KikulachoChako umenikumbusha enzi hizo, nilikuwa konda wa ruti ya Kimara Posta, siku ya siku mama mmoja akapandia Akiba, nauli ilikuwa 200 tu kufika posta (route yote ilikuwa sh 300).
Wakati wa kushuka mi namdai nauli yeye ananidai chenji eti anadai kanipa sh 5,000/-, mi nikamwambia sijapokea chochote kutoka kwako, abiria wengine wakaanza kunishambulia eti sisi makonda ndo tabia zetu, sasa yule mama nikamuuliza ilikuwaje kwanza utoe hela kubwa vile kwa sh 200 tu, akasema hana hela nyingine yoyote na kwa hasira akataka kuvua nguo eti nimsachi.
Baada ya abiria kupiga sana yowe nikamwambia suka peleka gari central police, tulivyofika tukatoa maelezo ya kina, kuja kumsachi
yule mama alikuwa ana sh 500 kama ishirini hivi kazichimbia kwenye mfuko wa nguo ya ndani. Tulimwacha police na sijui nini kiliendelea.