Huko sawa kabisa mkuu, cha msingi nadhani ni kutambua kuna mema na changamoto za kilimo cha tikiti. Na vile vile itambulike kuwa kuna walitajirika tena bado wana tajirika katika zao hili.
Tatizo kubwa ninaloliona mimi ni kwamba wale walifanikiwa ni wachache halafu wengi ya hawa wachache ni wachoyo wa kutoa taarifa ama kuamasisha jinsi walivyofikia hayo mafanikio, hii inasikitisha.
Kinachobaki sasa ni kuwa na watu wengi ambao hawajafanikiwa wanaokatisha watu tamaa.
Mimi ni binafsi tikiti nililima kama kujifunza katika eneo dogo sana.
Nilichojifunza
1. Tikiti linahitaji timing nzuri sana, ninapoongelea timing namaanisha kujua muda gani upande ili ukivuna uwe hujakutana na wauzaji wengi sokoni.
2. Tikiti linafaa kupandwa kwa kanuni za kisasa kupata matokeo bora. Hapa namaanisha kuchagua mbegu bora na kupanda kwa kuacha nafasi ya kutosha.
3. Madawa ni ya muhimu sana kupigwa kwa wakati.
4. Periodic inspication ya shamba ni muhimu sana sana.
Nina mpago mkakati ambao nilipewa na rafiki yangu hiko kwenye hard copy. Kwa anayetaka niko tayari kumpatia imeandikwa na mhadhiri wa chuo cha Sokoine.
Vijana tupende kusaidiana wakuu.