albuluushiy
JF-Expert Member
- Oct 2, 2013
- 1,404
- 687
Qaboos bin Said Al Said alizaliwa tarehe 18 Novemba mwaka 1940 katika mji wa Salala ulio kusini mwa Oman.Ndiye mtoto pekee wa Sultan Said bin Taimur.Mama yake ni malkia Mazoon al-Mashani.
Elimu ya msingi aliipata mjini Salala na baadae Pune nchini India.Alipofika miaka 16 alipelekwa kwa masomo ya juu nchini Uiengereza.Alipofika miaka 20 aliingia kwenye kikosi cha kijeshi cha kifalme kinachoitwa sandhurst. Baada ya kufaulu mafunzo katika chuo hicho alijiunga na jeshi la kiiengereza na kupangiwa shughuli za kijeshi kwenye bataliani ya 1 nchini Ujerumani ambako alikaa huko kwa muda wa mwaka mmoja na hata kushika nafasi za unadhimu kwenye jeshi hilo la kiiengereza.
Sultan Qaboos baadae aliacha shughuli za kijeshi na  akaanza kuchukua mafunzo ya namna ya kuendesha serikali za kiraia.Baada ya hapo alifanya ziara ndefu ya kuizunguka dunia kabla kurudi nyumbani kwao  Salalah.Alipofika Salala aliisoma dini yake ya kiislamu na historia ya nchi yake ya Oman.
Mwaka 1976 mfalme Qaboos alimuoa bint Ami yake, bi Kamila,nee sayyida Nawwal bint Tariq.Hata hivyo ndoa hiyo haikudumu na tangu aachane na mkewe huyo hajaoa tena na wala hana mtoto.
Mnamo mwezi Julai mwaka 1970 kikosi cha jeshi kilichomuunga mkono Qaboos kilipambana na kikosi cha jeshi cha mfame Said bin Taimur  na kufanikiwa kumpindua baba yake huyo.Serikali ya Uiengereza ilisaidia kuimarisha utawala wa mfalme Qaboos baada ya mapinduzi hayo.
Tangu mfalme Qaboos atawale Oman amefanikiwa kubadili hali za kiuchumi za raia wake na kuleta maendeleo makubwa nchini humo.
Ukoo wa mfalme Qaboos wa Abusaidy ndio uliokuwa na mahusiano makubwa na ukanda wote wa pwani ya mashariki ya Afrika na hata kuwa na utawala wa pamoja ambapo ulijenga makao makuu ya utawala wake nchini Zanzibar ambayo sasa ni nchi ndugu waTanganyika ambazo kwa pamoja zinaunda jamhuri ya muungano wa Tanzania.
Kwa zaidi ya karne moja raia wa ufalme huo waliweza kupenya kibiashara na kusambaa kote mashariki na kati ya Afrika.
Kutokana na ukweli huo wa kihistoria na mafungamano kati ya Oman na Tanzania zipo kila sababu kwa mfalme Qaboos bin Said kuja kutembelea Tanzania akianzia Zanzibar.
Kutokana na mapenzi makubwa ya wengi wetu kwake siku atakapofika tutajitokeza kwa wingi kwenye mitaa ya Shangani mjini Zanzibar au Kariakoo jijini Dar es salaam kujipanga barabarani kumpokea na kusalimiana nae.
Moja ya maeneo ambayo yanaweza kuwa kivutio na mapumziko ya sultan huyo wa Oman ni mbuga za wanyama za Serengeti,Loliondo na Ngorongoro. Kwa heshima na taadhima na kwa niaba ya wapenzi wa utawala wa Sultanate of Oman nachukua fursa hii kumkaribisha his majesty Sultan Qaboos bin Said aje kuitembelea Tanzania.
Elimu ya msingi aliipata mjini Salala na baadae Pune nchini India.Alipofika miaka 16 alipelekwa kwa masomo ya juu nchini Uiengereza.Alipofika miaka 20 aliingia kwenye kikosi cha kijeshi cha kifalme kinachoitwa sandhurst. Baada ya kufaulu mafunzo katika chuo hicho alijiunga na jeshi la kiiengereza na kupangiwa shughuli za kijeshi kwenye bataliani ya 1 nchini Ujerumani ambako alikaa huko kwa muda wa mwaka mmoja na hata kushika nafasi za unadhimu kwenye jeshi hilo la kiiengereza.
Sultan Qaboos baadae aliacha shughuli za kijeshi na  akaanza kuchukua mafunzo ya namna ya kuendesha serikali za kiraia.Baada ya hapo alifanya ziara ndefu ya kuizunguka dunia kabla kurudi nyumbani kwao  Salalah.Alipofika Salala aliisoma dini yake ya kiislamu na historia ya nchi yake ya Oman.
Mwaka 1976 mfalme Qaboos alimuoa bint Ami yake, bi Kamila,nee sayyida Nawwal bint Tariq.Hata hivyo ndoa hiyo haikudumu na tangu aachane na mkewe huyo hajaoa tena na wala hana mtoto.
Mnamo mwezi Julai mwaka 1970 kikosi cha jeshi kilichomuunga mkono Qaboos kilipambana na kikosi cha jeshi cha mfame Said bin Taimur  na kufanikiwa kumpindua baba yake huyo.Serikali ya Uiengereza ilisaidia kuimarisha utawala wa mfalme Qaboos baada ya mapinduzi hayo.
Tangu mfalme Qaboos atawale Oman amefanikiwa kubadili hali za kiuchumi za raia wake na kuleta maendeleo makubwa nchini humo.
Ukoo wa mfalme Qaboos wa Abusaidy ndio uliokuwa na mahusiano makubwa na ukanda wote wa pwani ya mashariki ya Afrika na hata kuwa na utawala wa pamoja ambapo ulijenga makao makuu ya utawala wake nchini Zanzibar ambayo sasa ni nchi ndugu waTanganyika ambazo kwa pamoja zinaunda jamhuri ya muungano wa Tanzania.
Kwa zaidi ya karne moja raia wa ufalme huo waliweza kupenya kibiashara na kusambaa kote mashariki na kati ya Afrika.
Kutokana na ukweli huo wa kihistoria na mafungamano kati ya Oman na Tanzania zipo kila sababu kwa mfalme Qaboos bin Said kuja kutembelea Tanzania akianzia Zanzibar.
Kutokana na mapenzi makubwa ya wengi wetu kwake siku atakapofika tutajitokeza kwa wingi kwenye mitaa ya Shangani mjini Zanzibar au Kariakoo jijini Dar es salaam kujipanga barabarani kumpokea na kusalimiana nae.
Moja ya maeneo ambayo yanaweza kuwa kivutio na mapumziko ya sultan huyo wa Oman ni mbuga za wanyama za Serengeti,Loliondo na Ngorongoro. Kwa heshima na taadhima na kwa niaba ya wapenzi wa utawala wa Sultanate of Oman nachukua fursa hii kumkaribisha his majesty Sultan Qaboos bin Said aje kuitembelea Tanzania.