Taarifa ya serikali juu ya mgomo wa madaktari

Taarifa ya serikali juu ya mgomo wa madaktari

waziri anaongea kwa hofu tupu, inaonekana jamaa ni mgeni sana kwani anaongea kwa kutetemeka

sio mgeni hata kule jimboni kwake aliiba kura huyo ....ni zezeta kweli hilo jamaaa..eti haji mponda??? majina haya ya Haji wanakuwaga madoktwa toka lini???
 
Huyu Waziri Mponda ni bure kabisa!. He desrves to be fired!. Hata ile ya kudai serikali iko tayari kuendeleza mazungumzo!.
 
Kwamba mgomo ule ni batili kwa kuwa sheria inawazuia madaktari na watumishi wengine wa sekta muhimu kugoma.

Sheria gani?? Mbona haisemi??

Je hii sheria ipo TZ tu au ni universal??

Mpotoshaji sana huyu!! Ila nimefurahi kuwa anatambua kuwa afya ni sector muhimu!!
 
machali anaomba kutenguliwa kanuni ili kauli ya waziri wa afya ijadiliwe
 
Kwani serikali Inapata Nini hasa ikidanganya Umma????!!!!??? .. Mbona hawasemi hoja za madaktari.. Sio Posho, hoja ni kitu kingine hawasemi hawa jamaa..
 
MAT ni chama cha madaktari wa Serikali? Mbona naiona MAT kama professional body kama NBAA,ERB nakadhalika kwamba ukijiunga unapata utambulisho kwamba wewe ni daktari unayetambuliwa nchini kulingana vigezo vilivyowekwa na haimaanishi kwamba wewe sio daktari! Sasa yawezekanaje Dr Ulimboka asiwe na sifa akawa mwanachama mpaka kuwa kiongozi? Na je issue nini mpaka sasa uhalali wa Ulimboka kuwa Dr au mgomo wa madaktari?
 
Nafikiri wa JF inabidi mbadili mtazamo. Ni vizuri sana kujadili hoja na sio kumjadili mtu.

Punguzeni Jazba na kujadili hoja.
 
-Ni kweli Dr Ulimboka hana usajili? Ni bodi ipi hiyo? Ninavyofahamu Madaktari hawana bodi kama ERB au NBAA.
-MaDaktari wetu wameanza kulipwa? Wamepewa na hizo "Green Cards za NHIF?

Drs na nurses hawawezi kufanya kazi kama hawajasajiliwa. Zipo bodi zao.
 
Waziri amesema Ulimboka sio daktari na anashangaa alipataje kuongoza kamati ya kudai haki za madaktari. Alifukuzwa mwaka 2005 na kuomba msamaha kwa Rais hakufafanua kama alipewa au la. Waziri anamwita bw. Ulimboka kwa sababu si Dk.

Si Dr. Kwa maana kwamba hajasomea udaktari kwa hiyo hana sifa ya kuitwa Dr. au?
Si Dr. Kwa maana kwamba hajasajiriwa na baraza la madaktari la Tanganyika au?

Na je yeye ni mwajiiriwa wa serikali au siyo mwajiriwa, na kama ni mwajiriwa, ameajiriwa kama daktari au kama paramedical?
Na kama siyo Dr. aliajiriwaje huku hana sifa za U-Dr.?

Haya ni baadhi ya maswali waziri anatakiwa ayajibu, lakini kwa upande wa pili, Ndugu Ulimboka naye aje atupe upande wa pili wa hadithi, atuthibitishie kweli yeye ni Dr. au siyo kama waziri anavyosema.
 
Ndugu Mponda needs to go back to IHI to continue doing whatever he was doing there. Hivi hakunaga recruiting agencies waje wajibebee madaktari wa Kitanzania wakahudumie nchi nyingine? Kama ni kiapo kwani kilisema kuhudumia watanzania tu? si binadamu yeyote?
 
hoja ya waziri itakosa mashiko kama hoja haito jadiliwa na wabunge/
 
Kanuni ya bunge imewanyima wabunge kujadili ripoti ya serikali kuhusu mgomo wa madaktari
 
Naibu spika karudisha hoja ya mgomo wa madaktari kwa kamati ya bunge ya huduma za jamii eti waonane na madaktari na serikali kuweza kujua undani wa issue nzima ya mgomo. Hivyo hakutakuwa na mjadala wa suala hilo. Jamaa wamemaliza kisiasa issue nzima..............kesi ya ngedere kapelekewa nyani aifanyie uamuzi
 
Back
Top Bottom