encyclopaedia Tanzaree
JF-Expert Member
- Sep 10, 2017
- 517
- 405
Habari zenu wanajamvi,
Ama baada ya salamu napenda niende moja kwa moja kwenye dhumuni la andiko hili.
Mimi ni kijana mwenye umri wa miaka 27 ninaishi Dar es Salaam.
Kuna jambo ambalo linanitatiza sana linalotokana na tabia yangu ya kupendelea zaidi kula matuda asubuhi kuliko chai, supu wala chakula kingine chochote. Ni mwaka wa 7 sasa sijui hata ladha ya chai ikoje kwani kila nikiamka asubuhi najikuta natamani kula matunda kama ndizi mbivu, machungwa, mananasi, matikiti n. K
Tabia hii ya kutokupenda kunywa chai nilianza tangu nikiwa mdogo kwani ilikuwa ikiachwa pesa ya matumizi nyumbani basi kwenye kipengele cha chai nilikuwa naiomba pesa ya vitafunwa naenda kununua matunda au vitafunwa vingine ambavyo nilikuwa nikipendelea kuvila bila ya chai.
Naomba ushauri wenu (ikiwezekana wa kitabibu) juu ya madhara au faida inayoweza kujengwa kutokana na tabia yangu hii.
NAWASILISHA
Ama baada ya salamu napenda niende moja kwa moja kwenye dhumuni la andiko hili.
Mimi ni kijana mwenye umri wa miaka 27 ninaishi Dar es Salaam.
Kuna jambo ambalo linanitatiza sana linalotokana na tabia yangu ya kupendelea zaidi kula matuda asubuhi kuliko chai, supu wala chakula kingine chochote. Ni mwaka wa 7 sasa sijui hata ladha ya chai ikoje kwani kila nikiamka asubuhi najikuta natamani kula matunda kama ndizi mbivu, machungwa, mananasi, matikiti n. K
Tabia hii ya kutokupenda kunywa chai nilianza tangu nikiwa mdogo kwani ilikuwa ikiachwa pesa ya matumizi nyumbani basi kwenye kipengele cha chai nilikuwa naiomba pesa ya vitafunwa naenda kununua matunda au vitafunwa vingine ambavyo nilikuwa nikipendelea kuvila bila ya chai.
Naomba ushauri wenu (ikiwezekana wa kitabibu) juu ya madhara au faida inayoweza kujengwa kutokana na tabia yangu hii.
NAWASILISHA