Tabora: Dk Slaa ataja orodha mpya ya mafisadi!

Tabora: Dk Slaa ataja orodha mpya ya mafisadi!

Status
Not open for further replies.
Sunday, 17 April 2011 09:18

dk%20slaatabora.jpg


Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dk. Willibrod Slaa, akionyesha nakala ya kitabu cha taarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabi za Serikali, wakati wa mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye Uwanja wa Chipukizi mjini Tabora jana. Picha na Joseph Senga

WAMO VIGOGO WA CHAMA, WAZIRI MMOJA
Geofrey Nyang’oro, Tabora

KATIBU Mkuu wa Chadema, Dk Willibrod Slaa na kada wa chama hicho, Mabere Marando, jana walitaja orodha mpya ya waliyodai kuwa ni mafisadi.Akihutubia mkutano wa hadhara uliofanyika katika Uwanja wa Chipukizi mjini Tabora, Dk Slaa aliwataja mafisadi hao kwa majina yao (yamehifadhiwa)kuwa ni pamoja na Waziri Mkuu mstaafu mmoja ambaye alimtuhumu kuhusika na wizi wa fedha za Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA).

Mwingine ni Rais mmoja mstaafu na waziri mmoja aliyekuwa Serikali ya awamu ya tatu na sasa yuko katika Serikali ya awamu ya nne kwa tuhuma za kuhusika na kuuza nyumba za Serikali bila kufuata utaratibu.

Wengine ambao wametajwa na Dk Slaa ni Katibu Mkuu wa zamani wa CCM ambaye amewahi kushika nyadhifa nyingine serikalini kwa tuhuma za kuhusika na EPA.

Wengine ni wafanyakazi wawili wa kampuni moja inayomilikiwa na kada mkongwe wa CCM ambao wanatuhumiwa kuchota mabilioni ya fedha kupitia Kampuni ya Kagoda ambao walitajwa na Marando.

Akifafanua tuhuma hizo, Marando alisema aliwafuatilia watuhumiwa hao wa kampuni ya kada huyo wa CCM na kugundua kuwa waliandika majina bandia katika hati za usajili wa Kagoda.

Marando alisema anaishangaa Serikali kutowachukulia hatua watu hao hadi sasa.

Alisema kama Serikali imeshindwa kufanya hivyo yeye ataisaidia kwa kuwa anao ushahidi wote.

"Tulipowataja mafisadi CCM walikanusha, sasa leo wanaibuka na kuwataja mafisadi hao na kuwataka wajiuzulu, huo ni uongo na sidhani kama watajiuzulu kwa kuwa wana urafiki mkubwa," alisema Marando.

Dk Slaa alitaja orodha hiyo katika mkutano huo ambao kabla ya jana ulipangwa kufanyika baada ya maandamano yao yaliyolenga kupinga Muswada wa Marejeo ya Katiba 2011, ambao tayari umeondolewa bungeni.

Dk Slaa alilituhumu Jeshi la Polisi kwa kushindwa kuwachukulia hatua yoyote watuhumiwa hao tangu walipotajwa na chama hicho mwaka 2007 na kuongeza kuwa ataendelea kuwataja kwa kuwa haogopi na yuko tayari kufa.

Alisema kauli inayotolewa na Rais Jakaya Kikwete kwamba nchi iko katika hali tete, inasababishwa na yeye mwenyewe kushindwa kuwachukulia hatua mafisadi.

Miaka minne iliyopita,Septemba 15, 2007 katika viwanja vya Mwembeyanga wilayani, Dk Slaa aliwataja vigogo 11 wanaodaiwa kuwa ni mafisadi.

Awali, msafara wa Dk Slaa ukiongozwa na pikipiki zaidi ya 30 na magari ya polisi uliwasili katika uwanja huo wa mikutano saa 9:47 alasiri, huku ukishangiliwa na mamia ya watu waliofika uwanjani hapo.

Dk Slaa aliongozana na aliyekuwa mgombea ubunge Jimbo la Segerea, Fred Mpendazoe, Profesa Abdallah Safari, Mabere Malando, Wilfred Rwakatale na Mkurugenzi wa Masuala ya Bunge na Halmashauri wa chama hicho, John Mrema.

Katika mkutano huo pamoja na Dk Slaa,wanachama na viongozi mbalimbali walipewa nafasi ya kuzungumza na kwamba Profesa Safari alizungumzia nyumba za serikali zilizouzwa pamoja na udini.

Kwa upande wake, Mpendazoe alizungumzia mwelekeo wa CCM na kifo chake kabla ya Dk Slaa kupigilia msumari wa mwisho kwa kutaja orodha mpya ya mafisadi.

“Wananchi hameni CCM, CCM kwa sasa ninaelekea kufa,”alisema Mpendazoe.

Mpendazoe ambaye awali alikuwa CCM kabla ya kutimkia CCJ na kisha kuhamia Chadema, aliichambua CCM na viongozi wake wapya akisema kuwa ni chama legelege kilichosabisha kuwa na Serikali legelege.

Alisema hata kauli Mwenyekiti wa CCM, Rais Kikwete kuwa chama hicho ‘kimejivua gamba’ ni ya kinafiki kwa kuwa chama hicho imeoza kuanzia kwenye mashina na matawi yake.

Mpendazoe alisema ulegevu wa CCM ulidhihirika katika sakata la kulipa ama kutoilipa Kampuni ya kufua umeme ya Dowans baada ya viongozi wa chama hicho na Serikali kugawanyika, wengine wakitaka Dowans ilipwe na wengine wakipinga.

Alisema kama kweli CCM kimedhamiria kujivua gamba, Katibu Mwenezi wake, Nnape Nauye, anatakiwa kuwataja kwa majina watuhumiwa wa ufisadi ambao CCM imewataka watoke ndani ya chama hicho na siyo maneno tu.

Awali, kundi la wasanii wa Chadema lilitoa burudani za nyimbo mbalimbali zilizogusia mauaji ya mkoani Arusha, uundwaji wa Katiba mpya itakaoushirikisha umma pamoja na ufisadi.

Hata hivyo, jana asubuhi baada ya maandamano ya chama hicho kuahirishwa kufuatia kuondolewa bungeni Muswada wa Marejeo ya ya Katiba 2011, kuliibuka taarifa kuwa mkutano huo usingefanyika hivyo kuwachanganya wananchi, kabla ya kutangaziwa upya kuwa mkutano huo utafanyika kama ilivyopangwa.

CCM na mafisadi

Naye Raymond Kaminyoge anaripoti kutoka Dar kuwa, Chama Cha Mapinduzi (CCM), kimesema kimegundua mbinu za mafisadi kutaka kumchafua Mwenyekiti wake Rais Kikwete na familia yake kupitia vyombo vya habari.

Vilevile, CCM imerejea kuwataka watuhumiwa wa ufisadi kuondoka kwenye Kamati Kuu ya chama hicho kwa amani, bila kukichafua chama.

Akizungumza kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika katika viwanja vya Bakhresa Manzese jijini Dar es Salaam jana, Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nnauye alisema mafisadi wametangaza vita ya kumchafua Mwenyekiti wa chama hicho na familia yake kupitia vyombo vya habari.

Alisema wamegundua mpango huo na kwamba sasa wanatangaza kuamua kupambana nao hadi wang'oke ndani ya CCM.

"Mafisadi waenguliwe katika Kamati Kuu kwani wametangaza vita ya kumchafua Rais Kikwete na familia yake, sasa tutapambana nao mpaka tuwaondoe," alisema Nnauye.

Aliwataka mafisadi waondoke kwa amani ndani ya chama hicho, na kuwaonya kuwa wasianzishe vita ambavyo hawataviweza.

"Mafisadi wapo kwenye nyumba ya vioo wanaanzisha vita ya mawe wataweza? alihoji Nape."
 
Slaa apasua jipu

• Ataja orodha mpya ya mafisadi, wafikia 17

na Waandishi wetu

KATIBU Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dk. Willibrod Slaa, ametaja orodha mpya ya vigogo wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wanaotuhumiwa kwa ufisadi. Vigogo hao ni Waziri wa Ujenzi, John Magufuli, John Samwel Malecela, aliyekuwa Waziri Mkuu, Fredrick Sumaye, na aliyekuwa Katibu Mkuu wa chama hicho, Philip Mangula, kwa kuhusika na wizi wa fedha katika Akaunti ya Malipo ya Madeni ya Nje (EPA) kupitia Benki Kuu.

Dk. Slaa alitangaza majina hayo jana mjini Tabora alipokuwa akiwahutubia wanachama na wananchi waliofurika kwenye viwanja vya Chipukizi.


Alisema majina hayo ni muendelezo wa yale ya vigogo wanaotuhumiwa kwa ufisadi aliyoyataja Septemba 15, 2007 katika viwanja vya Mwembe Yanga jijini Dar es Salaam ambayo ni 11 akiwemo Rais Jakaya Kikwete.

Katika orodha ya mwaka 2007, Dk. Slaa aliwataja aliyekuwa Gavana wa Benki Kuu (BoT), ambaye sasa ni marehemu, Dk. Daudi Balali, Mbunge wa Bariadi, Andrew Chenge (CCM) na Basil Mramba aliyekuwa mbunge wa Jimbo la Rombo (CCM).

Wengine ni Gray Mgonja aliyekuwa Katibu Mkuu mstaafu, Hazina, Katibu Mkuu wa Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Patrick Rutabanzibwa, kada wa CCM, Nazir Karamagi, Mbunge wa Musoma Vijijini Nimrod Mkono (CCM), Mbunge wa Igunga, Rostam Aziz (CCM), Mbunge wa Monduli, Edward Lowassa (CCM), Rais mstaafu, Benjamin Mkapa, na Rais Jakaya Kikwete.

Alisema katika orodha hiyo mpya Magufuli amehusika na kashfa ya uuzaji wa nyumba za serikali ambazo ziliuzwa kwa watu wasiostahili na nyingine hazikutakiwa kuwekwa sokoni.

Alibainisha kuwa katika kashfa hiyo, Rais mstaafu, Benjamin Mkapa naye alihusika kwenye uamuzi huo mbovu uliosimamiwa na Magufuli, ambaye hivi sasa amepewa Wizara ya Ujenzi. Mangula na Malecela, alisema wao walikuwa wakitoa ‘vimemo' vilivyokuwa vikitoa maagizo ya kwenda kuchotwa fedha za EPA ambazo zilikisaidia Chama Cha Mapinduzi katika kampeni zilizomuwezesha Rais Kikwete kuingia madarakani.

Alisema Mangula alikuwa akitumia kofia yake ya ukatibu mkuu wa chama na Malecela alikuwa akitumia wadhifa wa umakamu mwenyekiti wa Bara kwa wakati huo.


Aliongeza kuwa Sumaye naye alihusika kwa kuwa alikuwa waziri mkuu na alikuwa akijua kila kilichokuwa kikiendelea lakini aliamua kunyamaza kimya na kushirikiana na wabadhirifu hao.

Katika hatua nyingine, Dk. Slaa ametoa siku 90 kwa Rais Kikwete, kuueleza umma zilipo sh bilioni 70 zilizorejeshwa na wezi wa EPA.

Alisema Rais Kikwete aliahidi kuwa fedha hizo zitapelekwa katika Benki ya TIB, ambako kumeanzishwa dirisha la kuwakopesha wakulima.

Alibainisha kuwa kwa mujibu wa taarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), fedha hizo hazionekani zilipo kwa kuwa hakuna akaunti yoyote inayoonyesha zimewekwa.

Slaa, pia ametoa tuhuma kwa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kwamba kuna upotevu wa sh bilioni 220 kwa mujibu wa taarifa ya CAG.

Alisema mfanyabiashara mwenye malori kadi za magari yake zimekuwa zikishikiliwa na TRA kwa muda wa miaka 10 sasa na ameishitaki serikali na imeamriwa kumlipa kiasi hicho cha fedha.

"Sioni sababu ya serikali kulipa kiasi hicho cha fedha wakati aliyesababisha hasara hiyo yupo na bado anaendelea kufanya kazi TRA," alisema. Slaa alitumia fursa hiyo kumtaka Spika wa Bunge, Anne Makinda, asitumie nafasi ya uspika kama jukwaa la kisiasa kwa sababu yeye ni mjumbe wa Kamati Kuu ya Chama Cha Mapinduzi.

Alisema Makinda anatumia nafasi hiyo kuwa mwanasiasa badala ya kufanya kazi za uspika zilizoingiliana na kazi za siasa.


Slaa, ameahidi kuwa CHADEMA itazirudisha hoja zote za ufisadi kwenye mjadala ili zijadiliwe upya kwa kuwa Kikwete ameshindwa kuchukua hatua.

Naye Mwasheria wa CHADEMA, Mabere Marando, aliwataja wafanyakazi wawili wa kampuni ya Mbunge wa Igunga, Rostam Aziz (CCM) ya Caspian Ltd, ambao walighushi majina yao na nyaraka ili kufanikisha wizi wa sh bilioni 40.

Wafanyakazi hao ni John Kato, ambaye alijulikana kwa jina la Kamando William, na Bharaeti Goda, alijulikana kwa jina la Francis William, waliofanikiwa kuiba kiasi hicho cha fedha kupita Kampuni ya Kagoda Agriculture Ltd.

Alisema anao ushahidi wa jambo hilo na yuko tayari kuisaidia serikali kama ikiwapeleka mahakamani wahusika. Naye Fred Mpendazoe, alisema kilichofanywa na CCM kujidai kujivua gamba ni usanii mtupu, kwani katika uchaguzi mkuu uliopita Kikwete mwenyewe aliwanadi watuhumiwa wa ufisadi huku akiwasifu kuwa ni viongozi bora na hakuna kama hao. "Kama alivyo kuhani kanisani ndivyo walivyo waumini wake na kama alivyo sheikh msikitini ndivyo walivyo waumini wake…Kikwete hawezi kutenganishwa na hao waliovuliwa gamba", alisema Mpendazoe.
 
.................Mapambano bado yanaendelea..hakuna kulala...safi CDM no one to stop us...
 
Mwananchi failed to release names of Mafisadi why? Raia Mwema Did
 
Namwaminia Dk. wa ukweli. Lazima nchi ikombolewe na CDM:spy::spy:
A%20S%20465.gif
 
Mkuu W. J. Malecela, with due respect, ninazo facts 3 zifuatazo kuhusu EPA.
1. Sio kweli kuwa majina ya watu wote waliohusika na kashfa yalitajwa. Majina yote yaliyotajwa ni ya baadhi tuu, ndio maana mpaka leo, majina ya watu walio behindi baadhi ya makampuni yaliyochota EPA, hakutajwa na kamwe hayata tajwa!.
- Mkuu majina yote ya waliochota hela za EPA yalitajwa na waliepelekwa kwenye sheria, ni waliotajwa wana kesi only kwa sababu majina yao yapo kwenye kusaini makaratasi yaliotumika kuchota hela benki, waliochukua hela za EPA ni Mtandao, sasa Malecela alihusika vipi kuchota hela za vita against himself ndio ninapomuona Slaa akijishusha hadhi na wengine kama wewe mnaojaribu kushabikia bila FACTS!

2. Pia sio kweli kuwa majina ya wale wote waliotajwa kuhusika na EPA, walifikishwa mahakamani. Kati ya waliotajwa, ni baadhi tuu ndio waliofikishwa mahakamani, kuna wengi miongoni mwa waliotajwa, hawatafikishwa mahakamani kamwe!.
- Waliotajwa wote kuhusika na EPA walifikishwa mahakamani ni kwa sababu walisaini makaratasi na ushahidi wa kisheria upo, wale ambao hawakutajwa ni kwa sababu hakuna ushahidi wa kisheria wa kuwahusisha na kuvunja sheria, taifa haliwezi kuendeshwa kwa majungu kwamba fulani ni fisadi wa EPA ingawa hakutajwa na sisi wanannchi tunatakwia kukubali eti kwa sababu aliyesema ni Slaa, mkuu vipi litakuwa taifa au Banana Republic?

- I mean Sophia Simba amesema Chadema wanapewa hela kutoka nje kuleta vurugu basi ni kweli kwa vile aliyesema ni Sophia Simba, sasa mkuu hilo ni taifa au?


4. Huu ni ushauri tuu, itetee CCM kama chama, that they did nothing wrong with EPA money, in so doing, utakuwa umekisafisha chama chako na viongozi wake including Mzee Malecela. Ukimsafisha Mzee peke yake, trying to single him out from the rest, utetezi wako utaishia kuonekana ni utetezi nasaba, wa damu nzito kuliko maji.
- Well now ndio umeonyesha your true color, kwamba ni makosa kwangu kuuliza some serious question kwa sababu ya jina langu kufanana na la Malecela, ninarudia tena kukopa hela za EPA sio kuvunja sheria, isipokuwa kuchukuliwa kwa hela hizo na wasiohusika ndio kuvunja sheria, sasa huvunji sheria ya taifa kwa sababu kuna baadhi ya wezi ndani ya chama chako, yaani ni kama vile kusema kwa vile CCM ina mafisadi basi Wa-Tanzania wote ni mafisadi kwa nini wamekubali kutawaliwa nao for 50 years, mkuu vipi Slaa anatakiwa kuweka wazi ushahidi alionao kwamba Malecela ni mmoja wa waliosaini makaratasi yaliyoishia kuwaruhusu wasiohusika kuchukua hela za EPA.

- Mkuu kama mwananchi wa taifa hili nina haki ya kuuliza anything bila kujali jina wala chama, kama na wewe ulivyo na hiyo haki, now ninasema hivi kwenye hili Slaa amekosea sana na pia amejishusha hadhi na kufanya habari yake nzima ya safari hii kukosa credibility!


William @ NYC, USA.
 
Nina maoni yafuatayo kuhusu hii list mpya ya Mafisadi:

1. Uwezekano mkubwa ni kuwa CHADEMA wanataka sasa kuisambaratisha CCM baada ya kuona hoja yao ya UFISADI ya awali "imemtoa nyoka pangoni" kwa CCM "kujivua gamba" na "kuwa na nia ya kufukuza mafisadi katika chama".

2. Leo hii katika CCM: Mang'ula; Malecela na Magufuli ni members ambao kwa macho ya wana CCM na mashabiki wao walio wengi ni WASAFI na si MAFISADI. Kwa hiyo ina maana kwa kuwaweka katika kundi la mafisadi na kama kuna ushahidi mzito na unaokubalika kisheria na kisiasa ina maana CCM kwa asilimia kubwa itakuwa imejaa ufisadi.

3. Kama CCM au individuals waliotajwa hawatasimama na kutoa ushahidi wa kutosha na kuridhisha ku-prove their innocence na kuwa allegations za CHADEMA ni za uongo, basi mafisadi katika list ya awali hawatatoka katika chama. Wakilazimishwa kutoka, nao watadai walio katika list mpya watoke: this will mean mkorogano mkuu katika CCM na kama itakuwa handled vibaya ina maana CCM itaporomoka zaidi.

4. for sure kutakuwa na list mpya itakayohusisha mafisadi wa "Stimulus Package" lakini inawezekana unasubiriwa wakati mwafaka na ushahidi upatikane.

5. CCM wataendelea kucheza ngoma ya CHADEMA na wadau wengine mpaka hapo CCM itakapovaa nia ya dhati ya kukisafisha chama na kuwafukuza mafisadi wote CCM na Serikalini na kuwachukulia hatua za kisheria sambamba na kufanya mageuzi ya kweli katika matumizi ya pesa za walipa kodi.

Respect.

QED.

- Kama kuna ushahidi mkubwa unaokubalika kisheria, that is the point mkuu je upo?


William @ NYC, USA.
 
Hongera sana wapiganajai kwa kuendeleza vita hii maalum kwaajili ya ujombozi wa Taifa letu.

Kuhusu SiSi Emu kujivua gamba. Imejivua gamba gani hilo? Ikiwa Hao, kina Rosta, Lowasa na wengine ndio magamba, kwanini JK aliwashika mikono na kuwanadi wakati wa Kampeni juju tu? Au ni kuogopa nguvu ya hao watu katika mbio za CCM kumsaka mgombea urais 2015?

Pia wamejivua vipi gamba ikiwa Wabunge wa CCM bado wapo Bungeni Kushabikia Chama? Kwa wale waliofuatilia mjadala wa Muswada wa Kuboresha Idara ya Mahakama, jana 16 April mtakuwa shahidi kuwa Wabunge wa CCM bado wanaendelea kujivika magamba zaidi.

Wapiganaji mlioko Bungeni tunawategemea na tupo pamoja nanyi. Aluta Kontinua.

Nawakilisha.
 
mpambano wa kisiasa tanzania unavyozidi kuwa mkali, CDM waliahidi ndani ya siku 100 lazima mchakato wa Katiba mpya uanze na kweli wamefanikiwa japo hawapo madarakani lakini ilani yao ndio inayotekelezwa.

Wakati CCM inahangaika na gamba la kwanza tayari gamba la pili limejitokeza. CDM kiboko.

CUF, NCCR na wengine naona wao wamenasa kwenye tope la katiba. wamesahau sasa katiba ishaondoka kwa vyama vya siasi. CDM wametuachia wananchi na taasisi huru tuikabe koo serikali kuelekea utekelezaji.

game limenoga kwa kweli
 
Naomba kujuzwa kiongozi gani wa Tanzania ambaye ni msafi?jana Slaa ametaja orodha mpya ya mafisadi ila nakumbuka kuna wakati fulani Slaa nae alishatajwa ktk kashfa ya ufisadi akiwa katibu mkuu wa baraza la maaskofu,mbowe nae ameshalaumiwa ku2mia fedha za chama kwa matumizi yake binafsi,zitto nae ndo huyo anashutumiwa kila mara kuwa kambi ya mafisadi wa ccm
 
Mimi hapa,sina harufu ya ufisadi kabisa

Hata mimi. Ila ni kiongozi wa nyumba yangu. Sijui mtoa mada alikuwa akimaanisha viongozi gani. Kama ni viongozi wa kisiasa basi mimi naamini kabisa hakuna kiongozi msafi. Wasafi wote hawapo kwenye siasa; kuna waliojitoa na wengine waliondoka na Mwalimu Nyerere.
 
Naomba kujuzwa kiongozi gani wa Tanzania ambaye ni msafi?jana Slaa ametaja orodha mpya ya mafisadi ila nakumbuka kuna wakati fulani Slaa nae alishatajwa ktk kashfa ya ufisadi akiwa katibu mkuu wa baraza la maaskofu,mbowe nae ameshalaumiwa ku2mia fedha za chama kwa matumizi yake binafsi,zitto nae ndo huyo anashutumiwa kila mara kuwa kambi ya mafisadi wa ccm[/QUO

Sijakuelewa SENIOR MEMBER, Hebu nisaidie mie SENIOR EXPERT MEMBER
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom