Tabora iliyodidimia inahitaji kuinuliwa...

Tabora iliyodidimia inahitaji kuinuliwa...

Barubaru,

..unaposema Waswahili wamewekeza una maanisha wale wenye nywele za singa?

..je, wenye nywele kipilipili wana kasoro gani wasiweze kuwekeza kwenye biashara ya mafuta, majumba, etc etc?

..katika kutembea kwangu nchi hii sijaona mswahili mwenye nywele za singa ameshika jembe analima.

..nadhani wanaozungumziwa hapa kwamba wana hali ngumu ni wana Tabora, Wanyamwezi kindakindaki.

..kuna MIFUMO imekuwepo TANGANYIKA tangu enzi za UKOLONI ambayo inazuia wenye nywele za kipilipili kumiliki BIASHARA KUBWA.

Nafikiri unatakiwa kujitambua na kuacha kuficha ukweli na kutukuza uongo.

Hakuna Sera hiyo (NILIPO RED) kwani huo utakuwa ubaguzi wa rangi jambo ambalo TZ ni muasisi wa sera hiyo sio tu ndani ya Afrika bali pia katika UN.

Mimi nimekaa sana Tanzania na kufanya kazi sana Tanganyika katika mikoa mbalimbali. Tabora ni asli nako na najua fika kuwa watu wenye nywele ngumu wamekuwa waoga sana kujenga kwao nyumba nzuri au kuanzisha investment kubwa kubwa kwao wakiogopa Uchawi na kurogwa, kitu ambacho kwa waarabu au wahindi hakipo kabisa.

Kwa waarab tuna usemi mmoja (nitauweka katika tafsiri isiyorasmi kwa kiswahili). Waarabu wanasema, Kila palipo mwan'Adam unapimwa kwa kile unachoifanyia jamii kwa mikono yako, mali yako na ilmu yako. Na Mola atakulipa kwa hilo"

sasa utaona waarabu pale wanapoishi lazima wawekeze kwani ndio kwao na watalipwa na Mola kutokana na huduma zao kwa jamii ile na sio ilmu au utajiri wao kuutumia kibinafsi.

Hizo tofauti mbili ndio zinaifanya Tabora waarabu na wahindi wengi kuwekeza sana katika sekta mbalimbali. Wana wa Asli ndio kwanza wamezinduka na kuanza kuwekeza.

Binafsi nampongeza sana RAGE kuanza kuonyesha mwanga na chachu la kuizindua Tabora katika usafiri na mawasiliano ya radio na mengine mengi. Tushikamane kuikomboa Tabora yetu.

 
Hivi, wakereketwa wa Tabora Fighter, @ELNINO, KIKUNGU Sikonge; hatuwezi kukutana na kupanga mpango mkakati wa kuanzisha kitu ambacho chaweza inua mkoa pamoja na kuongeza ajira kwa vijana wa Tabora?

Najua kuna ambao wako nje ya nchi, lkn baada ya kupitia tena huu Uzi naona we have something in common, nacho ni uchungu wa mkoa wetu! We can do something l believe!

Nimeipenda sana hii kama mtakuwa na moyo wa kurudisha hadhi ya Tabora ya dahal na dahal katika uchumi na hata pia mambo ya kijamii.
Mimi ni mmoja kwani nina asli ya huko kupitia kwa mama yangu mzazi ambaye amezaliwa huko Na kabuli la bibi yangu lipo kule usoke. Hivyi kila mwaka lazima tufike kutembelea ndugu na jamaa.

Kuna project tumeianzisha huko Urambo na Sikonge ipo bado katika mchakato wa kuleta mashine ndogo ndogo tatu za kuweza kusindika asali na soko lake kuu tumeshalipata huku Oman, Saudia, Qatar na Yemen.

Tupo wengi sana wenye asili ya huko na tupo tayari kusaidia kama mtakuwa tayari. Mpaka sasa Mh Rage na Mh Sitta ndio watu pakee wanaounganisha watu wa huku kuangalia maendeleo ya huko na Mh Sitta alifanya kazi kubwa katika uwekezaji wakti akiwa pale TIC.

Tupo pamoja. mail yangu sirnaamani@gmail.com

 
nafikiri ni vema watoa mawazo wakajikita katika kuainisha nini matatizo ya tabora na nini kifanyike, kiukweli tabora inatia aibu sana, na ukifika pale watu wameridhika utafikiri hawana shida, bao, kahawa, majungu, kushinda kwenye vibaraza vya waarabu wanaomba pesa
 
jamani sijui wenzangu kama mmepata kung'amua kitu hiki mkoa wa Tabora ni kama vile umekufa kwa jinsi nionavyo mimi licha ya wakazi wake kuwa na chakula pengine cha kutosha lakini miaka nenda rudi nikipita hapo sioni mabadiliko utafikiri vile hakuna wazawa waliokwenda shule mpaka leo mbavu za mbwa ziko katika mji tatizo liko wapi?
-kwa wazawa wenyewe?
-serikali?
kwa kuwa kama ni viongozi waliosoma na kuwepo katika sytem hii ya serikali wapo tangu kitambo mbona kunadorola yaani huwa napata maswali mengi kichwani?
hebu nisaidiane hasa ninyi wazawa wa tabora na wenye kuufahamu vizuri unastahili kuwa kama ilivyo? ukizingatia kuwa ni mkoa wa kihistoria katika harakati za uhuru wa nchi hii.


Wewe mkuu watu wa kumpa kura Rage unategemea nini. Pia kilaza Mkumba wa Sikonge. Above all kuwa na mbunge kama Munde ni ukilaza wa hali ya juu.
 
Kusema ule ukweli ni kwamba mkoa huu unadidimia kimaendeleo kadri siku zinavyokwenda mbele. kwanza naomba niseme kuwa mimi ni mmoja wa wazawa wa mkoa huo, lakini kusema ukweli kila nikienda nyumbani likizo naona hali inazidi kurudi nyuma siku hadi siku.

Ofcourse kuna sababu nyingi sana za kupelekea hali hiyo, baadhi ni hizi zifuatazo:-

1. Kukosa maono kwa viongozi wetu wengi wazawa wa mkoa huo kama vile Marehemu Chief Abdallah Fundikira, Chifu Lugusha, Marehemu Kasanga Tumbo, na wale waliopo sasa kama kina Samweli Sitta, Prof Athuman Kapuya, n.k ni viongozi ambao ama walikuwa wabinafsi kupindukia au walijiingiza katika malumbano na ubishi na serikali hali ilisababisha TaBORA ipewe kisogo na watawala.

2. baadhi ya mila na desturi zetu zimekuwa kikwazo kwa maendeleo. Mfano, ndugu zangu wakulima wa tumbaku au wapasua mbao wamekuwa wanapata pesa sana lakini wakipata wanalewa sana na wanakuwa hawana malengo ya maisha na maono ya maisha kwa miaka ijayo. Aidha, wakulima wa tumbaku wamekuwa wanaoa wake kila msimu wa fedha badala ya kuwekeza katika mambo ya maana. Vilevile vi mila vya kuaa au kuolewa mapema ni vya kizamani na havina tija kwa maendeleo.

3. Mila na kasumba za Kiarabu kama ilivyo kwa baadhi ya mikoa ya pwani ambayo nayo haina maendeleo sana kwa wenyeji, kama yapo yameletwa na wakuja, hiyo nayo ni nadharia ya kueleza hali iliyopo Tabora kwa sasa.
4. Ukosefu wa uwekezaji wa uhakika kwa upande wa serikali kuu hali inayofanya uchumi wa mkoa kuwa duni.

Nadhani kama mzawa nimetoa mchango, nadhani wazawa na watu wengine mnayo haki ya kutoa mawazo ya kusaidia mkoa wetu ingalau uendelee.

Naomba kuwasilisha kwa michango yenu.
 
Kusema ule ukweli ni kwamba mkoa huu unadidimia kimaendeleo kadri siku zinavyokwenda mbele. kwanza naomba niseme kuwa mimi ni mmoja wa wazawa wa mkoa huo, lakini kusema ukweli kila nikienda nyumbani likizo naona hali inazidi kurudi nyuma siku hadi siku.

Ofcourse kuna sababu nyingi sana za kupelekea hali hiyo, baadhi ni hizi zifuatazo:-

1. Kukosa maono kwa viongozi wetu wengi wazawa wa mkoa huo kama vile Marehemu Chief Abdallah Fundikira, Chifu Lugusha, Marehemu Kasanga Tumbo, na wale waliopo sasa kama kina Samweli Sitta, Prof Athuman Kapuya, n.k ni viongozi ambao ama walikuwa wabinafsi kupindukia au walijiingiza katika malumbano na ubishi na serikali hali ilisababisha TaBORA ipewe kisogo na watawala.

2. baadhi ya mila na desturi zetu zimekuwa kikwazo kwa maendeleo. Mfano, ndugu zangu wakulima wa tumbaku au wapasua mbao wamekuwa wanapata pesa sana lakini wakipata wanalewa sana na wanakuwa hawana malengo ya maisha na maono ya maisha kwa miaka ijayo. Aidha, wakulima wa tumbaku wamekuwa wanaoa wake kila msimu wa fedha badala ya kuwekeza katika mambo ya maana. Vilevile vi mila vya kuaa au kuolewa mapema ni vya kizamani na havina tija kwa maendeleo.

3. Mila na kasumba za Kiarabu kama ilivyo kwa baadhi ya mikoa ya pwani ambayo nayo haina maendeleo sana kwa wenyeji, kama yapo yameletwa na wakuja, hiyo nayo ni nadharia ya kueleza hali iliyopo Tabora kwa sasa.
4. Ukosefu wa uwekezaji wa uhakika kwa upande wa serikali kuu hali inayofanya uchumi wa mkoa kuwa duni.

Nadhani kama mzawa nimetoa mchango, nadhani wazawa na watu wengine mnayo haki ya kutoa mawazo ya kusaidia mkoa wetu ingalau uendelee.

Naomba kuwasilisha kwa michango yenu.

Baada ya wewe kulalamika sana naomba nikuulize je umeifanyia nini Tabora katika kuhakikisha unainua uchumi wake.

waarabu kule ukitembelea wilaya zote kuanzia Igunga, Nzega, Tabora mjini, Uyui, Sikonge mpaka Urambo wemewekeza sana katika sekta za Mafuta ( Fuel stations), kilimo hususan kuwa na Matrekta, maduka makubwa ya jumla na rejareja, usafiri wa mabasi na malori na majumba.

Je wewe umewekeza katika nini?

 
nafikiri ni vema watoa mawazo wakajikita katika kuainisha nini matatizo ya tabora na nini kifanyike, kiukweli tabora inatia aibu sana, na ukifika pale watu wameridhika utafikiri hawana shida, bao, kahawa, majungu, kushinda kwenye vibaraza vya waarabu wanaomba pesa

Matatizo makubwa sana ya Tabora kiasi cha kuweza kukosa kuvutia wawekezaji ni haya
1. Miundo mbinu ya barabara mibovu sana na kutokuwa na uhakika wa usafiri wa ndege.
2. Hakuna umeme wa uhakika.
3. Maji taabu
4. Wazawa kuogopa kujenga Tabora kwa kukhofia kurogwa au mambo ya ushirikina.
5. Wazawa kuwa na choyo (kuoneana wivu wenyewe kwa wenyewe hivyo kubaniana) hivyo kutoa fursa kwa wageni kumiliki uchumi wao
6. Kukosa mtu/watu makini wa kudai haki zao Serikalini.



 
Guys,Sikonge,Itegematwi,Kaunga,Mapambazuko,ELNINO,Fighter,Hossam etc lets be real,Tbr ni kwetu na hatuwezi tukazungumzia hizi challenges kijujuu tunatakiwa tuanzie somewhere na hapo somewhere ni sisi wenyewe kuanza kwa pamoja kuungana na ku-have consesus kwamba tufanyeje.Nitawa-PM kila mmoja tupeane contacts(if you don't mind) then we will take from there.Hii thread imeni-touch sana na mimi naweza kuwa mmoja wa kulaumiwa kama ulivyo wewe mwana TBR mwenzangu.

Mbarikiwe sana

Msula eve, wanyivila kunguno ke? Mbe kudime ndikugulazya! Nimo nami jamani!
 
Mkome kuwapa ubunge Wasomali na waarabu.Tabora mtabaki na mataruma ya reli hata treni yenyewe inapita mara moja kwa wiki,barabara ya maana kuwaunganisha na mikoa mingine hakuna. Badilikeni muache kupewa kofia,fulana na vitenge vya njano na kijani wakati wa uchaguzi chagueni watu watakaowapigania katika harakati za Maendeleo yenu,au mmesahau ya Igunga mwaka jana hao ndo wabunge wa kuwapigania kweli kama si kutafuta posho na bastola zao kwenye kampeni?
 
Baada ya wewe kulalamika sana naomba nikuulize je umeifanyia nini Tabora katika kuhakikisha unainua uchumi wake.

waarabu kule ukitembelea wilaya zote kuanzia Igunga, Nzega, Tabora mjini, Uyui, Sikonge mpaka Urambo wemewekeza sana katika sekta za Mafuta ( Fuel stations), kilimo hususan kuwa na Matrekta, maduka makubwa ya jumla na rejareja na majumba.

Je wewe umewekeza katika nini?


Kaka ni kweli nakubaliana na wewe kwamba Waarabu wa Tabora wamejitahidi kuwekeza katika petrol stations, mabus, malori, maduka n.k, mimi ndio nimemaliza shule tuombeane Insahallah huenda niktoa mchango.

Aidha, nisamehe kwa kugusa hisia zako kwani ni wengi huwa wanasema mila ya kunywa kahawa vibalazani, kucheza bao n.k ni mila za kiarabu ambazo Tabora, Dar, Pwani, Lindi, Mtwara, Morogoro iko ndio maana nikasema hivyo, samahani sana kwa kukugusa nisamehe lakini nakubaliana na mchango wa ndugu zetu wenye asili ya kiarabu walioko Tabora.
 
Wana Tabora mlioko huko Tanzania na waTz kijumla. Kuna good news nimepata sasa hivi. Kuna group la wafanyabiashara wakubwa wa Saudi Arabia watakuja huko Tanganyika taarih 7 mpaka 9 May 2012 na kufanya mkutano na wadau mbalimbali wa huko katika kutoa ufadhili au kuingia ubia na wafanya biashara wa huko Tz katika miradi mbalimbali ikiwemo kilimo, ufugaji na mitambo. Mkutano wao watafanya taarih 8 May 2012, Kilimanjaro Hotel.

Mkutano huo unaratibiwa na Ubalozi wa Saudia uliopo Dar na TIC. Nawashauri mjitokeze kwa wingi na project writeup zenu na kuziwakilisha kwao. Kuna mwanatabora mmoja ambaye ni mfanyabiashara maarufu sana Riyadh (Soud Hashim Hamoud Al Baharaan) atakuwepo naye nimempa hints za kiwanda cha kusindika asali na kutoa mikopo na kuwawezesha walina asali.
writeup ipo tayari na ipo chini ya PPP za Serikali itawasilishwa.

Pateni more info kupitia TIC kuweza kuhudhuria
 
Thanks Barubaru, l can not be in Dar hiyo 8th of May. Lkn natumaini baadhi yetu waliopo Dar waseize hiyo opportunity.

Pia nakubaliana na mtazamo wako wa sababu za mkoa wetu kuwa nyuma. No moja ni miundo mbinu mibovu lkn pia biashara ya kurogana ilihamisha wanyamwezi wengi sana!

Ila kwa sasa kuna nafasi ya mabadiliko; na uwezekano wa mkoa kufunguka kutokana na miradi inayoendelea ya barabara ni fursa kubwa sana kwetu!
 
Last edited by a moderator:
Hivi, wakereketwa wa Tabora Fighter, elnino, KIKUNGU Sikonge; hatuwezi kukutana na kupanga mpango mkakati wa kuanzisha kitu ambacho chaweza inua mkoa pamoja na kuongeza ajira kwa vijana wa Tabora?

Najua kuna ambao wako nje ya nchi, lkn baada ya kupitia tena huu Uzi naona we have something in common, nacho ni uchungu wa mkoa wetu! We can do something l believe!

Habari, nimefatilia hii kitu kwa karibu saana na sasa something constructive just pop in.
Tupo pamoja, naomba tufahamishane ili tupate njia bora ya kuuletea maendeleo mkoa wetu.
Sikonge,fighter,barubaru,kaunga na wengine mnao utakia mema mkoa wetu wa Tabora mbarikiwe saana.
 
Last edited by a moderator:
Dah...maendeleo Tabora???? Unyuma wa Tabora kimaendeleo hautokani na mambo ya vyama, ni watu wenyewe, ni asili yao, tuseme hivi, kuwa nyuma ya kila jambo muhimu kwa ustawi wa jamii ni sehemu muhimu sana ya wana Tabora, utake usitake huo ndiyo ukweli.
Mwaka 2010 Shinyanga ilikuwa nyuma sana ukiringanisha na Tabora, lakini sasa hivi Shinyanga inabadilika kila mwezi, na ndani ya mwezi au miezi kadhaa lazima project ikamilike au uone improvements, iwe NGO's, individuals au public.
Lakini ukiingalia Tabora, pamoja na kurundikiwa vyuo na ofisi tofauti kuweka zonal offices pale, bado ina drop kila uchao.

Mkuu acha hizo, huo mtazamo ni finyu na inaonesha upeo wako ulivyo mdogo.

Tatizo kubwa sana ambalo ndilo kiini cha maendeleo duni ni kukosekana miundombinu muhimu ya mawasiliano. Unalinganisha na Shinyanga ambayo imefunguka kimawasilino, ngoja barabara zijengwe utaona itakavyopepea kimaendeleo.
 
Kaka ni kweli nakubaliana na wewe kwamba Waarabu wa Tabora wamejitahidi kuwekeza katika petrol stations, mabus, malori, maduka n.k, mimi ndio nimemaliza shule tuombeane Insahallah huenda niktoa mchango.

Aidha, nisamehe kwa kugusa hisia zako kwani ni wengi huwa wanasema mila ya kunywa kahawa vibalazani, kucheza bao n.k ni mila za kiarabu ambazo Tabora, Dar, Pwani, Lindi, Mtwara, Morogoro iko ndio maana nikasema hivyo, samahani sana kwa kukugusa nisamehe lakini nakubaliana na mchango wa ndugu zetu wenye asili ya kiarabu walioko Tabora.

waarabu wenyewe siyo wavivu, ni wachapa kazi na wafanya biashara wazuri sana (angalia hata wapemba ambao wengi wao wana asili kubwa ya kiarabu) tatizo na hawa waswahili wanaojifanya waliondolewa tamaduni zao za asili za kiafrica na kubaki katikati ..hawa wamanyema, wazalamo, wadengereko, wakwere, watu wa ujiji pale, hawa siyo waarabu kwa hiyo hawana maarifa asilia ya waarabu, na wamenyan'ganywa tamaduni yao ya kiafrika sasa hata kulima na kazi ngumu hawawezi wanakalia kujifanya wajanja wa mjini kunywa kahawa, ujanja janja wa kijinga mjini, kuuza hata ardhi yao ili wacheze ngoma, kutopenda shule, nk hawa ndiyo tatizo letu tabora na sehemu nyingine za pwani, kigoma, kusini na maeneo mengine yaliyotawaliwa na yaliyofanya biashara na waarabu..kumbuka waarabu hawakua na long term vision na maendeleo ya wakazi au wale macollaborator wao tofauti na wazungu, waarabu walikuja na simple exploitation na kueneza dini (hata watu waliotawalia na nchi zenye ukatoliki mkubwa ziko hiv
 
Habari, nimefatilia hii kitu kwa karibu saana na sasa something constructive just pop in.
Tupo pamoja, naomba tufahamishane ili tupate njia bora ya kuuletea maendeleo mkoa wetu.
Sikonge,fighter,barubaru,kaunga na wengine mnao utakia mema mkoa wetu wa Tabora mbarikiwe saana.

Nafikiri KIKUNGU amejitolea kucoordinate mawasiliano ya mwanzoni; ni vyema pamoja na kuchangia humu pia kuMP (contacts na details nyingine) ili tujitambue ni wangapi tuko interested in investing au doing something for our homeland (nchi ya asali na maziwa).
 
Last edited by a moderator:
, kutopenda shule, nk hawa ndiyo tatizo letu tabora na sehemu nyingine za pwani, kigoma, kusini na maeneo mengine yaliyotawaliwa na yaliyofanya biashara na waarabu..kumbuka waarabu hawakua na long term vision na maendeleo ya wakazi au wale macollaborator wao tofauti na wazungu, waarabu walikuja na simple exploitation na kueneza dini (hata watu waliotawalia na nchi zenye ukatoliki mkubwa ziko hiv

Mharakati,

Mimi naona wewe una chuki binafsi na waarabu kiasi cha kuwapa swifa ambazo si zao bali na za wazungu. Nafikiri kabisa unasukumwa na kuwa na chuki na mila na desturi za watu wa Pwani kwani wewe umezoea kuwa kila pahala lazima kuwe na kilabu cha pombe au Bar , jambo ambalo mila za pwani hakuna.

Lakin labda nikupe suala la msingi sana. Wakati wa ukoloni mpaka Tanganyika inapata uhuru wake Dec 1961, sehemu walizokuwa wanakaa waarabu kama Ujiji- Kigoma, Nzega, Tabora, Usoke, Urambo , Kaliua n.k zilikuwa zipo juu kiuchumi ukilinganisha na sehemu walizokuwa wanaishi wazungu na wenye kufuata mila za kizungu?

Kama unakubaliana na hilo. Jiulize kwanini sehemu hizo uchumi wake ulishuka mara baada ya uhuru wenu? Jiulize kulikoni?wakati watu wale wale. Jiulize kwanini mzungu (mkoloni) aliona umuhimu wao?

Lakin la kukusaidia zaidi ni kukujuza kuwa waarabu walikuwa na long term vision na ndio maana wakawekeza zaidi katika mambo ya kilimo kwa kununua matrekta, Usafiri kwa kununua mabasi ya abiria na magari ya mizigo, kuwekeza katika mafuta kwa kujenga fuel stations mbalimbali huko Tabora na kwingineko bila kusahau biashara za jumla jumla isipokuwa Pombe.

Walishirikiana vizuri sana na wananchi wa huko mpaka kufikia kuoleana na hivyo kusababisha tuwe na ndugu wengi sana ambao wana nywele ngumu na weusi lakin sote tunawapenda na kuwaheshimu sana.

Lakin cha mwisho ni kujua bottom line ya maisha ya mwan'Adam ni kupata pesa na kuishi vizuri na jamii yote na kuzitumia fedha zake kwa manufaa ya jamii husika. Kitu ambacho waarabu wanafanya na ndio maana wao ndio wawekezaji wakubwa sana kule tabora na kwengineko. Elimu haina maana kama huitumii kwa faida ya jamii yako kwani si kila msomi ameelimika.

Nakupa pole kwa kuchukia waarabu sababu hawapendi pombe.
 
Tabora tunatoa Asali wingi, Mbao bora za Mninga kwa wingi
Tuna Hifadhi za taifa - Tabora ni miongini kwa mikoa ya kitalii
Tuna ardhi yakutosha unutilized - leo hata nikitaka hekari 100 napata for free you cant believe.
Tuna Kilimo cha Tumbaku kama zao kuu la biashara

Tabora hasa wilaya ya Sikonge nafikiri ndiyo ipo kwenye hali mbaya sana kiuchumi siwezi kubisha. Nikifika nyumbani ugali kwa nsansa na swalu, majani ya muhongo na maboga kwa wingi..Tunawakaribisha.

Ekari 100 for free! Labda kule Kitunda, Mibono na Ulyanyama!
 
Barubaru said:
Mimi nimekaa sana Tanzania na kufanya kazi sana Tanganyika katika mikoa mbalimbali.
Barubaru said:
Tabora ni asli nako na najua fika kuwa watu wenye nywele ngumu wamekuwa waoga sana kujenga kwao nyumba nzuri au kuanzisha investment kubwa kubwa kwao wakiogopa Uchawi na kurogwa, kitu ambacho kwa waarabu au wahindi hakipo kabisa.


Barubaru,

..cha kwanza, ni kama ulivyoeleza kwamba miundombinu ya Tabora ni mibaya, na hivyo inasababisha kuwepo na ugumu ktk kufanya biashara.

..kitu cha pili, nadhani ni upatikanaji wa mitaji ya kuanzisha biashara na viwanda vidogo-vidogo. watu wa Tabora tayari wana sifa ya uchapakazi["mzigo mzito mpe mnyamwezi"]. naamini wakiwezeshwa kwa mitaji basi watakuwa wafanyabiashara wazuri tu.

..suala la imani za kichawi na kishirikina mimi sikubaliani nalo sana. nasema hivyo kutokana na experience ya jamii moja wenyeji wa mkoa wa Iringa. Jamii hiyo, ambayo sitaitaja jina, ilikuwa inadharaulika kwa kuwa watu wa chini, wafanyakazi ngumu wanaoamini ktk ushirikina. Leo, baada ya mkoa wa Iringa kufunguka kwa miundombinu, jamii hiyo imeibuka na kuwa nguzo ya biashara kubwa kubwa[haswa mabasi] ktk mkoa wa Iringa.

NB:

..niliposema kwamba kuna "mifumo" ambayo imekuwa ikiwaumiza wazawa nilikuwa namaanisha zile sheria za enzi za mkoloni zilizokuwa zikizuia mabenki au mtu yeyote yule kumkopesha fedha mtanganyika mwafrika[native]. baada ya uhuru tulikuja na siasa ya ujamaa ambayo nayo ikachelewesha waafrika kujitumbukiza kwenye biashara. mambo yamekuja kufunguka kidogo miaka awamu ya 2 na 3, lakini bado access to capital na mazingira ya kibiashara is something that needs to be worked on.

..wananchi[wazazi,waalimu,wahadhiri,serikali..] wenyewe inabidi tubadili mitizamo yetu kuhusu biashara na kujiajiri. kwa mfano sina uhakika kama chuo kikuu cha sokoine wana mradi wowote ule wa kusaidia wahitimu wao kuwa wakulima, au wafugaji, wa kibiashara. vyuo vikuu vya wenzetu vinasifika kwa makampuni yaliyoanzishwa na wanafunzi wao. Kwa mfano Facebook ilianza Harvard Univ, Yahoo ilianza Stanford Univ.


 


Barubaru,

..cha kwanza, ni kama ulivyoeleza kwamba miundombinu ya Tabora ni mibaya, na hivyo inasababisha kuwepo na ugumu ktk kufanya biashara.

.
.kitu cha pili, nadhani ni upatikanaji wa mitaji ya kuanzisha biashara na viwanda vidogo-vidogo. watu wa Tabora tayari wana sifa ya uchapakazi["mzigo mzito mpe mnyamwezi"]. naamini wakiwezeshwa kwa mitaji basi watakuwa wafanyabiashara wazuri tu.

..suala la imani za kichawi na kishirikina mimi sikubaliani nalo sana. nasema hivyo kutokana na experience ya jamii moja wenyeji wa mkoa wa Iringa. Jamii hiyo, ambayo sitaitaja jina, ilikuwa inadharaulika kwa kuwa watu wa chini, wafanyakazi ngumu wanaoamini ktk ushirikina. Leo, baada ya mkoa wa Iringa kufunguka kwa miundombinu, jamii hiyo imeibuka na kuwa nguzo ya biashara kubwa kubwa[haswa mabasi] ktk mkoa wa Iringa.

NB:

..niliposema kwamba kuna "mifumo" ambayo imekuwa ikiwaumiza wazawa nilikuwa namaanisha zile sheria za enzi za mkoloni zilizokuwa zikizuia mabenki au mtu yeyote yule kumkopesha fedha mtanganyika mwafrika[native]. baada ya uhuru tulikuja na siasa ya ujamaa ambayo nayo ikachelewesha waafrika kujitumbukiza kwenye biashara. mambo yamekuja kufunguka kidogo miaka awamu ya 2 na 3, lakini bado access to capital na mazingira ya kibiashara is something that needs to be worked on.

..wananchi[wazazi,waalimu,wahadhiri,serikali..] wenyewe inabidi tubadili mitizamo yetu kuhusu biashara na kujiajiri. kwa mfano sina uhakika kama chuo kikuu cha sokoine wana mradi wowote ule wa kusaidia wahitimu wao kuwa wakulima, au wafugaji, wa kibiashara. vyuo vikuu vya wenzetu vinasifika kwa makampuni yaliyoanzishwa na wanafunzi wao. Kwa mfano Facebook ilianza Harvard Univ, Yahoo ilianza Stanford Univ.



Nakubaliana na wewe kabisa.

Watu wako wengi sana ambao wangependa kuwekeza huko Tanzania hususan tabora. Lakin wanakwamishwa na Sera na sharia zenu katika uwekezaji.

Mimi nakupa changamoto kama utapata mtu mwenye hecta 50 mpaka 200 na anazimiliki kisharia kabisa pasi na shaka zozote basi tuwasiliane na mimi ili kufanya upembuzi yakinifu na kisha kuandika mchanganuo makini wa matumizi ya ardhi hiyo iwe kilimo au viwanda ikiwa pamoja na kujua virutubisho na chachu za kukuza mradi huo na changamoto zake. Kisha pasi na shaka yoyote mimi nitakusaidia 100% kupata wabia wa kufanya nao kazi.

Kumbuka kuwa huku Uarabuni pesa zipo nyingi lakin hakuna pahala pa watu kuweza kuwekeza na ndio maana wanaamua kuwekeza nje ya huku hususan Africa.

Nilibainisha hapo awali kuwa kuna kundi la wawekezaji toka Saudi Arabia wanakuja huko Tz tarih 8 May 2012 kuangalia fursa za kuwekeza na ujio wao unaratibiwa na TIC. Nakuomba wasiliana nao uende ukakutane nao na kubadilishana nao mawazo. Kizuri zaidi mmoja ni mzaliwa na Usoke.

kama kuna ziada tunaweza kuwasiliana na maelekezo zaidi.

 
Back
Top Bottom