Tamko la CHADEMA - Aprili 14, 2013

Tamko la CHADEMA - Aprili 14, 2013

Status
Not open for further replies.
Chadema inaelekea kusambaratika. It's time tu

Say nooooooooooo to ugaidi na mauaji na mateso dhidi ya aria wema

Kwann chadema wanapenda kuzungumzia mambo yaliyopo mahakamani...ni kujaribu kupreempty mahakama iwapendelee kwenye maamuzi..

chadema kila wiki wana tamko last week ilikuwa iringa wik hii marando may be wiki ijayo mushumbuzi kimekuwa chama cha matamko,maandamano.ugaidi,sumu,ukabila,ukanda bila kusahau propaganda badala ya hoja mbadala kwa ccm

Gaidi mtambue kwa ndevu nyingi, kufunga majini na kusoma minyoo!!
 
Naomba nimtetee kidogo swala la Msaky ni sawa na ungemwambia Lwakatare kwamba Ludo anamsaliti asingekuamini kabisa, na hata hapa Zitto kapigwa upofu. Ila anachonishangaza Zitto ni kumuona Msaky victim tu na hafai kuwa mtuhumiwa yaani hapa nimebaki mdomo wazi.

Zitto alikigeuka chama na sasa namuona bado yuko njia pana, au la ni mmoja kati ya wanaotumiwa na CCM kuendelea kumaliza chama ( bado na mimi nimepigwa upofu hapo)
Hapo ndipo panapotushangaza sisi wote, ni kwa vipi anamtetea Msacky ilihali mlolongo wa matukio unaonyesha wazi kwamba ni mhusika? Kwanini asiassume kwamba Msacky anaweza kumgeuka sawasawa na ambavyo Ludovick alimgeuka Lwakatare waliyekuwa wanafanya kazi ofisi moja? Ila mimi nina uhakika kabisa, kwamba Zitto ndiye atakayekwenda kusimama mahakamani against CHADEMA. Katika hili tusubiri tu wakati.
 
Last edited by a moderator:
DU,hivi hawa CCM nia yao mbona ni ya kizamani hivyo,wanazani watamkamata nani watanzani wa leo.
 
Ndugu zangu wana JF

Namba hiyo iliyotajwa hapo juu imewahi kuwa namba yangu ya Simu. Namba hii nimeacha kuitumia toka mwezi Juni/Julai mwaka 2012. Hata hivyo namba hii bado inaonekana kwenye businesscard yangu na kwenye email zangu sehemu ya anuani. Namba hii haijawahi kuwa ya Zoka. Imewahi kuwa ya Zitto Zuberi Kabwe peke yake. Namba hii haitumiki toka katikati ya mwaka 2012.

Kama JF inataka kuthibitisha hili waunde jopo la wanaJF watakaopata taarifa za namba hii popote wanapoweza kupata.

Mambo 2, ama namba hii imewekwa kwa bahati mbaya kwenye tamko tajwa au imewekwa makusudi kwa sababu maalumu zenye lengo la kutoa ujumbe fulani kwa watu.

Kwa namna namba hii ilivyochomekwa kwenye tamko hili au hapa JF au vyote kwa pamoja, ni dhahiri kuna juhudi za kunihusisha na upuuzi huu wa ugaidi na unyama dhidi ya binaadamu.

Napenda kusisitiza kwamba, sihusiki kwa namna yeyote ile katika kuwaza, kupanga au kutekeleza mipango yeyote ya kudhuru mtu ama kwa njia za kigaidi au za kijinai. Sihusiki kwa namna yeyote ile kupanga mpango wowote ule wenye lengo la kuhusisha chama changu na vitendo vyovyote vya kigaidi au kudhuru mtu yeyote yule. Juhudi zozote zinazofanywa na maadui wa chama changu za kunihusisha na mambo haya zitashindwa kwani siku zote ukweli huwa bayana.

Napenda kuweka wazi kwamba Mhariri wa Mwananchi ndugu Dennis Msacky ni rafiki yangu wa karibu sana. Ninaamini kabisa kwamba katika suala hili Dennis Msacky ni victim. Juhudi zozote zile za kutaka kumgeuza 'victim' kuwa mtuhumiwa lazima zitashindwa tu kwani siku zote HAKI hutamalaki.

Mtu yeyote anayetaka kutumia urafiki wangu na Dennis Msacky kutaka kujifurahisha kisiasa ajue kuwa furaha yake hiyo itakuwa ni ya muda mfupi sana maana ukweli ukidhihiri atapata aibu kubwa sana.

Ni muhimu sasa mambo haya tuiachie mahakama itende haki.

Zitto, hakuna mtu mwenye haki kukuingilia katika maisha yako. Simu yako na unalipa bill mwenyewe kwanini watu wakuingilie na kukupangia mtu wa kuongea naye kupitia simu yako?, kwanini wakuchagulie marafiki?. Kuwa mkali kidogo ama ala watakuchagulia mpaka chupi ya kuvaa.

Huna hata haja ya kuwajibu huu upuuzi wa mawasiliano kati yako na rafiki/ndugu zako. Sanasana unaweza kuwashitaki kwa kuingilia kwenye mambo yako.
 
Ridhiwani yule aliyeleta utani katika Facebook baada ya kutekwa Kibanda? Mahakama isse order hayo mazungumzo yatumike kama ushahidi ukweli upatikane
 
Ni wapi imesemwa
chadema ni Lwakatare na Lwakatare ni chadema? Marando anaongelea juhudi
chafu za kulifanya tukio la kiongozi mmoja kuwa la chama kizima. Kesi
iliyoko mahakamani ni Jamhuri v. Lwakatare na sio Jamhuri v. Chadema ila
harakati zinafanyika kufoji ushahidi kuonyesha tukio hilo ni la ugaidi
wa chama kizima na sio wa mtu mmoja au wawili. Mwenye akili lazima awe
ameshaelewa Marando anaongelea content ya mkanda au content ya fikra za
wabambikiaji na ubambimbikiaji unakuwa mchafu zaidi unapotaka kubambikia
hata chama ambacho sio sehemu ya mashitaka husika
umesomeka vizuri mkuu
 
Hili tamko limeshapoteza authenticity baada ya baadhi ya details zake za muhimu (namba ya simu), kuonekana kuwa si ya aliyetajwa katika tamko hilo. Kwa mantiki hiyo, nauomba uongozi wa JF, u-freeze thread hii kwanza, uwasiliane na watoa tamko, ili watoe clarification ya mkanganyiko uliotokea. Hapo wasomaji tutakuwa tumetendewa haki maana tangu Zitto alipothibitisha kuwa namba yake iliwekwa na kuitwa kuwa ya Zoka, mimi naona hata hizo nyingine na taarifa zinazozihusu ni unreal na nashindwa kuchangia chochote.

Naomba chondechonde, JF ilinde heshima yake, hasa kwa mambo yenye maslahi ya kitaifa kama haya kwa kuhakikisha tunachokisoma ni kweli, na kweli tupu..

cc Invisible
 
Hivi siku hizi suala likiwepo mahakamani ni ruksa kuliongelea au mimi ndiyo sielewi?hebu nielekezeni wadau.
 
hili ni pigo jingine takatifu kwa ccm,sielewi watachomoka vipi kwenye list hii mpya iliyowekwa hadharani na marando.
Wanaharakati wa chadema tuingie mitaani na kuwaanika hiki kikundi cha kigaidi.
 
tatizo ccm bado wanadhani CDM ni DR.Slaa na Mbowe, kila siku tunawaambie CDM ni taasisi iliyokamilika idara zote; sasa mambo yao yote ya mbinu za kitoto hadharani aibu tupu. we ulishaona mbinu ya kigaidi utungwe na Mwigilu eti Master Planer.
 
Gazeti hili nalo LITAFUNGIWA kama MwanaHalisi... subiria misukosuko itakayolipata
 
tatizo ccm bado wanadhani CDM ni DR.Slaa na Mbowe, kila siku tunawaambie CDM ni taasisi iliyokamilika idara zote; sasa mambo yao yote ya mbinu za kitoto hadharani aibu tupu. we ulishaona mbinu ya kigaidi utungwe na Mwigilu eti Master Planer.
nape mjanja kachomoa!
 
Hata wajioshe vipi swala la ugaidi limewashika pabaya watanzania wameshituka
 
Kama kuna Mungu na kama anawahurumia watu wanye maumivu makali hawezi kunyamazia maumivu aliyoyapata Ulimboka na Kibanda. Kungolewa kucha na meno na jicho! Du! Atawaweka peupe watesaji hao na kuwaadhibu siku moja tu!
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom