Table manners

Table manners

Kawaida unapokaribishwa chakula mwenyeji anatakakwa aanze kuweka chakula mdomoni labda ilwe imeruhusiwa vingine. Mwenyeji anaanza kula baada ya wageni wote kuweka chakula kwenye sahani na wote wamekaa mezani. Chakula lazima kionjwe kabla hujaongeza chumvi na pilipili. Kuongeza chumvi au pilipili kabla ya kuonja ni kama dharau kwa mpishi au kuonyesha kuwa mpishi hajui kazi yake au huna imani nae. Inategemea na mkusanyiko wa watu, kama wana Imani basi baraka za chakula zitaanza kabla mwenyeji hajaweka chakula kinywani. Kama ni sherehe wageni wanaweza kuongeza maneno ya ucheshi mbele ya chakula na kumshukuru mwenyeji. Si tabia njema kuanza kula kabla watu wote hawajapata chakula na kuwa tayari kuanza kula.

Umma unashikwa mkono wa kushoto na kisu mkono wa kulia. Kisu mara nyingi kinakuwa chini, na kinatumka kukata chakula au kusaidia kuweka chakula kwenye umma. Kama kisu hakitumiki, umma unaweza kutumika kukita chakula kama vipande vya nyama au vipande vya viazi/chips. Usishike umma kama chepe na vidole kuvizungusha . Kwa kukita chakula umma unaweza kuudhibiti umma kwa kidole cha kunyooshea (cha pili kutoka gumba). Wakati wa kunywa supu, kijiko kinashikwa kwa mkono wa kulia. Kijiko kisiingie mdomoni chote, supu ivutwe kutoka kwenye kijiko bila kelele. Kisu kisisogelee mdomo au kulambwa. Chakula kinapotafunwa, mdomo uwe umefungwa, si tabia njema kuongea na chakula mdomoni, kulamba vidole au kula taratibu pia si uungwana.

Kama ni chakuila maalum (formal dinner) inakubalika kuweka siagi kutoka kwenye bakuli lake kutumia kisu kisu cha mkate na kuweka kwenye sahani ya pembeni. Hii itasaidia siagi kutoka kwenye bakuli kupata chenga za mikate wakati linazungushwa. Visu vitumike kupakia siagi lakini si kukata mkate na mikate inaweza kupasuliwa kati kati kwa kutumia mikono.

Mvinyo (wine) nyeupe au rose ishikiliwe kwenye glass iliyonyooka; nyekundu inakuwa kwenye glass pana. Mvinyo mweupe unapitishwa kabla ya mwekundu na wine nyepesi kabla ya nzito au mpya kabla ya yazamani (vintage). Kujimiminia wine inaruhusiwa kama mko wengi lakini ni tabia njema kuuliza watu wa upende wa pili kama watahitaji.


temp-in-video.jpg

Chakula mara nyingi kinakuwa katikati ya meza. Si uungwana kunyoosha mkono ufikie bakuli au sahani ya chakula, moumbe aliye karibu akusogezee. Kwa mpangilio huo huo chakula kipelekwe moja moja kwa yule aliyeomba. Si uungwa pia kutafuna kwa sauti, au kugonga uma na kisu kwenye sahani na kusababisha kelele.

Ukimaliza kula, kama ni formal dinner mnaweza kuongea na walaji wengine na kukubaliana kuwa mmemaliza, ukisubiri wahudumu, weka kisu na umma pamoja kwenye sahani kwa mpangilio wa saa kumi jioni, umma uwe chini ya kisu na ncha za umma ziangalie juu. Napkins ziwekwe juu ya meza bila kukunjwa chakula kinapokwisha.

Kwa chakula cha kifamilia, watoto wafundishwe kuomba ruhusa ya kuondoka mezani pindi wamalizapo chakula.

Simu za mkono au gadgets nyingine za kisasa hata gazeti au kitabu kiwekwe pembeni wakati wa chakula, kutext wakati wa kula, kuchat, kusoma kitabu au gazeti si uungwana. Kama kuna simu unaitegemea waeleze wenyeji na ikiita omba kutoka nje, fupisha maongezi na urudi ndani. Usicharge simu kwenye meza ya chakula hii si tabia njema.
table-set-jpg.382327

Adabu za kuanza kula chakula kwa Muislam ni:-
1. Kunawa mikono yako yote miwili kabla ya kuanza kula.
2. Kumtaja Mwenyezi Mungu kwa kusema ‘BismiLlaah’ (Jina la Allaah Subhanau Wa taala).
3. Kula kwa mkono wa kulia na kula kilicho mbele ya sahani upande wako kama mnakula kwa pamoja.
4. Inapendekezwa kukaa chini ( kwenye mkeka/ jamvi) ukiwa umekunja miguu.
5. Kuacha kuongea / mazungumzo wakati wa mlo.
6. Kumshukuru Mwenyezi Mungu baada ya kula na utamshukuru mwenyeji wako/ aliyeandaa chakula na kumwombea dua.

Nimewalilisha. Ahsanteni
 
sijawai alikwa lunch au dinner kwa mtu maishani
sijui ni huu usenior bachelor?
napelekwa tu kwenye michemsho,viti moto haramu nk
 


Msosi unageuzwa lecture..

Nilialikwa na rafiki yangu mmoja kumbe alikua na wageni wazungu bwana, akaanza kunipa somo jinsi ya kushika uma mara kuweka vitambaa shingoni ili uschafue nguo..

Nkamwambia braza eh, maisha mafupi haya.. sheria hizo tutazifuata tukiwatembelea nchi zao, kama wapo hapa mi nitanawa na nitakula kwa mikono

Respect our culture
kile kitambaa cha kama mtoto anaetoa udenda kile mimi siwezi kujifunga kamwe
bora waninyime msosi wao
 
Kawaida unapokaribishwa chakula mwenyeji anatakakwa aanze kuweka chakula mdomoni labda ilwe imeruhusiwa vingine. Mwenyeji anaanza kula baada ya wageni wote kuweka chakula kwenye sahani na wote wamekaa mezani. Chakula lazima kionjwe kabla hujaongeza chumvi na pilipili. Kuongeza chumvi au pilipili kabla ya kuonja ni kama dharau kwa mpishi au kuonyesha kuwa mpishi hajui kazi yake au huna imani nae. Inategemea na mkusanyiko wa watu, kama wana Imani basi baraka za chakula zitaanza kabla mwenyeji hajaweka chakula kinywani. Kama ni sherehe wageni wanaweza kuongeza maneno ya ucheshi mbele ya chakula na kumshukuru mwenyeji. Si tabia njema kuanza kula kabla watu wote hawajapata chakula na kuwa tayari kuanza kula.

Umma unashikwa mkono wa kushoto na kisu mkono wa kulia. Kisu mara nyingi kinakuwa chini, na kinatumka kukata chakula au kusaidia kuweka chakula kwenye umma. Kama kisu hakitumiki, umma unaweza kutumika kukita chakula kama vipande vya nyama au vipande vya viazi/chips. Usishike umma kama chepe na vidole kuvizungusha . Kwa kukita chakula umma unaweza kuudhibiti umma kwa kidole cha kunyooshea (cha pili kutoka gumba). Wakati wa kunywa supu, kijiko kinashikwa kwa mkono wa kulia. Kijiko kisiingie mdomoni chote, supu ivutwe kutoka kwenye kijiko bila kelele. Kisu kisisogelee mdomo au kulambwa. Chakula kinapotafunwa, mdomo uwe umefungwa, si tabia njema kuongea na chakula mdomoni, kulamba vidole au kula taratibu pia si uungwana.

Kama ni chakuila maalum (formal dinner) inakubalika kuweka siagi kutoka kwenye bakuli lake kutumia kisu kisu cha mkate na kuweka kwenye sahani ya pembeni. Hii itasaidia siagi kutoka kwenye bakuli kupata chenga za mikate wakati linazungushwa. Visu vitumike kupakia siagi lakini si kukata mkate na mikate inaweza kupasuliwa kati kati kwa kutumia mikono.

Mvinyo (wine) nyeupe au rose ishikiliwe kwenye glass iliyonyooka; nyekundu inakuwa kwenye glass pana. Mvinyo mweupe unapitishwa kabla ya mwekundu na wine nyepesi kabla ya nzito au mpya kabla ya yazamani (vintage). Kujimiminia wine inaruhusiwa kama mko wengi lakini ni tabia njema kuuliza watu wa upende wa pili kama watahitaji.


temp-in-video.jpg

Chakula mara nyingi kinakuwa katikati ya meza. Si uungwana kunyoosha mkono ufikie bakuli au sahani ya chakula, moumbe aliye karibu akusogezee. Kwa mpangilio huo huo chakula kipelekwe moja moja kwa yule aliyeomba. Si uungwa pia kutafuna kwa sauti, au kugonga uma na kisu kwenye sahani na kusababisha kelele.

Ukimaliza kula, kama ni formal dinner mnaweza kuongea na walaji wengine na kukubaliana kuwa mmemaliza, ukisubiri wahudumu, weka kisu na umma pamoja kwenye sahani kwa mpangilio wa saa kumi jioni, umma uwe chini ya kisu na ncha za umma ziangalie juu. Napkins ziwekwe juu ya meza bila kukunjwa chakula kinapokwisha.

Kwa chakula cha kifamilia, watoto wafundishwe kuomba ruhusa ya kuondoka mezani pindi wamalizapo chakula.

Simu za mkono au gadgets nyingine za kisasa hata gazeti au kitabu kiwekwe pembeni wakati wa chakula, kutext wakati wa kula, kuchat, kusoma kitabu au gazeti si uungwana. Kama kuna simu unaitegemea waeleze wenyeji na ikiita omba kutoka nje, fupisha maongezi na urudi ndani. Usicharge simu kwenye meza ya chakula hii si tabia njema.
table-set-jpg.382327
Hii ni kwa akina mboga saba. huku kwetu ni mwendo wa mduara, sinia la ugali/wali kati na vibakuli vya mboga, ukishanawa mikono (tena mara nyingi mkono wa kulia tu) unakula, ukishiba unanawa mkono unasepa. Kushukuru pia ni majaliwa.
 
hizo wine zatia hamu .. okey na wale wanao ongea na chakula mdomoni halafu unaona mchakula wake jamani jamani uwiiiii uwii... halafu tatizo hilo wanalo masista du wale wanaojifanya kila mada anajua .. basi sawa kujua si kosa meza kwanza ndiyo uongeee ..
 
Kuna siku nlikua mahali, nlikua na njaa nikapewa kuku (kidali) ilibidi nimle kwa mkono watu wakipita najifanya nimeshika umma na kisu, wakiondoka naendeleza kwa mkono
Hahaha umenifurahisha sana mm pia napenda kumla kuku kwa mkono
Cku moja nlkuwa mahala akaja dada mmja na jamaa akaagiza wali samaki alikuwa anapata shida kumla samaki hadi huruma,nkajisemea c amle kwa mkono tu?
 
Nyama zote zinabaki kweny mfupa.

Halafu hivi ni haki kweli kula wali kwa uma???? Unautani wa kichina kula wali kwa vijiti eeeh???
Wali kwa umma tena?..Hizo mbwembwe za kichina siziwezi..Hata kisu na uma natumia pale inapobidi kulingana na mazingira niliyopo
 
Kila jamii itabaki kuwa na tamaduni zake but kikubwa ni kutafuna na kumeza tu, zingine mbwembwe tu.
 
Looks delicious!, calories zake sasa..
Sure ni Delicious... Wajua beef iliyokatwa katwa kidogo kwenye Burger au pizza always huwa bomba sana... kuliko iliyosagwa.

Hii kitu ukiletewa lazima uombe Sahani na Uma midomo size hiyo hatuna... labda yule comedian Kazoa wa jambo na vijambo
 
  • Thanks
Reactions: kui
Back
Top Bottom