Ha ha ha ha mkuu unachukua tahadhari mapema,ukipanda gari unalazimishwa kurudi nyuna halafu kwenye kushuka wanakutaka uwahi,sasa na msongamano ule mpaka uje ushuke umeshatwishwa maneno machafu kibao.Kumbe wengi tu wapanda dala dala.
Wale watu wana matusi mi huwa nawaogopa, nikopanda nimeshika nauli kabisa, kama nashuka nawahi mbele kabla sijasikia maneno machafu
I wish angetokea konda hapa naye akaeleza kero zake kuhusu abiria. Kuna abiria wanakera jamani mweh!
Kutokana na pilika pilika za maisha nikajiukuta nimeangukia katika kazi ya ukondakta...........daladala yetu ilikuwa inapiga ruti za TEMEKE na MUHIMBILI........Nilichojifunza katika kazi ya ukonda ni kwamba abiria kwa kiasi kikubwa ndio wanaofanya makonda kuwa na lugha chafu kutokana na kukutana na watu mbali mbali na wenye hulka mbali mbali........kuna siku siku wakati naokoteza nauli zangu ,nikafika kwa jamaa Fulani wawili walokuwa wakipiga story....mmoja wapo alitoa akatoa noti ya shilingi elfu tano...nikamuuliza kistaarabu kuwa bosi wangu tukate ngapi...yule jamaa hata bila aibu akanijibu...unauliza ukate ngapi kwani uliniona nimepanda na mama yako...sikumkawiza nikamrukia kichwa cha mkizi kilichoacha meno yake mawili yakimwagika kama karanga...na huo ndio ukawa mwisho wa safari na tuakishia polisi...Abiria mwingine tena mwanamke, nakumbuka alipandia maeneo ya VETA kufika kituo cha Darajani namdai nauli anasema alishatoa elfu kumi na anadai chenji yake wakati mimi ndio kwanza naanza kukusanya njuruku.......yule dada kila nikijaribu kumuelekeza kuwa hebu jiangalie vizuri labda kuna sehemu uliiweka alafu umejisahau....yule dada akaanza kupayuka kwa sauti kubwa mpaka abiria wengine wakaanza kuniwakia kuwa sisi makonda ndio tabia zetu.....Gari Zima ikawa zogo mtindo mmoja.....Ili kuepusha zogo ikabidi dereva wangu atoe hela yake mfukoni na kumpa yule dada kama chenji huku akinilaumu kwa kutokuwa makini.....tulipofika maeneo ya fire sasa wakati anatoka nyuma kuelekea mlangoni ili ashuke ndipo ile elfu kumi ikaanguka chini pwah.....Watu wote wakahamaki na baadhi yao wakaanza kuniomba msamaha akiwemo na yule dada...aliniomba msamaha mpaka akaanza kulia maana hajanibakisha kwa mitusi mizito mzito ya nguoni......Namimi nikapata power sasa na nikaanza kuwashambulia abiria kuwa msiwe mnaingilia mambo yasiyowahusu.........Yaani abiria toka nyumbani anaamua kabisa kuwa ngoja nikamalizie hasira zangu kwa konda, majitu unayauliza mara kumi kumi kuwa kituo Fulani hakuna anayeshuka yote yanakutolea macho kama vile wewe sanamu....alafu ukimpitisha anaanza kukutukana na hapo ndipo ugomvi wa kukata na shoka unapoanzia..........Abiria wengine nao wanaleta ubishi uisio na kichwa wala miguu.....jitu unaliambia kuwa usishuke hapo gari inatembea lenyewe linajifanya kujua linakuvizia mlango upo wazi linaruka........likivunjika mguu linasema kuwa konda kanisukuma...........Yaani kazi ya ukonda lazima uonekane kama mwendawazimu japo una akili timamu kwa kero za abiria...njia ambayo niliinjoi kidogo ni ya mwenge ingawa nayo sijakaa sana....abiria wa njia ile bwana kama konda unionekana mchafu mchafu hawapandi gari yako......ni wa elewa kweli....hata kama mkipishana kauli mnaelewesha kwa upole.......DAH MAISHA YA UKONDA NI RAHA SANA........[/QoUOTE]woòoooow kweli wanaonekana kama wehu
Kutokana na pilika pilika za maisha nikajiukuta nimeangukia katika kazi ya ukondakta...........daladala yetu ilikuwa inapiga ruti za TEMEKE na MUHIMBILI........Nilichojifunza katika kazi ya ukonda ni kwamba abiria kwa kiasi kikubwa ndio wanaofanya makonda kuwa na lugha chafu kutokana na kukutana na watu mbali mbali na wenye hulka mbali mbali........kuna siku siku wakati naokoteza nauli zangu ,nikafika kwa jamaa Fulani wawili walokuwa wakipiga story....mmoja wapo alitoa akatoa noti ya shilingi elfu tano...nikamuuliza kistaarabu kuwa bosi wangu tukate ngapi...yule jamaa hata bila aibu akanijibu...unauliza ukate ngapi kwani uliniona nimepanda na mama yako...sikumkawiza nikamrukia kichwa cha mkizi kilichoacha meno yake mawili yakimwagika kama karanga...na huo ndio ukawa mwisho wa safari na tuakishia polisi...Abiria mwingine tena mwanamke, nakumbuka alipandia maeneo ya VETA kufika kituo cha Darajani namdai nauli anasema alishatoa elfu kumi na anadai chenji yake wakati mimi ndio kwanza naanza kukusanya njuruku.......yule dada kila nikijaribu kumuelekeza kuwa hebu jiangalie vizuri labda kuna sehemu uliiweka alafu umejisahau....yule dada akaanza kupayuka kwa sauti kubwa mpaka abiria wengine wakaanza kuniwakia kuwa sisi makonda ndio tabia zetu.....Gari Zima ikawa zogo mtindo mmoja.....Ili kuepusha zogo ikabidi dereva wangu atoe hela yake mfukoni na kumpa yule dada kama chenji huku akinilaumu kwa kutokuwa makini.....tulipofika maeneo ya fire sasa wakati anatoka nyuma kuelekea mlangoni ili ashuke ndipo ile elfu kumi ikaanguka chini pwah.....Watu wote wakahamaki na baadhi yao wakaanza kuniomba msamaha akiwemo na yule dada...aliniomba msamaha mpaka akaanza kulia maana hajanibakisha kwa mitusi mizito mzito ya nguoni......Namimi nikapata power sasa na nikaanza kuwashambulia abiria kuwa msiwe mnaingilia mambo yasiyowahusu.........Yaani abiria toka nyumbani anaamua kabisa kuwa ngoja nikamalizie hasira zangu kwa konda, majitu unayauliza mara kumi kumi kuwa kituo Fulani hakuna anayeshuka yote yanakutolea macho kama vile wewe sanamu....alafu ukimpitisha anaanza kukutukana na hapo ndipo ugomvi wa kukata na shoka unapoanzia..........Abiria wengine nao wanaleta ubishi uisio na kichwa wala miguu.....jitu unaliambia kuwa usishuke hapo gari inatembea lenyewe linajifanya kujua linakuvizia mlango upo wazi linaruka........likivunjika mguu linasema kuwa konda kanisukuma...........Yaani kazi ya ukonda lazima uonekane kama mwendawazimu japo una akili timamu kwa kero za abiria...njia ambayo niliinjoi kidogo ni ya mwenge ingawa nayo sijakaa sana....abiria wa njia ile bwana kama konda unionekana mchafu mchafu hawapandi gari yako......ni wa elewa kweli....hata kama mkipishana kauli mnaelewesha kwa upole.......DAH MAISHA YA UKONDA NI RAHA SANA........
Mkuu kuna haja gani ya kuuliza ukate wangape pindi unapopewa hela kubwa? Ni lazima kumlipia mtu?
Ni kweli kuna baadhi ya abiria ambao huwa wanawakera makonda pamoja na abiria wenzao lakini kwa ujumla makondakta wamezidi kuwa kero.
Kinachonikera sana pale daladala linakuja kituoni mida ya saa moja usiku watu kibao wanangombania alafu kondakita anafunga mrango na kusema gari haliendi huko anakaa kituoni hapo alafu baadae kidogo anapandisha watu anaotaka yeye,unakuta umekimbiza gari tokea kwa bakhare kariakoo alafu anasema haendi ili akukomoe tu abiria inaboha sana iyo
Kinachonikera sana pale daladala linakuja kituoni mida ya saa moja usiku watu kibao wanangombania alafu kondakita anafunga mrango na kusema gari haliendi huko anakaa kituoni hapo alafu baadae kidogo anapandisha watu anaotaka yeye,unakuta umekimbiza gari tokea kwa bakhare kariakoo alafu anasema haendi ili akukomoe tu abiria inaboha sana iyo
Unakuta mmekaa wawili na mnapiga story kama mnafahamiana, isitoshe mmepandia kituo kimoja, nikiomba nauli akatoa mmoja huku yule mwingine akiwa hata hajisachi inabidi niombe uhakiki kama unamlipia jamaa.
Hafu kila abiria anayeingia kwenye gari anatuona makonda kama vile hatujasoma, tumeishia la tatu c, acheni dharau bana.