Sumaye awekeza Shilingi Milioni 931 Benki ya CRDB

Sumaye awekeza Shilingi Milioni 931 Benki ya CRDB

Nawashangaa mnaomtuhumu Tumbili kwa kutoa taarifa za umiliki wa hisa wa waziri mkuu mstaafu,

Ni nani kawaambia kuwa suala la kumiliki hisa esp amount kubwa kiasi hicho kinaweza kuwa siri? Lazima mtambue kuwa kuna majority shareholders na wale wanaomiliki hisa za kubangaiza.

ukiishakuwa majority shareholder basi unakuwa na voting power na pia lazima utakuwemo kwenye vikao vya bodi. Ukiingia kwenye tovuti utawakuta hawa wanahisa na hata kwenye kila ripoti ya mwaka wanakuwepo disclosed.

Nyi mnaomtuhumu Tumbiri fanyeni utafiti kwanza ndo mzungumze.
Nakala: Kimbunga, Mingoi, Ndallo, Matola, Crashwise, Mzee Mwanakijiji, Malaria Sugu, chama, mandingo6262, Rejao, Mungi, Putin, Salary Slip, etc
Last edited by TUMBIRI; 7th June 2013 at 21:08. Reason: Extension
 

Attachments

Don't criticize much source of information is not "PRIVATE"

[SUP]1 [/SUP]CRDB Bank Annual Report 2012 (Page 66).
 
1..naomba kama kuna mtu ana data kidogo ya mchakato mzima wa crdb katika kuingia katika soko la hisa.........aziweke hapa ili tujue tukimhukumu mtu kweli tunamhukumu kihalali.... Dse kama mpo humu tunaomba ule mchakato..... 2. Kama kuna mtu anaikumbuka ile formula iliyotumiwa na crdb kwa ajili ya wanahisa wao waliotoka nao toka wakati crdb inaanzishwa airushe hapa.....3... Mchakato mzima wa "ipo" ulivyokuwa na jinsi share zilivyokuwa zinauzwa kwa wanahiza wa mwanzo..na wale waliokuwa wapya......4...tunaomba tujue, kama sumaye mwenyewe yupo huku, au yoyote mwenye data zake "sahihi" atuambie alinunua lini hisa...... Kwa tsh ngapi kwa hiza.... Na zilikuwa ngapi......!!!! Au hata crdb wenyewe kama wanaruhusiwa kutoa data hizo kwa public wanaweza kutuambia.... Baada ya kupata majibu ya maswali haya sasa tunaweza kuingia katika discussion ya jambo hili na kujua tunamhukumu mtu kwa haki...... Asanteni wana jf
 
Hizo hisa so kosa jamani,na kusema anamiliki ngurudoto huo ni uwongo mtupi,ngurudoto inajulikana ni ya kina nani jamani wacheni majungu Sumaye kidogo tunaweza sema yeye ni msafi na sio fisadi kivile
 
this is not a news kwa mtu aliyewai kua prime minister kuwa na mil 900 is not an issue!!!
 
Kama hivyo ndivyo hakika haqa viongozi wastaafu wanatufanya vibaya. Hata waliojiuzulu bado is wanalipwa jamani?


Sent from my BlackBerry 9860 using JamiiForums

Kuna wakati walipitisha sheria ya kuhusu malipo ya viongozi wastaafu na nadhani kama kumbukumbu zangu ni sahihi, wanalipwa asilimia 80 ya mishahara yao ya mwezi.
 
Upumbavu huu, Diamond-mwanamuziki tu ana account ya billion, ex -PM asiwe na utajiri wowote??

ndio maana unaishia kusoooooma weee na ma PHD kibao wakato hayakuingizii hela unaishia stress tu

embu oneni,,,,,,,,,,,,,,,mikozi yote hii kwa Tanzania ya nini?? ebu oneni

TUMBIRI (PhD Candidate, CPA(T), MBA(UDSM), Bcom(Accounting), PCM(Mzumbe High School).
tumbiri@jamiiforums.com,
Upanga, Dar es Salaam, Tanzania.

Kweli mkuu kuna watu wanafikiri watu wote sawa!!!

Ex Pm kuwa na hela hizo kitu kidogo sana.
 
you can be sure its Tanzanian when someone skips details and jumps into conclusion based on a headline.No wonder our leaders keeps hoodwinking us on daily basis.

RTFU all who keeps blaming TUMBIRI for disclosing private information,shit aint private when its posted on public domain.I.E the internet,annual reports of private traded companies. back on topic,its a sad state looking at a public figure in one of the poorest country boasting over $600K in investment on a for profit company,something is not right.

Either we should STFU when public funds are embezzled or we should not expect any efficiency from a dude who clearly looks to be a career business person. and for those claiming $600K is not a lot of money,you are missing a huge point. Such amount of money should not be concentrated on one public figure for such a poor country.,its morally wrong in every level. Nyerere was a genius when he proposed leaders be separated from business especially for a country with non existent or strong institutions.

No wonder former president registered a company while at the state house. food for thought, if these people think their position does not merit 100% of their mind body and soul what makes you poor mwananchi think that your problems occupies even 1% of their mind?if anyone gives less than 100% WTF are we electing that person into office for a country that is like 300 years behind?we need guys who give 100% and more,nothing less
zumbukuku ulimwengu uko huku.
 
Heshima mbele wana JF wote,
Ni muda mrefu sana nimekua sipatikani hapa JF. Baadhi yetu wamekuwa mkini PM na kuniuliza Vipi TUMBIRI? Umeng'olewa meno na kucha au?

Kimsingi nimebanwa na shule Wakuu. Lakini leo wakati napita pita huku na huku kutafuta literature za kusapoti Dissertation yangu nimegundua kitu kimoja.

Waziri Mkuu Mstaafu Mh. Frederick T. Sumaye anamiliki idadi ya hisa 6,206,980[SUP]1 [/SUP]za Benki ya CRDB ambazo kwa mujibu wa Ripoti ya Mwaka ya Benki hiyo, bei ya hisa moja kwa Soko la hisa hadi kufikia tarehe 31 Disemba 2012 ilikuwa ni Sh.150 kwa hisa. Kwa maana hiyo Mh. Sumaye anamiliki hisa zenye thamani ya Shilingi 931,047,000/=.

Hata hivyo kwa mujibu wa tovuti ya soko la hisa leo tarehe 07/06/2013 saa 20:50 hisa moja ya CRDB ina thamani ya Sh.205. Kwa maana hiyo Mh. Sumaye kwa sasa anamiliki hisa zenye thamani ya Sh.1,272,430,900/=.

Haijaelezwa na ripoti ya Benki ni lini Mh. Sumaye alinunua hisa hizo na kwa bei gani.

Uwekezaji wa kiasi hiki cha fedha ni kikubwa hasa ikizingatiwa Mmiliki ni aliyewai kuwa Mtendaji Mkuu wa Serikali ndani ya Serikali iliyopita.

Hii ni taarifa tu.

TUMBIRI (PhD Candidate, CPA(T), MBA(UDSM), Bcom(Accounting), PCM(Mzumbe High School).
tumbiri@jamiiforums.com,
Upanga, Dar es Salaam, Tanzania.

[SUP]1 [/SUP]CRDB Bank Annual Report 2012 (Page 66).


Nakala: Kimbunga, Mingoi, Ndallo, Matola, Crashwise, Mzee Mwanakijiji, Malaria Sugu, chama, mandingo6262, Rejao, Mungi, Putin, Salary Slip, etc

Kaka nadhani ulikuwa una hoja nzuri lakini umechemsha jinsi ya kuiwasilisha. Benki ya CRDB kwa kipindi kirefu ikielekea kwenye listing ilikuwa ikitoa bonus shares for a share. Yaani ukiwa na hisa moja unapewa moja zaidi. Baadae ikaja double bonus hivyo Kama una tatu inakuwa Sita. Baadaye ikaja split ambayo ilizidisha mara 4!so Kama una 6 utakuwa na 24.Hivyo Kwa Mzee Sumaye kufikikisha hapo inaweza kabisa kuwa ni zao la uwekazaji wa kwanza uliozaa zao hili Leo. Kufikia thamani ya Tsh millioni 900 ni zao la utendaji mzuri wa kampuni aliyowekeza,this has nothing to do with Sumaye. Angeweza pia kuwa alipata hasara, huo ndio uwekezaji! Ningekuwa wewe nisingeanzia jamvini na vitu nisivyokuwa na uhakika navyo. Kila la kheri kwenye shahada yako ya uzamivu.Kumbuka Kuwekeza kwenye hisa za Benki.
 
Kumiliki fedha au mali yoyote sio kosa,muhimu ni kuwa muwazi amezipataje fedha au mali husika,kam ni kwa njia haramu ndo tatizo ila kama ni kwa njia halali na ya wazi hakuna tatizo,cha msingi hapa ni kuangalia njia alizotumia kupata fedha hizo.
 
Nawashangaa mnaomtuhumu Tumbili kwa kutoa taarifa za umiliki wa hisa wa waziri mkuu mstaafu,

Ni nani kawaambia kuwa suala la kumiliki hisa esp amount kubwa kiasi hicho kinaweza kuwa siri? Lazima mtambue kuwa kuna majority shareholders na wale wanaomiliki hisa za kubangaiza.

ukiishakuwa majority shareholder basi unakuwa na voting power na pia lazima utakuwemo kwenye vikao vya bodi. Ukiingia kwenye tovuti utawakuta hawa wanahisa na hata kwenye kila ripoti ya mwaka wanakuwepo disclosed.

Nyi mnaomtuhumu Tumbiri fanyeni utafiti kwanza ndo mzungumze.
Nakala: Kimbunga, Mingoi, Ndallo, Matola, Crashwise, Mzee Mwanakijiji, Malaria Sugu, chama, mandingo6262, Rejao, Mungi, Putin, Salary Slip, etc
Last edited by TUMBIRI; 7th June 2013 at 21:08. Reason: Extension

Mkuu, nimeisoma taarifa hii kwa kina ukurasa wa 66 wa CRDB Bank annual report ya mwaka 2012 uliyoambatanisha , ambapo pamoja na Mh. Sumaye kuna wenye hisa wengine wengi waliotajwa katika ripoti hiyo ambayo wengine wana-JF wanadhani CRDB Bank Annual report ni siri wakati ipo katika mtandao mfano google www.crdbbank.com/index.php?...annual-report...annual-reports...2012 . Asante Madingo6262 na TUMBIRI PhD Candidate kwa kutufungua macho tununue hisa ktk makampuni/mashirika yetu ya Tanzania badala ya kuficha Uswisi na visiwa vya Isle of Man n.k
Swali la msingi ni juu ya term ''Insider Trading'' je kuna watu hubonyezwa/wanapewa taarifa kwanza kabla ya wengine kuhusu uwezekano wa kupata ulaji kupitia kununua hisa husika ndani ya benki/taasisi kabla ya wengine Insider trading continues to be a high priority area for the SEC's enforcement program. The SEC brought 58 insider trading actions in FY 2012 against 131 individuals and entities. Over the last three years, the SEC has filed more insider trading actions (168 total) than in any three-year period in the agency's history. These insider trading actions were filed against nearly 400 individuals and entities with illicit profits or losses avoided totaling approximately $600 million. Many of these actions involved financial professionals, hedge fund managers, corporate insiders, and attorneys who unlawfully traded on material non-public information, undermining the level playing field that is fundamental to the integrity and fair functioning of the capital markets.
Examples of the SEC's recent insider trading actions include:.........SEC Enforcement Actions: Insider Trading Cases
 
TUMBIRI
Unaanza kutupa wasiwasi na Ph.d yako; kama ulikuwa huna taarifa kamili ungefanya utafiti wa kina sio kuandika vitu kama Professor Jay; biashara ya stock ipo wazi; tueleze hisa alinunua lini na kwa kiasi gani je kulikuwa na re investment wakati wa gawanyo la hisa; hapo ndipo utapata ukweli wenyewe; fanya utafiti wa kampuni ya Ford hisa zake zilianguka kwa kiasi kikubwa sana kiasi cha kutishia wana hisa; hivi sasa hisa za Ford zipo juu; kwa siwezi kukubaliana au kukataa hadi hapo utakapotuletea taarifa kamili; usiaandike kama vile wasomaji ni Matola na Molemo peke yao.
 
Last edited by a moderator:
Nami naunga mkono hoja ya hizo 900mil ni zao la muda mrefu la hisa zake kuzaa na kuzaa kila mwaka!
 
Kipi cha ajabu jamani?nadhani ni miwivu tuu inawasumbua
Watu wanakaa vibarazani kuongea mambo ya wengine badala ya kusaka noti!
Wana lala mlango wazi wakisubiri noti ipige hodi!!

Hao wanakufa na umasikini licha ya kwenda shule.
 
Hicho ni kiasi kidogo sana cha hela. mshahara plus marup rup ya waziri mkuu bila masurufu kwa miaka miwili ni zaidi ya hicho kiasi. Mkuu umekurupukaa!
Na matumizi kwa miaka miwili ni sifuri ndio maana anaweza kuwa na akiba zaidi ya hiyo...
 
Bora hata SUMAYE yeye kaamua kuwekeza nchini. Je wengine waliokwapua rasilimali zetu na kuamua kutokomea nazo gizani. Hongera SUMAYE kaza buti...!
 
Back
Top Bottom