Tabora iliyodidimia inahitaji kuinuliwa...

Tabora iliyodidimia inahitaji kuinuliwa...

Bro nimesoma Tabora Boys pale 2005/07 at the Heart of Tabora, ukiangalia waliokua wanakuja kama intake ya either form one au Five 98.5% ni wageni hasa toka Kanda ya ziwa na huku dsm, moro, kusini na kaskazini. Wazawa shule zao ni zile za kawaida za day pale mjini na wengi utawakuta wakisaka CREDIT kwa kureseat ili wapate japo nafasi za uaskari.

Kikubwa mwamko wa elimu alipokaa mwarabu hua mdogo sana. Kwanza ukipata div2 unajulikana pale town pote na mara nyingi tulikua tunaheshmika sana wanafunzi wa Tabora boys kwa kua walikua wakituona kama malaika wa mji ule. Kuna zaidi ya elimu kuwapatia wananchi wa Tabora coz resources walizonazo ni zaidi ya wanavyodhaniz.

Mzalendo JR; you are right BUT in a wrong way! Kumbuka wewe na wenzio mliokwenda Tabora Boys - (and it is a special school remember) - na shule nyingine za serikali MLICHAGULIWA kwenda huko. Inawezekana hulijui hili, ila kuna sera ya kuchagua wanafunzi kutoka mkoa/mikoa mingine. Kwa mfano, mimi kwetu ni Tabora lakini nilisoma Mazengo - na nilikuwa na wenzangu kama 10 hivi (japo toka wilaya tofauti za mkoa wa Tabora) na hakukuwa na mwanafunzi hata mmoja kutoka Dodoma kwenye darasa letu.

Ningekuelewa ungesema kuwa hata shule za day wazawa hawapo.
 
Kumbuka kuwa bottom line ya kusoma kwako ni pesa. Je unajuwa uchumi mkubwa sio tu wa tabora bali hata Tanganyika nzima umeshikwa na watu gani?

tatizo la tabora ni wenyeji kujitenga na maendeleo kuwaachia wageni. Utaona ukiondoa matajiri waarabu wengine labda wenye vijisenti ni wachaga akina WADADU na mwenyeji ni Contructor Mabula.

Kumbuka kila ngoma ina wenyewe, Je tabora wenyewe wapo wapi?


Asante kaka, ila kumbuka Tabora boys ni shule ya serikali na wakati huo mi naigia A-level ada ya O-level ilikua 40 kwa mwaka na A-level ni 70 elfu tu. Mi hapa nazungumzia jitihada hafifu za wazawa wa mkoa huu juu ya elimu kiasi cha kufeli kwa watoto wao kua ni kama sheria(by law). Zao la hawa ni kua wakulima wa tumbaku ila ni ule tunaouita Substansive farming kwa matumizi ya kujikimu tu kwa mwaka. Mwaka 2004 watoto tuliomaliza form 4 na kufaulu kwenda kidato cha tano 2005 tulikua kunafahamiana, na wote wazazi wetu wako Tabora kikazi kiasi kwamba tulikua tunafahamiana na hata leo twawasiliana......!

Setback kuu ni mizizi ya kutofanya kazi na kukaa vijiweni kpata kahawa kwa wazawa wa Tabora hasa wazazi wetu wa mkoa huu. Watoto wakimaliza form4 au kuishia kidato cha pili basi hua walanguzi wa maziwa kijijini na kuleta mjini kuuza au wakulima wa nyanya na vitunguu basi. Tembelea eneo lote la Kanyenye, kachoma, tukutuku ni vilabu mtaa mzima na gest bubu.
 
Ndo maana mimi binafsi napata shaka saana na moyo wa kizalendo wanaojifanya wanao watu hawa, kiasi cha kuomba au kufikiria ridhaa ya kuongoza nchi 1.Samuel Sitta. na Prof Ibrahim Haruna Lipumba , hivi kweli viongozi hawa wameshindwa kuwasaidia wakazi wa Tabora kujiinua kiuchumi kutokana na fursa walizonazo kisiasa ndani ya nchi na nje ya nchi. Kama alivyojaribu kufanya Mh, Augustino Lyatonga Mrema kwa wananchi wa Kilimanjaro ktk zao la kahawa. binafsi nawachukia saaaaana 1. Kapuya 2. Sitta 3. M, sitta na wengine wenye uwezo wa kuwasaidia wakaazi wa Tabora , huku wakijikweza kuwa wanauchungu na nchi.
 
Hahaha Sikonge umenikumbusha mbali sana enzi nipo Tabora Boys. Tulikuwa na rafiki yetu mmoja yeye alikuwa anakuwa anatukaribisha kwao maeneo ya Kanyenye au Ng'ambo kama sijasahau, nakumbuka tulikuwa tunapikiwa nsansa za karanga aisee unsahau ule ugali wa dona la maharage ya Alexander Ndeki (Nasikia huyu ni marhum kwa sasa).

Nilichokiona pale Tabora ni kimoja, mzunguuko wa pesa ulikuwa mdogo sana, kingine kama nilivyokuwa wakati huo vibanda vya kahawa vilikuwa vingi ikiingia jioni. Mazungumzo makuu sehemu hizi yalikuwa ni kujadili watu wenye mafanikio na jinsi walivyofanikiwa na hata kusema yule mtoto amezaliwa tunamuona.

Kuna jamaa aliwahi kuniambia siku za karibuni kuwa miji yote iliyokaliwa na waarabu kwa muda mrefu wakazi wake wanakuwa hawana wasiwasi na maendeleo. Ila kwa mji wa Tabora kikubwa kinacho changia ni land locked region inayotegemea zaidi reli ya kati zaidi ya barabara kama Kigoma. Elimu katika mikoa hii ukiangalia wanaosoma zaidi ni wageni zaidi ya wakazi ambao haipi kipaumbele sana. wanaojenga kwa wingi Tabora ni watu wa kuja kama wachaga n.k ambao ni wafanya biashara maarufu hapo Tabora. Wahindi wao wapo ila wanaishi kwenye nyumba za Msajili.

Tabora ina neema nyingi sana kama asali, tumbaku, karanga na mazao mengi ya chakula, tabu kubwa ni soko kwani wengi wa wakulima wanajikuta wanadhulumiwa na wafanyabiashara wajanja ambao hununua kwa bei za kutupa kutokana na ufahamu mdogo na soko kuwa gumu. Majority ya nyumba za katikati mji ni za biscuit kwani ndiyo hasa wanazokaa wana-Tabora asilia ambao ndiyo kuna vibanda vingi vya kahawa na mihogo ya makopa na karanga + Kashata.

Kuna wakati kulikuwa na dhana ya kwamba vijana wazawa wanaofanikiwa na kuwasaidia wazazi wao basi huwa wanashughulikiwa kisayansi ya Sheikh Yahya na kupoteza maisha hivyo wengi kujikuta wanaogopa kuendeleza miji yao kwa hofu ya kushughulikuwa kienyeji.

Tatizo lingine nililoliona pale Tabora ni watu kuridhika na maisha hasa kama ana uhakika wa asubuhi kunywa chai na makopa, mchana ugali na mlenda/kihembe/nsansa/kauzu/ngege/kisamvu/mchunga/ et al. Kwa ujumla uswahili ni mwingi sana Tabora hakuna tofauti na Tanga/ Kigoma/ Bagamoyo/ Plus mikoa yote yenye influence ya mwarabu.

Kuna hitajika sana elimu katika mikoa hii ili kushindana na hali halisi ya mentali za wakazi wake ambao kila kitu hukimbilia kujifariji kuwa KAZI YA MUNGU.


Well said!
 
Miji iliyojengwa na waarabu haikui.....ongeza na Kigoma pia
 
Tatizo la Tabora ni wazawa wenyewe: we angalia wazawa walioendela hata majumbani kwao in Tabora kuko hovyo kuliko unavyoweza kudhania, just check home kwao na Prof Lipumba palivyokuwa!!!!!!
 
Tatizo la Tabora ni wenyeji wenyewe; angalia hata wenyeji wa Tabora walioendelea kielimu/kiuchumi their home places ziko hovyo kinyume na status zao; mfano ni home place ya Prof Lipumba!!!!! If that is the case unategemea kuna wa kuleta maendeleo at the regional level?
 
TUMBAKU, TUMBAKU, TUMBAKU, zao hili halimneemeshi mkulima aslan bali kumuangamiza tu kiafya na KUHARIBU mazingira, sasa hivi Tabora inaongoza kwa JOTO nchini. Pana zao la ALIZETI lakini linapigwa vita mno kulimwa sababu ya tumbaku. Wanyamwezi bwana waajabu kweli kweli, akipanda train tu kwenda Mzizima anajiendeleza na kuhamia Kigamboni!
 
Tatizo ni SERA na sio WAARABU. Angalia Mzizima inavokimbia kimaendeleo Msimbazi siku hizi ni Waswahili na Wachina ndio wengi. Mbona nchi za Waarabu zinapiga hatua kimaendeleo? Nimeambiwa ni mbunge mmoja tu ambaye aliishi Tabora kabla na baada ya kuchaguliwa nae ni NDUGU Paulo Misigalo, wengi wao hutumwa na utamkuta MGUU mmoja Mzizima na mwengine (usio muhimu) Tabora. Tafakari!
Hahaha Sikonge umenikumbusha mbali sana enzi nipo Tabora Boys. Tulikuwa na rafiki yetu mmoja yeye alikuwa anakuwa anatukaribisha kwao maeneo ya Kanyenye au Ng'ambo kama sijasahau, nakumbuka tulikuwa tunapikiwa nsansa za karanga aisee unsahau ule ugali wa dona la maharage ya Alexander Ndeki (Nasikia huyu ni marhum kwa sasa).

Nilichokiona pale Tabora ni kimoja, mzunguuko wa pesa ulikuwa mdogo sana, kingine kama nilivyokuwa wakati huo vibanda vya kahawa vilikuwa vingi ikiingia jioni. Mazungumzo makuu sehemu hizi yalikuwa ni kujadili watu wenye mafanikio na jinsi walivyofanikiwa na hata kusema yule mtoto amezaliwa tunamuona.

Kuna jamaa aliwahi kuniambia siku za karibuni kuwa miji yote iliyokaliwa na waarabu kwa muda mrefu wakazi wake wanakuwa hawana wasiwasi na maendeleo. Ila kwa mji wa Tabora kikubwa kinacho changia ni land locked region inayotegemea zaidi reli ya kati zaidi ya barabara kama Kigoma. Elimu katika mikoa hii ukiangalia wanaosoma zaidi ni wageni zaidi ya wakazi ambao haipi kipaumbele sana. wanaojenga kwa wingi Tabora ni watu wa kuja kama wachaga n.k ambao ni wafanya biashara maarufu hapo Tabora. Wahindi wao wapo ila wanaishi kwenye nyumba za Msajili.

Tabora ina neema nyingi sana kama asali, tumbaku, karanga na mazao mengi ya chakula, tabu kubwa ni soko kwani wengi wa wakulima wanajikuta wanadhulumiwa na wafanyabiashara wajanja ambao hununua kwa bei za kutupa kutokana na ufahamu mdogo na soko kuwa gumu. Majority ya nyumba za katikati mji ni za biscuit kwani ndiyo hasa wanazokaa wana-Tabora asilia ambao ndiyo kuna vibanda vingi vya kahawa na mihogo ya makopa na karanga + Kashata.

Kuna wakati kulikuwa na dhana ya kwamba vijana wazawa wanaofanikiwa na kuwasaidia wazazi wao basi huwa wanashughulikiwa kisayansi ya Sheikh Yahya na kupoteza maisha hivyo wengi kujikuta wanaogopa kuendeleza miji yao kwa hofu ya kushughulikuwa kienyeji.

Tatizo lingine nililoliona pale Tabora ni watu kuridhika na maisha hasa kama ana uhakika wa asubuhi kunywa chai na makopa, mchana ugali na mlenda/kihembe/nsansa/kauzu/ngege/kisamvu/mchunga/ et al. Kwa ujumla uswahili ni mwingi sana Tabora hakuna tofauti na Tanga/ Kigoma/ Bagamoyo/ Plus mikoa yote yenye influence ya mwarabu.

Kuna hitajika sana elimu katika mikoa hii ili kushindana na hali halisi ya mentali za wakazi wake ambao kila kitu hukimbilia kujifariji kuwa KAZI YA MUNGU.
 
Wenyeji wa Tabora ni wakarimu, nakumbuka baada ya mbarara kali za nyali, unyuka au umwamba, ukimiss unashuka zako kariakoo au ng'ambo kuchukua Nyangala.. Asikwambie mtu nyangala za Tabora ni tamu mno, Watoto wa Afande Warioba pale TS wamenielewa .
 
TUMBAKU, TUMBAKU, TUMBAKU, zao hili halimneemeshi mkulima aslan bali kumuangamiza tu kiafya na KUHARIBU mazingira, sasa hivi Tabora inaongoza kwa JOTO nchini. Pana zao la ALIZETI lakini linapigwa vita mno kulimwa sababu ya tumbaku. Wanyamwezi bwana waajabu kweli kweli, akipanda train tu kwenda Mzizima anajiendeleza na kuhamia Kigamboni!

Leo sijui ilitokea bahati mbaya gani wakati natafuta station kwenye redio yangu nikakutana na TBCCCNM nikataka kubadilisha lakini nikamsikia Malima Nderema nikataka nijikumbushe kidogo enzi zile alikuwa napenda ngoma za kienyeji. Kwenye kipindi chake alikuwa na mgeni wake kutoka Tabora nia hasa ilikuwa ni kuongelea ngoma za usukumani lakini kabla ya yote alianza kumulizia hali ya maisha huko tabora, ndipo alipotoboa kitu cha ajabu ambacho hata malima nadhani hadi sasa atakuwa hajaamini. Mimi pia nataka apatikane mtu hapa athibitishe hilo.

Mzee huyu alipoulizwa kuhusu zao la tumbaku akasema yaani chama chao cha tumbaku kimewalazimisha kuwakata 50% ya malipo yao iliwafidie hasara ya chama chao cha ushirika. Alipoulizwa wewe mwaka huu ulipata shilingi ngapi za tumbaku yako akasema alipata 1,600,000 lakini ameambulia 800,000 zingine NGHI zimekatwa! Mzee alipoulizwa kwanini wanafanya hivyo, bila kumng'unya maneno akasema ni ufisadi tu wa serikali.

Wakuu kama kuna mwanaTabora hapa JF ajaribu kufatilia hiki kitu maana imetuduwaza mimi na malima nderema wa TBCCCM!
 
Tabora utatalii nini? Matoborwa?

Dhahabu yenyewe wanauza akina Junius kwa kuipeleka Uarabuni.

Na kesho wanadai hawataki Muungano.......

Ngoja tubaki tu tunajilia ugali wa Nsansa na kuichagua CCM yetu. Kesho tunaamkia Kihembe ........

Naona umekata tamaa kabisa umebaki unakula nsansa na kihembe bila kusahau matoworya na ntalali, mbaya zaidi hata asali ambayo labda ingekuwa mkombozi nayo wataalamu wanasema ina nicotine na misitu ya mininga ya kule Malongwe nayo imekwisha.
 
Mzalendo JR; you are right BUT in a wrong way! Kumbuka wewe na wenzio mliokwenda Tabora Boys - (and it is a special school remember) - na shule nyingine za serikali MLICHAGULIWA kwenda huko. Inawezekana hulijui hili, ila kuna sera ya kuchagua wanafunzi kutoka mkoa/mikoa mingine. Kwa mfano, mimi kwetu ni Tabora lakini nilisoma Mazengo - na nilikuwa na wenzangu kama 10 hivi (japo toka wilaya tofauti za mkoa wa Tabora) na hakukuwa na mwanafunzi hata mmoja kutoka Dodoma kwenye darasa letu.

Ningekuelewa ungesema kuwa hata shule za day wazawa hawapo.

Ni kweli Mazengo kwa O-level ilikuwa ukiona mtu ametoka palepale Dodoma ujue huyo alikuwa ni mkali flani but wengi walikuwa wanasoma day k.m Dodoma secondary labda kwa A-level ndio utakuta wanafunzi wa palepale. shule nyingi za boarding kwa miaka niliyosoma mie ilikuwa huwezi kuingia hivihivi lazima uwe umepiga sana na wengi walikuwa wanatoka nje ya mkoa wa shule ilipo. Ingekuwa labda kwa shule zile za day zinajazwa na wageni hapo ni sawa tunaweza sema kazi inahitajika kuhamasisha wazawa wa Tabora wanapeleka watoto wao.
 
Nzega na Igunga inakuja kasi muda si mrefu zinaweza kuunda mkoa mwingine changanya siku hizi kuunda mkoa mpya ni deal, sasa Igunga na Nzega zikijitenga toka Tabora si ndio itadidimia kabisa inakuwa kama vile mkoa wa Njombe ulivyoanzishwa imesababisha mkoa wa Iringa kubaki na wilaya chache zenye uchumi mkubwa wakati wilaya ya Njombe (Njombe mjini na Makambako) pekee zilikuwa ni sehemu ambazo zipo juu kiuchumi
 
Tabora kuna wasomi wengi sana,wote wamekimbilia DAR,tatizo la mkoa ni kwamba hamna hata kiwanda kimoja,kuna wkorea sijui wachina sasa hivi wanavuna mazao ya misitu(asali,nyuki) wameanzisha mashamba darasa vijijini.
wanabeba asali na nyuki wazima wanapeleka makwao,wanyeji wamekalia kulima tumbaku tu,kiwanda cha tumbaku chenyewe kipo mkorogoro.
pale Tabora mjini kila muhula wanabadilisha mbunge,ukiangalia mji wa urambo na kaliua wageni(waha) ndio wameinvest na kuleta develop miji hiyo.
 
Mkuu, mie sijakata tamaa.Ndiyo maana unaniona hapa JF mara kwa mara. Nikizidiwa shughuli nakimbia ili kutafuta hela ya sadaka maana Jumapili si mbali na Mchungaji inabidi apewe sadaka na Jenga kanisa lako.

Huo ndiyo ukweli wa Sikonge. Ila siku ikiunganishwa na mikoa mingine basi maendeleo yatafika kwa kasi.

Ukifika Sikonge kama hujafika siku nyingi basi utashangaa kidogo maana pamebadilika sana. Ukiacha umeme na waya za umeme, kuna watu wanajenga hadi maghorofa binafsi. Kistandi cha bus kimetulia ingawa bado cha vumbi.

Anyway, kuna siku ntakaa niiandike makala kuhusu Tabora na kuituma hapa.....
Naona umekata tamaa kabisa umebaki unakula nsansa na kihembe bila kusahau matoworya na ntalali, mbaya zaidi hata asali ambayo labda ingekuwa mkombozi nayo wataalamu wanasema ina nicotine na misitu ya mininga ya kule Malongwe nayo imekwisha.
 
Mkuu, mie sijakata tamaa.Ndiyo maana unaniona hapa JF mara kwa mara. Nikizidiwa shughuli nakimbia ili kutafuta hela ya sadaka maana Jumapili si mbali na Mchungaji inabidi apewe sadaka na Jenga kanisa lako.

Huo ndiyo ukweli wa Sikonge. Ila siku ikiunganishwa na mikoa mingine basi maendeleo yatafika kwa kasi.

Ukifika Sikonge kama hujafika siku nyingi basi utashangaa kidogo maana pamebadilika sana. Ukiacha umeme na waya za umeme, kuna watu wanajenga hadi maghorofa binafsi. Kistandi cha bus kimetulia ingawa bado cha vumbi.

Anyway, kuna siku ntakaa niiandike makala kuhusu Tabora na kuituma hapa.....

Kiukweli Sikonge, nilichojifunza ni kwamba hii nchi si kubwa kama watu wanavyofikiria tatizo ni miundombinu tu. Mfano mtu anatoka Mwanza kwenda Mbeya unakuta anakwenda mpaka Morogoro kisha anapita Iringa mpaka Mbeya wakati kama miundombinu ingeboreshwa angekuwa na option ya kupitia Dodoma kisha Mtera - Iringa then Mbeya au kama barabara ya Nzega - Tabora - Sikonge - Chunya - Mbeya ingekuwa ktk kiwango cha lami maana yake mtu angekuwa anatumia masaa machache kufika Mbeya kisha anaunganisha magari kama anakwenda Tunduma mpaka Zambia mpaka DRC (Lubumbashi) pia kama barabara ya Sikonge - Mpanda - Sumbawanga nayo ingeboreshwa maana yake pia safari za kuunganisha mikoa ya Mwanza - Tabora - Sikonge - Mpanda mpaka Sumbawanga achilia mbali hii barabara ya Kigoma kupitia Urambo na Kaliua. (pongezi kwa kampuni ya mabasi ya Sabena inajitahidi kufanya safari katika mazingira hayo kutoka Mwanza to Mbeya via Sikonge)

Ninaungana na wewe kwamba miundombinu hii ikitengenezwa itakuwa rahisi ku-promote shughuli mbalimbali za kiuchumi ikiwa pamoja na kusafirisha bidhaa mbalimbali kutoka sehemu moja kwenda sehemu nyingine plus intervention ndogondogo kama kuuza maji na biscuit maeneo ya stand pamoja na biashara za guest house kwa watu wanaounganisha safari.

Ni imani yangu kuna future nzuri kuhusu Tabora kama miundo mbinu ikipewa kipaumbele maana kwa mtu anaetoka Arusha kwenda Sumbawanga au Mbeya inakuwa rahisi sana kupitia Singida - Itigi - Tabora - Sumbawanga kuliko kuonyoosha kuitafuta Chalinze maana mpaka afike Mbeya saa 4 usiku analala alafu anaendelea na safari kesho yake kwenda Sumbawanga wakati kwa njia ya Tabora kutoka Arusha anaweza akafika Sumbawanga siku hiyohiyo tu. (kikubwa hapa kutakuwa na vishughuli vingi vinavyotegemeana na taasisi mbalimbali za elimu kama chuo cha ardhi na uhazili vikaboreshwa vikaanza kutoa shahada mbona patakuwa poa sana, mfano mzuri unaonekana kwa Dodoma ambayo since 2007 mpaka sasa kuna mabadiliko makubwa sana baada ya kuunganishwa na barabara pia kujengwa taasisi za elimu tofauti na miaka ya nyuma)
 
Last edited by a moderator:
Tabora kuna wasomi wengi sana,wote wamekimbilia DAR,tatizo la mkoa ni kwamba hamna hata kiwanda kimoja,kuna wkorea sijui wachina sasa hivi wanavuna mazao ya misitu(asali,nyuki) wameanzisha mashamba darasa vijijini.
wanabeba asali na nyuki wazima wanapeleka makwao,wanyeji wamekalia kulima tumbaku tu,kiwanda cha tumbaku chenyewe kipo mkorogoro.
pale Tabora mjini kila muhula wanabadilisha mbunge,ukiangalia mji wa urambo na kaliua wageni(waha) ndio wameinvest na kuleta develop miji hiyo.

Kiukweli tumbaku ni zao ambalo linaharibu ardhi though lina faida maana katika sehemu ambazo linalimwa mara nyingi huwa mazao mengine hayastawi vizuri maana yake sehemu wanazolima tumbaku huwa pana njaa (kigezo cha njaa kwa vijijini ni ile hali ya watu kutegemea kununua vyakula kitu ambacho kwa kijijini si cha kawaida), nilipita maeneo flani wilaya Serengeti nikakuta watu wamekomaa na kulima tumbaku huku wanatumia kuni kukaushia tumbaku na mistu iliyofunga hakuna (vipo vichaka tu) nikakumbuka jinsi tabora ilivyokuwa enzi hizo lakini sasa maeneo mengi yapo empty (jangwa kiaina) kwa huko itakuaje.
 
Tabora utatalii nini? Matoborwa?

Dhahabu yenyewe wanauza akina Junius kwa kuipeleka Uarabuni.

Na kesho wanadai hawataki Muungano.......

Ngoja tubaki tu tunajilia ugali wa Nsansa na kuichagua CCM yetu. Kesho tunaamkia Kihembe ........

Mkuu Sikonge, usilalamike, toa ushauri nini kifanyike. Haya sasa, nasikia dhahabu imeanza kufumuka kule Kitunda. Wanyamwezi wenzio wa mkoa wa Tabora hasa wilaya yako ya Sikonge wamelala tu; machimbo ya Kitunda yamejaa wachimbaji wadogo toka melelani, Kahama nk.
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom