Mr Dudumizi
JF-Expert Member
- Sep 9, 2020
- 6,880
- 12,320
Habari zenu wana JF wenzangu,
Kuna mshituko mkubwa umetukumba watanganyika, hasa kuhusu hili swala la serikali ya Zanzibar kudai kuwa ina eneo lake la ardhi huko wilayani Bagamoyo mkoani Pwani.
Kama ilivyo kawaida ya baadhi yetu, huwa hatukurupuki kulalamika bila kufuatilia kwa makini kina cha kile kilichoongelewa na serikali au mtu husika.
Ukweli ni kwamba hili swala limetumiwa kisiasa makusudi na namba 1 wa huko, ili aweze ku win kiurahisi katika mbio za kumchagua mgombea uraisi wa nchi hiyo kupitia chama anachotokea, na vile vile kupita katika uchaguzi mkuu ambao utafanyika miaka miwili tu ijayo.
Ikumbukwe kwamba namba 1 huyo babu zake ni wandengereko wa Mkuranga mkoani Pwani, ambapo baba yake mwenyewe alieleza kwamba alipelekwa katika kisiwa hicho na wazazi wake ili akajifunze elimu akhera na baadae kurudi mkuranga kuendelea na mambo mengine.
Ila kwa bahati mbaya au nzuri baba huyo alipofika huko, akaongeza na elimu dunia na mwisho wake kulowea huko hadi kuwa namba 1 wa Zanzibar na Tanzania kwa ujumla.
Sasa namba 1 wa sasa historia anaijua na kamwe hawezi kufanya mzaha wa kumega palipo asili yake, huku akijua kwamba huenda na yeye ikatokea siku 1 akawa namba 1 tena wa JMT kama ilivyotokea kwa baba yake.
Kuna msemo wa waingereza unasema "Home sweet Home" na ndio maana namba 1 huyo miaka yake yote ya siasani hakuwa kugombea huko alipo sasa, bali alikuwa anagombea kule ilipo asili yake (mkuranga)
Sasa kwa vile amezungukwa na wazalendo uchwara wa Zanzibar ambao wengi wao wanaonesha chuki ya dhahiri kwake kama mzanzibar-mtanganyika na Tanganyika yetu kwa ujumla. Basi ndo akaja na style ya kuwafubaza kwa kile wapendacho kukisikia ili iwe rahisi kuchagulika kwa kuamini kwamba namba 1 huyo yuko pamoja na wao katika kupigania masilahi ya kisiwa chao.
Mnaofikiri kuwa Bagamoyo itamegwa chini ya namba 1 huyu wa sasa basi mtasubiri sana na ukizingatia hata huyu wa Muungano nae asili yake ni huko udigoni Tanga. Maana angekuwa original wa kule kisiwani, kamwe asingepewa nchi kama ilivyokuwa kwa kina dr SAS alienyang'anywa tonge mdomoni na mzee rukhsa kwa sababu ya kile nilichoeleza hapo juu.
Karibuni kwa kuchangia kistaarab.
Tanganyika nitakupenda mpaka kufa.
Kuna mshituko mkubwa umetukumba watanganyika, hasa kuhusu hili swala la serikali ya Zanzibar kudai kuwa ina eneo lake la ardhi huko wilayani Bagamoyo mkoani Pwani.
Kama ilivyo kawaida ya baadhi yetu, huwa hatukurupuki kulalamika bila kufuatilia kwa makini kina cha kile kilichoongelewa na serikali au mtu husika.
Ukweli ni kwamba hili swala limetumiwa kisiasa makusudi na namba 1 wa huko, ili aweze ku win kiurahisi katika mbio za kumchagua mgombea uraisi wa nchi hiyo kupitia chama anachotokea, na vile vile kupita katika uchaguzi mkuu ambao utafanyika miaka miwili tu ijayo.
Ikumbukwe kwamba namba 1 huyo babu zake ni wandengereko wa Mkuranga mkoani Pwani, ambapo baba yake mwenyewe alieleza kwamba alipelekwa katika kisiwa hicho na wazazi wake ili akajifunze elimu akhera na baadae kurudi mkuranga kuendelea na mambo mengine.
Ila kwa bahati mbaya au nzuri baba huyo alipofika huko, akaongeza na elimu dunia na mwisho wake kulowea huko hadi kuwa namba 1 wa Zanzibar na Tanzania kwa ujumla.
Sasa namba 1 wa sasa historia anaijua na kamwe hawezi kufanya mzaha wa kumega palipo asili yake, huku akijua kwamba huenda na yeye ikatokea siku 1 akawa namba 1 tena wa JMT kama ilivyotokea kwa baba yake.
Kuna msemo wa waingereza unasema "Home sweet Home" na ndio maana namba 1 huyo miaka yake yote ya siasani hakuwa kugombea huko alipo sasa, bali alikuwa anagombea kule ilipo asili yake (mkuranga)
Sasa kwa vile amezungukwa na wazalendo uchwara wa Zanzibar ambao wengi wao wanaonesha chuki ya dhahiri kwake kama mzanzibar-mtanganyika na Tanganyika yetu kwa ujumla. Basi ndo akaja na style ya kuwafubaza kwa kile wapendacho kukisikia ili iwe rahisi kuchagulika kwa kuamini kwamba namba 1 huyo yuko pamoja na wao katika kupigania masilahi ya kisiwa chao.
Mnaofikiri kuwa Bagamoyo itamegwa chini ya namba 1 huyu wa sasa basi mtasubiri sana na ukizingatia hata huyu wa Muungano nae asili yake ni huko udigoni Tanga. Maana angekuwa original wa kule kisiwani, kamwe asingepewa nchi kama ilivyokuwa kwa kina dr SAS alienyang'anywa tonge mdomoni na mzee rukhsa kwa sababu ya kile nilichoeleza hapo juu.
Karibuni kwa kuchangia kistaarab.
Tanganyika nitakupenda mpaka kufa.