imewahi kuwa ya Zitto Zuberi Kabwe peke yake. Namba hii haitumiki toka katikati ya mwaka 2012.

Kama JF inataka kuthibitisha hili waunde jopo la wanaJF watakaopata taarifa za namba hii popote wanapoweza kupata.

Mambo 2, ama namba hii imewekwa kwa bahati mbaya kwenye tamko tajwa au imewekwa makusudi kwa sababu maalumu zenye lengo la kutoa ujumbe fulani kwa watu.

Kwa namna namba hii ilivyochomekwa kwenye tamko hili au hapa JF au vyote kwa pamoja, ni dhahiri kuna juhudi za kunihusisha na upuuzi huu wa ugaidi na unyama dhidi ya binaadamu.

Napenda kusisitiza kwamba, sihusiki kwa namna yeyote ile katika kuwaza, kupanga au kutekeleza mipango yeyote ya kudhuru mtu ama kwa njia za kigaidi au za kijinai. Sihusiki kwa namna yeyote ile kupanga mpango wowote ule wenye lengo la kuhusisha chama changu na vitendo vyovyote vya kigaidi au kudhuru mtu yeyote yule. Juhudi zozote zinazofanywa na maadui wa chama changu za kunihusisha na mambo haya zitashindwa kwani siku zote ukweli huwa bayana.

Napenda kuweka wazi kwamba Mhariri wa Mwananchi ndugu Dennis Msacky ni rafiki yangu wa karibu sana. Ninaamini kabisa kwamba katika suala hili Dennis Msacky ni victim. Juhudi zozote zile za kutaka kumgeuza 'victim' kuwa mtuhumiwa lazima zitashindwa tu kwani siku zote HAKI hutamalaki.

Mtu yeyote anayetaka kutumia urafiki wangu na Dennis Msacky kutaka kujifurahisha kisiasa ajue kuwa furaha yake hiyo itakuwa ni ya muda mfupi sana maana ukweli ukidhihiri atapata aibu kubwa sana.

Ni muhimu sasa mambo haya tuiachie mahakama itende haki.

Pengine badala ya kupoteza muda wa kuunda jopo la wanaJF kuchunguza namba yako, ingekua na itakua vizuri na rahisi zaidi kama wewe ukauliza chama chako kwamba, inakuaje namba yako inaonekana kwenye tamko kama namba ya Zoka??
au nawe ni victim kama Msacky ndomana huwezi uliza chama chako??
 
Comment moja ilitosha kuonyesha msimamo wako,unavyoendelea kuandika unaleta picha dhahiri mlivyo uchi baada ya tamko

we endelea kuhangaika na msimamo wangu ila nawapongeza woooooote waliofanikisha kupatikana kwa video ya kigaidi inayomwonesha lwaka akitoa maelekezo ya utekaji....hapa jukwaani nawafananisha na mchawi anayelia msibani baada ya kuuwa
 
sasa subiri mvua ya matusi kutoka kwa vijana wa kinondoni mtaa wa manhattan karibu na pale makaburini

Mkuu, kuna wakati ni lazima tujadili mambo kama watanzania kwa kuweka itikadi zetu za kisiasa pembeni. Kwa haya yanayoendelea tusipokuwa makini na werevu wa kufikiria yanaweza kutufikisha pabaya sana. Usalama wa nchi ni wa kila mwananchi bila kujali itikadi, rangi, kabila, jinsia nk. Ninawaomba viongozi wakuu wa vyama vya siasa wawe makini sana wanapozungumzia usalama wa Taifa letu.
 
ulinikera sana na 'bonafide genuine'
Mkuu Nyakageni, pole sana, na wengine wote mnaokereka na "bonafide genuine" pia poleni sana ila huu ndio ukweli halisi!, huu ni ukweli mchungu ambao piga ua galagaza, lazima muumeze!.

Sio peke yako unaokereka na kauli hii, mko wengi, haswa kwa kuzingatia kuwa mliisha aminishwa kuwa ile video ni fake!, aliyewaaminisha ni viongozi wenu mnawaaminia, na wengine wanawaabudia!, Pasco wa jf, is just a mare jf member!. how the hell can he dare challenge the authority you trust?!. Nasisitiza its "bonafide genuine!" na ukweli huu utasimama!.

Mpaka sasa, kwa vile mmeishaaminishwa video ni fake, naona hakuna hata mmoja wenu, anayejishughulisha na "contents" za video ile and the motive behind!, naisubiri kwa hamu, about turn ya hao viongozi wenu, watawaeleza nini baada ya kujui ni "bonafide genuine!". Rwaka ameisha mweleza Lissu kila kitu!, akashauri akubali mengine na mengine akanushe, but it won't work that way kwa sababu aliyeurekodi, amebinywa amesema!, Ludo is very cooparative!.

Salama ya Chadema lies on legal technicalities za "admissibility of evidence" kuwatumia hao wanasheria wake 6 na familia ya Rwakatare, wameisha gundua, katika timu yote ya hao wanasheria 6 wa Chadema, hakuna bingwa aliyebobea kwenye "criminology!", hivyo itamleta bingwa wa "criminoloy" kusaidiana na hawa wanasheria 7 wa Chadema, kujenga na historical record ya jopo la mawakili 7 kumtetea mtuhumiwa mmoja!, hivyo chances za kushinda kesi ni kubwa kwa kuzingatia baadhi ya majaji wetu, ni hawa majaji vilaza aliyewasema Lissu!. Wakipangiwa majaji wa ukweli, issues aliyoyaongea Rwaka, ni issie ndogo tuu kisheria inaitwa "actus reus!", ngoma nzito ni "mens rea" ambayo ndio the "motive behind!" na hakuna anayejishughulisha nayo!.

Kama X=Y na Y=Z, then X=Z, X-Rwaka, Y-Actus Reus, Z-Mens Rea.

Pasco.
 
mbowe na slaa ndo madereva katika hili na lazima wajumuishwe ndo maana wanahaha kila kukicha kuibua sinema mbalimbali kwa lengo la kupotosha ila wasipohonga mahakamani hawatoki ila kwa vile kunazile hela walizopewa na wadernmark watazipeleka zote kuhonga mahakama ili wapendelewe make ndo zao kuhonga.

Ni mwana CCM mwenzako lakini naona umekosa maneno ya maana kuzungumza. Tufanye siasa za kistaarabu ndugu, hata Mungu atatubariki
 
Nitoeni haya mashaka niliyo nayo; Je, mahakama haiwezi kukataa ombi la Chadema kutaka kutoa kibali cha makampuni ya simu kutoa taarifa za Namba hzo za simu? Ikiwa mahakama itaridhia ombi la Chadema, je haya makampuni ya simu hayawezi kurubuniwa na kuchakachua hizo taarifa za namba za simu za hao wahusika 10? Please naomba nijuzwe kuhusu hayo maswali yangu!
Hapa Marando kawatega UwT na nadhani hii kesi itaishia kufutwa maana mawasiliano ya maafisa usalama hayawezi kuwekwa hadharani. Kawakamata vizuri sana. Hii ni kesi ya kisiasa, lazima iende kisiasa!
 
Hofu yangu kubwa ni kwamba isijekuwa kiongozi wa CHADEMA anayetajwa kila siku na Mwigulu Nchemba kwamba yupo tayari kutoa ushahidi mahakamani ukawa ni wewe! Haiwezekani Msacky ashiriki kwenye propaganda hii ya kukiua chama halafu wewe usijue? Msacky alikuwa ana agenda gani na Ludovick? Tulia ndugu yangu.

Naomba nimtetee kidogo swala la Msaky ni sawa na ungemwambia Lwakatare kwamba Ludo anamsaliti asingekuamini kabisa, na hata hapa Zitto kapigwa upofu. Ila anachonishangaza Zitto ni kumuona Msaky victim tu na hafai kuwa mtuhumiwa yaani hapa nimebaki mdomo wazi.

Zitto alikigeuka chama na sasa namuona bado yuko njia pana, au la ni mmoja kati ya wanaotumiwa na CCM kuendelea kumaliza chama ( bado na mimi nimepigwa upofu hapo)
 
Last edited by a moderator:
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom