Table manners

Table manners

Huu uzi nimeufurahia sana na nampongeza mleta mada maana utatusaidia kujua pia tamaduni za wenzetu na ikiwezekana kupractise kabisa ingawa sio lazima. Kwa wale ambao hawajapendezwa na hii mada sio lazima sana mtokwe mapovu na kupinga, vingine viangalie tu kama hakikuhusu pita tafuta kinachokuhusu mtawafanya watu wawe waoga kila anapotaka kuleta jambo la maana. Kuna watu wanasomea maswala ya mahusiano ya kimataifa ambapo pamoja na mambo mengine hili pia wanahitaji kulifahamu na la muhimu kwao kujua tamaduni za wengine. Unasoma au kama umeshamaliza umesoma kwa kutumia lugha ya kiingereza ambayo siyo yetu waafrika hasa watanzania, kwa nini hukupinga au kuacha shule? sio kila kitu lazima kikuhusu au uchangie.
 
Dah...tunalewa vibaya hivi?? Vile vijiti viko wapi hapa? Au havitumiki? Tuache ujinga bana.. mbona juzi tu hapa tumeenda kwa shangazi faizafoxy katupa pilau mkekani tukalipiga kwa mikono tukaenjoy vizuri tu bana..
 
ila mama mimi nadhani kula na umma sio utaratibu wa huku nyumbani afrika sisi tulishazoeshwa kula na mkono na kwa upande wangu sijawahi kabisa kula kwa kutumia kisu.
 
Nakumbaka tulikaribishwa dinner nyumba flan hivi, wenyeji walikuwa wanaishi kizungu ila ni wabongo, mda wa msosi tukaanza wageni ....' Baada ya kuweka msosi wenye mboga saba bonge la mlima chura haruki....' Kufika kwenye vitendea kazi (kisu na uma).....' Wageni wote sita tuliishia kuchukua uma tu tena kwa shingo upande sababu chepe haikuwepo (kijiko)... Aiseee baada ya wenyeji kuchukua msosi kiasi wakadaka umma na kisu wakaànza kutumia kwa ufundi na kitable manner zaidi..: Ila nashukuru tulianza wageni ..maana wangeanza wenyeji kama unavyotujua wabongo tungecopy na kupaste hapo sasa tungeumbuka mezani ..' Mara kisu kidongoke...Mara kisu kigandane na umaa ..Mara umwagemwage menu
 
Mweeh mambo ya uma na kisu yalishaga nishinda mie full kutumia mikono
 
Asante kwa Elimu. Ila hii imekaa kikike zaidi, hii nafikiri inawafaa zaidi wanaume wa Dar. Kwa sisi wa mikoani haya ni maigizo, kwa style hii hata mke itakulazimu kumshughulikia kwa utaratibu huu na matokeo yake ni kupigiwa. Sipingani na mpangilio huo ila upo ktk familia chache sana hasa ukizingatia maisha ya Watanzania wengi kuwa pangupakavu.
 
Hapo kwenye umma na kisu ndipo patamu!!!

Haya madini wanawake wengi mjini hawayajui, kwanza kupika tu ni mziki sasa unatarajia haya atayajua??
wasiopika ndiyo wanaojua hayo mambo,.. muda mwingi appointment zinakua za hotel
 
hivi hizi taratibu aliweka nani?
binafsi nimefeli hili somo..
 
Kawaida unapokaribishwa chakula mwenyeji anatakakwa aanze kuweka chakula mdomoni labda ilwe imeruhusiwa vingine. Mwenyeji anaanza kula baada ya wageni wote kuweka chakula kwenye sahani na wote wamekaa mezani. Chakula lazima kionjwe kabla hujaongeza chumvi na pilipili. Kuongeza chumvi au pilipili kabla ya kuonja ni kama dharau kwa mpishi au kuonyesha kuwa mpishi hajui kazi yake au huna imani nae. Inategemea na mkusanyiko wa watu, kama wana Imani basi baraka za chakula zitaanza kabla mwenyeji hajaweka chakula kinywani. Kama ni sherehe wageni wanaweza kuongeza maneno ya ucheshi mbele ya chakula na kumshukuru mwenyeji. Si tabia njema kuanza kula kabla watu wote hawajapata chakula na kuwa tayari kuanza kula.

Umma unashikwa mkono wa kushoto na kisu mkono wa kulia. Kisu mara nyingi kinakuwa chini, na kinatumka kukata chakula au kusaidia kuweka chakula kwenye umma. Kama kisu hakitumiki, umma unaweza kutumika kukita chakula kama vipande vya nyama au vipande vya viazi/chips. Usishike umma kama chepe na vidole kuvizungusha . Kwa kukita chakula umma unaweza kuudhibiti umma kwa kidole cha kunyooshea (cha pili kutoka gumba). Wakati wa kunywa supu, kijiko kinashikwa kwa mkono wa kulia. Kijiko kisiingie mdomoni chote, supu ivutwe kutoka kwenye kijiko bila kelele. Kisu kisisogelee mdomo au kulambwa. Chakula kinapotafunwa, mdomo uwe umefungwa, si tabia njema kuongea na chakula mdomoni, kulamba vidole au kula taratibu pia si uungwana.

Kama ni chakuila maalum (formal dinner) inakubalika kuweka siagi kutoka kwenye bakuli lake kutumia kisu kisu cha mkate na kuweka kwenye sahani ya pembeni. Hii itasaidia siagi kutoka kwenye bakuli kupata chenga za mikate wakati linazungushwa. Visu vitumike kupakia siagi lakini si kukata mkate na mikate inaweza kupasuliwa kati kati kwa kutumia mikono.

Mvinyo (wine) nyeupe au rose ishikiliwe kwenye glass iliyonyooka; nyekundu inakuwa kwenye glass pana. Mvinyo mweupe unapitishwa kabla ya mwekundu na wine nyepesi kabla ya nzito au mpya kabla ya yazamani (vintage). Kujimiminia wine inaruhusiwa kama mko wengi lakini ni tabia njema kuuliza watu wa upende wa pili kama watahitaji.


temp-in-video.jpg

Chakula mara nyingi kinakuwa katikati ya meza. Si uungwana kunyoosha mkono ufikie bakuli au sahani ya chakula, moumbe aliye karibu akusogezee. Kwa mpangilio huo huo chakula kipelekwe moja moja kwa yule aliyeomba. Si uungwa pia kutafuna kwa sauti, au kugonga uma na kisu kwenye sahani na kusababisha kelele.

Ukimaliza kula, kama ni formal dinner mnaweza kuongea na walaji wengine na kukubaliana kuwa mmemaliza, ukisubiri wahudumu, weka kisu na umma pamoja kwenye sahani kwa mpangilio wa saa kumi jioni, umma uwe chini ya kisu na ncha za umma ziangalie juu. Napkins ziwekwe juu ya meza bila kukunjwa chakula kinapokwisha.

Kwa chakula cha kifamilia, watoto wafundishwe kuomba ruhusa ya kuondoka mezani pindi wamalizapo chakula.

Simu za mkono au gadgets nyingine za kisasa hata gazeti au kitabu kiwekwe pembeni wakati wa chakula, kutext wakati wa kula, kuchat, kusoma kitabu au gazeti si uungwana. Kama kuna simu unaitegemea waeleze wenyeji na ikiita omba kutoka nje, fupisha maongezi na urudi ndani. Usicharge simu kwenye meza ya chakula hii si tabia njema.
table-set-jpg.382327


Cha kukumbuka pia unapomaliza kula hakikisha kiti unakirudisha mahala pake yaani pale ulipokitoa ukitaka kukaa
 
hizo wine zatia hamu .. okey na wale wanao ongea na chakula mdomoni halafu unaona mchakula wake jamani jamani uwiiiii uwii... halafu tatizo hilo wanalo masista du wale wanaojifanya kila mada anajua .. basi sawa kujua si kosa meza kwanza ndiyo uongeee ..
Mara viparticles vya chakula vinakurukia kwenye sahani😀😀
 
Nakumbaka tulikaribishwa dinner nyumba flan hivi, wenyeji walikuwa wanaishi kizungu ila ni wabongo, mda wa msosi tukaanza wageni ....' Baada ya kuweka msosi wenye mboga saba bonge la mlima chura haruki....' Kufika kwenye vitendea kazi (kisu na uma).....' Wageni wote sita tuliishia kuchukua uma tu tena kwa shingo upande sababu chepe haikuwepo (kijiko)... Aiseee baada ya wenyeji kuchukua msosi kiasi wakadaka umma na kisu wakaànza kutumia kwa ufundi na kitable manner zaidi..: Ila nashukuru tulianza wageni ..maana wangeanza wenyeji kama unavyotujua wabongo tungecopy na kupaste hapo sasa tungeumbuka mezani ..' Mara kisu kidongoke...Mara kisu kigandane na umaa ..Mara umwagemwage menu
ha ha hahaha
 
Asante kwa Elimu. Ila hii imekaa kikike zaidi, hii nafikiri inawafaa zaidi wanaume wa Dar. Kwa sisi wa mikoani haya ni maigizo, kwa style hii hata mke itakulazimu kumshughulikia kwa utaratibu huu na matokeo yake ni kupigiwa. Sipingani na mpangilio huo ila upo ktk familia chache sana hasa ukizingatia maisha ya Watanzania wengi kuwa pangupakavu.
Ni akiba ya maneno tu mkuu. Nilikwenda kusuka mitaa flani dar, nilikaa kwa msusi siku nzima, basi lunch wakaniuliza tukuletee chakula gani, kulikuwa na muuza chips pembeni, nikaagiza zege na mishikaki, basi sahani imeletwa na toothpick, nikauliza hakuna umma, nikaambiwa umma ni mmoja na ni kitendea kazi cha kukorogea mayai, nikipewa inamaana kazi itasimama. Niliienjoy kula zege kwa toothpick.
 
vizuri
na ni vyema wamama wakawafunza watoto wao haya mambo mapema sana
 
Back
Top Bottom