samirnasri
JF-Expert Member
- Nov 8, 2010
- 1,388
- 215
Safi daktari endelea kuwafunua mafisadi waliojificha ndani ya chama tawala najua magamba ndani ya chama tawala ni mengi na hayawezi kuisha wakisema wayamalize yote basi chama chote kitakufa.
ndio maana mzee aling'oa mabomba na koki zake kule mtela...........hili sitalisahau........na kwakuwa sasa hivi amewekwa kwenye list atuthibitishie kuwa hakuiba............
Si waende mahakamani kama alivyofanya Sumaye!!!!
- Kama kuna ushahidi mkubwa unaokubalika kisheria, that is the point mkuu je upo?
William @ NYC, USA.
Mkuu,nimekuwa nathamini sana michango yako lakini nadhani kwa vile damu ni nzito kuliko maji,naona umeamua kuzipa likizo busara zako.Kuna usemi kuwa mahakama ya umma ina nguvu zaidi ya mahakama ya kisheria.Walichofanya Chadema ni kumshtaki Malecela kwa umma (yaani mahakama ya umma).Sasa haihitaji hata busara ndogo tu kumaizi kuwa mwanasiasa huyo ambaye ameutumikia umma kwa miongo kadhaa asingependa akumbukwe zaidi kwa kutajwa kama fisadi badala ya kumbukumbu nyingine njema.- Hana sababu ya kuthibitisha anything kama vile Chadema ambavyo hawana sababu ya kuthibitisha anything kuhusu kupewa hela toka nje kuleta vurugu nchini.William @ NYC, USA.
- Chadema mbona hawajaenda mahamamani kumshitaki Sophia Simba mkuu, au?
William @ NYC, USA.
Kaka pole na uchovu, niko Dodoma Sasa hivi namalizia shughuli zilizotuleta hapa na majira ya saa moja jioni nitakuwa Dar es salaam Naangalia mpira na kinywaji baridi kufurahia jinsi tulivyowapiga bao CDM na ilani yao ya UFISADI, sasa haina market tena na hii inatokana na kile tulicho kiona Tabora jana jioni.
Huyu dkt Slaa hana lake jipya, na hatimaye baada ya kuisaidia CCM kutoka nje atarudi kulekule alikotoka kama wenzake wengi wanavyofanya.Tambwe Hiza,Akwilombwe......
Chama cha upinzani halisi ni CUF tu.
Nina maoni yafuatayo kuhusu hii list mpya ya Mafisadi:
1. Uwezekano mkubwa ni kuwa CHADEMA wanataka sasa kuisambaratisha CCM baada ya kuona hoja yao ya UFISADI ya awali "imemtoa nyoka pangoni" kwa CCM "kujivua gamba" na "kuwa na nia ya kufukuza mafisadi katika chama".
2. Leo hii katika CCM: Mang'ula; Malecela na Magufuli ni members ambao kwa macho ya wana CCM na mashabiki wao walio wengi ni WASAFI na si MAFISADI. Kwa hiyo ina maana kwa kuwaweka katika kundi la mafisadi na kama kuna ushahidi mzito na unaokubalika kisheria na kisiasa ina maana CCM kwa asilimia kubwa itakuwa imejaa ufisadi.
3. Kama CCM au individuals waliotajwa hawatasimama na kutoa ushahidi wa kutosha na kuridhisha ku-prove their innocence na kuwa allegations za CHADEMA ni za uongo, basi mafisadi katika list ya awali hawatatoka katika chama. Wakilazimishwa kutoka, nao watadai walio katika list mpya watoke: this will mean mkorogano mkuu katika CCM na kama itakuwa handled vibaya ina maana CCM itaporomoka zaidi.
4. for sure kutakuwa na list mpya itakayohusisha mafisadi wa "Stimulus Package" lakini inawezekana unasubiriwa wakati mwafaka na ushahidi upatikane.
5. CCM wataendelea kucheza ngoma ya CHADEMA na wadau wengine mpaka hapo CCM itakapovaa nia ya dhati ya kukisafisha chama na kuwafukuza mafisadi wote CCM na Serikalini na kuwachukulia hatua za kisheria sambamba na kufanya mageuzi ya kweli katika matumizi ya pesa za walipa kodi.
Respect.
QED.
- Kumshitaki kwa umma kiongozi aliyepumzika na siasa ni dalili za siasa za Desparation za kutaka kumuingiza kila mtu kwenye siasa za kuropoka ropoka, ili kujipatia attention kwa mshitaki, sasa kama unaijua vizuri siasa unajua kwamba huyu sasa amefika mwisho hana agenda tena sasa anajaribu kuanzisha agenda isiyokuwepo ili kuendelea na zile 15 minutes of fame ambazo sio siri kwamba sasa zimefika mwisho. Kwa mwendo huu mpya wa Slaa hata neno fisadi linakosa maana kabisa mkuu, ingawa ni hadithi nzuri kwa media, elewa kwamba wananchi sio wajinga na hizi siasa za kulipua mabomu hata kama hayapo haziwezi kuisaidia Chadema kwenda mbele.Mkuu,nimekuwa nathamini sana michango yako lakini nadhani kwa vile damu ni nzito kuliko maji,naona umeamua kuzipa likizo busara zako.Kuna usemi kuwa mahakama ya umma ina nguvu zaidi ya mahakama ya kisheria.Walichofanya Chadema ni kumshtaki Malecela kwa umma (yaani mahakama ya umma).Sasa haihitaji hata busara ndogo tu kumaizi kuwa mwanasiasa huyo ambaye ameutumikia umma kwa miongo kadhaa asingependa akumbukwe zaidi kwa kutajwa kama fisadi badala ya kumbukumbu nyingine njema.
- Well kwa mwendo huu wa Slaa ni kwamba ni fair kila mwanasiasa kukurupuka na kuanza maneno ya kizushi, ili mradi yashile the media attention, mimi mkuu ninasema hivi Tanzania hatuna sheria ya Political finance Campaign kwa hiyo ni sawa kwa chama cha siasa kupokea pesa toka mahali popote pale, however kama unamshitaki kiongozi yoyote kwa wizi wa benki basi ni lazima uwe na karatasi linaloonyesha kwamba amesaini na zile pesa kuchukuliwa, lakini ukisema chama cha yule kiongozi kilipewa hela ndio hapo sasa unakuja mtego wa Political Campaign Finance Laws ambazo bongo hatuna, kwa sababu huwezi with a straight face kusema vyama vyote vya siasa Tanzania vinapokea hela safi kisheria na ukichunguza ukagundua ukweli wa uchafu wake basi viongozi wote wa kile chama ni mafisadi, please Mkuu chadema wanapewa hela na ile Charity ya Tony Blair ambayo pia ndio wanaompa hela Tshangarai kule Zimbabwe, sasa kweli unasema ukizichunguza hizo hela zitakuwa na usafi 100%? Na zisipokuwa basi viongozi wote wa Chadema sio wasafi? Pleasee!Upo Marekani,na una upeo mkubwa wa siasa za kimataifa.Sitaki kuamini kuwa ndani ya moyo wako unaamini kuwa Chadema wanapewa fedha kutoka nje kuchochea vurugu nchini Tanzania.Katika global financial crisis hii ni nchi gani yenye hela za kuchezea kwa kuzimwaga kwa Chadema ili isababishe vurugu Tanzania?Na baada ya vurugu hizo,Chadema itanufaika vipi?Au baada ya fedha hizo kumwagwa,hao wafadhili watanufaika vipi?Nani anayeweza kuwekeza kwenye vurugu?
- Malecela atakuwa mwendawazimu kwenda kumjibu Slaa anywhere kwa sababu atakuwa anajiingiza kwenye mtego wa Slaa wa kujitafutia umaarufu kwa nguvu hata kama time imekwisha, Malecela sio kiongozi wa taifa tena hahitaji kwenda popote, isipokuwa ni haki yangu kujadili anything humu JF kama mwananchi wa Tanzania, na ndicho ninachofanya hayo mengine ni yako mkuu!Kama nilivyokushauri jana,iwapo mzee wako anaamini kuwa amezushiwa tu tuhuma hizo za ufisadi,basi afanye uungwana wa kwenda mahakamani kudai amekashifiwa.Mahakama ya sheria inaweza kumsafisha iwapo hatokutwa na hatia,na mahakama ya umma pia itaridhia hukumu hiy😵therwise,unaweza kuendelea kusema kila baya dhidi ya Chadema-kwa mfano tuhuma hizo za kupokea fedha kutoka nje kuchochea vurugu-lakini unfortunately,hiyo haitosaidia kumvua mzee Malecela joho la ufisadi alilovikwa na Chadema.
- Ha! ha! hapa imenibidi nicheke kwamba kwa vile Chadema hawajaenda mahakamani basi sio lazima na Malecela asiende mahakamani, hilo limenivunja mbavu mkuu na sina la kuongeza zaidi!Duh,this is too low.Kwanza,Chadema ni political organisation sio an individual.Pili,Chadema hawajatangaza kinyume cha dhamira yao ya kumshtaki Sophia Simba.Last we heard from them ni kuwa wanakusudia kumshtaki.Third,two wrongs do not make a right.Kama Chadema hawajamstaki Sophia Simba kwa tuhuma mfu ambazo hata wawakilishi wa jumuiya ya kimataifa walizitolea macho to an extent mwanamama huyo mropokaji akaruka kauli yake,haimaanishi kuwa Mzee Malecela naye asiende mahakamani kukanusha tuhuma kuwa naye ni fisadi.
Mkuu William, with due respect again, hoja nilizokupa ni facts, facts huwa zina supportive evidence, hivyo you are wrong Sir once again. Kwa vile mimi nimetoa facts yenye hoja nzito na wewe ikazipamgua kwa hoja nyepesi, nikuweke evidence humu it will prove you wrong nakuomba ujitidhishe tuu mwenyewe kwa haya yafuatayo.
I. Pata taarifa ya CAG ya ukaguzi wa EPA soma majina ya waliohusika na EPA halafu ufanye reference na waliotajwa, utagundua sio wote waliohusika, wametajwa kwa majina.
2. Soma tena majina ya hao waliotajwa ufanye reference ya majina ya waliofikishwa mahakamani utagundua kuna waliotajwa na hawakufikishwa mahakamani na hawatafikishwa!.
3. Nimekusisitizia itetee CCM as chama that it did nothing wrong in EPA scandal, if CCM did something wrong no matter nani alisaini, viongozi wote wa juu kwenye ngazi za maamuzi hawawezi kukwepa 'collective resiponsibility' kwa makosa ya chama.
4. Hili la true colors, hizi ndizo rangi zangu daima dumu, mimi ni mkweli daima niko crystal clear, I don't beat around the bush, I just speak my mind. The truth has a cost, nimesha ilipa sana gharama ya kusema ukweli. I've even paid by my job na kugeuka jobless. Just tell the truth, and the truth will set you free. I'm free!.
JK hawezi kumfikisha mahakamani kwa sababu Dr. Slaa hajaeleza chochote cha kumfanya JK alazimike kumfikisha mahakamani, Dr. Slaa ametoa loop hole ya JK kumpuuza na mwishowe kuonekana kama ni porojo tu kama zile za JK NDIYE MMILIKI WA DOWANS.
Kwa mwendo huu mpya wa Slaa hata neno fisadi linakosa maana kabisa mkuu, ingawa ni hadithi nzuri kwa media, elewa kwamba wananchi sio wajinga na hizi siasa za kulipua mabomu hata kama hayapo haziwezi kuisaidia Chadema kwenda mbele.
Nakubaliana na wewe mkuu.
Kwa mtu anayemfahamu Mzee Mangula na hali yake ya kiuchumi atamshangaa sana kuwa jana Dr. Slaa amemtaja kama fisadi, naona sasa anatajataja majina tu kama wanamuziki wa Bongo Flavour mpaka itapoteza maana.
Hawezi Kumpuuza anajua Madhara ya Kumpuuza, CCM wamekosea Step sasa CDM watawamaliza
Atampuuza na katika hili zaidi ya Dr.Slaa kufanya kazi kwa niaba ya Rostam na Lowassa, hana atakacho-accomplish zaidi ya kupoteza credibility yake!!
Hivi sikuhizi Augustino Mrema akitangaza anakwenda kulipua mabomu kuna mtu anamchukulia serious?huku ndipo anapoelekea Dr.Slaa.
Alianza na JK Mmiliki wa Dowans and the list go on!!
Mkuu William, nadhani kufikia hapa, lazima tukubali yaishe, mimi binafsi nakubaliana na wewe, sio busara kumuita kila mwana CCM fisadi, simply because kuna wana CCM mafisadi ambao wameifisadisisha CCM- Hamna jipya hapa zaidi ya kwamba eti kwa vile CCM imewahi kupokea hela chafu basi viongozi wote wa CCm ni mafisadi ndipo ninapouliza zile hela za Chadema toka kwa Tony Blair alizopewa na Gadafi kumsafisha na yale mauaji ya wananchi wa marekani 350 kwenye ile ndege aliyoibomu kule Lockerbee, unasema ni safi? Sasa kwa vile Chadema wanazipokea zile hela unasema na wao wana damu ya wale wananchi 350 waliokufa kwa kuuliwa na Gadafi?
- It does not make a sense at all!
William @ NYC, USA.
Mzee Malecela namfahamu kwa kina, at one time or another, nimetokea kusoma shule moja na wanae 4 at diferrent times tangu primary mpaka UD hivyo namfahamu at heart, sio fisadi, ila hawezi kukwepa collective resiponsibility kama ilivyo kwa mzazi kuwajibika kwa makosa ya mtoto wake.
NB. Nimefurahi kukuona ukirudi in full swing kwenye issue hii, nakuomba isiwe hii tuu, tuendeleze mapambano, safari bado ni ndefu. Pia tusiogope kutofautiana na marafiki zetu au hata kugombana kwa jambo ambalo mtakuja kupatana. Naamini Watanzania wote wenye nia njema na Taifa hili, wanauchukia ufisadi kwa dhati toka ndani ya mioyo yao, hivyo ukisikia wale tunaowaaminia nao kujumlishwa kwenye listi ya mafisadi, ni lazima tuwatetee kwa nguvu zetu zote!.
Pasco.