Sumaye awekeza Shilingi Milioni 931 Benki ya CRDB

Sumaye awekeza Shilingi Milioni 931 Benki ya CRDB

Heshima mbele wana JF wote,
Ni muda mrefu sana nimekua sipatikani hapa JF. Baadhi yetu wamekuwa mkini PM na kuniuliza Vipi TUMBIRI? Umeng'olewa meno na kucha au?

Kimsingi nimebanwa na shule Wakuu. Lakini leo wakati napita pita huku na huku kutafuta literature za kusapoti Dissertation yangu nimegundua kitu kimoja.

Waziri Mkuu Mstaafu Mh. Frederick T. Sumaye anamiliki idadi ya hisa 6,206,980[SUP]1 [/SUP]za Benki ya CRDB ambazo kwa mujibu wa Ripoti ya Mwaka ya Benki hiyo, bei ya hisa moja kwa Soko la hisa hadi kufikia tarehe 31 Disemba 2012 ilikuwa ni Sh.150 kwa hisa. Kwa maana hiyo Mh. Sumaye anamiliki hisa zenye thamani ya Shilingi 931,047,000/=.

Hata hivyo kwa mujibu wa tovuti ya soko la hisa leo tarehe 07/06/2013 saa 20:50 hisa moja ya CRDB ina thamani ya Sh.205. Kwa maana hiyo Mh. Sumaye kwa sasa anamiliki hisa zenye thamani ya Sh.1,272,430,900/=.

Haijaelezwa na ripoti ya Benki ni lini Mh. Sumaye alinunua hisa hizo na kwa bei gani.

Uwekezaji wa kiasi hiki cha fedha ni kikubwa hasa ikizingatiwa Mmiliki ni aliyewai kuwa Mtendaji Mkuu wa Serikali ndani ya Serikali iliyopita.

Hii ni taarifa tu.

TUMBIRI (PhD Candidate, CPA(T), MBA(UDSM), Bcom(Accounting), PCM(Mzumbe High School).
tumbiri@jamiiforums.com,
Upanga, Dar es Salaam, Tanzania.

[SUP]1 [/SUP]CRDB Bank Annual Report 2012 (Page 66).


Nakala: Kimbunga, Mingoi, Ndallo, Matola, Crashwise, Mzee Mwanakijiji, Malaria Sugu, chama, mandingo6262, Rejao, Mungi, Putin, Salary Slip, etc


Sasa tufanyeje TUMBIRI?
 
acha utani wewe milin 900 sio pesa ya kukustua kwa mtu aliyewahi kuwa waziri mkuu,unajua kiinua mgongo cha pm ni kiasi gani,tatizo uzembe kufanya kazi unakuaminisha kuwa hizo ni pess mingi,hata machinga kariakoo kibao wanazo


mmmmhh i doubt ur words,with the money i can do bussiness,send my boy to massacheutes institute ot technology(m.i.t),establish an empire and live a fancy life,,,but if you are the likes of mafuruki or bakhressa am sorry for this comment but if you aint am sure you also need that cash badly,,
 
Bora hizi pesa zimewekezwa hapa na sio ughaibuni. Natumaini mapesa yake mengine yote yapo katika nchi hii hii.
 
Hivi watanzania ni nani aliye tuloga? Watu wanaona 1.2b ni pesa ndogo sana kwa kiongozi kuwanazo ,na kabla hajawa kiongozi hakuwahi kuwa na hata robo ya kiasi hicho. Ama kweli siku hizi wa Tz tumekuwa misukule.
 
Yeye anapinga mapendekezo ya rasimu ya katiba kuwepo kwa serikali tatu na hoja yake ni gharama, gharama zinakuwa kubwa kwa serikali kwa wenye madaraka kujichotea kama hivi kwa maslahi yao, amekuwa akimnyoshea kidole Loawasa kwa utajiri, ama kweli nyani .........
usilolijua damia litakusumbua

cha kwanza ni kujua alupata shares kwa shilingi ngapi?? kumbuka shareas value change

pili, hata kama sumaye angekua na bilioni 10, bado asingefikia hata silimia 15 ya EL
 
Hicho ni kiasi kidogo sana cha hela. mshahara plus marup rup ya waziri mkuu bila masurufu kwa miaka miwili ni zaidi ya hicho kiasi. Mkuu umekurupukaa!

yani wewe ndo ----.huyo m2 kumiliki kiasi hcho cha pesa ni kikubwa sana,ukizingatia umaskin wa watu wengne,huyo mmoja je wale tusiowajua?
 
Hicho ni kiasi kidogo sana cha hela. mshahara plus marup rup ya waziri mkuu bila masurufu kwa miaka miwili ni zaidi ya hicho kiasi. Mkuu umekurupukaa!

Rejao ungedadavua(breakdown) mafao ya waziri mkuu yakoje maana mkianza kulaumiana kukurupuka sisi wengine ndo mnatuchanganya
 
Umekurupuka sana mbona kawaida sana wala siyo issue.

siku hizi kijana haufikiri mbali kabisa umepoteza uwezo sana.... mtu kama si mfanyabiashara yet anamiliki hisa 1 billion ndani ya bank moja and that is a little we know. rais mwenyewe wa tz mshahara wake ni 400 kwa mwaka na miaka kumi ni 4 billion total.je kwa mali anazomiliki sumaye angefikishaje kwa hela hata kama angekuwa rais.
 
Sasa tufanyeje TUMBIRI?
Tufanyeje? Tuelezwe tu alizipata vipi hizo pesa. Kama alifanya biashara, tujue alilipa kodi kiasi gani. Akishindwa kutupatia majibu tumsulubu sawa na vibaka wengine tunavyowasulubu.
 
Waziri mkuu anafanya shoo?

Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Mkuu kwanza hongera kwa elimu ....

Jibu ya swali lako mbona umeshatoa hint...kachunguze hizp hisa alizipata lini, alizipataje na kama alinunua mwenyewe je alinunua kwa shilingi ngapi

Kwenye hisa za makampuni kuna watu wametajirika sana kwa kuweza kununua hisa kwenye kampuni ambazo miaka michache zinakuwa na thamani kubwa sana kama apple,etc...


Ila hiyo ni thamani tu maana mambo yakiharibika wanaweza kujikuta wanalipwa shilingi 10 kwa hisa...si jambo geni
 
Nakumbuka kipindi hicho CRDB wamefanya IPO(Initial Public Offer) watu wengi waliomba kununua hisa zao ila cha kushangaza hata kama ulilipia hisa walikuwa wanakurudishia pesa yako(share refund) yaani walikuwa wameweka kiwango cha kununua hisa zao na hakika hii ilikuwa kwa watu wa kawaida ila kwa watu kama akina Sumaye kwao ilikuwa hawana ukomo wa idadi ya hisa ni pesa yao tu ndio iliongea ulikuwa ukiuliza mbona hivyo wanakwambia maombi yamekuwa mengi(over subscription) kwahiyo wanajaribu kufanya utaratibu kila mtu apate idadi kadhaa lakini ukweli wa mambo ni kuwa wakubwa walikuwa washatuma maombi yao tayari hata kama walichelewa kuomba hivyo kipaumbele lazima walikuwa wapewe wao kutokana na nyadhifa zao.
 
Sumaye alikuwa mkufunzi wa kilimo/mifugo kwenye vyuo vya mifugo kabla ya kuwa waziri,hivyo alianza kuwekeza kwenye mifugo miaka mingi.Ukijumlisha na marupurupu ya uwaziri mkuu,Kwa sasa anaweza kabisa kumiliki fedha nyingi kutokana na uwekezaji huo.
Uzuri wake aliwekeza humu nchini na watu wengi wamepata ajira kutokana na uwekezaji wake,Tofauti na wale wenye vijisenti benki za nje.
Mwandishi wa thread hii umeanza kutoa judgment kabla hujakamilisha research yako inaonyesha jinsi usivyo makini,kwani Hypothesis zako zimeendana na findings?Na unawezaje kurelease searched information kwenye forums bila kibali?Angalia ethics za research,kabla hujaharibu na kufanya wengine kunyimwa ku collect data kwa makosa uliyoyadhihirisha hapa.
 
Nje anazo pesa nyingi sana!na hizo ni ktk hisa za kampuni moja tuu,bado makampuni mengine
 
Mkuu TUMBIRI nashukuru kwa taarifa hii, ila kitu kimoja tu, Avatar yako sijaikubali hata kidogo, hivi kweli wewe ni Phd Candidate? Samahani lakini kama nitakuudhi mkuu!
 
tusiubari ufisadi ndugu zangu, nyie mnaotaka ushaidi mmeipata wapi hiyo mamlaka? nyie ni mahakama?. kutoa taarifa ya malalamiko ni universal right, ushaidi ni hatua ingine tofauti.
 
Hicho ni kiasi kidogo sana cha hela. mshahara plus marup rup ya waziri mkuu bila masurufu kwa miaka miwili ni zaidi ya hicho kiasi. Mkuu umekurupukaa!

Hoja ya Tumbiri ni kutaka kujua aliwekeza lini hisa hizo na alizinunua kiasi gani,hiyo ndo hoja,mkimwambia mtu amekurupuka bila kuangalia mantiki ya swali wewe ndiye utaonekana umekurupuka.
 
Umekurupuka sana mbona kawaida sana wala siyo issue.

Kukurupuka lazima ionekane hivyo ukizingatia kuna vijana wadogo ambao wamekuwa multimillionaire kwa kipindi kifupi cha miaka nane lakini haguswi
 
Back
Top Bottom