Tabora iliyodidimia inahitaji kuinuliwa...

Tabora iliyodidimia inahitaji kuinuliwa...

Bonge la thread.......!

Shukrani kwa wote waliotoa michango yao ya kujenga, nimekuwa nikiisoma mara kwa mara kujikumbusha JF mijadala ya maana hapa jamvini.....
 
Ndo maana mimi binafsi napata shaka saana na moyo wa kizalendo wanaojifanya wanao watu hawa, kiasi cha kuomba au kufikiria ridhaa ya kuongoza nchi 1.Samuel Sitta. na Prof Ibrahim Haruna Lipumba , hivi kweli viongozi hawa wameshindwa kuwasaidia wakazi wa Tabora kujiinua kiuchumi kutokana na fursa walizonazo kisiasa ndani ya nchi na nje ya nchi. Kama alivyojaribu kufanya Mh, Augustino Lyatonga Mrema kwa wananchi wa Kilimanjaro ktk zao la kahawa. binafsi nawachukia saaaaana 1. Kapuya 2. Sitta 3. M, sitta na wengine wenye uwezo wa kuwasaidia wakaazi wa Tabora , huku wakijikweza kuwa wanauchungu na nchi.


Hao ni banyamulenge unadhani watakuwa na uchungu wa kweli wa Tabora??? Huo ni wengine walitaka hata kuuza KWA Katavi eneo alilozaliwa Mtemi Milambo, HUYO utasema ni mwanatabora??????
 
jamani kama kuna watu wa tabora humu mtakubaliana waraka huu juu ya maisha ya wana tabora.....

kwa wale wanaofatilia historia ya mkoa wetu mtakumbuka kuwa harakati za kudai uhuru wa tanganyika ulianzia tabora
na ni moja kati ya mkoa uliotoa watu mashuuhuli na maarufu kama
1.profesa ibrahim lipumba

2.samweli sitta....wazili africa mashariki na alishawahi kuwa speaker wa bunge...

3.rostam azizi..alishwahi kuwa mjumbe wa nec ccm na pia ni mmiliki wa vyombo vya habali vya chanel ten na magic f.m

4.magreth sitta...alishwahi kuwa wazili wa elimu na mjumbe ccm

5.profesa kapuya...alishawahi kuwa wazili wa ulinzi,wazili wa elimu na wazili wa vijana na michezoo

6.ismail aden rage...alishawahi kuwa mwenyekiti fat,sasa hivi mwenyekiti wa simba na mbunge wa tabora mjini

7.dk.hamis kigwangala.....huyu ni dokta na mbunge
8.dk.kafumu mbunge na alishawahi kuwa katibu mkuu wizala ya madini...
9.bado wakurugenzi wa juu wa serikali....sijawataja na ma profesa tulionaooo

matatizo yaliyopo ukiangalia mpaka leoo hii
1.barabara ya kutoka tabora mjini mpaka urambo ni mbovuu mpaka sasa
2.viwanja vya ndege vya tabora mjini na urambo ...vibovuuu
3.hali ya maisha imekuwa ni ngumu sana.....

kuna umuhimu wa wana tabora kuacha kuwekeza dar turudi nyumbani tulipotoka...na 2015...tuchague watu makini
tumeshachoka na haya maisha
 
hilo ni suala ambalo linaumiza sana vichwa vya watu wengi, kukosa maendeleo tabora licha ya kuwa na watu mashuhuri
 
hilo ni suala ambalo linaumiza sana vichwa vya watu wengi, kukosa maendeleo tabora licha ya kuwa na watu mashuhuri

jamaa wanajifanya wengii kuwekeza dar...ila 2015 kipindi cha uchaguzi wanarudi kusumbua watu....inauma sana
 
hilo ni suala ambalo linaumiza sana vichwa vya watu wengi, kukosa maendeleo tabora licha ya kuwa na watu mashuhuri

Nani kakwambia umashuhuri wa watu ndo chanzo cha maendeleo ya eneo fulani?
Maendeleo ya mahali yanatokana na moyo wa uzalendo na kupenda nyumbani, hao ulio wataja baada ya kupata umashuhuri tu wote wakakimbilia dar es salaam.
Kwa hao ulio wataja tu inabidi kila mmoja akawekeze kwa naomna moja au nyingine tabora.
 
Wa kukaya kwakweli naungana na wewe kuulilia mkoa wetu wa Tabora,lakini katika hili wakulaumiwa ni serikali.Hakuna vivutio vyovyote vya kimaendeleo ambavyo serikali imeupa mkoa wetu!Ona mpaka sasa ndiyo mkoa pekee mkongwe nchi nzima ambao haujaunganishwa kwa lami,viwanda vilivyokuwepo kama cha nyuzi, na maziwa na vingine vingi vimebaki magofu kule kiloleni. Maji mpaka leo mkoa wetu ni ya shida wakati kijiografia ni mkoa ambao umekaa sehemu nzuri sana kwa maendeleo ya nchi. Kwa challenge hizo na nyingine nyingi vimesababisha mzunguko wa hela kuwa mdogo sana na hicho ndiyo kinachowafanya Wanyamwezi wengi kukimbilia kuwekeza Dar na mikoa mingine wakiamini angalau wataambulia shilingi.

Madhali kama mkoa wetu ungekuwa umeunganishwa kwa lami kila upande basi ungekuwa ndiyo njia panda kuu ya magari yanayokwenda nchi za jirani kama Congo D.R,Burundi na Rwanda pia ingekuwa ndiyo njia kuu ya kwenda mikoani (Yaani kutoka bara kwenda pwani) lakini serikali bila haya mpaka leo inaendelea kuudharau mkoa wetu. Bado tunasafari ndefu sana kufikia mafanikio wanatabora na mafanikio hayo yataletwa na sisi kwa msaada mkubwa wa serikali pia, Mikoa kama Tabora na Singida ilitakiwa serikali iipe vipaumbele maalumu kwa maana ya kwamba iwekeze sana katika kuchohcea uchumi wake maana haina rasilimali nyingi za kujiendeleza yenyewe kama ilivyo kwa wenzetu wa kaskazini wenye vivutio vya utalii,au kusini walivyo na gesi au hata kanda ya ziwa kwa uwepo wa madini kila kona na ziwa victoria na hivi ndivyo wanavyofanya serikali za nchi nyinginezo duniani. Kweli inauma sana na huwa natamani kulia kila mara ninapopata nafasi ya kuutembelea mkoa wangu.
 
Techman umenena! Hoja zako zimetosha kuufunga mjadala huu.

Maendeleo ya mahali yanapelekwa na watu wenyewe. Kama Tabora mlilala mkajiaminisha kwamba kwa kuwa na kina Sitta, Lipumba, Rostam na wengine, maendeleo yatakuja yenyewe, mlikosea sana.

Amkeni. Fanyeni kazi kwa juhudi na maarifa. pambaneni na wezi na wanyonyaji wanaowaumiza wakulima wa tumbaku. Komesheni ushirikina, na mhakikishe wale vijana waliojazana stesheni ya treni wakivizia mizigo ya abiria, wanarejea mashambani.

Maendeleo ya Watu yanaletwa na Watu wenyewe! Utegemezi ambao umeenea hadi kwenye familia zetu, ndiyo sumu ya maendeleo. Kama ni umaarufu wa watu, basi mkoa wa Mara leo ungekuwa kama Ulaya! Wananchi wenyewe waamke.

Lakini jingine la muhimu ni kuhakikisha Tabora inapata wabunge wa upinzani ili waweze kupiga kelele za kweli, siyo hawa wa "ndiyoooooooo!"
 
Manyerere Jackton

wewe kama kwa miaka 50....tokea uhuru....
1.hakuna barabara ya lami mpaka leo barabara ni za vumbii
2.tatizo la maji.....limekuwa kubwa...mpaka leo...
3.uwanja wa ndege wa tabora mjini na urambo...umekufaaa
4.shida ya usafili tokea dar mpaka tabora
5.umeme mpaka leo shida

unavyofikilia mwanachi wa kawaida hata akifanya kazi kwa kujituuma anaweza kujenga barabara,kutengeneza maji na kutengeneza umeme..hebu jaribu kufikilia kati yeye na serikali ni jukumu la nani

2.kitu kingine usidhalau kazi za watu....hao vijana unaowasema wamekaa na matoroli wakisubili abilia....asilimia 90
wengi wamejisomesha mpaka chuo kikuu...kwa kazi ile ile....
 
Last edited by a moderator:
Weak herufi kubwa Tabora. Ongezea na Eng.Fighter tupo bana
 
Pole sana Mkuu, lkn ngoja nijaribu kujibu swali lako kwa kukuuliza swali: NI MKOA AU WILAYA GANI ILYOTEMBELEWA NA WAARABU WENGI ENZI HIZO NA INA MAENDELEO SASA?? Samahani lkn!!
 
Maendeleo hayapatikani kwa kua na watu mashuhuri , kuna factors nyingi sana ikiwemo ya watu wenyewe (wazawa) kujituma kufanya kazi.
 
Hao wote wanatakiwa waondoke CCM
waende chama chochote cha Upinzani
ili wawe huru pale walipo wanaburuzwa.
 
Hawataki maendeleo, ndivyo walivyojiamulia...
Wewe na akili zako timamu huwezi kumchagua Aden Rage awe mbunge wako halafu ukategemea ukapata maendeleo
 
tabora-town_aerial-view1.jpg
2c.JPG
24022010335.jpg
IMG_2161.JPG
20.jpg
25.jpg
31.jpg
40.jpg
35.jpg
30.jpg
 
Back
Top Bottom