Kwahiyo Mkapa alivyokopa Millioni 500 NBC alikuwa anatusanifu siyo!!
Kweli CCM hakuna msafi!
Heshima mbele wana JF wote,
Ni muda mrefu sana nimekua sipatikani hapa JF. Baadhi yetu wamekuwa mkini PM na kuniuliza Vipi TUMBIRI? Umeng'olewa meno na kucha au?
Kimsingi nimebanwa na shule Wakuu. Lakini leo wakati napita pita huku na huku kutafuta literature za kusapoti Dissertation yangu nimegundua kitu kimoja.
Waziri Mkuu Mstaafu Mh. Frederick T. Sumaye anamiliki idadi ya hisa 6,206,980[SUP]1 [/SUP]za Benki ya CRDB ambazo kwa mujibu wa Ripoti ya Mwaka ya Benki hiyo, bei ya hisa moja kwa Soko la hisa hadi kufikia tarehe 31 Disemba 2012 ilikuwa ni Sh.150 kwa hisa. Kwa maana hiyo Mh. Sumaye anamiliki hisa zenye thamani ya Shilingi 931,047,000/=.
Hata hivyo kwa mujibu wa tovuti ya soko la hisa leo tarehe 07/06/2013 saa 20:50 hisa moja ya CRDB ina thamani ya Sh.205. Kwa maana hiyo Mh. Sumaye kwa sasa anamiliki hisa zenye thamani ya Sh.1,272,430,900/=.
Haijaelezwa na ripoti ya Benki ni lini Mh. Sumaye alinunua hisa hizo na kwa bei gani.
Uwekezaji wa kiasi hiki cha fedha ni kikubwa hasa ikizingatiwa Mmiliki ni aliyewai kuwa Mtendaji Mkuu wa Serikali ndani ya Serikali iliyopita.
Hii ni taarifa tu.
TUMBIRI (PhD Candidate, CPA(T), MBA(UDSM), Bcom(Accounting), PCM(Mzumbe High School).
tumbiri@jamiiforums.com,
Upanga, Dar es Salaam, Tanzania.
[SUP]1 [/SUP]CRDB Bank Annual Report 2012 (Page 66).
Nakala: Kimbunga, Mingoi, Ndallo, Matola, Crashwise, Mzee Mwanakijiji, Malaria Sugu, chama, mandingo6262, Rejao, Mungi, Putin, Salary Slip, etc
Muwe mnaona hata Aibu ....mmezidi kufuata Sumaye...wakati ukweli hakuna mtu muwazi Kama yeye ....kuna ajabu gani mtu ambayo amekuwa Waziri mkuu kwa miaka kumi ...kumiliki Hisa ???za Bilioni ???? Inawezekana kanunia kwenye IPO kwa milioni 400 ..hakuna ajabu hapo ...mbona wengine wana Bilioni 50 za Libya?
Karibu tena mkuu.Hicho ni kiasi kidogo sana cha hela. mshahara plus marup rup ya waziri mkuu bila masurufu kwa miaka miwili ni zaidi ya hicho kiasi. Mkuu umekurupukaa!
Na hapo ni CRDB tu bado kwingine,pia hizo ni hisa tu baada biashara nyingi,na wanaosma marupurupu wasiwe wavivu wa kufikiri marupurupu hayo ni kiasi gani?Sophia Simba alisema hakuna msafi CCM,sasa kama huyo ni Sumaye ,je Mzee aliyehamia Kifungilo ana kiasi gani?je akina Mramba,yona,Mamvi wana kiasi gani?ndio maana Chenge alisema ana vijisenti tu.Tutaendelea kurumbana na kutoa mapovu kwenye JF wakati ''wakali wenyewe'' wanakula bata.Kama hivyo ndivyo hakika haqa viongozi wastaafu wanatufanya vibaya. Hata waliojiuzulu bado is wanalipwa jamani?
Sent from my BlackBerry 9860 using JamiiForums
TUMBIRI sina tatizo na taarifa zenyewe, na unalosema ni kweli ila hapa palinitatiza kidogo "...Uwekezaji wa kiasi hiki cha fedha ni kikubwa hasa ikizingatiwa Mmiliki ni aliyewai kuwa Mtendaji Mkuu wa Serikali ndani ya Serikali iliyopita..." Maana kama hutupi more evidence juthibitisha hili mfano mshahara wake kwa mwezi, marupurupu ya safari na ya uongozi n.k. na ukizingatia kwa miaka yote tangu akiwa Waziri mheshimiwa huyu alikuwa na interest sana na ardhi na kilimo na uwekezaji wowote halali/usio halali alioufanya na ni wa thamani gani basi hapo tunaweza kujadili kiasi hii kina maana gani? Bahati mbaya au nzuri viongozi hawa wanachofanya ni kutumia mwanya wa taarifa walizonazo kuhusu opportunity za nchi hii, upatikanaji wa mikopo, ardhi, mitaji ambayo wengi wetu huwa taarifa hizi tunazipata kwa shida kidogo haziko tu avaiable mpaka uwe na skills na uwe umekuwa exposed jinsi ya kuzipata. Ukiachilia mbali zinazotolewa na mabenki ya kibiashara ambazo nyingi ni viini macho kwa mtu wa kawaida. So ninaafikiana na wewe ni idadi ya pesa ya kushtua kidogo, ila tunahitaji evidence zaidi kabla ya kumrukia shingoniMkuu Profesa,
Nakuheshimu sana Profesa wangu. Kwanza kwa jina lako na maono yako humu jamvini lakini kwa hili naona umepotoka kidogo Mkuu wangu. Annual Report za Public Listed Company ni Public Reports. Sheria ya Makambuni pamoja na Kanuni za uendeshaji wa Stock Exchange zinaagiza Annual Reports of every listed company must be published contained Chairman Statement, Directors Report, Auditor Report, Financial Statement, etc.
Sasa mimi nimedisclose kitu ambacho tayari kipo mitaani na kinapaswa kijulikane kisheria. After all Mh. Sumaye namuheshimu sana sina personal ugomvi nae kama unavyotaka kuaminisha jukwaa kwamba nina introduce personal attack. Hata wewe ukitaka hiyo ripoti just google ipo na free of charge.
Regard,
TUMBIRI.
TUMBIRI sina tatizo na taarifa zenyewe, na unalosema ni kweli ila hapa palinitatiza kidogo "...Uwekezaji wa kiasi hiki cha fedha ni kikubwa hasa ikizingatiwa Mmiliki ni aliyewai kuwa Mtendaji Mkuu wa Serikali ndani ya Serikali iliyopita..." Maana kama hutupi more evidence kuthibitisha hili mfano mshahara wake kwa mwezi, marupurupu ya safari na ya uongozi n.k. na ukizingatia kwa miaka yote tangu akiwa Waziri mheshimiwa huyu alikuwa na interest sana na ardhi na kilimo na uwekezaji wowote halali/usio halali alioufanya na ni wa thamani gani basi hapo tunaweza kujadili kiasi hii kina maana gani? Bahati mbaya au nzuri viongozi hawa wanachofanya ni kutumia mwanya wa taarifa walizonazo kuhusu opportunity za nchi hii, upatikanaji wa mikopo, ardhi, mitaji ambayo wengi wetu huwa taarifa hizi tunazipata kwa shida kidogo haziko tu avaiable mpaka uwe na skills na uwe umekuwa exposed jinsi ya kuzipata (Kutokana na kutokuwajibika na kukosa uzalendo kwa tuliowaeka madarakani bila shaka). Ukiachilia mbali zinazotolewa na mabenki ya kibiashara ambazo nyingi ni viini macho kwa mtu wa kawaida. So ninaafikiana na wewe ni idadi ya pesa ya kushtua kidogo, ila tunahitaji evidence zaidi kabla ya kumrukia shingoniMkuu Profesa,
Nakuheshimu sana Profesa wangu. Kwanza kwa jina lako na maono yako humu jamvini lakini kwa hili naona umepotoka kidogo Mkuu wangu. Annual Report za Public Listed Company ni Public Reports. Sheria ya Makambuni pamoja na Kanuni za uendeshaji wa Stock Exchange zinaagiza Annual Reports of every listed company must be published contained Chairman Statement, Directors Report, Auditor Report, Financial Statement, etc.
Sasa mimi nimedisclose kitu ambacho tayari kipo mitaani na kinapaswa kijulikane kisheria. After all Mh. Sumaye namuheshimu sana sina personal ugomvi nae kama unavyotaka kuaminisha jukwaa kwamba nina introduce personal attack. Hata wewe ukitaka hiyo ripoti just google ipo na free of charge.
Regard,
TUMBIRI.
Hicho ni kiasi kidogo sana
cha hela. mshahara plus marup rup ya waziri mkuu bila masurufu kwa miaka
miwili ni zaidi ya hicho kiasi. Mkuu umekurupukaa!
Mkuu kwa ninavyofahamu mimi data za research zinapaswa kutumika kwa ajili ya research, when you disclose other people information unakuwa unakosea. That is not academics mkuu. Hayo ungeweka kwenye research paper yako baada ya kufanya utafiti kwa undani. Japokuwa na-appreciate pia kwamba inaweza ukawa umefanya kwa nia njema jaribu pia kuliangalia hilo. By the way kwa mtu mwenye akili akipata pesa alizokua anapata sumaye kwenye career yake yote ku-raise pesa hizo sio jambo la ajabu.