Tafadhali Rais Samia... Hakuna anayekuamini...

Ni vigumu kuaminika kuwa uliguswa, kuumizwa, kustushwa au kuchukizwa na matukio ya Oktoba 29, 2025. Ni vigumu kufanya watu wasadiki kuwa wewebkama Rais wa nchi yetu hujui kilichotokea au hata kufanya jitihada za kutaka kujua...
Mimi nitaendelea kukumbusha tu, hiyo heshima unayompa mtu asiyeistahili sijui unalenga kitu gani.
Ukimwita tu Samia haitoshi hadi umpe heshima na cheo kisichoendana kabisa na hadhi yake?

Hilo moja.

Mbona unakuwa na mashaka juu ya anachoamini Samia hadi utake kumlazimisha afanye kinyume na uamini wake.
Hujasikia kauli zake mbalimbali juu ya swala hilo hilo la "kujutia"?

Au labda nikupe mfano ulio karibu naye:

Bi Asha Migiro ambaye ni Katibu Mkuu wa Chama kasema waziwazi kwamba "vyombo vya dola vilifanya kazi ya kutukuka", unaeleewa maana ya maneno hayo?
hayo anaweza kuyasema Katibu Mkuu wa chama; na Mwenyekiti wake awe na msimamo tofauti?

Jameni, kwa nini mnatafuta kumlazimisha Samia jambo ambalo haliamini kabisa. Aguswe na watu waliotaka kumnyima fursa ya kuwa mtawala (kwa uamini na fikra zake)?
 
💯%.
 
Paskali uandishi wako unapaswa kuwaamsha WaTanganyika wengi waliolala!
Anyways, tuendelee kukusanya ushahidi wa kimazingira!
Duh!

Kuna Paskali mwingine au huyu huyu mwenye magazeti?

Kama ni huyu wa magazeti, nitakuomba wewe, mkuu 'Mfikirishi' uniunganishe na makala/habari iliyokusisimua na kuona kwamba itaamsha waTanganyika wengi waliolala!

Kama unayo, naomba uitupie hapa na sisi wengine tupate kuisoma na pengine tutoke usingizini kama ulivyotoka wewe.
 
Mkuu katibu wa chama kasema juzi hapa kuwa POLISI WALIFANYA ILIYOTUKUKA.
Pia mwenyekiti sa💯 alisema kuwa polisi walifanya kazi nzuri kwa muda mfupi.
Sasa atueleze hii tume aliyyounda juzi ni ya kazi gani?
 
Huu msemo huwa unanikera kwelikweli; sasa wewe ukaona uusilibe kabisa kwenye maoni yangu!
Basi tu sina la kufanya.
Hahahaa. Relax bana. Yaani hapo maana yake ni kwamba nimekubaliana na wewe kwenye kila kitu ulichokiandika mpaka nikakosa maneno ya kuandika.

Btw, Victor Wembanyama is going to the NBA Finals……
 
Unasema tume? Tume ambazo ripoti zake ni mali yake binafsi!?
 
- hujajaribu kujua au kukutana waliopoteza ndugu zao. Yaani, wale watoto/vijana waliouwa pale Mwanza hutaki kujua wazazi wao? Na yule mama na mwanae waliouawa mbele ya kamera hutaki kabisa kujua?
Maana ya mada hii hasa ni nini?

Unampa Samia ushauri ili ajitakase kwa maovu aliyoyafanya?

Mbona amechelewa sana!

Lakini pia ngoja nikukumbushe kama umesahau.
Jitihada za Samia kujitakasa zinaendelea hata bila ya yeye kufanya hayo unayomshauri.
Yeye anazo njia zake anazoziamini.
Kaunda hizo tume na mwisho wa siku ataanzisha mazungumzo/maridhiano anayofikiri yeye yatahitimisha na kufunga 'chapter' nzima ya hahya yaliyotokea.

Sijui kama katika mipango yake hii ya kujitakasa kaweka vipengere vinavyohusu waTanzania kuukata mpango mzima wa ulaghai wake.

Ataendelea kupoteza na kuua waTanzania hadi lini?
 
Tena ngoja nikutupe kwenye Dustbin chap ,huvumiliki


Hilo Mwashambwa na Tlaatlaah, mimi nilikwishayatupa jalalani muda mrefu, nikayapeleka huko kwenye Ignore list. Kujadiliana na watu wanaoshabilia mauaji, kimsingi majitu ambayo ni uzao wa shetani, ni kuyapatia heshima yasiyostahili:

Ignore Mwashambwa, Tlaatlaah, Dr wa Manesi.
 
Kwani hujui hata wajinga huzeeka na kuota Mvi? Au unafikiri Umri unaongeza akili? Kama huna akili ni huna tu hata ungeota Mvi kichwani. Hata majambazi huzeeka na ujambazi wao
Kupitia wewe leo nimeamini kweli kichaa huwaona watu timamu kuwa wao ndiyo vichaa.
Wewe unajilinganisha utimamu, au kiwango cha ujinga na Mzee Mwanakijiji ?
 
Mmmmh !
Maridhiano ya kweli kweli kabisa ni muhimu katika kutatua mgogoro wowote ule mahali popote pale mgogoro utakapokuwa umetokea !
 
Wahanga wote wameahidiwa matibabu na uangalizi wa bure, anataka Mheshimiwa SSH awe anaamka asubuhi na kuwapigia simu kujua wamelala vipi!.

Ukiwa kiongozi mkuu wa nchi huna tofauti na jalala, kila mtu lazima atakukosoa, kukushauri, kukukebehi na wachache sana watakithamini kile unachokifanya.
 
Majibu kama haya yanamstahili mvuta banging au mtu mwenye ufanano na ex mkimbiza mwenge Kenani Kihongosi
Hiyo tume ameunda sio kutafuta ukweli bali simply ku buy time baada ya waangalizi wote wa uchaguzi isipokuwa wa makomred wake EAC kuonyesha uchaguzi ulikuwa ni komedy tuu huku mauuji yakilaaniwa waziwazi na rais wa Namibia, wa staafu wa Botswana na South Africa ,EU nk
Nakualika Arusha uongee na familia ya yule mama mja mzito aloyepigwa risasi na goons sijui na askari wa RCO Mahita ,askari wa Uganda au KMKM uweze kusikia maumivu yao ujue kusifia kina Wambura ni ukichaa uliojificha.
 
Moja ya kauli ya kipumbavu kabisa kuwahi kutolewa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…