Tabibu Mwaka akaidi amri ya serikali

Tabibu Mwaka akaidi amri ya serikali

....nionavyo ni kwamba JJ Mwaka kagusa maslahi yenu maana mnamtafuta kutoka angles zote
unaelewa lakini anachokifanya jj mwaka kwa sasa???tega muda wako channel tena tangazo lake kwa siku linarushwa zaidi hata ya mara 20,,,,,ubaya sio tangazo angalia maudhui ya tangazo lake ni dhahiri anapingana na mamlaka zilizo muadhibu
 
Huwa napenda kusikiliza hapa tu " Naitwa JJ Mwaka ila wengi wanapenda kuniita Doctor Mwaka..."

Tanzania yetu nzuri sana.unaweza kuta Dispensary imefungiwa kwa alama ya maneno "Huduma imesitishwa " lakini bado raia wanapata huduma, tena zahanati ipo barabarani kabisa.

Siamini kwamba wahusika waliomfungia hawajui kuwa anaendeleza tiba kwa mlango wa nyuma.

Usifikiri sana, ndio nchi yetu hiiii
 
Huyu jamaa anapata wapi jeuri maana naangalia Channel Ten bado anaendelea kujitangaza licha ya kupigwa Ban na Serikali.
Jeuri yake inatoka wapi?
 
Ukiona anaendelea kutoa hizo huduma ujuwe alishamalizana na mamlaka husika zilizokuwa zimemfungia. Laa sivyo angekuwa ameshakamatwa na angekuwa lupango saa hizi.

Hivyo msiwe na wasi wasi, endeleeni kupata hizo huduma za kuzaa na kusikiliza matangazo ya obstetrics & gyaecology toka kwa Dr bingwa J. J. Mwaka ndani ya Foreplan Company Ltd.
 
Elimu ni muhimu sana, hii kampuni ni nyingine ila kaongeza Tanzania limited
 
Mjanja wa town hafuatilii mambo ya wanaume wenzake Fanya yako kijana mwisho wa siku wenzenu tunakula kuku kwa mrija mnaishia kutuita wanaume wa dar
 
Baada ya kufungiwa amekaidi agizo hilo na anaendelea na utabibu kama kawaida,na hata leo alikuwa na kipindi kilichorushwa na channel 10.

Je, mtu huyu yupo juu ya sheria? Yale maagizo hayamuhusu?

Mwenye ufahamu anifahamishe maana nimeshangazwa na hili tukio.

Huyu mtu yuko vizuri anajua kujieleza
 
Jamani sio wivu au unafiki , ukweli inaboa sana kumwona Dr Mwaka sasa hivi channel ten. Kwa maneno yake yamenichefua sana.
Anasema" nimeokoa ndoa za watu weng, mama akiniona analia anasema bila wewe Dr Mwaka nisingepata huyu mtoto, nilikuwa natibu mpaka kutoka duniani kote."

Kaniuzi sana kwa kauli inamaana huyu Mwaka ni nani? Mwenye uwezo zaidi ya Mungu? Nimebadilisha Chanel anaboa sana, mm mwenyew nilitumia kiasi kikubwa cha pesa lkn sikupona. Huyu tapeli mkubwa.
 
Usiwe na wasiwasi, suala la muda tu atakuwa historia, Believe ME
 
Kwani hao mnaosema wametapeliwa kwani aliwalazimisha kwenda au walimfuata wenyewe?
 
Anaijaribu serikali ile mbaya...hata hivyo TCRA wanawajibika kuwahoji Channel ten
 
Mi Nadhani sio dr. Mwaka aliyekaidi, ni baadhi ya watendaji wa magufuli ndo wamezingua....hapa kuna harufu ya urushwa.
 
Kwani hao mnaosema wametapeliwa kwani aliwalazimisha kwenda au walimfuata wenyewe?
Walimfuata kwa sababu alijinadi anaweza kutatua tatizo, mwisho tatizo linamshinda, mtu anatoa zaidi ya million 1 kugharamia matibabu. Aponi sasa si utapeli nini?
 
Back
Top Bottom