Tajiri Mo itisha kikao cha Ukoo utuletee Mayele na Feitoto

Tajiri Mo itisha kikao cha Ukoo utuletee Mayele na Feitoto

Naomba tajiri uitishe kikao cha ukoo mapema sana ili waidhinishe fedha utuletee Mayele na Feitoto kabla dirisha halijafungwa.

Wanatupigia kelele sana huku mtaani. Pia natoa wito kwa mashangazi, mashemeji na dada za Moo msimkwamishe tafadhali.
Bora ww Ponjoro mwenzie useme, labda atakusikia.
 
Wazee wa kuchimba dawa
 

Attachments

  • 1785260576190.jpg
    1785260576190.jpg
    52 KB · Views: 8
Naomba tajiri uitishe kikao cha ukoo mapema sana ili waidhinishe fedha utuletee Mayele na Feitoto kabla dirisha halijafungwa.

Wanatupigia kelele sana huku mtaani. Pia natoa wito kwa mashangazi, mashemeji na dada za Moo msimkwamishe tafadhali.
Haaaa haaaaa.....Ponjoro yule bahiri balaa.
 
Msimamizi wa mirathi anawaita warithi?

Yanga ndiyo timu pekee ya mpira wa miguu hapa chini Tanzania
 
Tatizo lonalo tutesa Simba ni Misifa ya GSM. Yule Bwana Garbu saidi Mohamed na mwenzake injinia ni misifatu.


Sio kwamba Wana hela kama Bwana mo ila boss wetu Ni mbaili sana ndio kinacho tuangusha Simba ubahili wa mo.


Kule utopoloni tajiri wao ni Mr Misifa.
 
Kwa kifupi MO asipobadilika atateseka sana hapo Simba na ataendelea kuwatesa wapenzi, mashabiki na wanachama wa Simba. Na Simba itateseka sana mpaka wanachama akili ziwakae. Kule Yanga Hersi na GSM ndio wametangulia mbele wanaonekana lakini huku nyuma kuna matajiri kibao wanachanga pesa kwa ajili ya usajili na kuendesha timu. Na sio kitu kigeni kwani hata "friends of Simba" ndio walikuwa wanautumia huu mfumo na uliwatesa sana Yanga kipindi kile. Sasa hivi wakati MO anajadiliana na kulialia apunguziwe fedha za usajili kwa mchezaji fulani wenzake upande wa pili nao wakimhitaji huyo huyo mchezaji wanaitana wanapiga "donations" fasta Hersi anapewa mzigo anaenda pindua meza Simba wanabaki wameduwaa.

Shida ya MO yupo peke yake na hataki watu wengine waingie kwa sababu anazojua yeye. Walau basi angefanya juhudi mchakato wa kuruhusu wanachama wapya waingie walau ingempunguzia maumivu ya yeye kutumia pesa nyingi peke yake kwani ada za uanachama zingemsaidia asitoe pesa nyingi peke yake. Mo alimkubali tu Hanspope (RIP) na alikuwa anajitolea sana na fitina za mpira alikuwa anaziweza ndio maana wakati ule Yanga wakitaka kusajili mchezaji ghafla unashtukia yupo Simba.

Kwa kifupi kusipokuwa na mabadiliko ya haraka pale Simba basi wanachama na wapenzi watakuwa wanaendelea kushangaa tu mchezaji fulani mzuri Simba wanaanza kumfuatilia mwisho wa siku anaishia Yanga. Na mabdiliko ni mawili tu aidha Mo akubali matajiri wengine na wanachama maarufu wapewe nafasi pale Simba yeye awe msimamizi wao kama anavyofanya GSM au waanze mchakato wa wanachama wapya ili klabu iingize pesa za ziada. Vinginevyo huu mburuzo hautaisha leo wala kesho na hata Yanga wanaposema watabeba "back to back" miaka kumi mfululizo wanaamanisha maana wameshaona huo udhaifu pale Simba.
 
Back
Top Bottom