Suala la elimu na likizo za watoto

Raia Fulani

JF-Expert Member
Mar 12, 2009
10,883
2,765
Nasoma gazeti la Mwananchi hapa kuhusiana na mvutano aidha watoto waende likizo au wabaki shuleni kujisomea. Mjadala huu ulikuwa Bungeni. Kuna hoja kuwa baadhi ya mikoa kupitia wakuu wa mikoa imepanga utaratibu wa kuongeza "ufaulu". UFAULU kwenye maeneo yao.

Sehemu nyingine Mbunge na mmiliki wa shule, ndugu Rweikiza anasema, "wanajitolea (wazazi) wakati wa likizo, kwenye madarasa wanaweka magodoro na wasio na uwezo wanaweka nyasi nyingi, wanaweka taa watoto wabaki pale wasome usiku na mchana waweze "kufaulu". KUFAULU. Hoja hapa ni kufaulu. Hawa wadau hawaoni aibu katika kujadili hili. Wafaulu then what?

Kwa mwenendo huu, huu mtaala mpya wa elimu upite tu haraka ili kuwajenga hawa watoto kuelewa na sio kufaulu. Wakuu wa shule wanatafuta status za shule zao zionekane zimefaulisha kumbe wamewakaririsha watoto. Wanatoka na spirit hiyo toka sekondari kwenda vyuoni na wanaendeleza kukariri na kutoka huko na GPA za kutisha. Baadae unakutana na wasomi, madokta, na maprofesa wenye elimu ila hawana akili.

Ukweli uko wazi. Hawa wasomi wanajua zaidi mambo waliyojifunza kuliko wanayokutana nato katika maisha halisi. Ndio hawa unawakuta kila siku wanapinduana kwenye familia. Mume mbabe, mke mbabe. Wote wasomi. Majirani wanaonekana vijakazi, n.k.

Wakati mwingine unamsikiliza kijana anazungumza kwenye TV akitoa hoja unamuona kabisa akivuta kumbukumbu ya kile alichosoma darasani na mbaya zaidi anatumia na kingereza kwenye baadhi ya maneno kuashiria kuwa hawezi free style.

Watoto waachwe waende likizo, tena isiwe hiyari. Na huu mtaala mpya uje mapema ili kuwapa hawa watoto machaguo ya kufanya kuloko kuanza kukariri sepal, petal, kikonyo, n.k.
 
Waacheni waende tu, wakipata zero watajuana na wazazi wao ambao wao walibaki shule wakati wa likizo
 
Kusema iwe lazima kwenda likizo nao ni ujinga.

Watu waachwe huru mtoto anayetaka kubaki shule abaki, asiyetaka pia asilazimishwe kubaki.

Sisi vijana wengine tumemaliza hatuna ajira, wakati wa likizo ndio tunapata vipesa kwa kupiga pindi mashuleni.
 
Mimi kama mwalimu siwezi kuacha utaratibu wa kufundisha wanafunzi mwanzo wa kozi hadi mwisho wa mwaka, nioneshe likizo zote kwenye azimio la kazi lenye mihula miwili halafu nisilifuate.

Hakuna ofisa wa elemu wa ngazi yeyote atakayenipangia kazi za kufundisha wakati wa likizo nitampinga kwa hoja za misingi ya elimu na sitatii agizo lake.

Wanafunzi wanatakiwa wapumzike ili ku fresh mind akili zao zipate uwezo mpya wa kujifunza mada mpya. Huu ni ujuha na ukiukaji wa kanuni za ufundishaji kufululiza kuwapa dozi wakati wa likizo.

Hoja kuwa watafaulu sana ni ya kipuuzi na kizembe katika ufundishaji unaofuata taratibu za ufundishaji.
 
Nasoma gazeti la Mwananchi hapa kuhusiana na mvutano aidha watoto waende likizo au wabaki shuleni kujisomea. Mjadala huu ulikuwa Bungeni....
Uko sahihi mkuu,

Mimi kama mwalimu nasema kuwa walimu baadhi yetu ni wahuni wahuni ,hakua uhusiano kati ya mtoto kubaki akisoma wakati wa likizo na ufaulu wake,eti unakuta mwalimu anadai huu ndo muda wa kufanya ukamilishaji wa syllabus sasa kma ndivyo,

fundisha bure basi nasio kuwatoza watoto,mwisho wa siku unabaki unajiuliza huyu mwalimu kakaa na mtoto siku almost 90 hajakava silabasi,sasa siku ushirini za kazi wakati wa likizo ataweza !? Unabaki na jibu la kuwa hizi ni project zetu sisi walimu kujipatia pesa.
 
KUFAULU. Hoja hapa ni kufaulu. Hawa wadau hawaoni aibu katika kujadili hili. Wafaulu then what?
Safiii....☝️☝️
Kwa mwenendo huu, huu mtaala mpya wa elimu upite tu haraka ili kuwajenga hawa watoto kuelewa na sio kufaulu.
Safi tena ☝️☝️☝️
Wakuu wa shule wanatafuta status za shule zao zionekane zimefaulisha kumbe wamewakaririsha watoto.
Safi zaidii...☝️☝️ 👏👏👏
Ukweli uko wazi. Hawa wasomi wanajua zaidi mambo waliyojifunza kuliko wanayokutana nato katika maisha halisi.
Safii tena..👏👏👏
Watoto waachwe waende likizo, tena isiwe hiyari. Na huu mtaala mpya uje mapema ili kuwapa hawa watoto machaguo ya kufanya kuloko kuanza kukariri sepal, petal, kikonyo, n.k.
Mkuu wewe ni Brain.. sina la kuongeza.
 
Uko sahihi mkuu,Mimi kama mwalimu nasema kuwa walimu baadhi yetu ni wahuni wahuni ,hakua uhusiano kati ya mtoto kubaki akisoma wakati wa likizo na ufaulu wake,eti unakuta mwalimu anadai huu ndo muda wa kufanya ukamilishaji wa syllabus sasa kma ndivyo,fundisha bure basi nasio kuwatoza watoto,mwisho wa siku unabaki unajiuliza huyu mwalimu kakaa na mtoto siku almost 90 hajakava silabasi,sasa siku ushirini za kazi wakati wa likizo ataweza !? Unabaki na jibu la kuwa hizi ni project zetu sisi walimu kujipatia pesa.
Kweli kabisa. Inakuwaje syllabus inapangwa mwanzo wa muhula na haikamiliki, hivyo ije kukamilikia kipindi cha likizo?
 
Uko sahihi mkuu,Mimi kama mwalimu nasema kuwa walimu baadhi yetu ni wahuni wahuni ,hakua uhusiano kati ya mtoto kubaki akisoma wakati wa likizo na ufaulu wake,eti unakuta mwalimu anadai huu ndo muda wa kufanya ukamilishaji wa syllabus sasa kma ndivyo,fundisha bure basi nasio kuwatoza watoto,mwisho wa siku unabaki unajiuliza huyu mwalimu kakaa na mtoto siku almost 90 hajakava silabasi,sasa siku ushirini za kazi wakati wa likizo ataweza !? Unabaki na jibu la kuwa hizi ni project zetu sisi walimu kujipatia pesa.
Shida ni walimu...
 
Kusema iwe lazima kwenda likizo nao ni ujinga.

Watu waachwe huru mtoto anayetaka kubaki shule abaki, asiyetaka pia asilazimishwe kubaki.

Sisi vijana wengine tumemaliza hatuna ajira, wakati wa likizo ndio tunapata vipesa kwa kupiga pindi mashuleni.
Lakini hao hao huja likizo na kusoma hizo tuisheni
 
We nenda likizo sisi acha tufanye Kazi wewe Mwalimu wa kijijini
Walioweka likizo ni wajinga?

Hivi kumlisha mtoto masomo zaidi ya saba kwa mwaka mzima ataelewa nini?

Acheni kuendekeza njaa fungua miradi mingine yabkukuingizia kipato wakati wa likizo.
 
Kuna watu wanawaona walimu maskini sana na wanataka hela za wanafunzi za likizo, kufundisha likizo ni moyo na sio pesa, wazazi mnajisahau sana kua hata uyo mtoto akija likizo utampeleka tuition na utalipa, ssa swali linakuja tuition anasoma nn kipya ambacho shule hafundishwi?? Kila mtu atabeba mzigo wake matokeo yakitoka
 
Kusema iwe lazima kwenda likizo nao ni ujinga.

Watu waachwe huru mtoto anayetaka kubaki shule abaki, asiyetaka pia asilazimishwe kubaki.

Sisi vijana wengine tumemaliza hatuna ajira, wakati wa likizo ndio tunapata vipesa kwa kupiga pindi mashuleni.
Heh!!!
 
Walioweka likizo ni wajinga?

Hivi kumlisha mtoto masomo zaidi ya saba kwa mwaka mzima ataelewa nini?

Acheni kuendekeza njaa fungua miradi mingine yabkukuingizia kipato wakati wa likizo.
Kaka walimu sio maskini kma unavyofikiria, wewe ulisoma masomo mawili wakati unasoma?? Ulikua wapi kutoa hoja hii wakati unasoma?? Tuache kufata mihemko ya wanasiasa
 
Back
Top Bottom