Sumaye awekeza Shilingi Milioni 931 Benki ya CRDB

Sumaye awekeza Shilingi Milioni 931 Benki ya CRDB

Nami naunga mkono hoja ya hizo 900mil ni zao la muda mrefu la hisa zake kuzaa na kuzaa kila mwaka!
Tatizo letu ni utamaduni wa kutokuwa wazi kwa viongozi wetu.. unapaswa ukiingia madarakani tujue una nini na siku ukitoka tujue umevuna nini sio swala la siri ukishakuwa mtumishi wa umma, sheria ipo ila kwakuwa nchi hii viongozi wanaongoza kwa kuvunja sheria basi huwa mambo hayatekelezwi.
 
TUMBIRI (PhD Candidate, CPA(T), MBA(UDSM), Bcom(Accounting), PCM(Mzumbe High School)

Wewe jamaa unadhalilisha hii Elimu yako, sasa what's the issue?? Mbona pesa ndogo sana hiyo. Na kwa kuwa wewe ni mtafiti, ulitakiwa ufanye utafiti wako wa kujua kaanza kununua lini hizo hisa, na pia by then hizo hisa zilikuwa ni Shs. ngapi kwa hisa?? Kuna Wanahisa kibao pale CRDB wanahisa above 500 Million na ni Individuals.
 
Heshima mbele wana JF wote,
Ni muda mrefu sana nimekua sipatikani hapa JF. Baadhi yetu wamekuwa mkini PM na kuniuliza Vipi TUMBIRI? Umeng'olewa meno na kucha au?

Kimsingi nimebanwa na shule Wakuu. Lakini leo wakati napita pita huku na huku kutafuta literature za kusapoti Dissertation yangu nimegundua kitu kimoja.

Waziri Mkuu Mstaafu Mh. Frederick T. Sumaye anamiliki idadi ya hisa 6,206,980[SUP]1 [/SUP]za Benki ya CRDB ambazo kwa mujibu wa Ripoti ya Mwaka ya Benki hiyo, bei ya hisa moja kwa Soko la hisa hadi kufikia tarehe 31 Disemba 2012 ilikuwa ni Sh.150 kwa hisa. Kwa maana hiyo Mh. Sumaye anamiliki hisa zenye thamani ya Shilingi 931,047,000/=.

Hata hivyo kwa mujibu wa tovuti ya soko la hisa leo tarehe 07/06/2013 saa 20:50 hisa moja ya CRDB ina thamani ya Sh.205. Kwa maana hiyo Mh. Sumaye kwa sasa anamiliki hisa zenye thamani ya Sh.1,272,430,900/=.

Haijaelezwa na ripoti ya Benki ni lini Mh. Sumaye alinunua hisa hizo na kwa bei gani.

Uwekezaji wa kiasi hiki cha fedha ni kikubwa hasa ikizingatiwa Mmiliki ni aliyewai kuwa Mtendaji Mkuu wa Serikali ndani ya Serikali iliyopita.

Hii ni taarifa tu.

TUMBIRI (PhD Candidate, CPA(T), MBA(UDSM), Bcom(Accounting), PCM(Mzumbe High School).
tumbiri@jamiiforums.com,
Upanga, Dar es Salaam, Tanzania.

[SUP]1 [/SUP]CRDB Bank Annual Report 2012 (Page 66).


Nakala: Kimbunga, Mingoi, Ndallo, Matola, Crashwise, Mzee Mwanakijiji, Malaria Sugu, chama, mandingo6262, Rejao, Mungi, Putin, Salary Slip, etc


Mkuu TUMBIRI hebu njoo huku umalizie mjadala wako uliouanzisha.

KWA HISANI YA MTU WA TANZANIA
 
Back
Top Bottom