Ndugu yangu
JF-Expert Member
- Aug 3, 2013
- 680
- 365
Hakuna chama kibaya kilichowahi kutokea chini ya jua kama ccm, zaidi ya laana
Kwa vile Tanu ndie baba wa CCM, na Tanu ndicho kilichotupatia ukombozi, then like father like son, CCM ni chama cha ukombozi wa Watanzania.Sijui wewe mwenzangu unaifananisha na nini CCM katika mawazo yako. Kwa uzuri au kwa ubaya!
sisiem mm nafananisha na govi umefika muda wa kuliondoa kwa sasa lina madhara mengi!
Kwanza, CCM haikutanguliwa na TANU pekee bali ilitanguliwa na TANU na ASP, vyama viwili vilivyokuwa na sera na malengo tofauti kabisa.Kwa vile Tanu ndie baba wa CCM, na Tanu ndicho kilichotupatia ukombozi, then like father like son, CCM ni chama cha ukombozi wa Watanzania.
Wengine wetu kama sisi tunakifananisha na mkombozi, muokozi!.
NB. Huku kuendelea kueneza chuki dhidi ya CCM kwa njia ya kuivoke ridicules, its not gonna add up the votes come 2015!, CCM itarudishwa kwa sympathetic votes kuwa ilitukanwa sana!.
Pamoja na CCM kuwa ndie chama mwokozi wetu, bado hajaweza kutufikisha kwenye ile nchi ya ahadi!. Kufuatia hali hii, watu sasa wanaijengea chuki CCM na kuifanya ionekane kama ni li zimwi!. Kwa kuwa hakuna mwingine as of now aliyeonyesha uwezo wa kutufikisha, then 2015, kuna hatari ya kuendelea kulichagua hili hili li zimwi CCM maana ndilo likujualo!
Pasco.
Mkuu Lukolo, pole for disappointment, kama ulivyonifahamu, ni tofauti na sasa, then ulidhani unanifahamu, nikimaanisha hunifahamu!.You disappointed me Pasco! Ninavyokufahamu na ulivyoandika hapa ni tofauti kabisa.
Kilichonidisappoint mimi si huo mtazamo wako wa CCM kuwa Zimwi lisilotaka kuachia ngazi, bali ni mtizamo wako wa kwamba CCM ni chama cha ukombozi ilihali kwa ushahidi wa wazi usio na shaka CCM inaonyesha dhahiri dhalili kwamba ni chama cha kinyonyaji. Kukiita chama cha ukombozi ni kama kukipaka mafuta kwa mgongo wa chupa. Na kwa mtizamo huo sikuoni kama msema ukweli bali nakuona kuwa ni mnafiki.Mkuu Lukolo, pole for disappointment, kama ulivyonifahamu, ni tofauti na sasa, then ulidhani unanifahamu, nikimaanisha hunifahamu!.
Nakiri moja ya madhaifu yangu ni kuwa mkweli too much!. Nimeifananisha CCM na zimwi, ambayo baada ya miaka 50 bado haijaweza kutufikisha nchi ya` ahadi zaidi ya kuendelea kututafuna!.
Ukweli mchungu ni kuwa, kuelekea 2015, as of now, bado hakuna mbadala wa CCM!, japo Chadema angalau inaonyesha dalili, lakini bado!. Kwa vile uchaguzi mwingine ni 2015, ukweli mchungu ninausemea hapa, ambao ndio umeku disappoint ni hii fact kuwa japo CCM ni li zimwi, 2015 ni zimwi hili hili!.
Calling CCM names, gonna change nothing kwa matokeo ya 2015!. Tusiichukie CCM!, akitokea mbadala tuiondoe CCM kwa upendo kwa shangwe na mapambio na sio kuijengea chuki, ili tuiondoe kwa hasira, itaumia kwa kinyongo, na matokeo yake sio mazuri!.
Pasco.
Mkuu Lukolo, kusema maji yamejaa nusu glasi, au yamepungua nusu, wote wako sawa!. Japo tunatofautiana kuhusu CCM, ila kwa matokeo ya 2015 hatutofautiani sana.Kilichonidisappoint mimi si huo mtazamo wako wa CCM kuwa Zimwi lisilotaka kuachia ngazi, bali ni mtizamo wako wa kwamba CCM ni chama cha ukombozi ilihali kwa ushahidi wa wazi usio na shaka CCM inaonyesha dhahiri dhalili kwamba ni chama cha kinyonyaji. Kukiita chama cha ukombozi ni kama kukipaka mafuta kwa mgongo wa chupa. Na kwa mtizamo huo sikuoni kama msema ukweli bali nakuona kuwa ni mnafiki.
Lakini pia hoja ya ama kushinda au kushindwa kwa CCM mwaka 2015, haiifanyi CCM ionekane nzuri. KUshinda au kushindwa kwake kutatokana na level ya uelewa wa watanzania hasa wale wa vijijini ambao tayari CCM ilishawatia upofu kwa kuwanyima haki halali ya elimu na kuhabarishwa. Maskini wale watu wale wa vijijini ambao bado wanaamini kwamba CCM ni chama cha Nyerere, haitakuwa rahisi kuikataa CCM kwa kuwa kwao Nyerere ni mkombozi. Lakini kama wangeujua ukweli kwamba CCM hivi sasa ipo mikononi mwa fisadi Kikwete, katu wasingekubali kuipa CCM kura yao. Kwa hiyo hapa hoja isiwe CCM ina likelihood kubwa kiasi gani ya kushinda uchaguzi wa mwaka 2015 bali iwe ni ina sifa gani?
Mwanakijiji keshasema kwamba CCM ni kama mbwa mwitu aliyejifanya bibi. Na ndivyo ambavyo CCM imekuwa ikifanya ikifika huko vijijini ambako huwa inajifanya bibi mwenye nia ya kuwaokoa, lakini ikishakubalika inawatafuna.
Hizi zote ni sifa za wanafamilia wa nyumbani kwenu kuanzia yule wa juu mpaka wale wa mwisho.
Nyumbani nimemuacha dada yako na wajomba zako.mkuu kati ya wewe na yule uliyemwacha nyumbani nani mzoga mkuu tukumbushe mkuu nasikia mmojawapo ndiye mzoga.