Tamba na Jicho 👁 la Ustawi wa Jamii Mtaa kwa Mtaa 🇹🇿

Tamba na Jicho 👁 la Ustawi wa Jamii Mtaa kwa Mtaa 🇹🇿

Wasalaam

Leo 24 Julai, 2025 asubuhi, nakiri kupokea taarifa kadhaa kutoka kwa Wananchi wa Kata ya Baraa, Mtaa wa Kibao cha Njano kwa Mrefu, Arusha.

Kwamba, mtu mmoja mzima analea binti wa umri kati ya miaka 8 hadi 10 hivi ambapo yaani ni anampa vipigo tu apendavyo yeye hivyo, mtoto amejaa makovu ya vipigo kila sehemu, ananyimwa chakula, anafungiwa mlango alale nje na mateso mengine aina hiyo hadi shuleni, maendeleo yanasua sua.

KILICHOFUATA: nimewasiliana na ofisi ya mkuu wa mkoa wa Arusha ambapo, maafisa ustawi wa jamii wameelekea eneo la tukio mara moja.

UJUMBE GANI KWA JAMII: tuache kutesa watoto, jicho la ustawi wa jamii linatamba alipo mwanajamii yeyote kwa ushirikiano na wananchi wenye mapenzi mema.

Hima, tuendelee kutamba na jicho la ustawi wa jamii 👁🇹 kuwadaka watu katili wa watoto popote/kokote 🇹🇿✍️

Pia, kumbuka kupiga 116 kituo cha taarifa za watoto. Vilevile, kuna namba za maafisa binafsi na za vituo vya huduma kwa wananchi hapa chini👇zikumbuke, mpe na mwingine.....

Mhe. Waziri Dkt. Gwajima, katika visa vingi vya matukio ya Mauaji, unyanyasaji na matukio mabaya ya kuwatesa watoto ambayo yamekuwa yakitokea katika jamii siku hizi ambayo tumekuwa tukielezwa kuwa sababu ni Wivu wa Mapenzi. Lakini ukifanya utafiti wa kina kabisa utagundua kwamba sababu halisi za kutokea kwa matukio haya ni:-
1. Kukosekana kwa Uaminifu katika Ndoa na kwenye Mahusiano (INFIDELITY).
2. Mwanamke Kumbambikizia Mwanaume, au Mpenzi wake kuhusu Mimba/ Mtoto ambaye siyo wake biologically, yaani PATERNITY FRAUD.

Sababu hizi mbili za hapo juu ndio zinaonekana kuwa zinaongoza kwa kusababisha Matukio mabaya ya Visa vya Mauaji, Vifo na Utesaji kwa Wanandoa, Watoto au wenzi katika siku hizi.

Mhe. Waziri, kutokana na kushamiri kwa matukio haya ya Mauaji kwa Wanandoa, Wapenzi pamoja na Watoto wao, Je, huoni haja ya kuanzisha Mpango wa LAZIMA kwa Wanandoa au Wapenzi wa KUPIMA DNA Mara tu Mtoto anapozaliwa ili kudhibiti na kupunguza kabisa matukio haya mabaya ya Mauji, vifo na mateso kwa Wananchi?

Kwa kuwa Uwaziri wako uko mwishoni Sana kwa Sasa kabla ya kufikia tamati yake, Je, huwezi kutumua siku hizi chache zilizobaki katika Kuandaa Mwongozo au Kanuni za kuwezesha Utekelezaji wa Jambo hili kwa vitendo la kuwalazimisha Wazazi kupima DNA kwa lazima mara tu Mtoto anapozaliwa?
 
Kila nionapo andiko lako Mhe. Waziri napaki gari pembeni nisome kwanza bandiko lako.
Tunakupenda Mhe. Waziri piga kazi kazi.
 
Taarifa haijajitosheleza,
Huyo Binti ni mtoto wa huyo Mwanaume aliyekua anamlea?
Mama wa huyo Binti yuko wapi?

Kama mpaka binti maendeleo yake ya Shule yalikua yana sua sua ina maana kua hayo mateso ameyapitia kwa muda mrefu bila kujulikana,

Watoto waelimishwe kua wanapopata matatizo kama hayo,watoe taarifa kwa Walimu wao Shuleni kama hawana uwezo wa kutoa taarifa Polisi au sehemu nyingine yeyote ile.
 
Upewe Wizara zote uongoze. Hawa wengine kazi kusifu na kulamba viatu.
Tatizo la serikali hii ukimsifu sana waziri, basi mwisho wa siku huondolewa au kuhamishiwa kungine.

Jerry Slaa alisifika sana kwa utendaji wake wa kazi pale wizara ya ardhi. Matapeli ya ardhi yalipoanza kuhenyeshwa kwa kukamatwa, kunyang'anywa ardhi na kurudishwa kwa wamiliki halali, Clinic za maswala ya ardhi kufunguliwa kwa ajili ya kushughulikia maswala ya ardhi.

Ghafla akaondolewa na kwenda kutupwa kwenye liwizara ambalo linaweza kuongozwa hata na Mwijaku.
 
Dawa ni kula kwa mama ntilie na chakula kingine unakipeleka nyumbani kwa ajili ya watoto. Mke akigusa anachezea kwenzi tu mpaka atapojirekebisha.
Msosi atakula ila hapo sitakula chakula kwangu tena, hapo ni lazima nitafute mwanamke mwingine wa kumsaidia kunipikia, yeye abaki kuwa mfanyakazi wa watoto wetu, sishiriki chochote nae
 
Kazi nzuri, ilitakiwa ustawi wa jamii wa Mkoa wapewe taarifa Kwanza.

Au hata wilayani.

kama hawakupewa, ukapewa wewe Waziri, Maana yake kuna Tatizo.
Hapo tafsir ni kwamba Waziri yupo makini anafuatilia shida za watu

Huku chini hawapo serious,hii ni shida kubwa,siku zote huwa tunawapa ushirikiano wanao tupa ushirikiano
 
Wasalaam

Leo 24 Julai, 2025 asubuhi, nakiri kupokea taarifa kadhaa kutoka kwa Wananchi wa Kata ya Baraa, Mtaa wa Kibao cha Njano kwa Mrefu, Arusha.

Kwamba, mtu mmoja mzima analea binti wa umri kati ya miaka 8 hadi 10 hivi ambapo yaani ni anampa vipigo tu apendavyo yeye hivyo, mtoto amejaa makovu ya vipigo kila sehemu, ananyimwa chakula, anafungiwa mlango alale nje na mateso mengine aina hiyo hadi shuleni, maendeleo yanasua sua.

KILICHOFUATA: niliwasiliana na ofisi ya mkuu wa mkoa wa Arusha ambapo, maafisa ustawi wa jamii mara moja walielekea eneo la tukio na kumfikia mtoto. Hii ni kuonesha kuwa, ustawi wa jamii wako speed... wewe tu toa ushirikiano.

Watuhumiwa wataijibu sheria ya mtoto na vifungu vyake.

UJUMBE GANI KWA JAMII: tuache kutesa watoto, jicho la ustawi wa jamii linatamba alipo mwanajamii yeyote kwa ushirikiano na wananchi wenye mapenzi mema.

Hima, tuendelee kutamba na jicho la ustawi wa jamii 👁🇹 kuwadaka watu katili wa watoto popote/kokote 🇹🇿✍️

Pia, kumbuka kupiga 116 kituo cha taarifa za watoto. Vilevile, kuna namba za maafisa binafsi na za vituo vya huduma kwa wananchi hapa chini👇zikumbuke, mpe na mwingine.....
Hii unatia moyo sana Mh waziri maana ni jukumu letu kulea na kulinda ustawi wa watoto.

Hongera kwa kazi yako Njema katiak Taifa letu.
 
Hapo tafsir ni kwamba Waziri yupo makini anafuatilia shida za watu

Huku chini hawapo serious,hii ni shida kubwa,siku zote huwa tunawapa ushirikiano wanao tupa ushirikiano
Kama huko chini hawapo serious,je ni nani anafaa kulaumiwa? Ni nani kiongozi wa hao waliopo chini?

Huoni kua hao waliopo chini,wapo chini ya waziri? Je ni jukumu la nani kuwarekebisha hao waliopo chini au kuwachukulia hatua?
 
Back
Top Bottom