Uchaguzi 2020 TAKUKURU yamshikilia mgombea wa ubunge kupitia CHADEMA jimbo la Mtama kwa tuhuma za kutoa rushwa ili atangazwe kuwa mshindi

Dah huu ssa ndo unaitwa upofu. Yaani mtu katoa rushwa kabisa na imethibitika, lakini eti bado anatetewa. CCM ndo inayoonekana imemfanyia mchezo, basi inaonekana huko CDM watu wote ni malaika hakuna binadamu.
Ndugu yangu mahakama pekee ndiyo inatakiwa kuthibitisha hilo. Hii ni michezo ya kisiasa tu, Mathew amfanya kazi kubwa ya kujenga chama, alijiandaa miaka mitano kushinda, hawezi kujidhalilisha namna hiyo.

Hizo ni mbinu za watu kupita bila kupingwa. Huko Ruangwa watu wamepigwa, huko Morogoro yaani ni aibu tupu. Hivi unawezaje kuwa na furaha ya kupita bila kipingwa kama sio woga wa uchaguzi. Nimemwona mh. Majaliwa akiwa anatoka meno tote nje eti amepita bila kipingwa. Hivi hata aibu haoni?
 
Tuliposema CCM ifute vyama vyote vingine ibaki yenyewe tulikuwa na maana kubwa. Kwa tamaa yao ya madaraka na vyeo wanatengeneza sumu kubwa huku chini ambayo itaangamiza taifa na utaifa wetu.
Wapo wengi wanashangilia upuuzi mwingi ambao unaendelea pasipo kutathmini athari zitakazofuatia.
Siasa zinazoendelea zitatutenganisha upendo na udugu wetu vinaelekea kuzimu sasa.

Usiwe na hofu, vyama vitafutika tuu, pamoja na chama cha Mbowe.
 
Nawaza tu, ikithibitika si kweli, uchaguzi utarudiwa? Maana mtu anaweza hata kumzushia mtu yeyote ili amkomoe kipindi hiki.
 
Unaongea upumbavu halafu unajiona una akili. Waliposema watamfikisha mahakamani unahisi wanaenda kuthibitisha kitu gani?

Yaani bora hata huko CCM kuna wajinga lakini huko Chadema kuna mazuzu.
Wapokee form waendelee na tuhuma zao mpaka mahakama ithibitishe
 
Tupu zenu ziko nje

1598413493954.jpeg
 
Wakristo huamini kwamba Mungu akitaka kukudondosha hukutia kwanza upofu, unakuwa unafikiri unaona kumbe huoni! Ndicho kinatokea sasa kwa CCM. Kama ulivyoandika hapa, huyu mtu ambaye hata hajathibishwa na NEC ampatie rushwa DED kwa ajili ya kumtangaza kushinda?
Hizi dhambi wanazojichotea zitakuja kuwarudi wao, watoto wao na vizazi vyao. Wajue Mungu yupo na anaona

Sent from my SM-A515F using JamiiForums mobile app
 
Haiwezi kuingia akilini hata kidogo.
Ni tuhuma ambazo hazina mantiki kabisa.

Yaani mgombea wa chama cha Upinzani (CHADEMA) aende kumhonga DED (msimamizi wa uchaguzi aliyeletwa kuja kuhakikisha CCM inashinda), tena vimilioni vichache, wakati hata fomu ya kugombea alikuwa bado hajarudisha.

Ni tuhuma za kiuwendawazimu kwa 100%
 
Hao wanaitwa majasiri. Yani hata kampeni bado unaweka mazingira salama. Kama ni kweli basi huyo ni mkali.
 
Back
Top Bottom