Suala la mzee Mwinyi kuzikiwa Zanzibar wala lisifanywe la kisiasa, pitieni hapa msome muelewe sababu

6 Pack

JF-Expert Member
Apr 17, 2022
1,826
4,074
Watanzania tupeane pole kwa msiba huu mzito katika taifa letu.

Kuna watu wanashangazwa na hili swala la kuamua kuhamisishia msiba wa mzee Mwinyi Zanzibar, wakidai kuwa mzee huyo alikuwa asha usia kuwa akifariki akazikiwe kwao Mkuranga walipozikiwa na kulazwa wazazi wake na babu zake.

Wengi wanalaumu bila kujua ni nini kilichojadiliwa kati ya mzee Mwinyi na familia yake kabla ya umauti kumkuta. Je, kama walijadiliana nae na mzee kuridhia kuzikiwa Zanzibar alipokulia, kuoa, na kuzaa watoto wake huko?

Ni kweli mzee Mwinyi ana asili ya kwetu bara, lakini ukiangalia muda alioondoka bara kwenda Zanzibar mpaka sasa ni almost miaka 90 ambayo ni sawa na karne nzima. Sasa mtu ambae aliondoka bara miaka 90 iliyopita inamaana kwa sasa wale watu waliokuwa wanamfahamu na kumjua kupitia wazazi wake kama vile mashangazi, wajomba, baba wadogo, mama wadogo nk wameshafariki muda mrefu sana. Hakuna anaemfahamu kiundani zaidi ya wale walioko Zanzibar.

Ni kweli wakati alipokuwa raisi na hata baada ya uraisi huenda alikuwa anakwenda kwao mara moja moja, lakini sasa wale watu wake wa muhimu ambao wangemfanya kuvutiwa na kwao wameshafariki hivyo alikuwa ni kama vile mtu mpya au muhamiaji asiefahamika kijijini kwao. Familia nzima mke na watoto ni wenyeji wa Zanzibar, sasa kuna ubaya gani watoto kuongea na mzee wao ili kumsihi azikiwe kule alipoanzia kujenga familia yake ambapo ana watu wengi wanaomfahamu zaidi ya huku alipotokea.

Binafsi nafikiri hili swala la kuzikiwa Zanzibar lina baraka zake baada ya watoto na mke / wake zake kukaa na kumuelewesha hadi mzee kubadili gia angani na kuridhia kuzikwa Zanzibar ila imekuwa siri tu ya kifamilia. Wao sio wajinga wa kukurupuka kupishana na usia wa baba yao, na wakati ni watu wazima wenye elimu zao lakini pia wanafahamu vizuri madhara ya kupishana na usia wa marehemu, hivyo naona wanabaraka zake wala hawakukurupuka yaje yawakute yaliowakuta wengine waliopishana na usia wa ndugu zao.
 
Hayo mambo yaliyojadiliwa kwenye familia ya Mwinyi kama kweli yalijadiliwa, ni siri yao.

Lakini kimsingi, siku zote mtoto lazima azikwe pale walipozikwa wazazi wake, huu ndio utamaduni wetu, unalazwa pale walipolazwa ndugu zako wengine.

Sasa leo Mwinyi badala ya kuzikwa Mkuranga anaenda kuzikwa Zanzibar, kisa alisoma huko, hebu tuambie, kwa uamuzi wenu huo, hivi hamuoni kama mmemtenga na ndugu zake wengine waliozikwa huku Bara?

Ndugu yake yupi tena atakaekwenda kuzikwa nae Zanzibar, kama ni Rais Dr. Mwinyi, hamuoni pia hawa wawili mtakuwa mmewatenga na ndugu zao wengine waliozikwa huku Bara?

Hapo ndipo unapopata picha kwamba, huu uamuzi wa kumzika Mzee Mwinyi Zanzibar, ni purely political motivated.

Ndio maana kwasababu hizo za kisiasa, watajikuta ni wao wawili pekee, baba mtu na mwanae [kama nae atataka kuzikwa huko, sababu wanasema anaogopa baba yake kuzikwa bara sababu naye ataonekana sio mzanzibar na maadui zake kisiasa, sijui akiondoka madarakani hiyo hofu itabaki au ataondoka nayo] kama itabaki, ndio wawili pekee watakaozikwa Zanzibar, huku ndugu zao wengine wote wakizikwa Bara.

I never thought kama siasa ina nguvu kiasi hiki, au ni uoga tu wa mwanasiasa mwenyewe anayeamua kuchukua maamuzi yatakayokwenda kinyume na mila na desturi zetu, kwa maslahi yake ya kisiasa, hiki kilichofanyika kwa Mzee Mwinyi, binafsi sijakipenda, tunatakiwa siku yetu ya mwisho sote tulazwe pale walipolazwa ndugu zetu kama nafasi ipo.

Na ndio maana pia, wengine wetu ambao hawana uwezo wa kusafirisha ndugu zao, hupeleka udongo wa pale alipozikwa ndugu yao nyumbani kwao uende kuzikwa huko, yote hii ni ili kuonesha umuhimu wa kumzika marehemu pale alipozaliwa, nashangaa na kusikitika kwanini wamemuondolea Mzee Mwinyi haki yake hii, ikiwa uwezo wa kumsafirisha na kumzika nyumbani kwao Mkuranga upo, sio fair.

Sent from my SM-G900H using JamiiForums mobile app
 
Watanzania tupeane pole kwa msiba huu mzito katika taifa letu.

Kuna watu wanashangazwa na hili swala la kuamua kuhamisishia msiba wa mzee Mwinyi Zanzibar, wakidai kuwa mzee huyo alikuwa asha usia kuwa akifariki akazikiwe kwao Mkuranga walipozikiwa na kulazwa wazazi wake na babu zake...
Mwinyi ameishi zwnx8bar miaka 90? Hauko serious, nusu ya maisha yake smeishi mikocheni hata alipistaafu aliishi mikocheni
 
Watanzania tupeane pole kwa msiba huu mzito katika taifa letu.

Kuna watu wanashangazwa na hili swala la kuamua kuhamisishia msiba wa mzee Mwinyi Zanzibar, wakidai kuwa mzee huyo alikuwa asha usia kuwa akifariki akazikiwe kwao Mkuranga walipozikiwa na kulazwa wazazi wake na babu zake...

Mwinyi ameishi maisha yake zaidi Bara kuliko huko visiwani. Ndiyo maana hata baada ya kufa ameendelea kuishi bara na si visiwani.

Na nyumba yake ya kustaafu akajengewa na Magufuli Dar kwa nini hawakumjengea kwao Zanzibar.

Hata Mwanaye pia maisha yake ameishi zaidi bara, wanamzika kule kimkakati!!
 
1709302700237.png
 
Back
Top Bottom