Tambiko Ofisini. Tutafika kweli??

Tambiko Ofisini. Tutafika kweli??

nimeshangaa tu. Kumbe kuna watu wanaumiza kichwa juu yangu
Ukiona hivyo jua umeshawapiga bao!
Usijali upuuzi wao piga maombi,pika kazi,
Ipo siku watatafutana uchawi wao na waganga wao wakikuona unazidi kufanikiwa!
 
Katika hali isiyo ya kawaida leo asubuhi nimefika Ofisini kwangu. Si unajua tena mambo ya kujiajiri. Nina ka salon kangu na mtaani kuna salon mbili nyingine. Lakini kufika mlangoni nikakuta kuna kichwa cha kuku, kitamba chekundu na damu. Pembeni kidogo nikaona kuna shimo limechibwa ndani kukiwa na kuku mweupe. Mi sio mtu ya kuamini Mambo ya kishirikina. Nimefanya usafi na kuendelea na biashara yangu.
Lakini kwa nini tunafanyiana hivi. Tunarudisha nyuma.

Umesema huamini mambo ya kishirikina sasa nani anakurudisha nyuma kitambaa au kichwa cha kuku au kuku mweupe?
 
Uswahilini bana, tunarudishan nyuma sana, mi mwezii uliopita niliibiwa laptop yangu na vichaa wa kitaaa
 
katika hali ya kawaida mteja wako akisikia mambo kama haya. Siku nyingne hataogopa kuja hapa saluni.
maadam umeshafanya usafi... Basi endelea na kazi, ila kama inakuuma sana basi kesho rudi na mifupa ya kuku weka hapo na bango likisema asanteni yule kuku nimemla
 
Hayo ni mambo ya mikoa ya pwani
 
Umerudishwa nyuma na nani? kuku?

haha dada hawa wanaokuita mwalimu hawajakosea huwa unakuwa na reasonable questions ambazo zinamfanya mleta thread awe katika ile awkward moment ndani ya dakika 5


 


haha dada hawa wanaokuita mwalimu hawajakosea huwa unakuwa na reasonable questions ambazo zinamfanya mleta thread awe katika ile awkward moment ndani ya dakika 5



aaaa huyu kanishangaza sana. Anasema haamini mambo hayo lakini karudishwa nyuma! ....:]
 
Ukimjua aliyeweka mpe za uso ie mpe live ndo ataacha kuleta huo upuuzi
Wee komaa apo apo jari wateja na weka huduma nzuri na usafi zingatia pia!
 
Uswahilini bana, tunarudishan nyuma sana, mi mwezii uliopita niliibiwa laptop yangu na vichaa wa kitaaa

hata mimi hapo uswahilini kwenu niliibiwa vocha ya 250 iliyotumika..
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom