Subaru Forester ina matatizo gani?

Subaru Forester ina matatizo gani?

Sifa za gari nzuri:
1. Ikidhi mahitaji yako
- mfano kama weye ni mkulima na unaenda kweye mashamba kupitia kwenye bara bara mbaya na mitope, 4xWD is a must.
- Kama weye ni mfugaji unapeleka mapumba kila siku shambani, ya nini ununue gari iliyofunikwa halafu uanze kukodi gari kufanya kazi zako.
- Kama unakaa 20km+ kutoka ofisini kwako hadi nyumbani na hii ni gari ya kuendea kazini cc 3000 za nini?????
2. Iendane na uwezo wako
Kununua gari sio shida sana. Unaweza kuvuta mkwanja benki ukanunua gari na kuendelea kurudisha kila mwezi mwajiri akicheka. swali ni je, utaweza kulipa hiyo monthly bila kuadhiri matumizi mengine - chakula, mavazi, karo za watoto? au ndo utaamua wande kwa kayumba alimradi weye barabarani kila mtu anageukia gari yako?
3. Garama ya spea: nadhani sio issue ya kuangalia juu juu hapa hapa. Kwa mtazamo wangu, angalia rate of consumption of spares vs price yake.
nakupa mfano kimahesabu kulinganisha gari X na Gari Y kwenye spear "S"

Ukichunguza vizuri jedwali hapa chini utaona kuwa aliyenunua Gari X atabadilisha spear "S" mara 2 tu ndani ya miezi 36 (miaka 3) na itamgarimu jumla ya 10,000 ila atatoa 5,000 kununua spea hiyo dhidi ya 2,000 ya yule wa gari Y ambaye atatoa hiyo kila miezi miwili lakini atatumia 36,000 mwisho wa kipindi cha miaka 3.
[TABLE="width: 500"]
[TR]
[TD][/TD]
[TD]Gari X
[/TD]
[TD]Gari Y
[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]Bei ya Spea "S"
[/TD]
[TD="align: right"]
5,000​
[/TD]
[TD="align: right"]
2,000​
[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]Spea hubadilishwa kila miezi mingapi?
[/TD]
[TD="align: right"]
18​
[/TD]
[TD="align: right"]
2
[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]Matumizi ya spear kwenye miaka 3
[/TD]
[TD="align: right"]
10,000
[/TD]
[TD="align: right"]
36,000
[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD][/TD]
[TD][/TD]
[TD][/TD]
[/TR]
[/TABLE]
 
Nashukuru kwa kitia moyo. Nafikiri hatupaswi kuogopa sana bei za spare kwa sababu sio kila kukicha unabadilisha spare ya gari. Wenzetu wanasema if you use it take care of it. If you take care of it, it is going to last longer.

Na mkuu uzuri wa hizo spare ni halisi sio kama za toyota unazofunga kila baada ya miezi!
 
Gari zote duniani nzuri hata ikiwa ni TATA cha umuhimu ni utunzaji
 
SUbaru is one of the Best Cars ,kama unapenda comfortability na Power.
Fuel Consumption haina ni ya kawaida sana ,min ni 8km/l and yet gari inakimbia vizuri.

Spare tangu 2010 imekuwa sio shida ,Subaru zipo kibao hapa town ,ukienda kwa Karim ,Nyange bei ya kutupa tu na ni spare Original.

Atown ,kenya maspare kibao. Sioni Sababu ya kuogopa.

Ila kama wadau walivyosema angalia matumizi yako na interest zako pia. Kuna watu wanakatisha tamaa wakati wao wanamiiki ROver au Volvo.
 
Kwa nini uliwaza kununua Forester toka mwanzo?
Hpo ndy tunatakiwa kuanzia mjadala. Wife anaendesha forester!
 
Subaru Forester ni gari zuri na imara ila ugumu unaweza kujitokeza pale litakapohitaji matengenezo. Spea za Subaru bado ni adimu sana Tanzania. Na hata zikipatikana, ni ghali. Jambo lingine ni uchache wa mafundi wanaomudu kuzifanyia matengenezo injini za Subaru ambazo kitaalam zinaitwa flat-four au boxer engines. Kama ukiamua kununua Subaru Forester hakikisha unaitunza vizuri ili kuepuka matengenezo ya mara kwa mara.
 
Nashukuru kwa kitia moyo. Nafikiri hatupaswi kuogopa sana bei za spare kwa sababu sio kila kukicha unabadilisha spare ya gari. Wenzetu wanasema if you use it take care of it. If you take care of it, it is going to last longer.

Mkuu, suala la spare si la kufanyia mzaha hata kidogo, unaweza kushindwa kuliendesha kwa kukosa spare ndogo kabisa! Ni vizuri ukaelewa ni wapi unaweza kupata spare za gari lako taraja. Kama hapa nyumbani ukikosa basi unaweza kuagiza toka Japan, ukishalipia unaweza kupata mzigo ndani ya siku 5-7.
 
SUbaru is one of the Best Cars ,kama unapenda comfortability na Power.
Fuel Consumption haina ni ya kawaida sana ,min ni 8km/l and yet gari inakimbia vizuri.

Spare tangu 2010 imekuwa sio shida ,Subaru zipo kibao hapa town ,ukienda kwa Karim ,Nyange bei ya kutupa tu na ni spare Original.

Atown ,kenya maspare kibao. Sioni Sababu ya kuogopa.

Ila kama wadau walivyosema angalia matumizi yako na interest zako pia. Kuna watu wanakatisha tamaa wakati wao wanamiiki ROver au Volvo.

Naendesha VW na Spare napata ndo sembuse Subaru watanzania inabidi tuondokane na Kasumba za Toyota yaani ukimtajia Mtanzania gari tofauti na toyota kitu cha kwanza atakuambia spare wakati spare siku hizi unaweza hata kuagiza mwenyewe na within 3days tu imeshakuja
 
Subaru Forester ni gari zuri na imara ila ugumu unaweza kujitokeza pale litakapohitaji matengenezo. Spea za Subaru bado ni adimu sana Tanzania. Na hata zikipatikana, ni ghali. Jambo lingine ni uchache wa mafundi wanaomudu kuzifanyia matengenezo injini za Subaru ambazo kitaalam zinaitwa flat-four au boxer engines. Kama ukiamua kununua Subaru Forester hakikisha unaitunza vizuri ili kuepuka matengenezo ya mara kwa mara.
Mimi wakati nanunua Mitsubishi mini wakati huo nilitishwa sana, kwamba hakuna spare mara ooh, kakianza kuharibika nitakakimbia. Lakini hivi ninavyoongea hakajawahi kuharibika halafu nikakosa spea. Na zaidi ya yote, zaidi ya kubadili oil ya injini na gea box, spea niliyowahi kubadilisha ni mafula na injini mounting tu na kama miaka miwili sasa tangu ninunue. Na ninaenjoy kuendesha kwa shilingi 10000 tu kwa siku kutokea Mbagala hadi ubungo kwenda na kurudi kila siku. Sasa najiuliza vile vitisho vya mara spea, mara kakianza kuchoka, mbona sivioni? Wewe nunua kile roho inapenda. Mengine yote yatajulikana mbele ya safari.
 
Nataka kununua gari ya Subaru Forester. Naomba mtu mwenye uzoefu na hiyo gari aniambie mazuri na mabaya yake.

Kaka kama unapesa za mawazo ikimbie mbali hiyo gari jichukulie Toyota. Kwanza kama ukinunua jua ni yako hiyo hadi inakufia. Mbili kuna rafiki yangu inayo auto imeng'ang'ania gia no. 3 na mbaya zaidi yupo mkoani mafundi wote huko wamechemsha kampata mmoja hapa Dar ratiba yake mpaka March na awe na 3 M cash hapo bila spare. Now anafugia kuku tu. huo ni ushauri wangu.
 
Haina Tatizo lolote kwani katika magari mawili ya Toyota nilioendesha hili ni zuri kuliko hayo.Mimi nimeendesha sasa naenda mwaka wa tatu sijawahi kupata tatizo lolote.Ni utunzaji tu ukiwa mzuri service kama inayotakiwa .Kubota ni vijana wanapenda hivyo na kuna namna fundi anakufanyia pale kwenye bomba la kutolea moshi.haya magari huwa yanatoa huo mlio kwani asili ni magari ya mashindano
 
Subaru forester has a very unique drive experience. U will enjoy it. Consumption sio ya kutisha kiivyo but huwezi kuilinganisha na toyota saloon, but from my experience its better than rav4 or noah. If u take a good care of it, u shud not worry about spare.

Hiv unaijua Rav4 kweli mkuu.
U cant b serious here
 
Mimi wakati nanunua Mitsubishi mini wakati huo nilitishwa sana, kwamba hakuna spare mara ooh, kakianza kuharibika nitakakimbia. Lakini hivi ninavyoongea hakajawahi kuharibika halafu nikakosa spea. Na zaidi ya yote, zaidi ya kubadili oil ya injini na gea box, spea niliyowahi kubadilisha ni mafula na injini mounting tu na kama miaka miwili sasa tangu ninunue. Na ninaenjoy kuendesha kwa shilingi 10000 tu kwa siku kutokea Mbagala hadi ubungo kwenda na kurudi kila siku. Sasa najiuliza vile vitisho vya mara spea, mara kakianza kuchoka, mbona sivioni? Wewe nunua kile roho inapenda. Mengine yote yatajulikana mbele ya safari.

Mkuu kwa distance ya Mbagala tu ubungo kwenda na kurud about 60km!!!!!!!!!!!!
 
Back
Top Bottom